Kaka niache tu🙌 nikifa, nikiishi Mungu ndio anaejua😭

Kaka niache tu🙌 nikifa, nikiishi Mungu ndio anaejua😭

Mmakedonia

Member
Joined
Sep 1, 2021
Posts
21
Reaction score
12
Katika maisha yangu ya elimu kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne sikuwahi kushindwa darasani, mimi kwangu kupitwa katika mtihani nilichukulia ni zaidi ya tusi, baba yangu alinisifia akisema kwamba nina akili kama alizokua nazo yeye ijapokua hakua mtu wa kunipa mahitaji muhimu ambayo mtoto anatakiwa kupata kutoka kwa baba yake.

Kila shule ambayo nilisoma niliamini kwamba naweza kuliko wanafunzi wote hivyo ilikua sio rahis kwa mwanafunzi kunishinda, nakumbuka moja kati ya vitu vilivyonipa umaarufu katika shule niliyomaliza kidato cha nne ni kwamba hiyo shule ilikua ya mwisho mwaka fulani kitaifa (sitoutaja) lakini pia kwa miaka minne mfululizo haikuwahi kufaulisha mwanafunzi yeyote lakini mwaka nilio kuwa mimi kidato cha nne Mungu alisaidia tukafaulu wanafunzi wanne huku wenzangu watatu wakipelekwa vyuo vya kati na mimi peke yangu nikachaguliwa kwenda Advance (PCM)

Kutokana na hali ya wazazi kutokujali kwao kuhusu elimu ijapokua ni kweli kwamba katika kipindi hicho walikua wameshaanza kuchoka ( kuishiwa pesa) hivyo sikubahatika kusoma hata pre-form five lakini nilijipa moyo kwamba ninaweza kufanya kitu cha tofauti licha ya ugumu wa masomo husika.

Hali ilikua tofaut baada ya kuingia kidato cha tano na kukutana na watu waliosoma twishen na ambao wapo bora kuliko mimi, kila nikijaribu kusoma nilikua nikipaniki baada ya kuona kuna watu wana uwezo kuliko mimi ila nilijipa imani kuwa nitashinda na nitafaulu japo kua mambo yalikua magumu sana kwa upande wangu.

Nilikuja kuamini kua ni kweli "ng'ombe wa maskini hazai" baada ya kumaliza kidato cha sita na matokeo kutoka nilikua na div 3 ya 15 yaani kila somo nilikua na "E" hivyo nilikua sina "principal pass" za kuniwezesha kwenda chuo, mara gafla kauli zikabadilika mtaani wale walio nisifu wote wakaanza kunikebehi kwamba nilienda kucheza shule (lakini hakuna mtu yoyote aliyenipa msaada kipindi nasoma hadi kuna kipindi nilikua nakosa hata ela ya kununulia sabuni ya kufulia)

Nikiangalia hali ya wazazi wangu ni ngumu na wote wamezeeka kwa sasa ( walitengana ningali bado mdogo sana hivyo malezi yangu muda mrefu nilipata kwa mama zangu wa kambo ambao baba aliwaleta nyumbani) naona kama nipo kwenye msitu wenye giza nene sioni njia ya kutokea kwani hakuna pa kupata msaada.

Mtu mmoja akanishauri niombe nafasi kwenye vyuo vya serikali ili nikipata nikaombe udhamini kwenye makampuni binafsi lakini mimi mtoto wa maskini sina anaenijua huko serikalini hivyo juhudi zangu ziligonga mwamba kwani nimeomba nafasi lakini bado nimekosa baada ya matokeo ya vyuo kutoka. Only God know ... Nimebakiza dua na sala tu walau nisikose ata mkate wa kila siku🙏. (This is my real life not story)

Naomba pia kura yako hapo hapo chini 👇👇👇 kwa kubofya hilo neno "vote" kama hautojal
 
Katika maisha yangu ya elimu kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne sikuwahi kushindwa darasani, mimi kwangu kupitwa katika mtihani nilichukulia ni zaidi ya tusi, baba yangu alinisifia akisema kwamba nina akili kama alizokua nazo yeye ijapokua hakua mtu wa kunipa mahitaji muhimu ambayo mtoto anatakiwa kupata kutoka kwa baba yake.

