Muumba wa ubongo anajua kinachotukia tunapokufa. Anajua ukweli na katika Neno lake, Biblia, anaeleza hali ya wafu. Biblia inafundisha hivi waziwazi: Mtu anapokufa, hayupo tena. Kifo ni kinyume cha uhai. Wafu hawaoni, hawasikii wala kufikiri. Hakuna sehemu yoyote ya mwili wetu inayoendelea kuishi baada ya mwili kufa. Hatuna nafsi au roho isiyoweza kufa.Baada ya Sulemani kutaja kwamba walio hai wanajua kwamba watakufa, aliandika hivi: “Lakini wafu, hawajui lolote kamwe.” Kisha akafafanua kweli hiyo ya msingi kwa kusema kwamba wafu hawawezi kupenda wala kuchukia na kwamba “hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi.” (Mhubiri 9:5, 6, 10) Vivyo hivyo, andiko la Zaburi 146:4 linasema kwamba mtu anapokufa, “mawazo yake hupotea.” Sisi hufa wala hatuendelei kuishi baada ya mwili kufa. Maisha yetu ni kama moto. Unapozimika, hauendi popote. Haupo tena.