Kama chanzo cha uhai kinaweza kubadilika basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti hadi sasa. Je, ni upi msingi wa uhai?

Kama chanzo cha uhai kinaweza kubadilika basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti hadi sasa. Je, ni upi msingi wa uhai?

Ungekuwa umesoma elimu ya atomic energy physics usinge kujakusumbua watu nahisi.
Sijasoma ndio maana nimeileta humu ili mliosoma mtuelezee... Haya lete vitu kutokea upande huo mkuu.
 
Hapa unajibana mkuu na kujipa excuse ya kurudi nyuma katika kuyafikira mambo.
Nimerudi nyuma nikakuuliza hivi...👇

Kama uhai lazima uwe na msingi wake, Je msingi wa "msingi wa uhai" ni nini?

Umeshindwa kujibu.

Sasa najibana vipi?

Au ni wewe umeshindwa kutoa majibu?

Narudia tena kukwambia,

Hatuwezi kujua tusivyo vijua, ila tunaendelea kupunguza tusivyo vijua.

Ndio maana umeshindwa kujua na kujibu msingi wa "msingi wa uhai" ni nini?

Kwa sababu bado hatujui.

Hata wewe mwenyewe umekiri hujui msingi wa uhai ni nini, Ndio maana umeanzisha hii mada.
 
Nimerudi nyuma nikakuuliza hivi...👇

Kama uhai lazima uwe na msingi wake, Je msingi wa "msingi wa uhai" ni nini?

Umeshindwa kujibu.

Sasa najibana vipi?

Au ni wewe umeshindwa kutoa majibu?

Narudia tena kukwambia,

Hatuwezi kujua tusivyo vijua, ila tunaendelea kupunguza tusivyo vijua.

Ndio maana umeshindwa kujua na kujibu msingi wa "msingi wa uhai" ni nini?

Kwa sababu bado hatujui.

Hata wewe mwenyewe umekiri hujui msingi wa uhai ni nini, Ndio maana umeanzisha hii mada.
Mbona nimekujibu hilo swali ya kwamba tunajadili msingi wa uhai kwasababu tunaona vyanzo so hatuwezi kuruka hatua ni Bora tuutafute msingi wake kwanza then ndio tuje tujadili huo msingi wa msingi wake ni nini.😅😅😅
 
Mbona nimekujibu hilo swali ya kwamba tunajadili msingi wa uhai kwasababu tunaona vyanzo so hatuwezi kuruka hatua ni Bora tuutafute msingi wake kwanza then ndio tuje tujadili huo msingi wa msingi wake ni nini.😅😅😅
Chanzo kinaweza kuwepo au vyanzo vinaweza kuwepo bila msingi.

Chanzo hakihitaji msingi.

Maana kuna vitu vinatokea bila msingi wowote ule.
 
Mkuu unajua maana ya Nishati ? Kwamba nikitumia nishati ya moto kupika nyama ni moto ndio unaiambia nyama zile protein ziwe denatured ...

Unaongelea kwamba kwanini parachichi isitoe muembe au ? Mbona hio ni rahisi sana ukienda leo kutoa photocopy ya NIDA kitatokea kitambulisha cha kupigia Kura.

Na kuhusu mbegu mbona rahisi sana kuna chakula kipo stored kwenye mbegu ukikipa favorable conditions; maji n.k. kunatokea germination ambayo baada ya majani kutoka inaanza kupata chakula kwa usaidizi wa jua... (photosynthesis


What don't you understand na ninaposema what is known to be factual ?!!! Which means kutokana na kufuatilia tumefikia conclusion fulani hata kama we can not prove it directly hence we know it to be a fact (the truth)
Turudi kwenye mada,.. Msingi wa uhai ni nini?



NB: Unalazimisha theory iwe fact, lakini kamwe theory haiwezi kuwa fact mpaka itakapokoma kuwa theory.
 
Bila shaka mko salama waungwana...

Kikawaida neno msingi na chanzo ni maneno mawili ambayo ukiangalia kwa jicho la kawaida ni kama yanafanana hivi lakini ni maneno yaliyo na utofauti mkubwa.

Kwa maana chanzo huwa kinatengeneza muendelezo usio na ukomo lakini msingi huwa unatengeneza muendelezo mgumu ambao huwa haueleweki pasipo kurudi tena kwenye msingi kwa maana nyingine ni kwamba msingi ndio unaounda vyanzo mbalimbali.