Kila shule ambayo nilisoma niliamini kwamba naweza kuliko wanafunzi wote hivyo ilikua sio rahis kwa mwanafunzi kunishinda, nakumbuka moja kati ya vitu vilivyonipa umaarufu katika shule niliyomaliza kidato cha nne ni kwamba hiyo shule ilikua ya mwisho mwaka fulani kitaifa (sitoutaja) lakini pia kwa miaka minne mfululizo haikuwahi kufaulisha mwanafunzi yeyote lakini mwaka nilio kuwa mimi kidato cha nne Mungu alisaidia tukafaulu wanafunzi wanne huku wenzangu watatu wakipelekwa vyuo vya kati na mimi peke yangu nikachaguliwa kwenda Advance (PCM)

Kutokana na hali ya wazazi kutokujali kwao kuhusu elimu ijapokua ni kweli kwamba katika kipindi hicho walikua wameshaanza kuchoka ( kuishiwa pesa) hivyo sikubahatika kusoma hata pre-form five lakini nilijipa moyo kwamba ninaweza kufanya kitu cha tofauti licha ya ugumu wa masomo husika.

Hali ilikua tofaut baada ya kuingia kidato cha tano na kukutana na watu waliosoma twishen na ambao wapo bora kuliko mimi, kila nikijaribu kusoma nilikua nikipaniki baada ya kuona kuna watu wana uwezo kuliko mimi ila nilijipa imani kuwa nitashinda na nitafaulu japo kua mambo yalikua magumu sana kwa upande wangu.

Nilikuja kuamini kua ni kweli "ng'ombe wa maskini hazai" baada ya kumaliza kidato cha sita na matokeo kutoka nilikua na div 3 ya 15 yaani kila somo nilikua na "E" hivyo nilikua sina "principal pass" za kuniwezesha kwenda chuo, mara gafla kauli zikabadilika mtaani wale walio nisifu wote wakaanza kunikebehi kwamba nilienda kucheza shule (lakini hakuna mtu yoyote aliyenipa msaada kipindi nasoma hadi kuna kipindi nilikua nakosa hata ela ya kununulia sabuni ya kufulia)

Nikiangalia hali ya wazazi wangu ni ngumu na wote wamezeeka kwa sasa ( walitengana ningali bado mdogo sana hivyo malezi yangu muda mrefu nilipata kwa mama zangu wa kambo ambao baba aliwaleta nyumbani) naona kama nipo kwenye msitu wenye giza nene sioni njia ya kutokea kwani hakuna pa kupata msaada.

Mtu mmoja akanishauri niombe nafasi kwenye vyuo vya serikali ili nikipata nikaombe udhamini kwenye makampuni binafsi lakini mimi mtoto wa maskini sina anaenijua huko serikalini hivyo juhudi zangu ziligonga mwamba kwani nimeomba nafasi lakini bado nimekosa baada ya matokeo ya vyuo kutoka. Only God know ... Nimebakiza dua na sala tu walau nisikose ata mkate wa kila siku[emoji120]. (This is my real life not story)

Naomba pia kura yako hapo hapo chini [emoji116][emoji116][emoji116] kwa kubofya hilo neno "vote" kama hautojal
Ni hatari kwa mtoto wa kiume kukata tamaa usipanic tulia changa karata zako vzuri mambo yatajipa tu
 
Mkuu mimi sikuvunji moyo, ila kwenye haya maisha usije kutegemea kuonewa huruma ndio usaidiwe... wakati ww unalalamika wazazi wako ni wazee na maskini, kuna watu hawana hata hao wazazi na wengine hawajawahi hata kuwasikia lakini wanapambana na maisha na kutoboa.

mimi binafsi siwezi kukupigia kura kwa sababu wewe ni maskini na una shida sana.

