Kafulila na Adan- Namtilia shaka Kafulila kulungulwa

Kafulila na Adan- Namtilia shaka Kafulila kulungulwa

Hili halifai kupingwa hata kidogo ingefaa kila Mtanzania mzalendo mwenye mapenzi na nchi yake aweze kusikia harufu mbaya, harufu mbaya ya rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.

Inafaa kila mtu mwenye akili timamu ahoji ujumbe wa Kafulila kwenda India je kuliambatana na maafisa wa usalama taifa pamoja na takukuru kufuatilia kwa karibu majadiliano na makubaliano ya Kafulila na kama kulikua na kuzingatia maslahi mapana ya taifa na kutokuwepo kwa rushwa.
Kwa bahati mbaya taasisi nilizozitaja hapo juu ya pili ndio kinara wa Rushwa na ya kwanza ina kazi maalumu ya kulinda wezi na kuilinda ccm na viongozi wake huku vijana wao wakikaa baa na kutishia watu bastola.

Ni wasi wasi wangu kwamba gharama kubwa anayoitumia kafulila kudalalia PPP ni dhahiri kwamba anatumikia rushwa aliyopewa na hao mabepari uchwara na wanaolenga kuvuna rasilimali zetu kwa kipindi kifupi ambacho wanaamini namba one sio mwelewa wa kutosha juu ya mambo magumu na makubwa ya nchi hasa maeneo ya miradi mikubwa ya maendeleo.

Wenzetu huko duniani wametumia idara husika kupata taarifa sahihi na kuamua kumtia nguvuni bwana Adani hasa kwamba wenzetu wana taarifa za uhakika, hawkamati kwanza ndio uchunguzi uanze la hasha. Jirani zetu kenya baada ya kupata taarifa hizi maramoja wamefuta mikataba na huyu jamaa. Changamoto ni kwamba sisi kwa sababu ya rushwa na ujinga, tulibadilisha sheria zetu kwa ajili ya wawekezaji badala ya waekezaji kufuata sheria zetu ili kumjengea mwarabu wa DP njia ya kutumia rasilimali zetu, kwa sheria zinazotufunga sisi hutasikia tumbili akitamka neno wala kitika akibwabwaja neno. Tutakaa kimya na kumpigia debe chini chini ale hiyo tenda ya umeme na huku akitafuna Bandarini.

Shida inakuja kwamba hisa za Adani zimeshuka ghafla na speculators wameanza kutoa fedha zao kwenye soko la hisi mpaka jana imeshuka kwa 20 percent. Kinachoendelea ni kwamba ufanisi utakua zero, tukimfukuza atatushtaki tumlipe na baadae tuje tuwsingizie chadema. Taasisi za ndani zikifanya kazi kwa maslahi ya nchi na si maslahi ya ccm na kafulila tutafika mbali Lucas Mwashambwa aisome kwenye faili lake mana anampiga debe kuliko angefanya Jesca Kishoa na ndugu Pascal Mayalla utusaidie ni namna gani hizo taasisi nilizotaja zinaweza kutusaidia. https://www.reuters.com/world/india...dicts-group-chairman-bribery-case-2024-11-21/
Asante sana Mkuu Dolphin T. Hakika tusipopiga kelele hata kwa njia hii hapa JF huyu atatumaliza. Kama ulivyosema TAKUKURU na TISS wako kwenye majukumu ya kujinufaisha wao binafsi. Hawa wa Vibastola wanaeleweka na lugha yao ya " Unajua Minani?" Hawa TAKUKURU sasa ni TAASISI YA KUDAI NA KUCHUKUA RUSHWA. hawana hata aibu. Kuna mwaka walifanya sherehe nadhani ya kuukaribisha mwaka kule Kigamboni, sasa kuna dada alizinguliwa na Kaka kwenye kazi zao huko nyuma. Inasemekana huyu kaka alizuia dada asiweze kuchukua rushwa kwa tajiri mmoja hela kubwa sana. Sasa dada akawa na bifu na huyu kaka. Siku ya kuukaribisha mwaka mpya ilikuwa ni hitimisho la kupumua yule kaka na ikawa mwanzo wa maisha mapya gerezani kwa yule dada bastola ilifanya yake kwa kaka wa watu. Kwahiyo hawa si watu wa kuaminika tena ilikuwa zamani. Kulinganisha zamani na sasa ukisoma Makala ya Pascal Mayalla jinsi Mkurugenzi wa TISS Mzee Emilio Mzena alivyo staafishwa utaona viongozi wetu walivyokuwa committed kufanya kazi. Leo hii hawa watu wa Taasisi hizi mbili si watu wema tena kwa taifa letu. Nikiikumbuka kesi ya Loliondo na Ngorongoro nalia machozi tu. Naamini ipo siku Tanzania itarudi kwenye ramani yake. Asante Dolphin T.
 
Mkuu DolphinT , kwanza asante kwa mchango wako huu wa kizalendo, pili naunga mkono hoja, ya possibility ya uwepo wa rushwa ya the grand corruption.

Kwenye the corporate world, kuna rushwa za aina nyingi, rushwa kuu ya kwanza inaitwa "the enticement" hii sio rushwa ya fedha ni rushwa ya kindness to entice your prey kwa kumpa an invitation aje akutembelee.

Unamtumia 1st class plane ticket, from the airport una pick na chauffeur driven limousine na kumuweka in a 5 star hotel, siku ya kwanza unanuacha apumzike kuondoa uchovu wa safari.

Kesho yake unamletea bahasha nene ya cash money kufanyia shopping.

Siku ya 3 unamtembeza kwenye vitega uchumi vyako, na kila akimaliza kutembelea mahali, yeye na ujumbe wake wote wanapewa vi parcel vya zawadi
, expensive gifts, watches, jewelry pens za mont blanc Etc.

