Kama chanzo cha uhai kinaweza kubadilika basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti hadi sasa. Je, ni upi msingi wa uhai?

Kama chanzo cha uhai kinaweza kubadilika basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti hadi sasa. Je, ni upi msingi wa uhai?

"Muktadha huo" ni muktadha gani?

Hutakiwi kuongelea kitu cha msingi kama chanzo kwa kutumia kitu derivative.

Habari ya chanzo si habari fundamental, inaweza kuwa na maana katika muktadha fulani tu.

Kwa hivyo, unapoongelea chanzo, ni lazima uweke muktadha.
Chanzo kinaingia kwenye muktadha wowote wa kilimwengu mkuu.

Na ikiwa tunazungumzia chanzo ndani ya ulimwengu wetu wa asili, basi lazima tukubali kuwa muda na causality vina nafasi.

Ila ikiwa tunatafuta chanzo absolute kisichotegemea muda wala causality, basi tunazungumzia kitu ambacho kiko nje ya upeo wa uelewa wetu wa kawaida.

Kwa hivyo, swali la kuwa, tunajadili chanzo cha nini na ndani ya mfumo gani? Litakua mjadala mzito kama utaendelea kubaki kwenye msimamo wako ila kwa muktadha wa kilimwengu huwezi kupingana na hoja iliyopo.
 
Ujaelewa alpha na omega ili neno.
Wewe sio elimu za kundalini sana kuhusu jicho la tatu.
 
Kwa nini ujadili msingi wa uhai ni nini, wakati hujui msingi wa msingi wa uhai ni nini?

Kwa sababu kuna vitu vipo lakini havina msingi.

Hata uhai na wenyewe hauna msingi.

Kuwa na chanzo si lazima kuwe na msingi.

Chanzo kinaweza kuwepo bila msingi.
Hii hoja yako ndio uijenge kwa kuelezea kwa kina kama ambavyo Mimi nimeelezea kwenye uzi, ya kwamba kwa namna gani jambo linaweza kuwa na chanzo pasipo kuwa na msingi?

Lakini pia hauwezi kujua msingi wa msingi wa uhai ni nini wakati vilivyopo ni vyanzo, na wala tusingejadili msingi wa uhai kama vyanzo vyake visingezungumziwa.

Kwahiyo tupo hapa kwasababu tumekua tukiona vyanzo tu, na andiko limejikita hapo kwakuelezea chanzo na msingi na sababu za kwanini tujadili msingi wa uhai.
 
Chanzo kinaingia kwenye muktadha wowote wa kilimwengu mkuu.

Na ikiwa tunazungumzia chanzo ndani ya ulimwengu wetu wa asili, basi lazima tukubali kuwa muda na causality vina nafasi.

Ila ikiwa tunatafuta chanzo absolute kisichotegemea muda wala causality, basi tunazungumzia kitu ambacho kiko nje ya upeo wa uelewa wetu wa kawaida.

Kwa hivyo, swali la kuwa, tunajadili chanzo cha nini na ndani ya mfumo gani? Litakua mjadala mzito kama utaendelea kubaki kwenye msimamo wako ila kwa muktadha wa kilimwengu huwezi kupingana na hoja iliyopo.
Unajuaje chanzo kinaingia kwenye muktadha wowote wa ulimwengu?

Katika muktadha wa ulimwengu ambao hauna chanzo, ni cyclic, there is cause A, which has effect B, but also the effect B is the cause of the cause A, hapo kati ya A na B chanzo ni nini?
 
Bila shaka mko salama waungwana...

Kikawaida neno msingi na chanzo ni maneno mawili ambayo ukiangalia kwa jicho la kawaida ni kama yanafanana hivi lakini ni maneno yaliyo na utofauti mkubwa.

Kwa maana chanzo huwa kinatengeneza muendelezo usio na ukomo lakini msingi huwa unatengeneza muendelezo mgumu ambao huwa haueleweki pasipo kurudi tena kwenye msingi kwa maana nyingine ni kwamba msingi ndio unaounda vyanzo mbalimbali.

Ndio maana mkusanyiko wa vyanzo vingi vya habari fulani unaweza kuleta mkanganyiko wa mambo hasa inapotokea vyanzo vyote vinaongelea habari moja ila vinatofautiana katika taarifa zao, hii hufanya mtu ashindwe kuelewa aamini chanzo kipi kati ya hivyo, na ili kuondoa huu mkanganyiko basi mtu hupaswa arudi kwenye msingi wa habari yenyewe na baada ya kufanya hivyo basi ni rahisi kujua kati ya vyanzo hivyo ni kipi na kipi kimeandika habari kwa kuzingatia msingi wake.