Ndio maana mkusanyiko wa vyanzo vingi vya habari fulani unaweza kuleta mkanganyiko wa mambo hasa inapotokea vyanzo vyote vinaongelea habari moja ila vinatofautiana katika taarifa zao, hii hufanya mtu ashindwe kuelewa aamini chanzo kipi kati ya hivyo, na ili kuondoa huu mkanganyiko basi mtu hupaswa arudi kwenye msingi wa habari yenyewe na baada ya kufanya hivyo basi ni rahisi kujua kati ya vyanzo hivyo ni kipi na kipi kimeandika habari kwa kuzingatia msingi wake.

Kwahiyo kuna nyakati neno chanzo hutumika zaidi kwenye mambo ambayo msingi wake haujulikani au uhakika wa moja kwa moja juu ya msingi wake haupo lakini msingi ndio ambao unabeba chanzo.

Lakini pia chanzo wakati fulani huwa kinakua na mbadala wake wakati msingi huwa hauna mbadala (ndio maana habari unaweza kuipata jamiiforum, milard ayo na media zingine ila msingi wa habari hiyo hauwezi kubadilika).

Kwamfano wewe ni chanzo cha watoto wako kuzaliwa na wao ni chanzo cha wajukuu zako kuzaliwa lakini pia wajukuu zako ni chanzo cha vitukuu kuzaliwa na hii itaendelea namna hii bila ukomo na wewe hujawa msingi kwasababu nyuma yako alikuwepo baba yako ambae alikua chanzo cha wewe kuzaliwa ila pia Kabla ya baba yako alikuwepo babu yako ambae yeye alikua chanzo cha baba yako kuzaliwa na hii itarudi nyuma katika umbali usio julikana na ndio maana tumetumia neno chanzo.

Lakini pia mtu ni roho, na kama hii ndio basi hizo roho ambazo wewe umezileta hapa duniani haimaanishi kwamba wewe ndio mtu pekee ambae unao uwezo wa kuleta roho hizo isipokua wewe uliwin tu kwenye ile probability ila usingezileta wewe basi angekuwepo mtu mwingine ambae angeweza kuzileta, na vivyo hivyo wewe kwa baba yako na baba yako kwa babu yako na kadhalika.

Kwahiyo neno chanzo linapotumika katika eneo lolote ujue tayari kuna hali isiyo na ukomo imetengenezwa kwa kwenda mbele au kwa kurudi nyuma kwa maana ule msingi kamili wa jambo hilo haujulikani au kuna namna mbadala ya jambo hilo kwenye kutokea kwake au kufanyika kwake ukiachana na namna hiyo ambayo imetumika.

Okay, wacha twende mbali kidogo, watu husema Mungu ni chanzo cha uhai, hii tayari ni sentensi ambayo haina ukomo, kwa kurudi nyuma au kwenda mbele, lakini pia kwa kusema hivi unamaanisha asingekua yeye basi chanzo cha uhai kingeweza kupatikana kwa namna nyingine.

Angalia hii, wewe ni chanzo cha mkeo kuolewa au tuseme ni chanzo cha ndoa yenu ila sio msingi wa hiyo ndoa kwa maana hata kama wewe usingemuoa basi angeweza kuolewa na mtu mwingine, na huyo mtu mwingine nae angekua tu chanzo ila wala sio msingi kwa maana huyo mtu mwingine asingemuoa basi angeolewa na mtu mwingine tena, kwahiyo hii unaona inakua ni infinity loop.

Kwahiyo kama Mungu ni chanzo cha uhai basi msingi wa uhai bado haujulikani na ukomo wa uhai huo huo haujulikani pia (naomba usome ukiwa katika utulivu wa akili ili unielewe vizuri hapa).

Hii inamaanisha nini? Hii inamaanisha kwamba ni eidha Mungu ni neno moja linalotumika kuwakilisha jamii ya viumbe fulani kama vile neno binadamu linavyotumika kutuwakilisha Mimi na wewe au ukiachana na Mungu basi kuna viumbe vingine venye uwezo wa kutoa uhai (wacha tusonge taratibu huku tukiongeza tafakuri juu ya tafakuri hapa).

