Kagera: Watuhumiwa tisa wa mauaji ya Asimwe Novart wafikishwa mahakamani na kusomewa shtaka la kuua kwa kukusudia

Kagera: Watuhumiwa tisa wa mauaji ya Asimwe Novart wafikishwa mahakamani na kusomewa shtaka la kuua kwa kukusudia

Kwanini hili suala la watuhumiwa kupelekwa mahakamani nakurudishwa bila ya kesi kusikilizwa,linajirudia?
Inamaana bado suala la kujua mahakama ipi ni sahihi au si sahihi,kwa kuwapeleka watuhumiwa wa kesi flani,halijawahi kutatuliwa?
Mambo ya kijingajinga sana haya.
Mambo yanaenda ngazi kwa ngazi.Ulipendelea wahukumiwe siku hiyohiyo?
 
Hapana. Huo ndo Utaratibu uliokubalika.
SIYO KWELI ulichosema.
Kwa kuwa Mwendesha Mashitaka yeye mwenyewe amekiri kwamba Upelelezi tayari umekamilika, na kwa kuwa Mjini Bukoba ipo Mahakama Kuu ambayo ina mamlaka ya kisheria ya ku-deal na Kesi hii, basi hapakuwa na sababu ya msingi ya kupeleka Kesi hiyo kwenye Mahakama hiyo ya chini walikopelekwa. Ilipaswa Kesi hii ipelekwe Mahakama Kuu moja kwa moja kwa ajili ya kuanza kusikiliza shauri husika.
 
Elpidius Alfred Rwegoshora miaka 49 ambaye ni padri..!! Yule padri nae yumo, Kanisa Katoliki lingefaa litoe tamko kali sana kulaani padri kuhusika katika huu uuaji, unyama na ukatili mbaya sana..!!
Kanisa limetoa taarifa kumsimamisha kwa sasa hawawezi kusema lolote maana bado mtuhumiwa ....akija kuachiwa kuwa hana hatia ....? Tusikurupuke kumaliza maneno.....acha haki itendeke...mudavni mwalim mkuu
 
Kwanini hili suala la watuhumiwa kupelekwa mahakamani nakurudishwa bila ya kesi kusikilizwa,linajirudia?
Inamaana bado suala la kujua mahakama ipi ni sahihi au si sahihi,kwa kuwapeleka watuhumiwa wa kesi flani,halijawahi kutatuliwa?
Mambo ya kijingajinga sana haya.
Nanukuu: "Mambo ya kijingajinga sana haya".
Hapana. Huo ni Utaratibu uliowekwa kisheria ili Haki iweze kuonekana kutendeka.
Hiyo mahakama yenye uwezo huo inafahamika lakini huko kwenye Mahakama hiyo nako kuna utaratibu wake wa kupokea na kusikiliza kesi hizo e.g. Muda au siku/Tarehe ambapo kutakuwa na nafasi ya kuisikiliza kesi hiyo ukizingatia na kukumbuka zipo kesi nyingi na zote lazima zisikilizwe.
 
Natamani sana kujua ukweli, uhakika na uhalisia juu ya tukio Hilo lote kabisa, sema tatizo ni kwamba Sheria za nchi hii ya Tanzania haziruhusu Independent Police Investigation, na kwa bahati mbaya sana kupita kiasi ni kwamba hata ripoti au taarifa za upelelezi za Jeshi la Polisi nazo haziaminiki kabisa. Hivyo, huenda tunaweza tusiujue ukweli halisi kuhusiana na tukio hili.
Mkuu nakubaliana na wewe 100% kwa Hawa watu waliopo hapa huenda wakawa ni madalali lakini yupo mtu nyuma ya hili tukio na kama Hawa watu watamaliza miaka 5 gerezani sijui. Hiki kiini macho kinachofanywa hapa na ukisikiliza maneno ya polisi kuna sintofahamu nyingi sana kuanzia upelelezi mpaka stori nzima.
Ni Nani aliyepo nyuma ya hili? Sijui ila muda utaamua
 
Nanukuu: "Mambo ya kijingajinga sana haya".
Hapana. Huo ni Utaratibu uliowekwa kisheria ili Haki iweze kuonekana kutendeka.
Hiyo mahakama yenye uwezo huo inafahamika lakini huko kwenye Mahakama hiyo nako kuna utaratibu wake wa kupokea na kusikiliza kesi hizo e.g. Muda au siku/Tarehe ambapo kutakuwa na nafasi ya kuisikiliza kesi hiyo ukizingatia na kukumbuka zipo kesi nyingi na zote lazima zisikilizwe.
Kwanini wasipelekwe moja kwa moja kwenye mahakama ambayo ina uwezo wa kusikiliza kesi husika,mara baada ya taratibu kukamilika,kuliko kuwapeleka mahakama ambayo haina uwezo,kupoteza muda tu?
Hivi hata huko Ulaya kuna mambo kama haya,ambako tunaiga?
 