Kwahiyo kuna nyakati neno chanzo hutumika zaidi kwenye mambo ambayo msingi wake haujulikani au uhakika wa moja kwa moja juu ya msingi wake haupo lakini msingi ndio ambao unabeba chanzo.

Lakini pia chanzo wakati fulani huwa kinakua na mbadala wake wakati msingi huwa hauna mbadala (ndio maana habari unaweza kuipata jamiiforum, milard ayo na media zingine ila msingi wa habari hiyo hauwezi kubadilika).

Kwamfano wewe ni chanzo cha watoto wako kuzaliwa na wao ni chanzo cha wajukuu zako kuzaliwa lakini pia wajukuu zako ni chanzo cha vitukuu kuzaliwa na hii itaendelea namna hii bila ukomo na wewe hujawa msingi kwasababu nyuma yako alikuwepo baba yako ambae alikua chanzo cha wewe kuzaliwa ila pia Kabla ya baba yako alikuwepo babu yako ambae yeye alikua chanzo cha baba yako kuzaliwa na hii itarudi nyuma katika umbali usio julikana na ndio maana tumetumia neno chanzo.

Lakini pia mtu ni roho, na kama hii ndio basi hizo roho ambazo wewe umezileta hapa duniani haimaanishi kwamba wewe ndio mtu pekee ambae unao uwezo wa kuleta roho hizo isipokua wewe uliwin tu kwenye ile probability ila usingezileta wewe basi angekuwepo mtu mwingine ambae angeweza kuzileta, na vivyo hivyo wewe kwa baba yako na baba yako kwa babu yako na kadhalika.

Kwahiyo neno chanzo linapotumika katika eneo lolote ujue tayari kuna hali isiyo na ukomo imetengenezwa kwa kwenda mbele au kwa kurudi nyuma kwa maana ule msingi kamili wa jambo hilo haujulikani au kuna namna mbadala ya jambo hilo kwenye kutokea kwake au kufanyika kwake ukiachana na namna hiyo ambayo imetumika.

Okay, wacha twende mbali kidogo, watu husema Mungu ni chanzo cha uhai, hii tayari ni sentensi ambayo haina ukomo, kwa kurudi nyuma au kwenda mbele, lakini pia kwa kusema hivi unamaanisha asingekua yeye basi chanzo cha uhai kingeweza kupatikana kwa namna nyingine.

Angalia hii, wewe ni chanzo cha mkeo kuolewa au tuseme ni chanzo cha ndoa yenu ila sio msingi wa hiyo ndoa kwa maana hata kama wewe usingemuoa basi angeweza kuolewa na mtu mwingine, na huyo mtu mwingine nae angekua tu chanzo ila wala sio msingi kwa maana huyo mtu mwingine asingemuoa basi angeolewa na mtu mwingine tena, kwahiyo hii unaona inakua ni infinity loop.

Kwahiyo kama Mungu ni chanzo cha uhai basi msingi wa uhai bado haujulikani na ukomo wa uhai huo huo haujulikani pia (naomba usome ukiwa katika utulivu wa akili ili unielewe vizuri hapa).

Hii inamaanisha nini? Hii inamaanisha kwamba ni eidha Mungu ni neno moja linalotumika kuwakilisha jamii ya viumbe fulani kama vile neno binadamu linavyotumika kutuwakilisha Mimi na wewe au ukiachana na Mungu basi kuna viumbe vingine venye uwezo wa kutoa uhai (wacha tusonge taratibu huku tukiongeza tafakuri juu ya tafakuri hapa).

Kama Mungu ni kiwakilishi cha jamii ya viumbe fulani kama lilivyo neno binadamu basi neno la tumfanye mtu kwa mfano wetu halitakua na maana yoyote iliyojificha zaidi ya lilivyo na limekuwepo pale kama uthibitisho wa kwamba Mungu ni neno la jumla linalowakilisha jamii fulani kama ilivyo kwa neno binadamu.

Na kwa uthibitisho zaidi wa jambo hili ni pale Mungu anaposema aabudiwe yeye na wala sio miungu mingine, hii inamaana anajua ya kwamba katika jamii ya kimungu hayupo peke yake.

Ni sawa na wewe utengeneze robot lako ikiwa wewe ndio mkuu wa mradi licha ya kwamba ndani yake kutakua na ma-engineer wengine ambao ni binadamu na ghafla ukaanza kuona yule robot anaanza kuwatii watu wengine kuliko wewe mkuu wa kitengo lazima urudi umwambie unaefaa kunyenyekewa ni wewe na wala sio binadamu wengine.