Kama Mungu ni kiwakilishi cha jamii ya viumbe fulani kama lilivyo neno binadamu basi neno la tumfanye mtu kwa mfano wetu halitakua na maana yoyote iliyojificha zaidi ya lilivyo na limekuwepo pale kama uthibitisho wa kwamba Mungu ni neno la jumla linalowakilisha jamii fulani kama ilivyo kwa neno binadamu.

Na kwa uthibitisho zaidi wa jambo hili ni pale Mungu anaposema aabudiwe yeye na wala sio miungu mingine, hii inamaana anajua ya kwamba katika jamii ya kimungu hayupo peke yake.

Ni sawa na wewe utengeneze robot lako ikiwa wewe ndio mkuu wa mradi licha ya kwamba ndani yake kutakua na ma-engineer wengine ambao ni binadamu na ghafla ukaanza kuona yule robot anaanza kuwatii watu wengine kuliko wewe mkuu wa kitengo lazima urudi umwambie unaefaa kunyenyekewa ni wewe na wala sio binadamu wengine.

Kama hiyo haitoshi lakini pia kuna maeneo kadhaa Mungu alijitokeza kwa kujitambulisha ya kwamba yeye ni Mungu wa vita mara Mungu wa maarifa na kadhalika, hii sio bahati mbaya na wala huna haja ya kuilazimisha ikae kwa namna tofauti na hiyo kwa maana hivyo ndivyo ilivyo na hii inaweza kuthibitisha kwamba Mungu ni sawa na kusema binadamu (yote ni maneno yanayowakilisha jamii ya viumbe fulani).

Na kwa hoja hiyo sasa, ndio maana ukisema Mungu ni chanzo cha uhai inamaana si Mungu wote ambao walishiriki kwenye mradi wa kumpa uhai binadamu ila ni jopo tu la Mungu kadhaa ndio ambao walifanya hii project na ndio maana neno chanzo limetumika kwa maana ya kwamba kama hao waliokaa wasingekaa basi Mungu wengine wangeweza kukaa na kumpa uhai binadamu kama wangeamua kufanya hivyo.

Lakini kama tukiendelea kubaki na msimamo wetu wa kwamba Mungu ni mmoja na wala sio jamii ya viumbe fulani basi hapa tunaweza kuibua hoja mpya ya kwamba kumbe ukiachana na Mungu katika puzzle hii pia kunao uwezekano wa kuwepo jamii fulani ya viumbe wenye uwezo wa kutengeneza watu au kumpa mtu uhai, na kama kweli chanzo cha uhai kinaweza kubadilika kinamna hii basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti.

Na hii ndio sababu ya neno chanzo kutumika badala ya neno msingi.

Najua kuna mtu hapa anaweza asielewe ila kama unataka uelewe zaidi unaweza Kutafakari kwa kina juu ya neno chanzo na msingi kisha ukishapata point urudi usome tena hili andiko.

Kwa mfano huwa tunasema chanzo cha mapato wala sio msingi wa mapato kwa maana kuna njia nyingi ambazo mtu anaweza akazitumia ili zimuingizie mapato.

Chanzo cha furaha yangu ni wewe, kwa maana usipokua wewe basi anaweza akawa mtu mwingine ambae anaweza akanipa hii furaha unayo nipa kwakua duniani binadamu haupo peke yako.

Chanzo cha Mimi kupata kazi ni wewe, hii inamaanisha hata usingekua wewe ningepata kazi kwa maana nisingekutana na wewe basi ningekutana na mtu mwingine ambae angekuwa chanzo kama ambavyo wewe umekua(kwa maana wewe si mtu wa kwanza na wa mwisho kuwa na connection au roho ya upendo wa namna hii).

Tengeneza msingi wa maisha yako, kwasababu wewe pekee ndio mwenye uwezo wa kutengeneza maisha yako na wala hakuna mbadala wa wewe.

Kwahiyo ukisoma kwa umakini na Kutafakari hapa, utagundua ya kwamba ndani ya chanzo kuna msingi, na msingi mmoja unaweza ukatengeneza vyanzo mbalimbali (usichanganyikiwe sasa na wewe, ili uelewe hapo rudi mwanzo mwa andiko nilikwambia msingi ndio hutengeza complex things na ili uweze kuondoa ucomplex ni lazima uanze kuyagawa mambo hayo kwenye namna fulani rahisi ili uufikie msingi wake).

