Kagoda: Ni Rostam

Kagoda: Ni Rostam

Haya maelezo huwezi ukaamini yametoka kinywani kwa mtu aliyeenda shule; utawezaje kutofautisha maelezo ya Feleshi na mlevi wa mataputapu? Kama huna maelezo ya msingi bora ukae kimya uendelee kufaidika na madaraka uliyopewa kwa fadhila ama kiurafiki badala ya kutoa majibu yenye kukera kiasi hicho.
 
Mambo mengine!! Hapa huyu DPP hakuwa na cha kusema, akaamua kusema chochote! Maneno kama haya, ni afadhali asingeongea tu kwa sababu inazidisha suspicion ya umma kwa viongozi wakuu.

Watu wanajua Kagoda ni nani kwani yameshaandikwa sana. Sasa unaposema hashitakiki kwa kuwa alitumwa, unazidi kuwachongea tuu. Mi naona afadhali angekaa kimya tu kuliko kuongea hicho alichoongea.

Sijui kama haya yana msaidia yeye au mkuu wake au nani!!! We are still too poor on the art of talking!
Wana JF,
Kwanza naomba radhi kwa kupotea kwa siku kadhaa. Tangu nimeenda Biharamulo sikuwa hewani na sababu za msingi zinajulikana. Umeme Biharamulo unagawanywa kati ya Biharamulo na Chato, na ni muda mchache sana unapatikana, hivyo ilikuwa vigumu sana kuwa kwenye mtandao.
Pili, Kuhusu Kagoda, Feleshi aseme asiseme, KAGODA tutaendelea kuipigia kelele hadi kieleweke. FELESHI ajiandae tu huko tuendake. Nashukuru kuwa sasa amefikia hatua ya kukiri kuwa walioenda "kubeba" au "kuchukua" walitumwa. Hii ni hatua nzuri, tuendelee kupiga kelele. Siyo kuchukua tu, i) Brella ilisajili KAGODA 29 September, 205, lazima wawaambie Watanzania hao waliosajili ni kina nani na wana back ground gani katika Biashara. 2) Ardhi lazima watuambie Plot ya Kipawa ilipo ofisi hiyo ni ya nani? Je aliyeenda kuchukua fedha katika matawi 6 ya CRDB kwa siku mmoja ni huyo huyo aliyesajiliwa au ni nani? Dr. Kimei lazima atuambie huyo aliyechukua fedha hizo ni nani wakati Benki za nje ikiwemo Kenya Commercial Bank iliandikia BOT kuwa Kagoda haijulikani hivyo kuwakatalia kuchukua fedha hizo kupitia Benki yao.
Watanzania wavute subira, wawe wavumilivu lakini Uzi ni ule ule. Utadanganya umma kwa muda na hutaweza kuwadanganya muda wote, ndio usemi unavyoenda. Hivyo tukiendelea kudai, kushikamana katika kudai haki zetu tutafika. Kazi ya kudai si lelemama, lakini hatimaye tutafurahia matunda.
 
Wana JF,
Kwanza naomba radhi kwa kupotea kwa siku kadhaa. Tangu nimeenda Biharamulo sikuwa hewani na sababu za msingi zinajulikana. Umeme Biharamulo unagawanywa kati ya Biharamulo na Chato, na ni muda mchache sana unapatikana, hivyo ilikuwa vigumu sana kuwa kwenye mtandao.
Pili, Kuhusu Kagoda, Feleshi aseme asiseme, KAGODA tutaendelea kuipigia kelele hadi kieleweke. FELESHI ajiandae tu huko tuendake. Nashukuru kuwa sasa amefikia hatua ya kukiri kuwa walioenda "kubeba" au "kuchukua" walitumwa. Hii ni hatua nzuri, tuendelee kupiga kelele. Siyo kuchukua tu, i) Brella ilisajili KAGODA 29 September, 205, lazima wawaambie Watanzania hao waliosajili ni kina nani na wana back ground gani katika Biashara. 2) Ardhi lazima watuambie Plot ya Kipawa ilipo ofisi hiyo ni ya nani? Je aliyeenda kuchukua fedha katika matawi 6 ya CRDB kwa siku mmoja ni huyo huyo aliyesajiliwa au ni nani? Dr. Kimei lazima atuambie huyo aliyechukua fedha hizo ni nani wakati Benki za nje ikiwemo Kenya Commercial Bank iliandikia BOT kuwa Kagoda haijulikani hivyo kuwakatalia kuchukua fedha hizo kupitia Benki yao.
Watanzania wavute subira, wawe wavumilivu lakini Uzi ni ule ule. Utadanganya umma kwa muda na hutaweza kuwadanganya muda wote, ndio usemi unavyoenda. Hivyo tukiendelea kudai, kushikamana katika kudai haki zetu tutafika. Kazi ya kudai si lelemama, lakini hatimaye tutafurahia matunda.


