Kafulila: Kwa Utafiti uliopo ndani ya miaka 25 ijayo Tanzania italazimika kujenga uchumi sawa au zaidi ya Afrika ya Kusini ya leo

Mwananchi Huru

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2021
Posts
2,128
Reaction score
1,896
===
Akihojiwa na kituo cha runinga cha Clouds Media Group Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia nchini Tanzania PPP -Centre David Zacharia Kafulila alikuwa na haya ya kusema ;-

"Tafiti zilizofanyika zilionesha kwamba mwaka 2015 mahitaji ya miundombinu yaliyokuwepo yalijitosheleza kwa asilimia 30% tu ya mahitaji ya miundombinu itakayohitajika mwaka 2050 yaani miaka 35 baadae,

Ukitazama mwenendo wa uchumi wa Tanzània wa sasa utagundua kwamba Tanzania itahitaji kujenga uchumi mkubwa zaidi ya ule wa Afrika kusini ya leo ndani ya miaka 25 ijayo.

Kujenga Uchumi zaidi ya Africa ya Kusini ya leo ni jambo ambalo kama tukitumia Kodi na Mikopo pekee hatutaweza kulifikia na hii ndio sababu muhimu ya kutumia PPP ili kufikia matarajio na matamanio haya makubwa ya Watanzania ifikapo mwaka 2050.

David Kafulila anaendelea kwa kusema, " Tunachakata kupata mwekezaji serious wa kujenga barabara ya kisasa ya kulipia kutoka Kibaha- Chalinze mpaka Morogoro.

Jambo la uhakika ni kuwa wawekezaji wanajua pamoja na uwepo wa Reli na treni mpya za SGR bado mahitaji ya usafiri na usafirishaji yataendelea kuwa ni makubwa kila wakati kutokana na ukubwa wa uchumi wa Tanzània unaojengwa chini ya Rais Samia na Chama chake Cha Mapinduzi CCM.



=====

Your browser is not able to display this video.
 
Yuko sahihi...

Heko kwake....

Tulipopata uhuru wetu ,Dar es salaam ilikuwa na wakazi laki 3 tu.....nchi nzima walikuwa milioni 9......

Leo tuko milioni 60+.....

Wawekezaji waijenge tu hiyo barabara ya kulipia kutoka Kibaha mpaka Morogoro.....

#Rais Samia na 4R's [emoji7][emoji7]
 
[emoji7][emoji7]
 
Hiki kizazi cha wapuuzi mpaka kiondokr
 
Kazi bado kabisa
 
Chifu Nkunda Kafulila mtanzania? Unafahamu yule mwasi wa Kongo Banyanulenge Nkunda?
Shida yako ni chuki na kukosa maarifa, majina ya kibatu yanafanana sana na siyo kigezo cha kukataa utanzania wq kafulila. Fatilia majina ya Watanzania wengi wanaotoka mikoa ya mipakani utagundua majina mengi yanapatikana nchi nyingine pia na hiyo siyo sababu ya kutilia shaka utanzania wao.
Nenda Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Kagera, Rukwa, Kigoma, Mtwara, Mwanza, Tanga (mpakani na Mombasa) n.k utagundua hilo na utajidharau. Mwisho wa siku tafuta hela upunguze wivu.
 
Kuna majina ni hatarishi kwa nchi hiyo mikoa mingine yote umetaja kasoro mkoa mmoja majina yao hata yaingiliane hayana shida

Sababu ni mipaka salama haizalishi wakimbizi wakorofi au watu wakorofi wenye silaha ni mipaka peaceful lakini sio hao wenye majina ya Nkunda watoka huko wataka kujipenyeza ikulu au kuwa karibu na Raisi jirani sana iwezekanavyo

Hapana.Bila shaka yeyote unaijua vizuri mipaka mikorofi kwa usalama wa Tanzania inayozalisha wakimbizi wakorofi na wasio raia Huko kwingine peace Usilinganishe ni vitu viwili tofauti kabisa kama mbingu na nchi
 
Kwahiyo huko kwingine wakitoa Rais asiye raia ni sawa tu ila siyo Kigoma!? Una chuki mno na bikashaka una maisha magumu Mangi, tafuta pesa...kuwachukia waliokuzidi maisha hakukufanyi ufanikiwe.
 
Kwahiyo huko kwingine wakitoa Rais asiye raia ni sawa tu ila siyo Kigoma!? Una chuki mno na bikashaka una maisha magumu Mangi, tafuta pesa...kuwachukia waliokuzidi maisha hakukufanyi ufanikiwe.
Huko kwingine wanajitambua sana na hutii sheria bila shuruti
Watu waungwana sana sio wababe baby na dharau kama kwingine.Sio rahisi mgeni akapenya kufikia uraisi kutoka huko kwingine

Kigoma mtu aweza shika ila Vetting yake sio ya kitoto imekakamaa hasa

Mbona Phillip Mpango ni makamu wa Raisi na anatokea Kigoma

Raisi kutoka kigoma Yawazekana ila Vetting yake kali kuliko kwingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…