SIYO KWELI ulichosema.
Kwa kuwa Mwendesha Mashitaka yeye mwenyewe amekiri kwamba Upelelezi tayari umekamilika, na kwa kuwa Mjini Bukoba ipo Mahakama Kuu ambayo ina mamlaka ya kisheria ya ku-deal na Kesi hii, basi hapakuwa na sababu ya msingi ya kupeleka Kesi hiyo kwenye Mahakama hiyo ya chini walikopelekwa. Ilipaswa Kesi hii ipelekwe Mahakama Kuu moja kwa moja kwa ajili ya kuanza kusikiliza shauri husika.
Bado inaelekea haujui Utaratibu. Hiyo Mahakama kuu inapokeaje kesi bila kuwa na Mleta kesi? (Referal). Halafu hao watuhumiwa watahifadhiwaje magereza bila kibali kupitia mahakama itakayotoa Warrant na au Dhamana? Kumbuka pia kwamba hiyo Mahakama inazo pia kesi nyingi nyingine zinazostahili kusikilizwa i.e. ni lazima ipangwe kwenye foleni
 
Mbona wapo nane (8) mkuu?? Usitetee wahalifu.Acha sheria ichukue mkondo wake.
Je, Una uhakika unacho kinena?

Picha iko wazi kabisa, dawati la nyuma wamekaa watuhumiwa watatu na dawati la mbele wamekaa watuhumiwa sita, jumla watuhumiwa Tisa.
Sasa Hilo Kanisa Katoliki hapo unalolituhumu limemficha mtuhumiwa gani zaidi ya hawa wanaoonekana kwenye picha???

Narudia Tena kusema kwamba Acha Chuki binafsi, uchochezi na uchonganishi dhidi ya Kanisa Katoliki.
Tazama picha hizi hapa chini ili uone kama watuhumiwa hao wapo wangapi.
 

Attachments

  • IMG-20240628-WA0015.jpg
    IMG-20240628-WA0015.jpg
    50 KB · Views: 2
  • IMG-20240628-WA0012.jpg
    IMG-20240628-WA0012.jpg
    45.7 KB · Views: 1
Natamani sana kujua ukweli, uhakika na uhalisia juu ya tukio Hilo lote kabisa, sema tatizo ni kwamba Sheria za nchi hii ya Tanzania haziruhusu Independent Police Investigation, na kwa bahati mbaya sana kupita kiasi ni kwamba hata ripoti au taarifa za upelelezi za Jeshi la Polisi nazo haziaminiki kabisa. Hivyo, huenda tunaweza tusiujue ukweli halisi kuhusiana na tukio hili.
Mkuu unaweza usiwaamini Tanzania police kwasababu flani flani nakubaliana na wewe,lakini sio kwenye case kama hizo.Ukitaka kujua Police Wa Tanzania wanafanya kazi na uwezo upo ni case zenye public interest kama hizo.Na ukitaka kuwadharau uwe na case yako binafsi.
 
Kwanini wasipelekwe moja kwa moja kwenye mahakama ambayo ina uwezo wa kusikiliza kesi husika,mara baada ya taratibu kukamilika,kuliko kuwapeleka mahakama ambayo haina uwezo,kupoteza muda tu?
Hivi hata huko Ulaya kuna mambo kama haya,ambako tunaiga?
Hiyo itakuwa ni sawa na kumpeleka mgonjwa MOI mojakwa moja bila kuwa na barua yoyote ya Referal.
Utaratibu unadai Mahakama yenye uwezo huo hupokea kesi kutoka mahakama iliyo ya chini kama inavyokuwa hospitali kubwa hupokea mgonjwa aliyetoka hospitali ya chini.
Halafu kama ni kuwapeleka moja kwa moja; Mahakama hiyo itakuwa na mlundikano wa watuhumiwa naitakuwa inafanya kazi zinazoweza kufanywa na Mahakama za chini e.g. Kuruhusu kutoa kibali au idhini ili watuhumiwa wahifadhiwe Magereza n.k. wakati taratibu zingine zikiendelea.
 
Je, Una uhakika unacho kinena?

Picha iko wazi kabisa, dawati la nyuma wamekaa watuhumiwa watatu na dawati la mbele wamekaa watuhumiwa sita, jumla watuhumiwa Tisa.
Sasa Hilo Kanisa Katoliki hapo unalolituhumu limemficha mtuhumiwa gani zaidi ya hawa wanaoonekana kwenye picha???

Narudia Tena kusema kwamba Acha Chuki binafsi na uchonganishi dhidi ya Kanisa Katoliki.
Tazama picha hizi hapa chini ili uone kama watuhumiwa hao wapo wangapi.
Kwa picha hii wanaonekana hao Nane

1719642737405.png


Lakini kwa picha uliyoiweka ni KWELI wapo tisa(9). Asante.
 

Attachments

  • 1719642601949.png
    1719642601949.png
    617.4 KB · Views: 2
Kwanini wasipelekwe moja kwa moja kwenye mahakama ambayo ina uwezo wa kusikiliza kesi husika,mara baada ya taratibu kukamilika,kuliko kuwapeleka mahakama ambayo haina uwezo,kupoteza muda tu?
Hivi hata huko Ulaya kuna mambo kama haya,ambako tunaiga?

