Uaskofu wa Kakobe sote tunaujua. Ni huyu huyu mwaka 2000 alitangaza kuwa kaoteshwa Mrema atakuwa rais! Akazunguka naye mikoani kupigia debe kwenye majukwaa ya urais. Sote tunajua kura alizopata. Juzi tu kaapa kwa jina la Yesu umeme hautawaka, kisa umepitishwa juu ya Kanisa lake. Umeme hadi leo unawaka, tena umepunguza kabisa mgao. Mtu wa aina hii bado mnaendelea kumwita askofu mwenye maono ya ki-Mungu!!! Kuwateka binadamu akili ndiyo njia hatari zaidi kuliko hata kuwalipua kwa mabomu!
TANESCO ,IKULU NA WIZARA YA NISHATI NA MADINI WAMEKWEPA KUJIBU MASWALI YA MAYAGE .S.MAYAGE HADI LEO.
Tarehe 7/3/2010 Waziri wa nishati na madini alisema kwamba , Askofu Kakobe wa Full Gospel Bible Fellow Ship , alikuwa amekwamisha Shughuri za mradi wa TANESCO kwa siku 77 , ambapo alisema imekuwa kero kwa serikali na kwamba sehemu iliyobaki ni kidogo ambayo ingekamilika mara moja baada ya kutumia Nguvu za dola kupitisha Umeme pale kwa kwa Mbwembwe.
Ngereja alitamka wazi kuwa umeme huo ungezinduliwa na rais Kikwete baada ya kukamilika mara moja mwezi April kabla hata Kikao cha Bunge la Bajeti halijaisha na kama Waziri wa Nishati na Madini alikuwa anahofia maswali kutoka kwa Wapinzani.
Ninakumbuka ndani ya press hiyo iliyofanyika wizarani kulikuwea na Prince Bagenda na Jacton Manyerere ambaye wakati huo yupo gzt Mtanzania alishangilia sana maamzi ya Ngereja na kesho yake akaandika story mbaya sana Kumkandia Kakobe.
Siku ile Jacton Manyerere aliongea sana na Badra Masudi ,msemaji wa TANESCO ambaye watu wengi wamekuwa wanamtuhumu kuwa aliwekwa na Mtandao wa Lowassa sambamba na mahusiano yake hapo TANESCO akitokea sehemu mbalimbali kabla ya wizi wa RICHMONDI.
Badra Masoudi na Jacton Manyerere wamekuwa wanafanya Lobing kutetea CCM kabla ya Mpasuko wa agenda ya Kujivua gamba na pesa nyingi za Kumshambulia Kakobe zilielekezwa hapo na mwandishi Masiaga Matinyi amefanya kazi hiyo kwa uaminifu mkubwa.
Ni Manyerere huyohuyo aliyepewa pesa na kuanzisha gazeti la Jamuhuri mwenye kuhoji maswali mazito ya serikali lakini hajawahi kuhoji suala la kutopita umeme na ufisadi wa Lowasa katika gazeti lake.
Wakati wa Kubomoa Mabango ya Kakobe Vyombo vyote vya dola vilihamia pale lakini wealisituka kuwa Kakobe haukuleta upinzani wowte na wao wakachukua mabango yale na kuyapeleka makao makuu ya TANESCO Ubungo hadi leo.
Jambo lilishangaza ni kwamba Kikwete hakuzindua ule mradi wala serikali ya Japani haikutembelea hapo isipokuwa zilivuja taarifa kutoka TANESCO kuwa Vikombe katika nguzo 19 na 20 havipitishi umeme na wafanyakazi wa TANESCO Mako makuu wakafukuzwa Kazi kwa kosa hilo. Nakumbuka Engineer Baregu wa TANESCO ndiye alikuwa anaongoza issue hiyo.
Kilichofanyika ni kwamba waliagiza vikombe vingine kutoka Japani na Engineer kutoka Japani wakaja kwa nguvu zote na kuweka Vikombe vipya lakini likajitokeza tatizo jingine kwa maana ya suddenly Drop in PD yaani umeme unapita lakini unapofika katika nguzo hapo Kwa Kakobe unafifia.
Hilo tatizo ndilo lililopo hadi sasa na kilichofanyika ni kwamba taa zinawaka lakini umeme huo hauwezi hata kusukuma motor jambo ambalo kwa wale waliosoma High voltage wanaelewa maana yake nini.
Kilichofanyika ni kwamba CCM na serilaki waliwaita waandishi wa TBC na kuwapeleka pale makumbusho na kuwaonyesha kuwa umeme unawaka , lakini hawakueleza kuwa unapita kwa kiwango gani??
Ni aibu kubwa waandishi wetu hawana utaalamu mwingine wa kuhoji masuala ya kiufundi isipokuwa wanatumika kuwasafisha wakubwa.
Hata hivyo Wajapani waliendelea na matengenezo katika nguzo mbele ya kanisa la kakobe tu na wakati wanafanya hivyo lile tingatinga lao walilotumia kupanga kwenye nguzo hizo lilizima ghafla jambo lililo washangaza Wajapani na kuondoka haraka hadi sasa.
