Kagera: Katibu Tawala aagiza uchunguzi wasababu ya Walimu wengi kuomba kustaafu kabla ya kufikisha miaka 60

Kagera: Katibu Tawala aagiza uchunguzi wasababu ya Walimu wengi kuomba kustaafu kabla ya kufikisha miaka 60

wizara husika inayo shughulikia masuala ya ajira wanapaswa watambue kuwa "lifespan" ya watanzania imeshuka, hivyo hakuna sababu ya kumtumikisha mtu hadi kufikia umri wa miaka 60!!
wizara ya kazi inapaswa ipunguze umri wa kustaaafu angalu mpaka miaka 45 hiari 50 lazima.maana tusitegemee tena umri wa miaka 50 ukaleta tija kubwa ktk jamii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali hii ya CCM imekuwa katili Sana kwa watumishi wa umma hakuna mtu Yuko tayari ku risk maslahi yake Kama muda wake wa kustahafu ushafika. Kuendelea kufanya kazi chini ya serikali hii ni kubeti.
 
Kustaafu kwa hiari umri wa miaka 55 ni haki ya msingi ya mtumishi.
Prof asijichoshe kufanya utafiti,awasaidie wastaafu.
 
Kustaafu kwa hiari umri wa miaka 55 ni haki ya msingi ya mtumishi.
Prof asijichoshe kufanya utafiti,awasaidie wastaafu.
Kwanza na korona hii wazee hawataki kubetia maisha yani sababu Ni nyingi.
 
We korona ipo wazee wanaambiwa haipo kwanini wasisepe na mahela Yao fasta.
 
umri wa kustaafu kwa hiari uwe miaka 45 na 50 lazima, ikiwa hivyo vijana wanao maliza elimu ya chuo kikuu watapata ajira lkn kama ndio tunawaachia wazee walio foji umri mpaka afikishe miaka 60, atakuwa ameifia kazini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati nikiwa mwanafunzi shule ya Msingi, Mwalimu mkuu alikuwa ni kati ya maafisa wakubwa sana wa Tarafa; yaani baada ya Division Executive Officer walikuwa wanafuatia ma-head teachers wa shule mbalimbali katika tarafa ile. Leo mwalimu mkuu nia kikaragosi tu.
 
😢😭☹😲😒😯🤐😮😌😔😖🙁😓😣😫😫😯😛
 
Copy n pest
CC katibu tawala

Mwalimu Atupele Ephraim
Hivi ndivyo mafao ya Kiinua Mgongo na Pensheni ya kila Mwezi yatakavyokuwa Katika Sheria Mpya ya PSSSF

ippmedia.com

Nov 13, 2018 4:00 AM

SHERIA mpya ya sekta ya hifadhi ya jamii imeweka utaratibu wa kulipa mafao kwa mkupuo kwa asilimia 35 na asilimia 75 inayobaki italipwa kama mshahara kwa mstaafu kwa miaka 12.5.

Kwa mujibu wa sheria hiyo, umri wa kustaafu ni miaka 55 kwa hiyari na miaka 60 kwa lazima, lakini kwa kada maalum kama vile madaktari na maprofesa, umri wa kustaafu ni miaka 60 kwa hiari na miaka 65 kwa lazima.

Sheria hiyo imeunganisha mifuko ya PPF, PSPF, LAPF na GEPF kuunda mfuko wa PSSSF unaohudumia watumishi wa umma na mfuko wa NSSF unaohudumia watumishi wa sekta binafsi.

Kanuni za sheria hiyo zinabainisha kuwa pensheni nzima inakokotolewa kwa kuangalia moja ya 580 (1/580) ikizidishwa mara miezi ya uchangiaji na mara mishahara mizuri ya miaka mitatu.

Kwa upande wa malipo ya mkupuo, kanuni hizo zinaeleza kuwa yatakuwa moja ya 580 (1/580) mara jumla ya miezi ya uchangiaji na mishahara ikizidishwa na miaka 12.5 ambayo ndiyo muda ambao mstaafu atalipwa pensheni yake ikizidishwa na asilimia 25 ambayo ndiyo malipo ya mkupuo.

Kwa mujibu wa kanuni hizo, kikokotoo cha pensheni ya mwezi ni moja ya 580 mara jumla ya miezi ya uchangiaji ikizidishwa na mishahara minono ya miaka mitatu mara asilimia 75 ambayo mwanachama atalipwa kama mshahara kwa kipindi cha miaka 12.5 ikizidishwa na moja ya 12 (1/12).

