Mwananchi Huru
JF-Expert Member
- Nov 20, 2021
- 2,128
- 1,896
Hili ni jambo baya sana kama ni kweli mtu wa aina hiyo yupo.Mwambieni Kijana.
Hao wengine wanaokopa wanajua nini wanachofanya sio kukopakopa tu na kuletea watu hela za kuhonga malaya na kustawisha maisha yao.
Uongo wa kutokutumia akili ni huuMiradi kama kuchimba matundu ya vyoo😂, chawa mna shida sana
Sasa kujenga Shule au Hospitali sio kustimulate uchumi au haufahamu maana ya kustimulate uchumi?Mwambieni Kijana.
Hakuna anayekopa huko na kujenga hospitali, uwanja wa mpira, barabara, mashule nk.
Watu wanakopa kustimulate uchumi na kuipeleka hela kwenye uwekezaji wa viwanda, technolojia, makampuni ya mafuta na uchimbaji wa madini na kufadhili oversee projects za uwekezaji na kuboost productions kwenye iconic companies zao kama Boeing, Airbus, Chevron, GMC, DP world, Maerky nk.
Watu hawakopi kuentartain makada na chawa watembee na vibunda, kulipa wanasiasa kupata influence ya kukaa madarakani au kufurahisha wapiga kura ili wakupigie kura.
Sasa kujenga Shule au Hospitali sio kustimulate uchumi au haufahamu maana ya kustimulate uchumi?
Tofautisha mkopo wa Binafsi na Mkopo wa Serikali,Hospitali na Shule ni basics ambazo zinaweza kufanywa kwa haraka kupitia investment nyingine zenye return kubwa na ya haraka kupitia uwekezaji kwenye hizi rasirimali zetu.
Ukiisimamia vizuri sekta ya madini, utalii nk, ukacontrol matumizi ya Serikali na kudhibiti wizi , shule na mahospitali unaweza kuyajenga kwa makusanyo hayahaya tu.
Mikopo inahitaji uwekeze kwenye strong investment ambazo zitakupa return haraka na faida kubwa pia mfano uwekezaji kwenye uchimbaji wa gas, chuma, dhahabu, mafuta, makaa ya mawe, bandari, uvuvi, utalii nk
Tofautisha mkopo wa Binafsi na Mkopo wa Serikali,
Serikali haifanyi Biashara ila huduma.
Mkuu naona unazunguka hapohapo,Serikali sio lazima ikafanye biashara, zipo Iconic projects za nchi ambazo zinakuwa mali ya state lakini operated na private entity.
Serikali inainvest kupitia giants company zake kwa kuweka hisa na mtaji ikiwa pamoja na kuyawezesha makampuni yaliyopo kwenye key projects kama uchimbaji wa chuma, gas, mafuta nk
Nimekupa mfano wa makampuni makubwa ambayo ni icon kwa mataifa kama USA, Russia, UK, Japan, China nk... Unafikiri makampuni kama Chevron, Gazprom, China Hydro, Hyundai Heavy equipment, Airbus, Boeing, Barrick Gold, Anglo Gold nk, unafikiri hizo stable companies ni hela kutoka mifumo ya watu tu, Hapana zipo hela za serikali kama mitaji na faida lazima irudi kwenye mzunguko sio mifukoni Kwa watu lakini pia operation zake ndio zinastimulate uchumi kwa kuleta supply ya mafuta, gas, chuma, usafiri nk hapa wengine hupiga hela pia na mwisho wa siku mzunguko wa hela unakuwa mkubwa sana na Serikali inakusanya kodi nyingi sana.
Anafaa maana tantalila Anaziweza huyuAtafaa sana akipewa ukurugenzi wa Mawasiliano ya Rais ikulu.kwa sababu anafahamu vyema Dunia inakwendaje na ni mtu anayesoma na kujisomea sana na hivyo kuwa na uelewa wa masuala mbalimbali.jambo ambalo ni la muhimu sana kwa mtu anayekuwa kwenye nafasi ya ukurugenzi wa Mawasiliano ya Rais ikulu.
Mheshimiwa Kafulila ni jembe kwelikweliAnafaa maana tantalila Anaziweza huyu
Ova
Hawezi kuelewa mambo haya.Sasa kujenga Shule au Hospitali sio kustimulate uchumi au haufahamu maana ya kustimulate uchumi?
Muache na umbumbumbu wake maana hata ukimuekeza vipi hataelewa kitu chochote kile.Mkuu naona unazunguka hapohapo,
Kila kazi inayotumia pesa inastimulate uchumi,
Nadhani hujaijua vizuri maana ya "ECONOMIC STIMULUS "
Mi hua najiuliza hao wanaotukopesha leo wao walikopeshwa na nani mpaka kufika walipoHakuna namna yoyote ya kutengeneza uchumi pasipo kukopa? Yaani lazima tukope ndio mambo yaende sawa?
Hata wao wanakopa,Mi hua najiuliza hao wanaotukopesha leo wao walikopeshwa na nani mpaka kufika walipo
NDIO Mikopo ni muhimu kwa Afya ya Uchumi wa nchiUjinga tu, unawasumbua hakuna lolote! (mikopo ni muhimu sana)
iwe kukopa bila kuiba. Tatizo la Tz ni kuiba kinachoingiaView attachment 3012355
David Kafulila, Mkurugenzi wa PPP TANZANIA katika ukurasa wake wa tweeter ( X ) amechambua haya kwa kifupi
Kafulila anasema, kukopa kwajili ya miradi ya maendeleo ndio njia sahihi na ndio mpango wa dunia nzima kwa sasa.
Kafulila anatufumbua macho kwamba nchi zote kubwa duniani tunazoziona zikimea zinajengwa kwa mikopo kwa wastani wa 97%
David anasema, wakati uchumi wa dunia umefikia US$ 105trilion, Deni lote la dunia ( serikali & private ) ni US$ 315 trilion.
Kwa lugha nyepesi, Sasa deni la serikali zote duniani ikiwemo ya Rais Samia limefikia US$ 97trilion sawa na 97% ya uchumi wa dunia,
Kafulila anazidi kufafanua kuwa deni lote la dunia kwa ujumla ni US$ 315 Trilioni ambalo ni zaidi ya 300% ya GDP ya dunia.
Vietnam ni nchi ya mfano duniani kwa muujiza wa kukuza uchumi ndani ya muda mfupi,
Mwaka 1990, uchumi wa Vietnam ulikuwa US$ 6.4bilion, mbele kidogo ya Tanzania iliyokuwa na US$ 4.5bilioni na nyuma ya Kenya iliyokuwa na US$ 8.4bilioni,
Lakini Leo miaka 30 baadae, uchumi wa Vietnam ni US$ 400bilion, karibu mara nne ya Kenya na mara tano ya Tanzania.
Hata hivyo, Mwaka 2007, wakati uchumi wa Vietnam ukiwa US$77bilion, sawa na Tanzania leo,
Mwaka huohuo wa 2007 uwiano wa deni kwa uchumi Vietinum ulikuwa asilimia 43% karibu sawa na uwiano wa deni kwa uchumi wetu Tanzania Leo.
Kukopa kujenga uchumi ndio njia na ndio Afya yenyewe ya nchi anasema David Kafulila.
View attachment 3011554
Tushughulike na hilo kwa sasai
iwe kukopa bila kuiba. Tatizo la Tz ni kuiba kinachoingia
Hakuna namna yoyote ya kutengeneza uchumi pasipo kukopa? Yaani lazima tukope ndio mambo yaende sawa?