Jitume, fanya kwa bidii na kwa ubora na umuombe Mungu.

Do your best and God will do the Rest.
 
Katika maisha yangu ya elimu kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne sikuwahi kushindwa darasani, mimi kwangu kupitwa katika mtihani nilichukulia ni zaidi ya tusi, baba yangu alinisifia akisema kwamba nina akili kama alizokua nazo yeye ijapokua hakua mtu wa kunipa mahitaji muhimu ambayo mtoto anatakiwa kupata kutoka kwa baba yake.

Kila shule ambayo nilisoma niliamini kwamba naweza kuliko wanafunzi wote hivyo ilikua sio rahis kwa mwanafunzi kunishinda, nakumbuka moja kati ya vitu vilivyonipa umaarufu katika shule niliyomaliza kidato cha nne ni kwamba hiyo shule ilikua ya mwisho mwaka fulani kitaifa (sitoutaja) lakini pia kwa miaka minne mfululizo haikuwahi kufaulisha mwanafunzi yeyote lakini mwaka nilio kuwa mimi kidato cha nne Mungu alisaidia tukafaulu wanafunzi wanne huku wenzangu watatu wakipelekwa vyuo vya kati na mimi peke yangu nikachaguliwa kwenda Advance (PCM)

Kutokana na hali ya wazazi kutokujali kwao kuhusu elimu ijapokua ni kweli kwamba katika kipindi hicho walikua wameshaanza kuchoka ( kuishiwa pesa) hivyo sikubahatika kusoma hata pre-form five lakini nilijipa moyo kwamba ninaweza kufanya kitu cha tofauti licha ya ugumu wa masomo husika.

Hali ilikua tofaut baada ya kuingia kidato cha tano na kukutana na watu waliosoma twishen na ambao wapo bora kuliko mimi, kila nikijaribu kusoma nilikua nikipaniki baada ya kuona kuna watu wana uwezo kuliko mimi ila nilijipa imani kuwa nitashinda na nitafaulu japo kua mambo yalikua magumu sana kwa upande wangu.

Nilikuja kuamini kua ni kweli "ng'ombe wa maskini hazai" baada ya kumaliza kidato cha sita na matokeo kutoka nilikua na div 3 ya 15 yaani kila somo nilikua na "E" hivyo nilikua sina "principal pass" za kuniwezesha kwenda chuo, mara gafla kauli zikabadilika mtaani wale walio nisifu wote wakaanza kunikebehi kwamba nilienda kucheza shule (lakini hakuna mtu yoyote aliyenipa msaada kipindi nasoma hadi kuna kipindi nilikua nakosa hata ela ya kununulia sabuni ya kufulia)

Nikiangalia hali ya wazazi wangu ni ngumu na wote wamezeeka kwa sasa ( walitengana ningali bado mdogo sana hivyo malezi yangu muda mrefu nilipata kwa mama zangu wa kambo ambao baba aliwaleta nyumbani) naona kama nipo kwenye msitu wenye giza nene sioni njia ya kutokea kwani hakuna pa kupata msaada.

Mtu mmoja akanishauri niombe nafasi kwenye vyuo vya serikali ili nikipata nikaombe udhamini kwenye makampuni binafsi lakini mimi mtoto wa maskini sina anaenijua huko serikalini hivyo juhudi zangu ziligonga mwamba kwani nimeomba nafasi lakini bado nimekosa baada ya matokeo ya vyuo kutoka. Only God know ... Nimebakiza dua na sala tu walau nisikose ata mkate wa kila siku[emoji120]. (This is my real life not story)

Naomba pia kura yako hapo hapo chini [emoji116][emoji116][emoji116] kwa kubofya hilo neno "vote" kama hautojal
Pole Sana kiongozi

Nimeona tatizo lako kubwaaa Sana ni kujiamini kupita kiasi

Na kujilinganisha Kwa sababu unajiamini kupita kiasi pia

Na ndio maana sasa hivi Maisha unayaona yamekuwa magumu Sana kwako Kwa sababu uhalisia wa Maisha umevunja ego yako ya siku zote kitu ambacho ndicho kimekuwa kama identity yako sikuzote