Ofisa Sheria wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Innocent Kyara, katika ufafanuzi wake kwa Nipashe kuhusu kikokotoo hicho, alisema mwanachama aliyeanza kazi na mashahara wa Sh. milioni moja, akiwa na kiwango cha uchangiaji cha asilimia 20 kwa muda wa miezi 420 (miaka 35) atakuwa na jumla ya michango yenye thamani ya Sh. milioni 84.

Kwa mujibu wa kikokotoo cha zamani, malipo ya mkupuo kwa mtu mwenye mshahara wa aina hiyo, yangekuwa Sh. milioni 71.6,* lakini kwa kikokotoo kipya atalipwa Sh. milioni 35.8, huku pensheni ya mwezi kwa zamani ikiwa Sh. 371,800 na ya sasa ni Sh. 557,800, ikiwa ni ongezeko la asilimia 15.

Kyara alisema kwa mwanachama huyo, jumla ya pensheni ya mwezi ni Sh. milioni 69.2 kwa kikokotoo cha zamani, lakini sasa atalipwa Sh. milioni 103.7, huku mafao yote yakiwa ni Sh. milioni 140.8 kwa kikokotoo cha zamani na Sh. milioni 139.6 kwa kikokotoo kipya.

Alisema mafao yameongezwa kwa asilimia 50 ya mfumuko wa bei ambao ni kati ya asilimia moja hadi 10 na kwamba mfumuko ukizidi asilimia 10, uthaminishaji wa mafao utakuwa asilimia tano na ukiwa chini ya asilimia moja kutakuwa hakuna uthaminishaji na kwamba utafanyika kila baada ya miaka mitatu.

Sheria hiyo ilipitishwa Oktoba 20, mwaka jana ikiunganisha mifuko ya pensheni na kuunda mfuko wa PSSF na kufanya marekebisho kwenye Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), ili uwe mahususi kwa ajili ya wafanyakazi wa sekta binafsi na sekta isiyo rasmi.

Sheria hiyo ilianza kazi Agosti Mosi, mwaka huu na kanuni zake zilishatangazwa kwenye gazeti la serikali.
 
Wakati nikiwa mwanafunzi shule ya Msingi, Mwalimu mkuu alikuwa ni kati ya maafisa wakubwa sana wa Tarafa; yaani baada ya Division Executive Officer walikuwa wanafuatia ma-head teachers wa shule mbalimbali katika tarafa ile. Leo mwalimu mkuu nia kikaragosi tu.
Sasa hivi Loan Officer wa Finca na Mkuu wa shule za kata hadhi yao sawa

Zaman Baba yako akijuana tu kwa urafiki wa juu juu na Mkuu wa shule kama Minaki au Pugu zinga la ujiko siku hizi haina kick
 
Yaani mtu anapakwa mafuta matakoni,unahitaji kuchunguza anataka kufanywa nini?
 
Matumizi mabaya ya rasilimali watu HUKO vyuo vikuu kuna uhaba mkubwa wa wamaprof lakn huyu kawa katibu tawala wakat angeandaa vijana vyuon tupate wataalam wakutosha.
Jamaa alinufunimdisha Mzumbe nashangaa mno kukubali juwa katibu tawala aisee
 
Ni sawa; lakini mbona rate ya maombi ya retirement imeongezeka sana kuliko miaka ya nyuma? Lengo ni kujua sababu ya hiyo trend hata kama ni haki yao kisheria lakini ni abnormal.
Nimefundisha kwa miaka 41 kabla ya kustaafu.
Sababu ni dhahiri na zipo nyingi kama unavyoona wanaoacha ualimu kuwa wanasiasa, wafanyabiashara, viongozi wa dini, kuajiriwa na mashirika binafsi nk
 
Matumizi mabaya ya rasilimali watu HUKO vyuo vikuu kuna uhaba mkubwa wa wamaprof lakn huyu kawa katibu tawala wakat angeandaa vijana vyuon tupate wataalam wakutosha.
Na yeye ni profesa wa kuunga unga na majungu. Ndiyo yaliyomfikisha hapo kuwa RAS. Cheo cha majungu. Muosha huoshwa.
 
Nimefundisha kwa miaka 41 kabla ya kustaafu.
Sababu ni dhahiri na zipo nyingi kama unavyoona wanaoacha ualimu kuwa wanasiasa, wafanyabiashara, viongozi wa dini, kuajiriwa na mashirika binafsi nk
... Profesa anataka research ifanyike kwa vitu vilivyo dhahiri. He wants to prove whether the Sun sets in the West or not!
 
Muhimu kuwapongeza kwani wanaachia nafasi kwa vijana kuajiriwa,pia mishahara yao midogo itaokoa hela kumalizia miradi chato
 
Back
Top Bottom