Kagera: Watuhumiwa tisa wa mauaji ya Asimwe Novart wafikishwa mahakamani na kusomewa shtaka la kuua kwa kukusudia

Kagera: Watuhumiwa tisa wa mauaji ya Asimwe Novart wafikishwa mahakamani na kusomewa shtaka la kuua kwa kukusudia

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
Watuhumiwa tisa wa mauaji ya mtoto Asimwe Novart aliyekuwa na ulemavu wa ngozi (ualbino) aliyeripotiwa kuibiwa nyumbani kwao Mei 30, 2024 na mwili wake kupatikana June 17, 2024 ukiwa umeondolewa baadhi ya viungo vyake, leo June 28, 2024 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba na kusomewa shtaka la kuua kwa kukusudia.
IMG-20240628-WA0012.jpg

Mkuu wa mashtaka Mkoa wa Kagera Waziri Mangumbo akisaidiana na wakili wa Serikali, Erick Mabagala wamewasomea mashtaka watuhumiwa hao tisa kuwa wanakabiliwa na shitaka la kuua kwa kukusudia , huku akisema kuwa uchunguzi wa shauri hilo no 17740 la mwaka 2024 tayari umekamilika.

Shitaka hilo limesomwa mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba, Elipokea Yona Wilson ambaye amesema Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo hivyo washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote, ambapo watuhumiwa wote wamerudishwa rumande mpaka July 12,2024 ambapo kesi yao itatajwa tena.

Watuhumiwa hao ni, Elpidius Alfred Rwegoshora miaka 49 ambaye ni padri,Novat Venant miaka 24 ambaye ni baba wa mtoto, Nurdin Ahmada, Ramadhan Selestine,Rwenyagira Alphonce,Dastan Buchard, Faswiu Athuman,Gozibert Arikad na Dezdery Everigist.

Mwili wa mtoto Asimwe Novath ulikutwa ukiwa umetupwa kwenye karavati na kuondolewa baadhi ya viungo vyake vya mwili katika kijiji cha Marere Kata ya Ruhanga wilaya ya Muleba.

Soma:
- Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji


IMG-20240628-WA0015.jpg
IMG-20240628-WA0011.jpg
IMG-20240628-WA0010.jpg
 
Elpidius Alfred Rwegoshora miaka 49 ambaye ni padri..!! Yule padri nae yumo, Kanisa Katoliki lingefaa litoe tamko kali sana kulaani padri kuhusika katika huu uuaji, unyama na ukatili mbaya sana..!!
 
Watuhumiwa tisa wa mauaji ya mtoto Asimwe Novart aliyekuwa na ulemavu wa ngozi (ualbino) aliyeripotiwa kuibiwa nyumbani kwao Mei 30, 2024 na mwili wake kupatikana June 17, 2024 ukiwa umeondolewa baadhi ya viungo vyake, leo June 28, 2024 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba na kusomewa shtaka la kuua kwa kukusudia.
View attachment 3028649
Mkuu wa mashtaka Mkoa wa Kagera Waziri Mangumbo akisaidiana na wakili wa Serikali, Erick Mabagala wamewasomea mashtaka watuhumiwa hao tisa kuwa wanakabiliwa na shitaka la kuua kwa kukusudia , huku akisema kuwa uchunguzi wa shauri hilo no 17740 la mwaka 2024 tayari umekamilika.

Shitaka hilo limesomwa mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba, Elipokea Yona Wilson ambaye amesema Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo hivyo washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote, ambapo watuhumiwa wote wamerudishwa rumande mpaka July 12,2024 ambapo kesi yao itatajwa tena.

Watuhumiwa hao ni, Elpidius Alfred Rwegoshora miaka 49 ambaye ni padri,Novat Venant miaka 24 ambaye ni baba wa mtoto, Nurdin Ahmada, Ramadhan Selestine,Rwenyagira Alphonce,Dastan Buchard, Faswiu Athuman,Gozibert Arikad na Dezdery Everigist.

Mwili wa mtoto Asimwe Novath ulikutwa ukiwa umetupwa kwenye karavati na kuondolewa baadhi ya viungo vyake vya mwili katika kijiji cha Marere Kata ya Ruhanga wilaya ya Muleba.

Soma:
- Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji


View attachment 3028650View attachment 3028651View attachment 3028652
Sijamuona Padre hapo, kanisa katoriki msilete ujuaji na kumficha Yule Padre mtuhumiwa! Maana kwa michezo hii mpo vzr
 
Watuhumiwa tisa wa mauaji ya mtoto Asimwe Novart aliyekuwa na ulemavu wa ngozi (ualbino) aliyeripotiwa kuibiwa nyumbani kwao Mei 30, 2024 na mwili wake kupatikana June 17, 2024 ukiwa umeondolewa baadhi ya viungo vyake, leo June 28, 2024 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba na kusomewa shtaka la kuua kwa kukusudia.
View attachment 3028649
Mkuu wa mashtaka Mkoa wa Kagera Waziri Mangumbo akisaidiana na wakili wa Serikali, Erick Mabagala wamewasomea mashtaka watuhumiwa hao tisa kuwa wanakabiliwa na shitaka la kuua kwa kukusudia , huku akisema kuwa uchunguzi wa shauri hilo no 17740 la mwaka 2024 tayari umekamilika.

Shitaka hilo limesomwa mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba, Elipokea Yona Wilson ambaye amesema Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo hivyo washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote, ambapo watuhumiwa wote wamerudishwa rumande mpaka July 12,2024 ambapo kesi yao itatajwa tena.

Watuhumiwa hao ni, Elpidius Alfred Rwegoshora miaka 49 ambaye ni padri,Novat Venant miaka 24 ambaye ni baba wa mtoto, Nurdin Ahmada, Ramadhan Selestine,Rwenyagira Alphonce,Dastan Buchard, Faswiu Athuman,Gozibert Arikad na Dezdery Everigist.

Mwili wa mtoto Asimwe Novath ulikutwa ukiwa umetupwa kwenye karavati na kuondolewa baadhi ya viungo vyake vya mwili katika kijiji cha Marere Kata ya Ruhanga wilaya ya Muleba.

Soma:
- Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji


View attachment 3028650View attachment 3028651View attachment 3028652
Natamani sana kujua ukweli, uhakika na uhalisia juu ya tukio Hilo lote kabisa, sema tatizo ni kwamba Sheria za nchi hii ya Tanzania haziruhusu Independent Police Investigation, na kwa bahati mbaya sana kupita kiasi ni kwamba hata ripoti au taarifa za upelelezi za Jeshi la Polisi nazo haziaminiki kabisa. Hivyo, huenda tunaweza tusiujue ukweli halisi kuhusiana na tukio hili.
 
Mastermind ni padri yeye ndio organizer na kupanga watu wa kazi na kufadhili tukio zima Baba mtoto alikuwa anaweka mazingira yawe rahisi ..

Yale mapesa wanajikusanyia Kila siku hayatoshi na huenda naye alipokea maagizo toka juu
 
Back
Top Bottom