Kafulila: UNDP imetoa orodha ya nchi 54 duniani zilizoelemewa na deni la Taifa. 25 zinatoka Afrika Tanzania haipo, tukope zaidi tujenge Uchumi zaidi

Kafulila atakuwa amefulia kweli kweli [emoji23]
Kukopa sio sifa na hasa kama mikopo hiyo inanufaisha ukoo wa panya, mchwa na mafisadi!.

Kwamba hatukuorodheshwa hivyo tukope tu eti deni letu ni stahimilivu? [emoji848]
Mwambie kweli huyo chawa!
 
Kafulila hii ni hazina KWELIKWEL
 
Fuatilia mikataba yake ndiyo utajua nchi inauzwa vipi.
Gesi ya mtwara inayotumika ni ile ya wakati wa mkapa inayokuja songas,hakuna gesi nyingine iliyouzwa,ya Lindi inahitaji $30b,michakato inaendelea,huo mkataba unaoujua wewe hebu uweke hapa walau terms zake
 
Gesi ya mtwara inayotumika ni ile ya wakati wa mkapa inayokuja songas,hakuna gesi nyingine iliyouzwa,ya Lindi inahitaji $30b,michakato inaendelea,huo mkataba unaoujua wewe hebu uweke hapa walau terms zake
Usijitoe ufahamu ,bungeni washa discuss sana mkataba wa gesi na ugaigai wake.
 
Sera mbovu za Ujamaa alizoleta Nyerere zinakwamisha uchumi. Hata mikopo iongezeke mara 1000 bado tutabaki nyuma kiuchumi.
 
Huyu atakuwa anaumwa ugonjwa wa akili ama anajitoa ufahamu kwa sababu anazozijua mwenyewe. Kudaiwa ni utumwa sio sifa
Jibu hoja. Great thinkers wa JF waliishia wapi? Yaani siku hizi mada hizi Huwa zinaingiliwa na wafia dini wa naniliu. Tabu sana hii
 
Usijitoe ufahamu ,bungeni washa discuss sana mkataba wa gesi na ugaigai wake.
Sasa si uweke hapa wewe uliyesikiliza bunge na kuelewa kwamba gesi mtwara ishauzwa, tatizo liko wapi!?..au unaimba tu kiitikio Cha gesi imeuzwa kipang'ang'a!?
 
Watu wengine mko wajinga sana,mnaona kukopa ni sifa,kukopa sio sifa,sifa ni kujitegemea dah!Kazi kweli kweli.Jamaa wamewalewesha na ujinga,hamuoni wala hamsikii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…