Lakini mind you mkuu nenda uendako sikuzote huwezi kuwa Bora katika Bora lazima Tu utashindwa au kuna mtu ataonekana Bora Tu kuliko wewe

Ukiliweka hili kichwani kamwe hutasumbuka pale utakapozidiwa

Hivyo basi Ondoa hiyo attitude kichwani mwako ya kujiamini kupita kiasi

Kisha badili mtazamo wako Maisha sio kuhusu kufanya vizuri Sana madarasani na kuwa na uwezo mkubwa sana kuwazidi wanafunzi wengi darasani

Hebu jaribu kuuugeuza huo uwezo wako mkubwa Sana uliokuwa nao darasani ufit na Maisha halisi ya jamii yetu ili uweze kujua nini utafanya kujikwamua kimaisha badala ya kujikatia tamaa mapema

Achana na yaliyopita Anza kudeal na sasa na ya wakati wako ujao

The past is history

Mwisho sijaona mahali pa kuvote nimekuwa na shida hii muda sasa,kwenye PC hata kureply mtu siwez angalau kwenye simu,labda unipe tutorial ya namna ya kuvote both Kwa simu na pc nivote

Mwisho nimeandika pia makala ya namna kujilinganisha kunavyoweza kutuathiri Sana kwenye Ukuzi na Ustawi Wetu Katika Jamii,nimejitahidi kukudadavua vile kujilinganisha kunaweza kuwa hatari Sana kwetu,andiko langu liko kwenye stories of change,kama utapata wasaa tafadhali nenda ukosome,labda utapata kitu kinachoweza kukufaidisha maishani mwako

Kisha kama ikikupendeza naomba pia Kura yako

Asante na kila la kheri mkuu
 
Unachokihitaji haswa ni kipi?

Heading na content ni quietly different.

Niliposoma Heading nilijua wewe ni mtoto wa kike na kuna kaka anakusumbua.

°Umeshaomba chuo chochote cha Serikali na kupata admission?

°Kama ndiyo, weka namba ya malipo hapa. Mimi na wenzangu hapa tunaweza kuwiwa kukusaidia. Kila mmoja akilipa hata 10,000 inapungua pungua na utaweza kukamilisha malipo ya ada.

Pole. Hayo ndiyo maisha.
 
We jamaa acha Hizo na Mimi nikitoa story yangu ya magumu niliyopitia utajiona mchumba tu
Sie wengine tumelelewa na bibi shule tumejipeleka wenyewe 🏃🏃🏃
Nilitimiza wajibu unaonipasa bila kushurutishwa na mtu

Yaani ukiona mpaka tohara nilijipeleka mwenyewe na hapo nipo shule ya msingi darasa la sita B
Hakuna mtu aliekua anajali kuhusu Mimi zaidi ya Mimi kujitambua na kujipambania mwenyewe
Japo nilimaliza O level na matokeo hayakua ya kuridhisha Sana niliamua kupambana japo nisomee hata fani ya Hotel management tu 😂
Nikajichanga mbaka nifanye field Huko Zanzibar Ili angalau ka CV Kangu kajae jae ila wapi wakulungwa hali ngumu hata kaajira sijawahi pata

Sijakata tamaa napa napambana tu kibishi ila humu forum raia wanadhani Mimi ni mtu mzima kumbe changamoto za life zimenikuza kuwa mtu mzima Kwa lazima!😂😂

Keep Fighting dude acha kulia Lia wewe ni kidume kaza roho upambane
Vijana Bado tunanafasi kubwa sana
Tupambane ipo siku tulete shuhuda humu Kwa ndugu zetu Ili nao wasikate tamaa
👊👊👊👊👊
 
Unachokihitaji haswa ni kipi?

Heading na content ni quietly different.

Niliposoma Heading nilijua wewe ni mtoto wa kike na kuna kaka anakusumbua.