Labda nikupe maelezo mafupi kuhusu uendeshaji wa mashauri ya jinai hususani kesi za mauaji kwa mujibu wa sheria zetu.

Ipo hivi mtuhumiwa wa kesi ya mauaji mara tu atakapokamatwa kwa kutuhumiwa kutenda kosa la mauaji, kwanza ni kesi ambayo haina dhamana maana yake mtuhumiwa atasota mahabusu hadi kesi isikilizwe.

Mahakama yenye mamlaka kusikiliza kesi ya mauaji ni Mahakama kuu, mtuhumiwa wa kesi ya mauaji akishakatwa anatakiwa kufikishwa mahakama ya hakimu mkazi au mahakama ya wilaya kwa ajili ya kusomewa shtaka lakini hatakiwi kujibu chochote kwa wakati huo.

Lengo la kumpekeleka mahakama ya chini isiyo na mamlaka ni kumpa taarifa nini kitamkabili mtuhumiwa mbele yake, kama upelelezi hadi hatua hii utakuwa umekamilika polisi wataandaa jarada la kesi pamoja na ushahidi na kuupeleka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka nchini.

Mkurugenzi wa mashtaka atapitia ushahidi ulioptikana dhidi ya mtuhumiwa, akisha jiridhisha ushahidi uliopo unatosha kuendesha shauri hilo la mauaji, Mkurugenzi wa mashtaka ataandaa hati ya mashtaka (information) na kuipeleka mahakama kuu kwa msajili wa mahakama kuu.

Mara tu msajili wa mahakama kuu atakapo pokea hati ya mashtaka kutoka kwa mkurugenzi wa mashtaka nchini, sheria inamtaka kurudisha jarada la kesi toka mahakama kuu na kupeleka mahakama ya chini ambako mtuhumiwa alisomewa shitaka kwa mara ya kwanza na alitakiwa asijibu chochote.

Wakati huu kesi inaporudi mahakama ya chini inaenda kufanyiwa mchakato unaitwa (Committal Proceedings) kwa bahati mbaya kiswahili chake sifahamu, ila nitaelezea lengo la committal proceedings na inafanyikaje.

Kwenye committal proceedings sheria inataka mtuhumiwa kusomewa tena shitaka lake, na wakati huu pia hakimu anatakiwa kumwambia mtuhumiwa hatakiwi kujibu chochote kwani kesi yake itasikilizwa mahakama kuu.

Baada ya shikata kusomwa tena na mtuhumiwa kukaa kimya bila kujibu chochote, hatua inayofuata upande wa Jamhuri ambao unashitaki utatakiwa kutoa idadi ya mashahidi wake itakao waita mahakama kuu kwenye usikilizaji wa kesi, pia maelezo mafupi ambayo kuhusu ushahidi utakaotolewa na hao mashahidi wa jamhuri.

Lakini pia jamhuri itatakiwa kutoa idadi ya vielelezo watakavyo wasilisha kwenye usikilizaji wa kesi huko mahakama kuu. Baada ya hapo upande wa jamhuri watakuwa wamemaliza kazi yao, sheria inataka mtuhimiwa na yeye kupewa nafasi ya kusema ataleta mashahidi wangapi pamoja na vielezo vya kutoa kama anavyo.

Hadi kufikia hapo Committal inakuwa imekamilika, hakimu atamtaarifu mtuhumiwa kwamba mchakato wa maandalizi kwa ajili ya kumpeleka mahakama kuu umekamilika hivyo atatoa amri rasmi ya kwamba anapelekwa mahakama kuu kwa ajili ya kesi yake kuanza kusikilizwa rasmi.

Kwanini huu mchakato wa committal huwa unafanyika japo umekuwa ukilalamikiwa kuchelewesha usikilizwaji wa kesi ya msingi, ni kwamba sababu ya kufaya committal ni kumuandaa mtuhumiwa ili ajipange ajue nini kitaenda kujili mahakama kuu na aandae utetezi wake ulioshiba( principle of fair hearing)

Lakini kingine majaji wamekuwa wakisema committal inafanyika huku chini ili kuchambua vitu vya msingi vya kwenda kuwasilisha mahakama kuu sio kila facts hasa zile zisizokuwa na msingi zifike kule juu.

Tafiti mbali mbali zimeshafanyika kupinga utaratibu wa committal proceedings lakini bado huo utaratibu upo kwenye sheria zetu.
 
Watuhumiwa hao ni, Elpidius Alfred Rwegoshora miaka 49 ambaye ni padri,Novat Venant miaka 24 ambaye ni baba wa mtoto, Nurdin Ahmada, Ramadhan Selestine,Rwenyagira Alphonce,Dastan Buchard, Faswiu Athuman,Gozibert Arikad na Dezdery Everigist.
Hahaha nimecheka hahaha nimecheka tena kumbe waislam nao walihusika kwenye mauaji hahahaha nimecheka kwa sauti kwikwikwi kobaaz mlisema padri haha.

adriz gammaparticles
 
Back
Top Bottom