Mastermind, unaonekana umebobea sana, kawasaidie na Lumumba maana wanashindwa hata kuset mashambilizi[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Mwambie amtafute police njaa yyte ampe mtonyo kisha amfungulie jarada la kisela ambalo maelezo yake yaseme kwamba kabakwa na kusababishiwa ujauzito kuhusu tarehe ya siku ya tukio ifojiwe kwa kukokotoa kurud nyuma kadri ya umri wa mimba after kutoka jera huyo bwana ake Og apewa maelezo na uthibitisho huo na Huyu jamaa mchepuko akijifanya kumfwatilia mtoto amwangushie jumba bovu kwa kumchana bwana ake kwamba huyo mchepuko ndy moja kati ya watu walio mbaka
Aliolewa miaka miwili iliyopita(2017),miezi miwili baada ya kuolewa mumewe akahukumiwa miaka 40 kwa makosa la unyang'anyi wa kutumia nguvu na makosa mengine(alimuoa akiwa nje kwa dhamana)
Bibie akawa amekata tamaa kabisa japokuwa walikata rufaa na kesi ilikuwa inaendelea,akaanza mahusiano ya kimapenzi na jamaaa mmoja kwa siri sana,hivi ninavyoandika uzi huu bibie keshatundikwa mimba na anatarajia mwezi wa nne mwakani ampokee Kijacho.
Wakati anatarajia kupokea huo ugeni mumewe naye kashinda kesi ya unyang'anyi wa kutumia nguvu na kesi zingine kwahiyo atatumikia jela miaka mitatu tu jela,panapo majaaliwa mwezi wa Saba mwakani jamaa atakuwa uraiani,ngoma nzito.B
ibie anawaza kuichomoa mimba ili ainusuru ndoa yake pia maisha yake,maana mumewe sio mtu wa mchezomchezo,kamshirikisha mtu wake kile anachofikiria kukifanya mtu wake anamwambia ukitoa mimba ama zako ama zangu la sivyo ukishajifungua mtoto siku hiyo hiyo niachie nitampeleka kwenye vituo vya kulelea watoto yatima ili akija mumeo muendelee na maisha yenu.
Ila sikubali mimba ichomolewe ikichomolewa na chomoka hukohuko,yupo njia panda anawaza hajui afanye nini kote kwa moto,kaniomba ushauri nimeshindwa kumpa ushauri hatimaye nimekuja kwenu wanajukwaa tiririkeni.
Dah wanawake wa siku izi ndo maana wagumba wamekuwa wengi, ye anaona ni jambo la kawaida sana kutoa mimba, ndo maana anasema yule baba hana akili anavosema mwenzie azaeKwahiyo unashauri afanye mauaji ya kiumbe kisicho na hatia,
Ndo maana tunasema wanawake wengine ( ukiwemo na wewe) ni masheteni tu.
Kwani hakuna watu wazima huko kwao?
Wewe unaweza kwenda kwa mtu mzima umwambie nimezini nje ya ndoa na nimetia mimba?
AiseeeNaam, ndio maana watu wazima wapo, wadhamini wa ndoa wapo na washenga wapo...
Mwambie afanye harakaNgoja Kaka Jambazi aje atoe ushauri
Jabakeke Huyo rafiki yako alipoamua kuzaa na jamaa mwingine walikua na mipango gani, kuzaa tuu au kuishi pamoja?
Kama ni kosa limeshatendeka na mimba imepatikana... mimi simshauri aue mtoto wake maana hilo ni kosa lingine kubwa ambalo atajutia. Na hata akifanya hivyo huyo aliye jela atajua tuu anaweza asimkubali mtoto na akamwacha vile vile.
Atulie azae huku akisubiri talaka yake
Vinginevyo atakosa bara na pwani - atamkosa mume jambazi, atamkosa mtoto na baba mtoto nae atamwacha