Kama hiyo haitoshi lakini pia kuna maeneo kadhaa Mungu alijitokeza kwa kujitambulisha ya kwamba yeye ni Mungu wa vita mara Mungu wa maarifa na kadhalika, hii sio bahati mbaya na wala huna haja ya kuilazimisha ikae kwa namna tofauti na hiyo kwa maana hivyo ndivyo ilivyo na hii inaweza kuthibitisha kwamba Mungu ni sawa na kusema binadamu (yote ni maneno yanayowakilisha jamii ya viumbe fulani).

Na kwa hoja hiyo sasa, ndio maana ukisema Mungu ni chanzo cha uhai inamaana si Mungu wote ambao walishiriki kwenye mradi wa kumpa uhai binadamu ila ni jopo tu la Mungu kadhaa ndio ambao walifanya hii project na ndio maana neno chanzo limetumika kwa maana ya kwamba kama hao waliokaa wasingekaa basi Mungu wengine wangeweza kukaa na kumpa uhai binadamu kama wangeamua kufanya hivyo.

Lakini kama tukiendelea kubaki na msimamo wetu wa kwamba Mungu ni mmoja na wala sio jamii ya viumbe fulani basi hapa tunaweza kuibua hoja mpya ya kwamba kumbe ukiachana na Mungu katika puzzle hii pia kunao uwezekano wa kuwepo jamii fulani ya viumbe wenye uwezo wa kutengeneza watu au kumpa mtu uhai, na kama kweli chanzo cha uhai kinaweza kubadilika kinamna hii basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti.

Na hii ndio sababu ya neno chanzo kutumika badala ya neno msingi.

Najua kuna mtu hapa anaweza asielewe ila kama unataka uelewe zaidi unaweza Kutafakari kwa kina juu ya neno chanzo na msingi kisha ukishapata point urudi usome tena hili andiko.

Kwa mfano huwa tunasema chanzo cha mapato wala sio msingi wa mapato kwa maana kuna njia nyingi ambazo mtu anaweza akazitumia ili zimuingizie mapato.

Chanzo cha furaha yangu ni wewe, kwa maana usipokua wewe basi anaweza akawa mtu mwingine ambae anaweza akanipa hii furaha unayo nipa kwakua duniani binadamu haupo peke yako.

Chanzo cha Mimi kupata kazi ni wewe, hii inamaanisha hata usingekua wewe ningepata kazi kwa maana nisingekutana na wewe basi ningekutana na mtu mwingine ambae angekuwa chanzo kama ambavyo wewe umekua(kwa maana wewe si mtu wa kwanza na wa mwisho kuwa na connection au roho ya upendo wa namna hii).

Tengeneza msingi wa maisha yako, kwasababu wewe pekee ndio mwenye uwezo wa kutengeneza maisha yako na wala hakuna mbadala wa wewe.

Kwahiyo ukisoma kwa umakini na Kutafakari hapa, utagundua ya kwamba ndani ya chanzo kuna msingi, na msingi mmoja unaweza ukatengeneza vyanzo mbalimbali (usichanganyikiwe sasa na wewe, ili uelewe hapo rudi mwanzo mwa andiko nilikwambia msingi ndio hutengeza complex things na ili uweze kuondoa ucomplex ni lazima uanze kuyagawa mambo hayo kwenye namna fulani rahisi ili uufikie msingi wake).

Ndio maana mtu akifariki huwa wale watu wanaomfahamu wanapopata taarifa huwa wanauliza chanzo cha kifo chake ni nini, kwa maana wanajua kifo kinaweza kusababishwa na mambo mengi ya msingi ambayo ndio huweza kuunda chanzo.

Kwahiyo kama haujui msingi wa jambo fulani huwezi kusolve puzzle yake, na hapa duniani mambo mengi yapo kwenye puzzle na puzzle ni muunganiko wa mambo mbalimbali ya msingi na ili uweze kusolve puzzle nyingi za kilimwengu lazima uuelewe vizuri msingi wake ni nini.

So, kama Mungu ndio chanzo cha uhai basi hii tayari inakua ni complex puzzle kwa maana iko na vyanzo vingi hadi kufikia ule msingi wake na ili tuweze kuisolve lazima tuujue msingi wake ni upi.

Je, msingi wa uhai ni nini?