Havache Tata Slaa
Tawile Tata Slaa
Ushomeri Tata Slaa
Umozeri Tata Slaa
Wakondya Rata Slaa
Thanks Mr.Slaa
Bedankt Manner Slaa
Ndaga Tata Slaa
 
Rostamu Aziz hakamatiki hata serikali ilishakili kupitia kwa waziri mkuu aliposema wakishitakiwa watu kama akina RA nchi itatikisika,mwingine amlisema pamoja na kutuibia lakini tuwaache wapumzike ili na yeye anapoendelea kuiba tuje muache apumzike.Naamini kwa ushahidi uliopo ambao hauna hata chembe ya shaka angepewa mtu yeyeto hata asiye na professional kama ya DPP mfano Dr.Slaa angelishawafikisha mahakamani maana kila kitu kipo clear details zote zipo.
Hii ndio Tanzania ya Wadanganyika.......
NASEMA KAZI TUNAYO
Wanasheria mnisaidie; fedha za EPA kupitia kagoda zimeibiwa Benki Kuu (BOT). Kisai cha Tsh. 40bil zimeibiwa kwa staili ya kuforgi nyaraka. DPP anasema walikuwa wanazichukua hizo fedha wanajulikana ila hawezi kuwashtaki eti walitumwa tu. Sasa anatafuta waliowatuma.
(a) amejuaje kwamba hao jamaa walitumwa?
(b) kama walitumwa si watakuwa wamewataja mabossi wao?
(c) fedha nyingi kiasi hicho si unaweza ku-trace kwa kuangalia bank transactions na kuzifuatilia akaunti husika?
(d) kama aliyewatuma ni Rais, au CCM, DPP atachukua hatua gani? atawaachia hao jamaa anaodai walitumwa?
 
Tanzania tumechoshwa na usanii. Wale walio iba fedha za umma mbona hatusikii mwisho wake?
Wale walio pokea fedha za rushwa ya Rada vipi nao mbona wanazidi kutanua na nasikia kuwa safari hii ndiye ametayarishwa kuwa speaker wa Bunge lijalo?
Kama watanzania mlijisikia vibaya katika kipindi hiki, jiandae kujisikia vibaya zaidi ikiwa ccm itarudi madarakani. Hebu jiulize vijisenti akiwa speaker wa TZ, nikipi tutarajie?
WATANZANIA MNAOMBWA KUACHA KUCHEZEA NAFASI YA UCHAGUZI HUU KUFANYA MAKOSA TENA.
 
Halafu bila aibu Kikwete anasema fisadi Rostam kasingiziwa!

Yaani Kikwete anachezea akili zetu haswaaaaaaaaaa. Anatuona kama mabwege vile, halafu bado watu wanampigia kura, mimi siwaelewi kabisa. Na watu wa Igunga nao sijuwi kawalisha nini huyu jangili mpaka wamchague kuwa mbuge wao.
 
Halafu bila aibu Kikwete anasema fisadi Rostam kasingiziwa!

Akawaambia wananzega, "RA ni mtu safi, anawapenda, anawajali, lakini pia kaenea kila nyanja kama timu ya mpira" watu wakapiga makofi. Hivi kwa mwendo huu Kikwete kweli ana nia ya dhati ya kupambana na mafisadi? kweli anatufaa jamani?
 
Kwa wana JF,yeyote aliyena ukaribu na muungwana tafadhali ampelekee ujumbe huu;
Mpendwa Rais wangu Jakaya, nakuomba sana usitumie muda wako mwingi kumsikiliza Salva na wapambe wengine waliokuzunguka kukuhabarisha nini kinaendelea nchini mwako kwani wanakuzuga tuu na kukupotosha. Tafadhali jaribu kutumia saa moja tuu kila siku kutembelea Jamiiforums uhabarishwe yale ambayo hao wapambe hawakuambii kwa faida zao. Ninahakika utafumbuka macho na kuokoka kwa kuchukua hatua maana hujachelewa sana ila una muda mfupi vinginevyo utaondoka na fedheha kinyume na sifa uliyoingilia.

