Kama CCM wakifuata utaratibu wao wa kutompinga Rais aliyepo katika kuteua mgombea, basi Samia Suluhu anaweza kuwa Rais wa Tanzania kwa miaka 14

Kama CCM wakifuata utaratibu wao wa kutompinga Rais aliyepo katika kuteua mgombea, basi Samia Suluhu anaweza kuwa Rais wa Tanzania kwa miaka 14

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Kumekuwa na ubishi kuhusu kama kwa sasa Samia Suluhu anaongoza awamu ya tano au ya sita. Labda hilo sio jambo la maana. Jambo la msingi ni kwamba rais Samia Suluhu anaongoza awamu ambayo haitambuliki kikatiba kama ni awamu yake ya kwanza ya uongozi, bali amechukua madaraka ya uraisi kutokana na kifo cha rais aliyekuwapo madarakani. Samia hakuchaguliwa kwa kura, hivyo uraisi wake wa sasa ni wa kuziba pengo tu.

Kwa jinsi hiyo basi, awamu ya kwanza ya Samia Suluhu itakuwa mwaka 2025 ikiwa CCM watampitisha kuwa mgombea wao wa uraisi. Na tukumbuke kwamba CCM wana utaratibu wa kumpitisha raisi aliyepo madarakani kuendelea kuwa chaguo lao la mgombea urais.

Ikiwa Samia atagombea urais mwaka 2025 na kupita, itakapofika uchaguzi wa 2030 atakuwa tena na haki ya kikatiba ya kugombea uraisi kwa awamu yake ya pili, na akipita atakuwa raisi hadi mwaka 2035.

Kwa hiyo basi, Samia anaweza kuwa Mtanzania wa kwanza kuwa rais kwa muda wa miaka 14 kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania. Hiyo ni habari njema kwa Watanzania wengi, na habari mbaya kwa wengine, lakini ndio ukweli uliopo.
 
Hivi unajua katiba inasemaje kuhusu hili au umejiandikia kwa jinsi unavyofikiria...!?

Kwa taarifa tu Kikatiba hii itakuwa ni awamu au kipindi chake cha kwanza. Na kipindi hake cha pili ni 2025 to 2030 kama CCM wataendelea na Kale kautaratibu kao ka kuachiana.
Mkuu, weka basi hapa hivyo vipengele vya Katiba ili tumalize jambo hili. Nakiri naweza kuwa nimekosea na sintabishana na Katiba
 
Rais wa kwanza mwanamke
Rais wa kwanza kurithi mikoba toka kwa rais aliyefariki
Rais wa kwanza kuongoza nchi kwa miaka zaidi ya kumi
Rais wa kwanza aliyewahi kuwa mkamu wa rais
Rais wa kwanza ....
 
Mkuu tunampenda sana Rais SSH.

Ila KATIBA inamruhusu KUGOMBEA kipindi kimoja tu kwa kuwa "AMECHUKUA" URAIS chini ya miaka 3 ya Rais aliyegombea.

Kwa hiyo CAP yake itakuwa ni MIAKA 9 tu.

#KaziIendelee
#StaunchSupporterOfSSH
#DieahardFanOfCCM
 
Kikatiba SSH kama akitaka kuongoza zaidi ya miaka hii mi4 aliyorithi...anaruhusiwa kugombea term moja pekee...2025... Ila angekuwa amerithi muda ambao ni chini ya miaka mi3...angeruhusiwa kugombea terms 2....kwa sasa anaruhusiwa kugombea term moja pekee kwa kuw hii anayoongoza saiv inahesabiwa kama term ya kwanza maana hata mwaka haukupita tangu waingie madarakan na JPM.
Naona unaishi kwa matumaini Mkuu. La sivyo weka vipengele vya katiba katika jibu lako vinavyoonyesha vinginevyo, sio kubisha kama Mwajuma wa Kimanzichane.
 
Back
Top Bottom