Kafulila: Serikali kubinafsisha Vivuko vya TEMESA nchini kwa Ubia

Kafulila: Serikali kubinafsisha Vivuko vya TEMESA nchini kwa Ubia

PPP imesoma ramani na kuona kuwa vingi vita paki eg. Mwanza & Ilagala Kigoma maana madaraja yanakamilika soon
 
Naona Kafulila sasa ameamua
---
Baada ya kusuasua kiuendeshaji, hatimaye Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (Temesa), imetangaza kubadili mfumo wa utekelezaji wa majukumu yake, kwa kushirikiana na sekta ya umma na binafsi kupitia ubia (PPP).

Kutokana na mabadiliko hayo, Temesa imewaita wawekezaji wa sekta binafsi kutoka ndani na nje ya nchi kuwasilisha mapendekezo ya ushirikiano huo katika huduma za vivuko, karakana za ufundi magari na ufundi umeme.

Kwa mujibu wa taarifa za Temesa, wakala unakuja na mpango huo ikiwa ni miezi mitatu tangu Mwananchi iliripoti mfululizo wa ripoti maalumu zinazoonyesha wakala huo kulemewa na majukumu, kuathiriwa na mifumo na hata kujikuta ikiangukia katika madeni.

Ripoti hiyo iliyotokana na uchunguzi uliofanywa kwa takriban miezi mitatu, ilionesha Temesa kukiuka mpango wa matengenezo ya vivuko na kudaiwa zaidi ya Sh30 bilioni na wasambazaji wa vipuli kwenye karakana zake za ufundi magari.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya ndani ya Temesa, wakala huo umewaalika wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya kuwekeza kwenye uendeshaji wa vivuko kupitia mpango wa PPP.

Kamishna wa PPP, David Kafulila akizungumza na Mwananchi leo Jumatano, Septemba 18, 2024 amesema ushirikiano huo unalenga kufanywa katika uendeshaji wa karakana 13 kati ya 30 za wakala huo, sambamba na majukumu mengine kama vivuko na ufundi.

Mwananchi
Kazi ni nzuri sanaa
 
Huyu dogo ni mjinga sana, kwa nini hao sekta binafsi wasilete vivuko vyao? Kwa nini wanataka waendeshe vivuko vya serikali? Hivi mtu kivuko sio chake, atakiwa na uzalendo wa kukitunza?

Hiyo Idara ya PPP ya Kafulila ni redundant, ni doublication ya kazi za kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC). Taasisi ya Kafulila ilifaa kuwa idara tu pale TIC. Naashangaa msajili wa hazina na Kitila Mkumbo wanataka kuondoa taasisi zisizo na umuhimu, halafu hii ikaundwa mbele ya macho yao.....
 
Huyu dogo ni mjinga sana, kwa nini hao sekta binafsi wasilete vivuko vyao? Kwa nini wanataka waendeshe vivuko vya serikali? Hivi mtu kivuko sio chake, atakiwa na uzalendo wa kukitunza?

Hiyo Idara ya PPP ya Kafulila ni redundant, ni doublication ya kazi za kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC). Taasisi ya Kafulila ilifaa kuwa idara tu pale TIC. Naashangaa msajili wa hazina na Kitila Mkumbo wanataka kuondoa taasisi zisizo na umuhimu, halafu hii ikaundwa mbele ya macho yao.....
Tatizo lako ni wivu tu,

Sikia Karibu nchi zote kubwa Afrika , ulaya na Asia kuna PPP CENTRE ili kuratibu mikataba na agenda ya PPP ingawa kuna vituo vya uwekezaji kama TIC.

Kituo cha uwekezaji kinahusika na investment promotion zaidi , kuhamasisha uwekezaji,

Wakati kituo cha ubia PPP kinasaidia mamlaka za serikali kuandaa miradi ya PPP na zaidi kufanyia uchambuzi miradi husika kuhakikisha pamoja na mchakato mzima wa mikataba kabla ya kuingiwa baina ya mamlaka za serikali na kampuni binafsi ili
kuhakikisha maslahi ya pande mbili.

Bodi yake ni makatibu wakuu na viongozi wa Taasisi kama TRA , TIC na Naibu Mwanasheria mkuu wakiongozwa na Katibu Mkuu wizara ya Fedha kama Mwenyekiti.

Kituo cha PPP hakiko chini ya TR wala wizara ya Mipango bali wizara ya Fedha.

Ni muhimu watu hasa nyie humu jf kujenga utamaduni kufuta ujinga kwa kujisomea kwan tafsiri ya ujinga dunia sasa sio kutokumudu KKK bali kutojisomea siku zote za maisha yako😂
 
Tatizo lako ni wivu tu,

Sikia Karibu nchi zote kubwa Afrika , ulaya na Asia kuna PPP CENTRE ili kuratibu mikataba na agenda ya PPP ingawa kuna vituo vya uwekezaji kama TIC.

Kituo cha uwekezaji kinahusika na investment promotion zaidi , kuhamasisha uwekezaji,

Wakati kituo cha ubia PPP kinasaidia mamlaka za serikali kuandaa miradi ya PPP na zaidi kufanyia uchambuzi miradi husika kuhakikisha pamoja na mchakato mzima wa mikataba kabla ya kuingiwa baina ya mamlaka za serikali na kampuni binafsi ili
kuhakikisha maslahi ya pande mbili.

Bodi yake ni makatibu wakuu na viongozi wa Taasisi kama TRA , TIC na Naibu Mwanasheria mkuu wakiongozwa na Katibu Mkuu wizara ya Fedha kama Mwenyekiti.

Kituo cha PPP hakiko chini ya TR wala wizara ya Mipango bali wizara ya Fedha.

Ni muhimu watu hasa nyie humu jf kujenga utamaduni kufuta ujinga kwa kujisomea kwan tafsiri ya ujinga dunia sasa sio kutokumudu KKK bali kutojisomea siku zote za maisha yako😂
Bado hujasema
 
Back
Top Bottom