°Umeshaomba chuo chochote cha Serikali na kupata admission?

°Kama ndiyo, weka namba ya malipo hapa. Mimi na wenzangu hapa tunaweza kuwiwa kukusaidia. Kila mmoja akilipa hata 10,000 inapungua pungua na utaweza kukamilisha malipo ya ada.

Pole. Hayo ndiyo maisha.

Dunia inabeba watu tofauti sana!
una moyo wa utoaji mkuu.
 
Pole Sana kiongozi

Nimeona tatizo lako kubwaaa Sana ni kujiamini kupita kiasi

Na kujilinganisha Kwa sababu unajiamini kupita kiasi pia

Na ndio maana sasa hivi Maisha unayaona yamekuwa magumu Sana kwako Kwa sababu uhalisia wa Maisha umevunja ego yako ya siku zote kitu ambacho ndicho kimekuwa kama identity yako sikuzote

Lakini mind you mkuu nenda uendako sikuzote huwezi kuwa Bora katika Bora lazima Tu utashindwa au kuna mtu ataonekana Bora Tu kuliko wewe

Ukiliweka hili kichwani kamwe hutasumbuka pale utakapozidiwa

Hivyo basi Ondoa hiyo attitude kichwani mwako ya kujiamini kupita kiasi

Kisha badili mtazamo wako Maisha sio kuhusu kufanya vizuri Sana madarasani na kuwa na uwezo mkubwa sana kuwazidi wanafunzi wengi darasani

Hebu jaribu kuuugeuza huo uwezo wako mkubwa Sana uliokuwa nao darasani ufit na Maisha halisi ya jamii yetu ili uweze kujua nini utafanya kujikwamua kimaisha badala ya kujikatia tamaa mapema

Achana na yaliyopita Anza kudeal na sasa na ya wakati wako ujao

The past is history

Mwisho sijaona mahali pa kuvote nimekuwa na shida hii muda sasa,kwenye PC hata kureply mtu siwez angalau kwenye simu,labda unipe tutorial ya namna ya kuvote both Kwa simu na pc nivote

Mwisho nimeandika pia makala ya namna kujilinganisha kunavyoweza kutuathiri Sana kwenye Ukuzi na Ustawi Wetu Katika Jamii,nimejitahidi kukudadavua vile kujilinganisha kunaweza kuwa hatari Sana kwetu,andiko langu liko kwenye stories of change,kama utapata wasaa tafadhali nenda ukosome,labda utapata kitu kinachoweza kukufaidisha maishani mwako

Kisha kama ikikupendeza naomba pia Kura yako

Asante na kila la kheri mkuu
kama unatumia app hauwez kuona ni had uingilie chrome
 
Unachokihitaji haswa ni kipi?

Heading na content ni quietly different.

Niliposoma Heading nilijua wewe ni mtoto wa kike na kuna kaka anakusumbua.

°Umeshaomba chuo chochote cha Serikali na kupata admission?

°Kama ndiyo, weka namba ya malipo hapa. Mimi na wenzangu hapa tunaweza kuwiwa kukusaidia. Kila mmoja akilipa hata 10,000 inapungua pungua na utaweza kukamilisha malipo ya ada.

Pole. Hayo ndiyo maisha.
Vyuo nimeomba lakini bahat mbaya sijapata hata kimoja, nachohitaji kama naweza kupata ufadhili wa kusoma japo katika chuo cha private nitashukuru, hata kama kutakua na mkataba ambao nitatakiwa kuufidia baadae pia nipo tayari 🙏
 
Hili tukio la mwaka gan?.

Nadhan options bado unazo.

Tafuta material mazuri alaf Omba/nenda kafundishe part time(shule ikulipe) au Tuition (wanafunzi wakulipe) kwenye shule uliyopiga vizur form four.
Naamin bado wanakukumbuka coz ulifanya wonders.

Ukipata uzoefu unasogea mjini na ufungue kituo kikubwa ili kupata wanafunz weng.
 
Back
Top Bottom