Mwaandishi wa Gazeti la Jibu la Maisha aitwaye Singo alikwenda pale na kushuhudia Tinga tinga likiwa limegota na kupiga picha.
Hata hivyo wakati wa Kampeni za Urais Jk alipanga kuzindua mradi huo lakini kabla hajafanya hivyo alishauriwa asizindue hasa pale alipoanguka Jangwani na kukimbizwa Bagamoyo.
Hata hivyo ,Tangu nyaya za umeme zilipopitishwa pale tarehe 9.3.2010, umeme uligoma kupita pale, na Ushahidi wa jambo hili serikalini ni kwamba suala hili lilihojiwa na Mbunge wakati huo Engineer Stella Manyanya ambaye alikuwa anapata hofu kuwa huenda serikali ikapata hasara na Waziri Ngereja alisema wazi kuwa kuna tatizo ila bado wanalishughulikia na hadi leo hajatokea hadharani kueleza kuwa tatizo hilo limekwisha hadi alipo onekanakana juzi anahojiwa na kamati kuu Dodoma juu ya kutoa rushwa na kuanza kampeni Mapema.
Kufuatia usiri huu Mayage .S. Mayage aliyekuwa Mhariri mtendaji wa gazeti la ANIKA UKWELI aliamua kufuatilia suala hili kwa kuyapeleka Maswali nane katika sehemu zifuatazo:
1.Mako Mkuu TANESCO(Badra Masodi)
2.Wizara ya Nisha na Madini (Tesha)
3.Ikulu(Salva)
4.Tanroad
Sehemu ya Maswali ya Mayage. S. Mayage yalikuwa kama ifuatavyo:
1.Ni kwa nini Uzinduzi wa Mradi wa umeme unaopita kwa Kakobe haujafanyika,wakati waziri Ngereja alimuahidi Stella Manyanya kuwa kunamatengenezo kidoga yanafanyika na mradi utazinduliwa na Kikwete kamaulivyo pangwa?
2.Kwa nini Jk ameacha kuzindiua mradi wa umeme Mkubwa uliohusisha serikali ya Tz na Japani uliojirani na Ikulu Dar lakini amethubutu kwenda kuzidua mradi mdogo wa Kanisa Katoliki tena uliombali na Ikulu?
3.Ni kwa nini matatizo ya mradi huo yatokee kwenye nguzo mbele ya Kakobe tu(Nguzo 19 &20) ilihali sehemu zingine zipo salama?
4.Kwa nini matengenezo yanafanyika katika mradi ambao hata hauja anza kufanya kazi wakati asimimazi walikuwa Wajapani waliobobea katika utalaamu wa Electronics na high voltage duniani?
5.Mabango ya Kakobe yanayogharimu Zaidi ya 150m yalionekana katika gari la TANESCO je yalipelekwa wapi baada ya kuyaondoa na kwa sasa ni mali ya nani?
Maswali haya yamekaa huko serikalini na kila akifuatilia hakupewa majibu na badala yakle TANESCO walimuahidi matangazo katika gazeti lake.
Baada ya maswali hayo kukaa mwezi mzima ndipo Mayage akaja na storynzito katika matoleo mawili ambapo yalisababisha aitwe na vyombo vya dola.
Ukitaka kujua undani wa nini kinaendelea mpigie Mayage .S. Mayage (0767 094534) mhariri asiyependa uoga atakueleza kwa undani ukweli juu ya suala hili.
Kama TANSCO ni wakweli basi waeleze walikuwa wanatengeneza nini mbele ya Nguzo pale kwa Kakobe na kama hakukuwa na tatizo ina maana Ngereja alidanganya Bunge aliposema kuwa kuna matengenezo yanafanyika??
Hivi kati ya wewe na Ngereja ni nani anayejua ukweli juu ya matengenezo haya??
Kama umetumwa fuatilia kwanza history lakini huwezi kuwadanga nya wato wate kama unavyotaka!!
Ushauli wangu :
Kama kweli umeme unapita basi nashauri TANESCO,IKULU na WIZARA YA NISHATI NA MADINI waitishe press kujibu maswali ya Mayage S. Mayage ili kuondokana na uposhaji vinginevyo serikali inaonyesha udhaifu mkubwa wa kutoheshimu vyombo vya habari na kupotosha umma kwa makusudi.
TBC wamekuwa wepesi kutangaza uongo kuwa KAKOBE ametoroka lakini hataki kueleza umma juu ya suala hili zito lenye maslahi ya Taifa.
Pamoja na kwamba Kamati yote iliyokuwa inashughurikia suala hilo imesambaratika na wengine wamepoteza Kazi na vyeo , lakini najua data hazijasambaratika.
Nakumbuka wachache waliokuwepo ni pamoja na>
1. William Ngrereja
2.Davidi Jairo
3.Bashiri Mrindoko
4.Philimon Luhanjo
5.Eliakim Maswi.