Kakosa Mume wa ndoto yake: Mdogo wangu wa mwisho kakosa mume kisa ana mtoto

Kakosa Mume wa ndoto yake: Mdogo wangu wa mwisho kakosa mume kisa ana mtoto

Kivipo sijakuelewa.
Wale wanaosema asiwe na mawasiliano na aliyemzalisha, hii inaweza ikakupeni furaha ya muda mfupi. Sababu kama mtoto anajua baba yupo hai na huna mawasiliano naye huku upo busy na mwanaume wako mwingine (mume wako), hii itampelekea mtoto kujenga chuki kwako na kwa mume wako na watoto wenu na hata akafikiria kuwadhuru.

Yeye atakua anajiona ni outsider tu, ikifika wenzake wanaenda kutembelea upande wa baba yao, yeye ataachwa pembeni au hata akienda basi kule lazima kuna mambo watamtenga sababu ni mtoto wa watu.
Yeye pia akienda kumtembelea baba yake au upande wa baba yake lazima kuna mambo wenzake watatengwa tu.
Hiyo hali inakua inajenga mpasuko mkubwa sana kwa watoto siku za baadaye, huku nyinyi mkijidanganya mnapendana wakati mfumo wa maisha umekaa.

Mbaya zaidi baba yake awe na uwezo duni kuliko nyie ndiyo chuki itakua zaidi kwa kuhisi kuna dhurma ilifanyika.
Haya mambo siyo mepesi, bora aendelee na maisha yake tu, lakini si kutafuta ndoa bali ije yenyewe na hata ikija atatakiwa kutafakari sana.
 
Mwambie atafute single father waishi humo, mwanaume yeyote asiye na mtoto kuoa single mother ni ngumu sana
Mimi nilishakuwa na kijana ila nimechukua mwanamke fresh asiye na rekodi mbovu ya kuwa single maza. Huu uhuni wa wasichana wa mjini kuzaa ovyo na kusingizia bahati mbaya ni wa kupuuzwa. Mwanamke hazai na mtu asiyempenda
 
Single faza ni mabaharia 🤣
Ndiyo tulivyoumbwa. Sasa ajichanganye kama hajaishia kuwa single mother, halafu akajikuta anaishia kutafuta fala au mtu aliye desperate ili ajipachike.
Wanawake wenyewe wakipata mtu wa hivyo na wao humuona kuwa jamaa ni fala ndiyo maana kwenye kumuelezea utasikia "nimempata mtu, jamaa anajielewa sana na yupo matured na amekubali kuwa na mimi pamoja na kuwa nina mtoto tayari". Ukishaona kwenye sentensi jamaa anapambwa kujielewa basi ujue tayari bibiye yupo kwenye kazi ya kumfichia mtu ufala wake uliomjaa 😃
 
Hawa single mothers kuna muda wanakua sio wa kweli ndo maana Imani kwao ni ndogo.

Kuna moja nlikutana nae nikampanga fresh akakubali ila hakuniambia kama ana mtoto, tukaendelea na maisha kuna siku nliingia FB nkaona jina nkacheki picha zake aiseeee vitu nliona 🤣nlichoka, nkalike picha Moja akiwa kambeba mwanae na nyingn akiwa na mtiamimba wake, kuona nimelike picha alinipigia tukaongea masaa 3+

Nliishia kumnyandua tu, inakata stimu hata kama una mpango wa kuoa
 
Uwezi amini jamani, nina mdogo wa mwisho anamika 27 miaka mitano iliyopita alipata mtoto wa kiume. Ila aliyempa ujauzito baadae alioa mwanamke mwingine.

Mwaka jana mwezi wa 8 alimpata kaka mmoja hivi ni mzuri sana na anamaisha yake. Mimi nilimpenda sana yule kaka, mdogo wangu aliniambie huyu ndo mume anayemtaka japo hakumwambia mapema kuwa anamtoto tayari.

Ila mwezi uliopita yule kaka alimwambia kuwa anahitaji kumjua zaidi kuusu familia yake na mahusiano yake ya mwanzo kabla hawajafika deep relationship.

Mdogo wangu akasema sawa, mimi nilimwambia kuwa mwambie mapema kuwa unamtoto tayari, pia usimfiche kuhusu uliyezaa nae mwambie tuu mahusiano yashakufa na tayari yeye anamke tayari. Mwembie mtoto wako hataaribu mahusiano yenu. Pia amwambie tuu kuwa haukupanga kuwa na mtoto ilitokea tuu.

Sasa wiki iliyopita alimwambie kuwa yeye tayari anamtoto, na aliyezaa nae yani Baba mtoto hana mahusiano nae wamebaki kuhudumia tuu mtoto na kuwasiliana kuhusu mtoto tu.

Baada ya kumwambia hivyo yule kaka jamani, jioni yake hakuwa anajibu hata sms , hata akimpigia anamwambia yuko busy. Alimfanyi hivyo kama siku 4 hivi.

Sasa juzi wamekutana yule kaka jamani akamwambia kuwa wewe tayari unamtoto nje. Mimi nataka kuwa na mwanamke ambaye tutakuwa na watoto wetu tuu wa ndoa peke yake.

Nilishangaa sana alimwambie kuwa kama unamtoto tayari tutawafundisha nini watoto wetu kuwa usizae kabla ya ndoa angali wewe tayari unamtoto kabla ya ndoa.

Huo ujasiri utautoa wapi. Lakini pia hata kuwaambia watoto usizini angalie wewe mama ushazini tayari.
Mawasiliano na baba mtoto yakizidi je mimi nitafanya nini. Mdogo wangu ameniambie hivyo.

Nimeshangaa sana jamani,

Hivi nyie wanaume mtoto anatatizo gani jamani. Kwani atazuia ndoa yenu isiwe na furaha jamani.

Kwa nini inakuwa ngumu kwenu kuoa mwanamke ambaye anamtoto tayari.

ACHENI UCHOYO NA ROHO MBAYA.
Kwahiyo unataka game ndo Kwanza inaanza kuwe na aggrigate 0-1
 
Back
Top Bottom