Kafulila: Ifikapo mwaka 2050 kipato cha kila Mtanzania kitakuwa kati ya TZS 12M na 20M pato la Taifa litafikia $700bn mara 9 zaidi ya leo

Mwananchi Huru

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2021
Posts
2,128
Reaction score
1,896

YAJAYO YANAFURAHISHA SANA

Mkurugenzi Mkuu wa kituo cha Ubia nchini PPPC Bwana David Kafulila ameandika haya katika ukurasa wake wa X zamani tweeter,

Kafulila akiifafanua Dira ya Maendeleo ya Taifa la Tanzània ya 2025- 2050 amesema yafuatayo,

1. Kafulila amewataka Watanzania wafahamu kuwa chini ya CCM hii na ifikapo mwaka 2050 Uchumi wa nchi yao utakua kwa Kasi na kufikia $700bn sawa na TZS 1,750 Trilioni.

2. Kafulila amewataka pia Watanzania watambue kuwa chini ya CCM hii Pato lao la mwaka litakuwa na kufikia kati ya $4,500 na $8,000 kwa mwaka yaani hapa karibu kila mtu itakuwa ni kula bata tu Cha msingi tuombe Uzima tu.

3. Kafulila amewataka Watanzania wafahamu yakuwa chini ya CCM hii vipato vyao na Pato la Taifa lao vitaongezeka kwa karibu mara tisa (9) zaidi hii hakuna nchi yoyote itaweza ila Tanzània na Watanzania.

4. Kafulila amewataka pia Watanzania wafahamu kuwa Uchumi wao kwa Sasa ni $80bn lakini chini ya CCM hii na kwa Miaka 25 ijayo utaongezeka kwa Kasi karibu mara 9 zaidi na kufikia 700bn na kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi Tajiri zaidi Africa na hii ni chini ya CCM.

5. Kila Mtanzania na afahamu ukuaji huu mkubwa wa maajabu wa Uchumi wa Tanzania na wa mtu mmoja mmoja ni chini ya CCM tu na wala sio vinginevyo.
 
Kuna kitu kinaitwa inflation, Mwaka 2050 hii elf 10 itakuwa ya kununulia pipi

Mwaka 2000 nauli ya daladala ilikuwa shilingi 10, chipsi yai shilingi 100

Leo hii 2024 shilingi 100 ni ya pipi mbili
 
Kipato ni mazao uliozalisha sio makaratasi pesa
 
Miaka 26 baadaye USD/TZS zitakuwa na thamani sawa na sasa? Je, miaka 26 nyuma zilikuwa na value/purchasing power ya mwaka huu 2024?
Kila kitu kinakua symuliteniously mkuu
 


Plan za kijinga sana kwa miaka 25 kutoka leo tuwe tunatengeneza $4500 ambayo ni sawa na $1,048.49 kwa mwaka kwa thanami leo kwa mfumuko wa bei wa 6% kwa mwaka.

Tatizo la siku hizi vijana wetu wanakariri shule hawaelewi haya🤦🏾‍♂️
 
Point ya 5 imenifurahisha sana
 
Hicho ni kipato cha chini tu kama sijakosea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…