Kafulila: Kwa Utafiti uliopo ndani ya miaka 25 ijayo Tanzania italazimika kujenga uchumi sawa au zaidi ya Afrika ya Kusini ya leo

Kafulila: Kwa Utafiti uliopo ndani ya miaka 25 ijayo Tanzania italazimika kujenga uchumi sawa au zaidi ya Afrika ya Kusini ya leo

===
Akihojiwa na kituo Cha runinga Cha Clouds Media Group Mkurugenzi Mtendaji wa PPP -Centre Bw David Zacharia Kafulila alikuwa na haya ya kusema "Tafiti zilionesha mwaka 2015 mahitaji ya miundombinu yaliyokuwepo yalijitosheleza kwa asilimia 30% tu ya mahitaji ya mwaka 2050.

Ukitazama mwenendo wa uchumi unaona kwamba Tanzania itahitaji kujenga uchumi mkubwa zaidi ya Afrika kusini ya leo ndani ya miaka 25 ijayo jambo ambalo ukitumia Kodi na Mikopo pekee hutaweza na hii ndio sababu muhimu wa kutumia PPP kufikia matarajio na matamanio haya makubwa mwaka 2050.

Tunachakata kupata mwekezaji kujenga barabara ya kisasa ya kulipia Kibaha - Chalinze mpaka Morogoro, wawekezaji wanajua pamoja na uwepo wa SGR ya kisasa bado mahitaji ya usafiri yataendelea kuwa makubwa kutokana na ukubwa wa uchumi unaojengwa na Tanzània chini ya Chama Cha Mapinduzi CCM-alisema Kafulila.



=====

View attachment 3074274
Utafiti hupingwa kwa utafiti🙏
 
Wewe ni
===
Akihojiwa na kituo cha runinga cha Clouds Media Group Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia nchini Tanzania PPP -Centre David Zacharia Kafulila alikuwa na haya ya kusema ;-

"Tafiti zilizofanyika zilionesha kwamba mwaka 2015 mahitaji ya miundombinu yaliyokuwepo yalijitosheleza kwa asilimia 30% tu ya mahitaji ya miundombinu itakayohitajika mwaka 2050 yaani miaka 35 baadae,

Ukitazama mwenendo wa uchumi wa Tanzània wa sasa utagundua kwamba Tanzania itahitaji kujenga uchumi mkubwa zaidi ya ule wa Afrika kusini ya leo ndani ya miaka 25 ijayo.

Kujenga Uchumi zaidi ya Africa ya Kusini ya leo ni jambo ambalo kama tukitumia Kodi na Mikopo pekee hatutaweza kulifikia na hii ndio sababu muhimu ya kutumia PPP ili kufikia matarajio na matamanio haya makubwa ya Watanzania ifikapo mwaka 2050.

David Kafulila anaendelea kwa kusema, " Tunachakata kupata mwekezaji serious wa kujenga barabara ya kisasa ya kulipia kutoka Kibaha- Chalinze mpaka Morogoro.

Jambo la uhakika ni kuwa wawekezaji wanajua pamoja na uwepo wa Reli na treni mpya za SGR bado mahitaji ya usafiri na usafirishaji yataendelea kuwa ni makubwa kila wakati kutokana na ukubwa wa uchumi wa Tanzània unaojengwa chini ya Rais Samia na Chama chake Cha Mapinduzi CCM.



=====

View attachment 3074274
Mungu ibariki Tanzània yetu
 
Back
Top Bottom