Ndio maana mtu akifariki huwa wale watu wanaomfahamu wanapopata taarifa huwa wanauliza chanzo cha kifo chake ni nini, kwa maana wanajua kifo kinaweza kusababishwa na mambo mengi ya msingi ambayo ndio huweza kuunda chanzo.

Kwahiyo kama haujui msingi wa jambo fulani huwezi kusolve puzzle yake, na hapa duniani mambo mengi yapo kwenye puzzle na puzzle ni muunganiko wa mambo mbalimbali ya msingi na ili uweze kusolve puzzle nyingi za kilimwengu lazima uuelewe vizuri msingi wake ni nini.

So, kama Mungu ndio chanzo cha uhai basi hii tayari inakua ni complex puzzle kwa maana iko na vyanzo vingi hadi kufikia ule msingi wake na ili tuweze kuisolve lazima tuujue msingi wake ni upi.

Je, msingi wa uhai ni nini?

NITARUDI.
Upo hapa duniani ili UFE unataka nini tena kufukua mambo ambayo yanafikirisha.?

Ishi ili ufe
 
Turudi kwenye mada,.. Msingi wa uhai ni nini?
Nini maana ya Msingi kwa muktadha wako ? Mimi nimekupa maana ya msingi kwa macho ya Nature (Ecosystem) / Sustainability kama huwezi ku conform na nature basi utakuwa extinct
NB: Unalazimisha theory iwe fact, lakini kamwe theory haiwezi kuwa fact mpaka itakapokoma kuwa theory.
Ni kitu gani huelewi kuhusu neno known (recognized, familiar, or within the scope of knowledge) Hio ndio maana ya known.., Sasa unganisha ni sentesi niliyosema known to be factual..., Je hio ina maana sawa na fact ?!!!!
 
Bila shaka mko salama waungwana...

Kikawaida neno msingi na chanzo ni maneno mawili ambayo ukiangalia kwa jicho la kawaida ni kama yanafanana hivi lakini ni maneno yaliyo na utofauti mkubwa.

Kwa maana chanzo huwa kinatengeneza muendelezo usio na ukomo lakini msingi huwa unatengeneza muendelezo mgumu ambao huwa haueleweki pasipo kurudi tena kwenye msingi kwa maana nyingine ni kwamba msingi ndio unaounda vyanzo mbalimbali.

Ndio maana mkusanyiko wa vyanzo vingi vya habari fulani unaweza kuleta mkanganyiko wa mambo hasa inapotokea vyanzo vyote vinaongelea habari moja ila vinatofautiana katika taarifa zao, hii hufanya mtu ashindwe kuelewa aamini chanzo kipi kati ya hivyo, na ili kuondoa huu mkanganyiko basi mtu hupaswa arudi kwenye msingi wa habari yenyewe na baada ya kufanya hivyo basi ni rahisi kujua kati ya vyanzo hivyo ni kipi na kipi kimeandika habari kwa kuzingatia msingi wake.

Kwahiyo kuna nyakati neno chanzo hutumika zaidi kwenye mambo ambayo msingi wake haujulikani au uhakika wa moja kwa moja juu ya msingi wake haupo lakini msingi ndio ambao unabeba chanzo.

Lakini pia chanzo wakati fulani huwa kinakua na mbadala wake wakati msingi huwa hauna mbadala (ndio maana habari unaweza kuipata jamiiforum, milard ayo na media zingine ila msingi wa habari hiyo hauwezi kubadilika).

Kwamfano wewe ni chanzo cha watoto wako kuzaliwa na wao ni chanzo cha wajukuu zako kuzaliwa lakini pia wajukuu zako ni chanzo cha vitukuu kuzaliwa na hii itaendelea namna hii bila ukomo na wewe hujawa msingi kwasababu nyuma yako alikuwepo baba yako ambae alikua chanzo cha wewe kuzaliwa ila pia Kabla ya baba yako alikuwepo babu yako ambae yeye alikua chanzo cha baba yako kuzaliwa na hii itarudi nyuma katika umbali usio julikana na ndio maana tumetumia neno chanzo.

Lakini pia mtu ni roho, na kama hii ndio basi hizo roho ambazo wewe umezileta hapa duniani haimaanishi kwamba wewe ndio mtu pekee ambae unao uwezo wa kuleta roho hizo isipokua wewe uliwin tu kwenye ile probability ila usingezileta wewe basi angekuwepo mtu mwingine ambae angeweza kuzileta, na vivyo hivyo wewe kwa baba yako na baba yako kwa babu yako na kadhalika.

