Kafara la kukimbiza moto linavyoligharimu Taifa

Kafara la kukimbiza moto linavyoligharimu Taifa

Wanachonikera ni hii michango yao ya lazima waliyoianzisha awamu hii ya tano! Watumishi wa umma wanatengenezewa mazingira ya kuchangia pasipo hiyari yao, ukija kwa wafanyabiashara mambo ni yale yale! Sasa unajiuliza, kama hata hela ya kukimbizia hamna, si bora ukahifadhiwa makumbusho badala ya kuwasumbua wananchi?

Kichekesho ni pale wanapokosa kitu cha kuzindua, utawaona wakienda kuzindua hadi nyumba za watu! eti nyumba bora ya mfano! ni upotevu tu wa muda na fedha za walipa kodi.
 
Kwa mujibu wa simulizi za kidini, ulimwengu umewahi kuadhibiwa mara mbili na mwenyezi Mungu kwa mapigo mawili makubwa.

Pigo la kwanza wakati wa Nuhu, Pigo la gharika hili lilipozwa kwakuwa maji ni uhai na watu walipewa muda wa kujiandaa. Hili ni pigo takatifu lenye nafasi ya uhai ndani yake.

Pigo la pili lilikuwa kwenye miji ya Sodoma na Gomora. Pigo la moto, hili liliteketeza kila kitu watu na mali na viumbe hai. Waliosalimika ni watatu tu Lutu na mabinti zake wawili. Mke wake alivunja sharti la kugeuka nyuma hivyo akawa jiwe la chumvi.

Moto huteketeza vibaya kuliko maji. Shambulio la silaha za nyuklia kule Hiroshima Japan athari zake zinaonekana mpaka kesho.

Kwenye uchawi na ushirikina uchawi wa kuchoma kitu ni hatari na mbaya zaidi ya uchawi wa maji na udongo.

Mwenge wetu wa uhuru ukiachana na sababu zake za kishirikina. Ulifanywa kama alama muhimu ya kukumbukwa na ukawekwa juu ya mlima Kilimanjaro. Kwenye barafu!? Yani ukayeyushe barafu?

Dhana ya kukimbiza huu moto unaoitwa mwenge ni kafara la kutisha lenye tafsiri mbaya kiroho. Hebu fananisha mwenge wa olimpiki na huu wa kwetu.

Moto ule ukimbizwao hufisha, huchoma na kuharibu kabisa fikra yakinifu, mawazo chanya.. Maono ya taifa bora, ujasiri, uthubutu na kujiamini.

Ni kafara la kufanya upande mmoja uendelee kusimama na kutawala wengine. Bila uthubutu dhahiri wa kuhoji ama kuchukua maamuzi magumu. Jamiii huishia kulalama na kulalamika tu kisha husahau na maisha kuendelea.

Siri ya huu moto ukimbizwao inaisha... Hakuna kiongozi wake aliyewahi kumaliza miaka mitano akiwa hai baada ya kuukimbiza nchi nzima.

Mwaka ambao tutashindwa kufanya hili kafara la kukimbiza moto uwakao ndio mwaka taifa litajikomboa na kukombolewa!


Edwin Kagasheki.M

IJUE HISTORIA YA KUANZISHWA KWA MWENGE:

Mnamo miaka ya zamani hizo kabla na baada kidogo ya ukoloni watu waliamini sana katika Mazindiko, Uchawi na Kafara tofauti kidogo na miaka ya hivi leo(miaka ya utandawazi) ambapo watu huyapooza mambo hayo kwa kukemea mila potofu na pengine ni ukiukwawaji wa haki za binadamu. Naam basi tuitizame miaka ya 1900 ambapo walizaliwa watu mashuhuri na baadaye waliitwa "wataalamu" walioweza kusaidiana na viongozi wa nchi yetu kwenye mambo mbalimbali ya kitaifa na waliaminika sana kwenye tawala za ki-chief na jamii kwa ujumla.

Miongoni mwao alikuwepo mtaalamu aliye julikana kwa jina la Forojo Ganze, huyu alizaliwa mwaka 1902 na alikuwa na jopo la wafuasi wake/wazee wenzake wa nyakati hizo ambao walikwenda sambamba na Mwl.Nyerere katika kutoa mchango wao wa kitaalamu kwenye maswala nyeti ya kitaifa.

Forojo Ganze, alikuwa ni mchawi maarufu na ni mmoja kati ya wazee waliotumwa kufanya zindiko la nchi baada ya uhuru kule bagamoyo, walipewa kazi ya kuhakikisha rais aliye madarakani (Mwl.Nyerere) hapingwi na mtu yeyote. Zindiko hilo lilifanyika bagamoyo katika moja ya mashimo yanayopatikana wilayani hapo, na zoezi hilo lilienda sambamba na kumuuliza shetani na malaika zake "ni jambo gani lifanyike ili Tanzania iendelee?".

Basi kiongozi wa msafara Forojo Ganze ndiye mtu pekee aliyeingia kwenye hilo shimo mithili ya pango kwaajili ya kuuliza , alikaa huko kwa muda wa siku 10 huku akiwa amewaacha wazee wenzake nje wakimgoja atakuja na jibu gani ili wakampatie rais na wazee wengine wa Dar es salaam, kilichoshangaza siku ya kumi na moja alitoka akiwa hoi hajiwezi alikuwa kama mtu aliyepigwa na alikuwa anaongea lugha isiyofahamika, wenzake wakiwa wanaongozwa na Yahaya Hussien walimbeba hadi ikulu Dar es salaam na walipomfikisha mbele ya mwalimu Nyerere alitamka maneno haya "Baba, sisi tunataka kuwasha mwenge na kuuweka juu ya mlima kilimanjaro, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini mahala pasipo na tumaini, faraja palipo na huzuni, upendo penye chuki na heshima palipo na dharau ".