NITARUDI.
Swali lako linagusa dhana za kina kuhusu maisha, fahamu, na ukweli wa kuwepo kwa uhai. Hebu tuchambue sehemu kuu:





1. Alpha na Omega





Hizi ni dhana za mwanzo na mwisho, zinazoashiria ukamilifu wa uwepo. Katika maandiko ya kidini na kifalsafa, “Alpha” inawakilisha chanzo, mwanzo wa kila kitu, na “Omega” ni mwisho wa kila kitu. Ikiwa tunahusisha na uhai, tunaweza kusema kuwa uhai una mwanzo (kuzaliwa) na mwisho (kufa), lakini je, kuna hali ya kudumu nje ya haya mawili?





2. Jicho la Tatu na Kundalini


• Jicho la Tatu linahusiana na fahamu ya juu, kuona ukweli wa mambo bila kutumia macho ya kawaida. Katika falsafa ya Kihindu, linahusishwa na tezi ya pineal, ambayo inadaiwa kuwa kituo cha kiroho na uwezo wa kuona zaidi ya ulimwengu wa kimwili.


• Kundalini ni nishati ya maisha inayodhaniwa kuwa inalala chini ya uti wa mgongo na inapowekwa huru kupitia mwamko wa kiroho, inaweza kuleta mabadiliko ya fahamu.





Ikiwa nishati ya kundalini ndiyo chanzo cha uhai, basi tunahoji: Je, nishati hii inaweza kubadilika? Ikiwa inawezekana kubadilika, basi inamaanisha kuwa hakuna msingi wa uhai ulio thabiti, kwani msingi wake unategemea hali zinazoweza kubadilika.





3. Je, Uhai Una Msingi Thabiti?


• Ikiwa uhai ni nishati inayobadilika, basi hauna msingi wa kudumu, lakini unategemea hali zinazobadilika.


• Ikiwa uhai una chanzo thabiti, basi tunahitaji kuelewa chanzo hicho—je, ni akili, nishati, au kitu kingine?





Katika falsafa na sayansi:


• Sayansi inasema uhai umetokana na michakato ya kibaolojia na kemikali.


• Falsafa ya Kiroho inasema uhai ni fahamu, nguvu ya kiungu, au nishati isiyokufa.
 
Hii hoja yako ndio uijenge kwa kuelezea kwa kina kama ambavyo Mimi nimeelezea kwenye uzi, ya kwamba kwa namna gani jambo linaweza kuwa na chanzo pasipo kuwa na msingi?
Kuna vitu vingi vipo, vinatokea vina chanzo lakini havina msingi.

Mfano ajali.

Ajali haina msingi wa kutokea, Bali ajali ina chanzo cha kutokea kwake. kama vile uzembe wa dereva, mwendokasi, ulevi, barabara mbovu n.k

Sasa unaona kwamba ajali ina chanzo, Lakini hakuna msingi wowote unaosababisha vyanzo mbalimbali vya ajali.
Lakini pia hauwezi kujua msingi wa msingi wa uhai ni nini wakati vilivyopo ni vyanzo, na wala tusingejadili msingi wa uhai kama vyanzo vyake visingezungumziwa.
Hakuna msingi wa kila kitu, ila kuna vyanzo mbalimbali vya kitu.

Hakuna msingi wa uhai, Kuna vyanzo vya uhai.
Kwahiyo tupo hapa kwasababu tumekua tukiona vyanzo tu, na andiko limejikita hapo kwakuelezea chanzo na msingi na sababu za kwanini tujadili msingi wa uhai.
Chanzo sio lazima kiwe na msingi.

Ndio maana hata Ajali husababishwa na vyanzo mbalimbali bila msingi wowote ule.
 
Kuna vitu vingi vipo, vinatokea vina chanzo lakini havina msingi.

Mfano ajali.

Ajali haina msingi wa kutokea, Bali ajali ina chanzo cha kutokea kwake. kama vile uzembe wa dereva, mwendokasi, ulevi, barabara mbovu n.k

Sasa unaona kwamba ajali ina chanzo, Lakini hakuna msingi wowote unaosababisha vyanzo mbalimbali vya ajali.

Hakuna msingi wa kila kitu, ila kuna vyanzo mbalimbali vya kitu.

Hakuna msingi wa uhai, Kuna vyanzo vya uhai.

Chanzo sio lazima kiwe na msingi.

Ndio maana hata Ajali husababishwa na vyanzo mbalimbali bila msingi wowote ule.
Nimesoma mwanzo mpaka mwisho wa andiko na maoni yake.
Nafurahi kuona watu wanauelewa mkubwa
 
Unajuaje chanzo kinaingia kwenye muktadha wowote wa ulimwengu?

