Kafulila: UNDP imetoa orodha ya nchi 54 duniani zilizoelemewa na deni la Taifa. 25 zinatoka Afrika Tanzania haipo, tukope zaidi tujenge Uchumi zaidi

Kafulila: UNDP imetoa orodha ya nchi 54 duniani zilizoelemewa na deni la Taifa. 25 zinatoka Afrika Tanzania haipo, tukope zaidi tujenge Uchumi zaidi

Unajua uchumi Wewe?!
Uchumi upi,huo uchumi fake tuliofundishwa vyuoni,tena kwa kutumia waalimu fake waliofundishwa na hao hao waliobuni mikakati ya kutuibia.Mmefungiwa kwenye ma-box ya ujinga,ili waendelee kuwaibia,poleni sana.Mimi simo kwenye ujinga huo,nimeshachomoka.
 
Sasa nyie BAVICHA simsubiri hayo mabaya mnayoiombea Tanzania yatokee

Hakuna anayeombea mabaya yatokee Tanzania Bali ni uongozi mbaya wa CCM . Deni limefika Trilioni 91 kwa uchache. Nani atatusaidia kulipa Hilo Deni?
 
Kafulila hii ni hazina KWELIKWEL

Hazina gani imetbmbuliwa ukuu wa mkoa?. Yule ni chawa tu. Hazina gani inashauri tukope baadala ya kushauri tupunguze madeni na namna ya kupunguza matumizi Kama V8.
 
Jibu hoja. Great thinkers wa JF waliishia wapi? Yaani siku hizi mada hizi Huwa zinaingiliwa na wafia dini wa naniliu. Tabu sana hii

Mtu kushauri kukopa ndio hoja?. Hakuna hoja ya kujibu maana ni kihoja. Kafulila angeshauri tuache kukopa kwa muda na kupunguza Deni lililopo ningemuona wa maana.

Nchi inadaiwa Trilioni 91 halafu kilaza anashauri tukope zaidi, huyo utamjibu Nini?.
 
Credit rating Tanzania iliyopewa na Moody’s ni sawa na F ya 35% darasani, inaonekana afadhali kwa sababu kuna wengine wana F za 20%, 10%, wengine hawana marks kabisa. Lakini in practice F kuanzia 39% wote ni sawa maana lazima warudie mtihani.

Kwa ivyo ukiona hawa jamaa wanajisifia kilichosemwa na Moody’s unajiuliza kama wazima huko vichwani.

Halafu wanataka kujifananisha na nchi zenye credit rating za AAA kama Japan. Akili zetu zinatutosha wenyewe.
 
Acha porojo za kijinga,unaelewa maana ya kujenga njia za Uchumi au unapayuka tuu?

Mipango madhubuti bila nyenzo utakusaidia Nini?

Acha ujinga wewe nzi wa kijani. Kwa hivyo Tanzania bila kukopa haitapata maendeleo. Jifanyeni wajanja wakati akili zenu haziwezi kuleta maendeleo zaidi ya kupambana na CHADEMA.
 
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe David Zacharia Kafulila kupitia ukurasa wake wa Instagram amewafunda wanaolalamika Kuhusu ukuaji wa deni la Taifa huku akisisitiza tukope zaidi ili tujenge uchumi wetu kwani hata Japan ambayo ni nchi ya tatu Duniani kwa Utajiri bajeti yake 40% ni mikopo tuache maneno maneno Tanzania tuko vizuri,
===
Kafulila anasema, Ripoti ya UNDP Nov2022, imetaja nchi54 zenye hali mbaya ya deni la Taifa Dunian, huku 25 zikitoka Afrika wala Tanzania sio miongoni mwao,

Kafulila anaendelea kwa kusema " Ripoti za Taasisi ya MOODY'S, ambayo ni moja ya taasisi 3 kubwa duniani kwa kupima afya ya uchumi kumudu kulipa deni ( MOODY'S, S&P na Fitch zinamiliki 95% ya biashara hii duniani), Agust 2021 na Oktoba 2022 imeonesha Tanzania bado inafanya vema usimamizi wa deni kutokana kupata mikopo ya muda mrefu na nafuu( concessional loans).

Anaendelea kusisitiza, Tukope kujenga uchumi,Ulaya ilikopa kujenga uchumi baada ya vita ya dunia kwa kusaidiwa na USA( Mashal Plan, ) Bajeti ya Japan ya mwaka 2021, nchi ya 3 kwa ukubwa wa uchumi dunaini, asilimia 40% ni mikopo.

Anasema, "Naam, tukope zaidi kujenga zaidi hasa mikopo ya muda mrefu ambayo uwekezaji miradi hii itaongeza msuli wa uchumi wetu kulipa deni.

Mwaka 2021/22 ndio mwaka deni limeongeka kwa trilioni10(BoT- MER) lakn ndio mwaka uchumi uliongezeka kwa zaidi ya dola bilioni 5.4 kufikia $67.7bn kutoka $62.3bn ambazo ni sawa na nyongeza ya uchumi kwa miaka miwili( 2019/20 na 2020/21),Ndio maana ya kukopa kujenga uchumi.

Marry X-mass & Happy New year
Shida hata hao UNDP sio wa kuaminika. Mfumo wote wa UN usiuamini sana kama wewe ni nchi masikini huku kajamba nani. Mashirika hayo yaliundwa kusaidia mfumo wa kinyonyaji wa nchi tajiri marekani na zile zilitutia kwenye ukoloni. Walitupa uhuru wa bendera tu huku wakihakikisha bado wanatutawala kiuchumi.
Kwa hivyo kama undp kakuonesha hujakopa sana usikurupuke kukopa ovyo.
IMF imeziingiza nchi nyingi matatani kiuchumi kwa masharti yao ya kukopesha. Nchi kama argentina wako hoi ndio maana hata rais na serikali yao hukuwaona kusherehekea kombe la dunia. Nchi iko hoi kiuchumi.
 
Shida hata hao UNDP sio wa kuaminika. Mfumo wote wa UN usiuamini sana kama wewe ni nchi masikini huku kajamba nani. Mashirika hayo yaliundwa kusaidia mfumo wa kinyonyaji wa nchi tajiri marekani na zile zilitutia kwenye ukoloni. Walitupa uhuru wa bendera tu huku wakihakikisha bado wanatutawala kiuchumi.
Kwa hivyo kama undp kakuonesha hujakopa sana usikurupuke kukopa ovyo.
IMF imeziingiza nchi nyingi matatani kiuchumi kwa masharti yao ya kukopesha. Nchi kama argentina wako hoi ndio maana hata rais na serikali yao hukuwaona kusherehekea kombe la dunia. Nchi iko hoi kiuchumi.
Sasa Unataka tumwamini nani?
 
Mtu kushauri kukopa ndio hoja?. Hakuna hoja ya kujibu maana ni kihoja. Kafulila angeshauri tuache kukopa kwa muda na kupunguza Deni lililopo ningemuona wa maana.

Nchi inadaiwa Trilioni 91 halafu kilaza anashauri tukope zaidi, huyo utamjibu Nini?.
Nchi haidaiwi 91 Bali Til.73
 
Back
Top Bottom