Kisha unakuwa advised ufungue a safe foreign account kule Switzerland, tutakuwekea asante yako kule. Hapo watu wa kazi wanakuwa wamemaliza kazi.

Nyerere amekufa masikini kwasababu alikataa vitu kama hivi!.

Laiti Watanzania wangemjua mdhamini na the cost ya kuitengeneza ile senema yetu ya royo tua na steling amelipwa kiasi gani, na nani, na kuangalia mwisho wa siku huyo mdhamini anakuja kupata nini ndio mtaelewa.

Hata DP World, walianzia mbali
, wamejenga ICD Kigali ya ukubwa 3x Dar port, with no sea access, hivyo piga ua galagaza lazima Dar port ipatikane!.

Watu wa kazi wakaingia kazini
, ujumbe wa Tanzania ukadhaminiwa with fully sponsored sponsorship kuhudhuria maonyesho ya Expo Dubai , kule ikaandaliwa Tanzania Day, Watu wakafanya mambo, mara paap... DP World, ndani ya Nyumba!.
P
Pascal Mayalla Mungu akulinde.
 
Kwanza hakuna mtu anaweza kukataa hela ya hongo Ili apate tenda ,na Kwa taarifa Yako tuu wakandarasi wote kuanzia Wachina Hadi wa Kawaida wanatoa hongo ndio wapate kazi so Wala hakuna Cha ajabu Kwa Adani au Kafulira ndivyo mambo yanaenda
Usitumie makalio kufikiri.

Unaona sawa kutoa rushwa kupata tenda??

Hivi umepitia tena ulichoandika. Kumbuka maandiko yako huwa yanasupport awamu hii na sidhani kama wahusika watafurahi kuona unaandika kama kutoa rushwa ni jambo la kawaida??
 
Aliporejea kutoka India alisema mengi, lakini hili la Adan akitaka apewe TANESCO kama mwekezaji nasikia harufu kwasababu wenzetu wamesikia harufu toka kwa Adan.

Namtaka Kafulila aje atwambie hii harufu ya Adan kule India hakuisikia kama siyo kupakazwa na yeye?

Ile TICS kachukua Adan. Kafulila kala matapishi yake kupitia sahani ya Adan?
Adani huwa hafanyi dili kubwa bila kuwalainisha watu kwa rushwa.

Ndiyo maana Wamarekani wamemkataa.

Kafulila kashachukua cha juu. Kama angekuwa hajachukua cha juu asingempigia debe mtu mchafu kama Adani.

Kafulila si mjinga ampigie debe mtu mchafu burebure.
 
Usitumie makalio kufikiri.

Unaona sawa kutoa rushwa kupata tenda??

Hivi umepitia tena ulichoandika. Kumbuka maandiko yako huwa yanasupport awamu hii na sidhani kama wahusika watafurahi kuona unaandika kama kutoa rushwa ni jambo la kawaida??
Ni sawa kabisa kama hutaki kutoa unda kampuni Yako uone kama hujaifunga 😆😆

Wewe Kwa akili Yako mbovu unajua kwamba watu Huwa wanapata Kwa Haki bin vuu,tukifuata Haki kazi zitakwama maana sheria inamtaka lowest bidder 😆😆
 
Adani ameshapewa Bandari.

Asipewe na Tanesco tena.

Please.
Ndio unaona Leo! Siku zote unapowasifia Hawa madalali wa nchi , badala ya kupigania mifumo imara inayolazimisha uwajibikaji, unakuja kusema asipewe, after sometime utakapokuja kujua DP world wanasaga mifupa utajua hujui
 
Ni sawa kabisa kama hutaki kutoa unda kampuni Yako uone kama hujaifunga 😆😆

Wewe Kwa akili Yako mbovu unajua kwamba watu Huwa wanapata Kwa Haki bin vuu,tukifuata Haki kazi zitakwama maana sheria inamtaka lowest bidder 😆😆
Wewe ni Mjinga na ni hasara kwa Familia Yako naTaifa
 
Aliporejea kutoka India alisema mengi, lakini hili la Adan akitaka apewe TANESCO kama mwekezaji nasikia harufu kwasababu wenzetu wamesikia harufu toka kwa Adan.

Namtaka Kafulila aje atwambie hii harufu ya Adan kule India hakuisikia kama siyo kupakazwa na yeye?

Ile TICS kachukua Adan. Kafulila kala matapishi yake kupitia sahani ya Adan?
Penye udhia tia shekeli
Wenye macho watakuwa vipofu
Wenye masikio watakuwa viziwi
 
Wewe ni maskini unazuza genge,duka nk huna kampuni ndio maana hujui nachoongea
In many poor countries Tanzania included, individuals who oppose corruption often face personal attacks rather than their arguments being addressed. This is an example of the ad hominem fallacy, where critics target the individual’s assumed characteristics, such as their poverty, to undermine their credibility. Instead of discussing the argument, attackers use irrelevant personal traits to discredit the person, which is logically flawed.

For instance, when someone advocates for fairness in awarding public tenders, they might be dismissed with statements like, “Why should we listen to you? You’re just a poor person.” This shift in focus from the issue of corruption to the person’s financial status distracts from the validity of their argument. Such reasoning is harmful, as a person’s financial condition has no bearing on the truth of their stance.

The broader implications of this tactic are significant. First, it silences opposition by discouraging individuals from speaking out, especially when they lack economic power. Second, it perpetuates inequality by implying that only the wealthy or powerful have the right to influence public discourse. Lastly, it misdirects attention, allowing corruption in public tenders to persist unchallenged. pascal Mayala
 
Back
Top Bottom