Kwahiyo neno chanzo linapotumika katika eneo lolote ujue tayari kuna hali isiyo na ukomo imetengenezwa kwa kwenda mbele au kwa kurudi nyuma kwa maana ule msingi kamili wa jambo hilo haujulikani au kuna namna mbadala ya jambo hilo kwenye kutokea kwake au kufanyika kwake ukiachana na namna hiyo ambayo imetumika.

Okay, wacha twende mbali kidogo, watu husema Mungu ni chanzo cha uhai, hii tayari ni sentensi ambayo haina ukomo, kwa kurudi nyuma au kwenda mbele, lakini pia kwa kusema hivi unamaanisha asingekua yeye basi chanzo cha uhai kingeweza kupatikana kwa namna nyingine.

Angalia hii, wewe ni chanzo cha mkeo kuolewa au tuseme ni chanzo cha ndoa yenu ila sio msingi wa hiyo ndoa kwa maana hata kama wewe usingemuoa basi angeweza kuolewa na mtu mwingine, na huyo mtu mwingine nae angekua tu chanzo ila wala sio msingi kwa maana huyo mtu mwingine asingemuoa basi angeolewa na mtu mwingine tena, kwahiyo hii unaona inakua ni infinity loop.

Kwahiyo kama Mungu ni chanzo cha uhai basi msingi wa uhai bado haujulikani na ukomo wa uhai huo huo haujulikani pia (naomba usome ukiwa katika utulivu wa akili ili unielewe vizuri hapa).

Hii inamaanisha nini? Hii inamaanisha kwamba ni eidha Mungu ni neno moja linalotumika kuwakilisha jamii ya viumbe fulani kama vile neno binadamu linavyotumika kutuwakilisha Mimi na wewe au ukiachana na Mungu basi kuna viumbe vingine venye uwezo wa kutoa uhai (wacha tusonge taratibu huku tukiongeza tafakuri juu ya tafakuri hapa).

Kama Mungu ni kiwakilishi cha jamii ya viumbe fulani kama lilivyo neno binadamu basi neno la tumfanye mtu kwa mfano wetu halitakua na maana yoyote iliyojificha zaidi ya lilivyo na limekuwepo pale kama uthibitisho wa kwamba Mungu ni neno la jumla linalowakilisha jamii fulani kama ilivyo kwa neno binadamu.

Na kwa uthibitisho zaidi wa jambo hili ni pale Mungu anaposema aabudiwe yeye na wala sio miungu mingine, hii inamaana anajua ya kwamba katika jamii ya kimungu hayupo peke yake.

Ni sawa na wewe utengeneze robot lako ikiwa wewe ndio mkuu wa mradi licha ya kwamba ndani yake kutakua na ma-engineer wengine ambao ni binadamu na ghafla ukaanza kuona yule robot anaanza kuwatii watu wengine kuliko wewe mkuu wa kitengo lazima urudi umwambie unaefaa kunyenyekewa ni wewe na wala sio binadamu wengine.

Kama hiyo haitoshi lakini pia kuna maeneo kadhaa Mungu alijitokeza kwa kujitambulisha ya kwamba yeye ni Mungu wa vita mara Mungu wa maarifa na kadhalika, hii sio bahati mbaya na wala huna haja ya kuilazimisha ikae kwa namna tofauti na hiyo kwa maana hivyo ndivyo ilivyo na hii inaweza kuthibitisha kwamba Mungu ni sawa na kusema binadamu (yote ni maneno yanayowakilisha jamii ya viumbe fulani).

Na kwa hoja hiyo sasa, ndio maana ukisema Mungu ni chanzo cha uhai inamaana si Mungu wote ambao walishiriki kwenye mradi wa kumpa uhai binadamu ila ni jopo tu la Mungu kadhaa ndio ambao walifanya hii project na ndio maana neno chanzo limetumika kwa maana ya kwamba kama hao waliokaa wasingekaa basi Mungu wengine wangeweza kukaa na kumpa uhai binadamu kama wangeamua kufanya hivyo.