Utabiri huo unatimia kwenye uchaguzi wa 31/10/2010
 
Yaani Kikwete anachezea akili zetu haswaaaaaaaaaa. Anatuona kama mabwege vile, halafu bado watu wanampigia kura, mimi siwaelewi kabisa. Na watu wa Igunga nao sijuwi kawalisha nini huyu jangili mpaka wamchague kuwa mbuge wao.

Mkuu juzijuzi hapa Baregu alisema mtaji wa CCM ni unyonge wa watanzania. Wanaopiga makofi ni beneficiaries wa ufisadi na wanyonge (wajinga, hasa wanaopewa T shirt na kofia na wanawapigia kura mafisadi). Kuna wengine wanatishiwa tu. Kuna wengi tu watawapigia kura wale wote waliotajwa kwenye ufisadi, hata ndio utajua kuwa kweli tunafanywa mabwege na sisi tunakubali kuwa ni mabwege.
 
Akawaambia wananzega, "RA ni mtu safi, anawapenda, anawajali, lakini pia kaenea kila nyanja kama timu ya mpira" watu wakapiga makofi. Hivi kwa mwendo huu Kikwete kweli ana nia ya dhati ya kupambana na mafisadi? kweli anatufaa jamani?

Kwa kutumia darubini yangu hii ishu ya EPA huko mbeleni itamfanya JK kuishi uhamishoni
 
Kaka Hofstede acha kuchemka,BRELA shareholders wa kampuni inayofunguliwa hawatoi picha wala hata copy ya vitambulisho wala passport...ni complete memart tu iliyosigned ,mchezo kwisha.....hata kama watu hawa-exist kitu kinakwenda tu....hakuna ku-visit ku-verify ofisi existance wala nini...full sanaa!
 
18
COMPANY NAME: Meregesi Law Chambers

Shareholders and Directors: Johnson Lukaza and Maregesi

Related Company: Proin Properties/Kernel

Office Location: Plot 73 Kinondoni Road

Residence Address: ?



Hivi Johnson Lukaza ni mwanasheria?

Sheria asomee wapi?

Kabla ya bumu la EPA mshikaji alikuwa mfanyabiashara ndogo ndogo, alishawahi kuwa na internet cafee huko masaki na alikuwa anaagiza magari mawili matatu hivi toka dubai anauza.

Baada ya EPA kumwagia, mshikaji alikuja juu si kawaida, Advertizer yake ya kwanza ni kwenda na mshikaji wake wa karibu kucheki game ya ufunguzi world CUP ujerumani, Kuagiza Vogue kwa Ndege na kununua majumba kibao.
 
Sheria asomee wapi?

Kabla ya bumu la EPA mshikaji alikuwa mfanyabiashara ndogo ndogo, alishawahi kuwa na internet cafee huko masaki na alikuwa anaagiza magari mawili matatu hivi toka dubai anauza.

Baada ya EPA kumwagia, mshikaji alikuja juu si kawaida, Advertizer yake ya kwanza ni kwenda na mshikaji wake wa karibu kucheki game ya ufunguzi world CUP ujerumani, Kuagiza Vogue kwa Ndege na kununua majumba kibao.

Mkuu wengi pengine hata mimi na wewe inawezekana tungeshawishika kabisa kuwa rubber stamp ya RA. From owning an internet cafe to Vogue. Umaskini ni ugonjwa mbaya sana! No wonder waandishi wengi mahiri huyu jamaa anawacontrol kama soksi zake!
 
Halafu mkumbuke huu wizi ni mdogo SANA. Yani ni wizi wa kipindi cha 2005/2006, tukichokonoa zaidi yanaweza kuibuka makubwa zaidi. Huo ni mwaka mmoja tu...

Kuna tetesi na mwaka huu 2010 wamechota teka kutoka serikalini!
 
Yaani wajinga ndio waliowao! sijui lini watanzania tutaendela kuliwa namna hii
 
Back
Top Bottom