Alitamka maneno hayo yanayohusu mwenge kwa kiswahili kisha akanyoosha juu mkono wake wa kulia ambao tayari ulikuwa umeandikwa namba hii 115, kisha akakata roho.

Baada ya mazishi mwalimu aliyafanyia kazi maneno ya Forojo Ganze akaanzisha mwenge wa uhuru bila kujua ulikuwa na maana gani, baada ya hapo alimuagiza Yahya Hussein atafasiri maana ya ile namba 115, kama kawaida ya Shekhe Yahaya alitafasiri akamwambia kuwa namba hiyo inamaanisha "Utakufa ukiwa na umri wa miaka 77 na taifa la Tanzania kwa kipindi hicho litakuwa na umri wa miaka 38 ".

Hii inamanisha ukichukua 77 umri wa mwalimu jumlisha 38 umri wa taifa utapata 115, na hii ndivyo ilivyokuwa, mwaka 1999 mwalimu alikufa akiwa na miaka 77 na taifa lilikuwa na miaka 38 ya uhuru (77+38=115) pia utamaduni wa rais kuongea na wazee wa Dar es salaam unaendelea hadi sasa na wamekuwa na maamuzi ya kitaifa na husikilizwa sana wanachokisema.
Jiulize, mbona haijawahi kutokea rais akaongea na wazee wa Bukoba ama wa Arusha jambo la kitaifa?
Jibu, Zindiko la bagamoyo linafanya kazi.

Safu iliyoagizwa kufanya zindiko ilikuwa ya watu watano(5) ambao ni.
1: Forojo Ganze mwenyewe,
2: Mzee Ramadhan, aliye zaliwa mwaka 1920,
3: Ally Tarazo, aliye zaliwa mwaka 1929,
4: Komwe wa Komwe, aliye zaliwa mwaka 1918 na
5: Shekhe Yahya Hussein, aliye zaliwa mwaka 1925
Nyerere amelaaniwa.
 
Alitamka maneno hayo yanayohusu mwenge kwa kiswahili kisha akanyoosha juu mkono wake wa kulia ambao tayari ulikuwa umeandikwa namba hii 115, kisha akakata roho.
Duh!
Noma sana.

Hii stori inaweza kutumika ku-derive mbinu ya kuweza kuiondoa ccm madarakani uchaguzi wa Oktoba 2025.
 
Hii inamanisha ukichukua 77 umri wa mwalimu jumlisha 38 umri wa taifa utapata 115, na hii ndivyo ilivyokuwa, mwaka 1999 mwalimu alikufa akiwa na miaka 77 na taifa lilikuwa na miaka 38 ya uhuru (77+38=115) pia utamaduni wa rais
Na baada ya Nyerere kufa , kila kitu alichokianzisha kikafa. Viwanda vilivyokuwepo enzi za utawala wake vilikufa .

Nyerere alikufa na namba 115 yake . Sasa hivi taifa halieleweki taratibu hazifuatwi , taifa lipolipo tu , ccm wameshaugua ugonjwa wa dementia ( akili za ccm zimeshadumaa) .
 
Nyerere amelaaniwa.
Mtazamo wako ni very negative, yaani wewe ni pessimist pro max! Moto ni alama ya power, na pia mwanzo mpya
Tuna kasumba ya kuona vitu vya wenzetu vya maana kama mwenge wa Olympic alafu mwenge wa uhuru hauna maana. Baadhi ya vitu vya kujivunia ambavyo ni vya kwetu hata wageni waje kuona ni Mwenge wa Uhuru. Uongezewe umuhimu . Badala ya kuuzungusha Tanzania nzima kila mwaka , uwekwe kanda moja kila mwaka alafu miuondo mbinu ya huo mkoa kama afya , maji shule viwekewe kipaumbele.
Julius Kambarage Nyerere ni Baba wa Taifa , mambo alioyafanya yatabaki kama historia isiofutika
 
Mtazamo wako ni very negative, yaani wewe ni pessimist pro max! Moto ni alama ya power, na pia mwanzo mpya
Tuna kasumba ya kuona vitu vya wenzetu vya maana kama mwenge wa Olympic alafu mwenge wa uhuru hauna maana. Baadhi ya vitu vya kujivunia ambavyo ni vya kwetu hata wageni waje kuona ni Mwenge wa Uhuru. Uongezewe umuhimu . Badala ya kuuzungusha Tanzania nzima kila mwaka , uwekwe kanda moja kila mwaka alafu miuondo mbinu ya huo mkoa kama afya , maji shule viwekewe kipaumbele.
Julius Kambarage Nyerere ni Baba wa Taifa , mambo alioyafanya yatabaki kama historia isiofutika
Baba wa taifa ambaye hakuwa baba Bora. Unamfahamu Nyerere kwa kumsoma kwenye vitabu vya kumsifu na kumtukiza, hujui upande wake wa pili
 
Back
Top Bottom