Lakini kama tukiendelea kubaki na msimamo wetu wa kwamba Mungu ni mmoja na wala sio jamii ya viumbe fulani basi hapa tunaweza kuibua hoja mpya ya kwamba kumbe ukiachana na Mungu katika puzzle hii pia kunao uwezekano wa kuwepo jamii fulani ya viumbe wenye uwezo wa kutengeneza watu au kumpa mtu uhai, na kama kweli chanzo cha uhai kinaweza kubadilika kinamna hii basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti.

Na hii ndio sababu ya neno chanzo kutumika badala ya neno msingi.

Najua kuna mtu hapa anaweza asielewe ila kama unataka uelewe zaidi unaweza Kutafakari kwa kina juu ya neno chanzo na msingi kisha ukishapata point urudi usome tena hili andiko.

Kwa mfano huwa tunasema chanzo cha mapato wala sio msingi wa mapato kwa maana kuna njia nyingi ambazo mtu anaweza akazitumia ili zimuingizie mapato.

Chanzo cha furaha yangu ni wewe, kwa maana usipokua wewe basi anaweza akawa mtu mwingine ambae anaweza akanipa hii furaha unayo nipa kwakua duniani binadamu haupo peke yako.

Chanzo cha Mimi kupata kazi ni wewe, hii inamaanisha hata usingekua wewe ningepata kazi kwa maana nisingekutana na wewe basi ningekutana na mtu mwingine ambae angekuwa chanzo kama ambavyo wewe umekua(kwa maana wewe si mtu wa kwanza na wa mwisho kuwa na connection au roho ya upendo wa namna hii).

Tengeneza msingi wa maisha yako, kwasababu wewe pekee ndio mwenye uwezo wa kutengeneza maisha yako na wala hakuna mbadala wa wewe.

Kwahiyo ukisoma kwa umakini na Kutafakari hapa, utagundua ya kwamba ndani ya chanzo kuna msingi, na msingi mmoja unaweza ukatengeneza vyanzo mbalimbali (usichanganyikiwe sasa na wewe, ili uelewe hapo rudi mwanzo mwa andiko nilikwambia msingi ndio hutengeza complex things na ili uweze kuondoa ucomplex ni lazima uanze kuyagawa mambo hayo kwenye namna fulani rahisi ili uufikie msingi wake).

Ndio maana mtu akifariki huwa wale watu wanaomfahamu wanapopata taarifa huwa wanauliza chanzo cha kifo chake ni nini, kwa maana wanajua kifo kinaweza kusababishwa na mambo mengi ya msingi ambayo ndio huweza kuunda chanzo.

Kwahiyo kama haujui msingi wa jambo fulani huwezi kusolve puzzle yake, na hapa duniani mambo mengi yapo kwenye puzzle na puzzle ni muunganiko wa mambo mbalimbali ya msingi na ili uweze kusolve puzzle nyingi za kilimwengu lazima uuelewe vizuri msingi wake ni nini.

So, kama Mungu ndio chanzo cha uhai basi hii tayari inakua ni complex puzzle kwa maana iko na vyanzo vingi hadi kufikia ule msingi wake na ili tuweze kuisolve lazima tuujue msingi wake ni upi.

Je, msingi wa uhai ni nini?

NITARUDI.
Uhai ni energy.kila kitu ni energy...vyote ni hai kwa mungu kufa ni kitu feki
 
Swali zuri kajifunza energy ni nini na sifa yake ...hapo utajua siri ya mungu ni nini na kaumba vitu vyote kwa mbinu gani?
Ni wapi kwa kwenda kujifunzia? Lakini pia hata kama unachosema ni kweli why huyo Mungu asionekane kama ndio msingi na badala yake yeye huonekana kama chanzo tu?
 
Chanzo halisi ni linear yaani kinakwenda mbele tu not cyclic,yaani ni umilele not kifo na hakina mwanzo maana hata mwanzo uliumbwa pia.
 
Ni wapi kwa kwenda kujifunzia? Lakini pia hata kama unachosema ni kweli why huyo Mungu asionekane kama ndio msingi na badala yake yeye huonekana kama chanzo tu?
Vitu vyote vipo ndani ya mungu vimeumba ndani yake...tupo ndani ya Mungu...sasa unataka kuona msingi gani tena
 
Msingi wa uhai ni Mungu mwenyewe na ndo maana hakuna mtu yeyote au kitu chochote kinaweza kutoa uhai

Biblia inasema
Mungu alimuumba mwanadamu kwa udogo kisha akampulizia pumzi ya uhai mwanadamu akawa hai
 
Back
Top Bottom