Kama anaamini wananchi hatuijui katiba ya sasa, yeye mwenyewe akae pembeni maana hatujui hiyo nafasi kaipataje

MGOGOHALISI

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2011
Posts
3,294
Reaction score
4,920
Ni rahisi sana kujitamkia maneno hasa unapokua na mamlaka ya kuitisha vyombo vyote vya habari virushe habari zako hata kama hazina mashiko. Ndio, ni rahisi kutamka lolote hasa kama mtu anaamini hakuna wa kumgusa.

Ndivyo ilivyotokea kwa mama yetu hapo juzi. Ni wazi mama na CCM wala keki ya taifa hawataki kusikia hoja ya katiba mpya. Sasa wamfundishe mama nini cha kuongea awapo jukwaani. Kuna mambo anaongea yanakua yanamlenga na yeye mwenyewe, yanamzodoa. Niseme moja tu kwa leo.

Mama alisikika akisema hii katiba watu hatuijui, eti wanaweka miaka mitatu watufundishe. Fine kama katiba hatuijui kwanini ianze kutumika? Amekuwaje raisi? Si hii katiba anayosema hatuijui? Kama hatujui katiba yeye tunamjuaje? Kwa sheria ipi? Basi nashauri akae pembeni tufundishwe katiba kwanza tuielewe, tujue kuwa baada ya JPM kufariki ni yeye alitakiwa kuapishwa na si mwingine

Iweje katiba iwe inajulikana pale inapomfurahisha yeye tu? Iweje iwe haijulikani pale tukisema ina mapungufu? Huku ni kupungukiwa busara, kukanyaga kitabu knachokupa mamlaka kisa tu hoja iliyopo inakuchefua.

Mama yetu akae pembeni tueleweshwe katiba. Isijekua aliyetakiwa kuapishwa ni mtu mwingine yeye akajitanguliza. Ndio! Si hatujui katiba jamani. Tunataka tukajiridhishe kama ni yeye kweli ama mtu mwingine ama marehemu anatakiwa kuendelea kuongoza hadi muda uishe.

Mama aelezwe kwamba asituonyeshe waziwazi kwamba katiba inamnufaisha na anachekelea tu pale inapokua upande wake. Asituonyeshe kuwa katiba ni nzuri pale inapompatia mamlaka. Asituaminishe kuwa katiba inajulikana kwa mema ya upande wake tu na sio taifa, hapana.

Sote tunajua katiba mpya ni kaa la moto kwa CCM. Nawashauri CCM hata kama wanataka kuchelewesha mchakato watafute danganya toto za maana sio hizi ngonjera zinazowavua nguo wao wenyewe.
 
Duh aiseee
Ni kweli, kama Rais SAMIA anataka tufundishwe katiba miaka mitatu, tukiijua ndio tuongelee katiba, basi na yeye atoke kwenye Urais miaka mitatu tukiijua katiba ndio arudi kuwa Rais. Tukubaliane kwamba na yeye akae nje miaka mitatu mpaka katiba tuijue.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Mama Abdul anaudhi sana!
 
Madman
 
Kauli anazoongea anafikiri zinamsaidia kumbe zinamteketeza.
 
Your browser is not able to display this video.
 
Hoja imeshiba vizuri kabisa, wale machawa wake na mboga mboga waje watoe ufafanuzi kama kawaida yao
 
Aione kwenye jalada FaizaFoxy Lucas mwashambwa
 
Safi sana, atakaa pembeni akishaijuwa katiba.
 
Sasa hv hata bandari mshaisahau, issue inayobamba sasa hv ni speech ya Rais tu
 
Haya sawa amekusikia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…