Katika muktadha wa ulimwengu ambao hauna chanzo, ni cyclic, there is cause A, which has effect B, but also the effect B is the cause of the cause A, hapo kati ya A na B chanzo ni nini?
Hapa wewe unazungumzia chanzo katika dhana ya cyclic causality wakati Mimi mifano mingi niliyoitoa hapo juu imejikita kwenye linear causality.

Kwenye namna hizi mbili dhana ya chanzo huwa katika namna tofauti na kwakua umekiri umejikita huko nadhani ndio maana hatubaki kwenye eneo moja.

Swala la chanzo cha uhai limekaa kilinear na si cyclic ndio maana wewe utazaa mwanao na mwanao atazaa mjukuu wako na mjukuu wako atazaa kitukuu wako na kizazi hiki kinaendelea hivyo na wala hakuna siku itatokea hii loop ikarudi ilipoanzia kwa maana ya kwamba kwenye hiko kizazi hakuna mtu atarudi kukuzaa tena wewe na wewe ukarudi kuwazaa tena wale wale watoto wako, nao wakazaa tena wajukuu zako, na ingekua hivi basi kusingekua na haja ya kujadili hili swala.

Kwasababu mambo yangekua yanaenda na kujirudia, kwahiyo labda useme je hivi ndivyo ambavyo unahisi wewe ya kwamba chanzo cha uhai ni cyclic?
 
Nimesoma mwanzo mpaka mwisho wa andiko na maoni yake.
Nafurahi kuona watu wanauelewa mkubwa
Kuna vitu vingi vina chanzo lakini hutokea bila msingi wowote ule.

Kwa hiyo sikweli kwamba msingi ndio mwanzo wa chanzo, Kama mleta mada anavyodai.
 
Hapa wewe unazungumzia chanzo katika dhana ya cyclic causality wakati Mimi mifano mingi niliyoitoa hapo juu imejikita kwenye linear causality.

Kwenye namna hizi mbili dhana ya chanzo huwa katika namna tofauti na kwakua umekiri umejikita huko nadhani ndio maana hatubaki kwenye eneo moja.

Swala la chanzo cha uhai limekaa kilinear na si cyclic ndio maana wewe utazaa mwanao na mwanao atazaa mjukuu wako na mjukuu wako atazaa kitukuu wako na kizazi hiki kinaendelea hivyo na wala hakuna siku itatokea hii loop ikarudi ilipoanzia kwa maana ya kwamba kwenye hiko kizazi hakuna mtu atarudi kukuzaa tena wewe na wewe ukarudi kuwazaa tena wale wale watoto wako, nao wakazaa tena wajukuu zako, na ingekua hivi basi kusingekua na haja ya kujadili hili swala.

Kwasababu mambo yangekua yanaenda na kujirudia, kwahiyo labda useme je hivi ndivyo ambavyo unahisi wewe ya kwamba chanzo cha uhai ni cyclic?
Lakini si ulisema chanzo kinaingia kwenye muktadha wowote wa ulimwengu?
 
Samaleko ... Umenikumbusha Falsafa za Dkt Adolf Mihanjo.

Falsafa na usanifu na hoja!
 
Ajali haina msingi wa kutokea, Bali ajali ina chanzo cha kutokea kwake. kama vile uzembe wa dereva, mwendokasi, ulevi, barabara mbovu n.k

Swali lako linagusa dhana za kina kuhusu maisha, fahamu, na ukweli wa kuwepo kwa uhai. Hebu tuchambue sehemu kuu:





1. Alpha na Omega





Hizi ni dhana za mwanzo na mwisho, zinazoashiria ukamilifu wa uwepo. Katika maandiko ya kidini na kifalsafa, “Alpha” inawakilisha chanzo, mwanzo wa kila kitu, na “Omega” ni mwisho wa kila kitu. Ikiwa tunahusisha na uhai, tunaweza kusema kuwa uhai una mwanzo (kuzaliwa) na mwisho (kufa), lakini je, kuna hali ya kudumu nje ya haya mawili?





2. Jicho la Tatu na Kundalini


• Jicho la Tatu linahusiana na fahamu ya juu, kuona ukweli wa mambo bila kutumia macho ya kawaida. Katika falsafa ya Kihindu, linahusishwa na tezi ya pineal, ambayo inadaiwa kuwa kituo cha kiroho na uwezo wa kuona zaidi ya ulimwengu wa kimwili.


• Kundalini ni nishati ya maisha inayodhaniwa kuwa inalala chini ya uti wa mgongo na inapowekwa huru kupitia mwamko wa kiroho, inaweza kuleta mabadiliko ya fahamu.





Ikiwa nishati ya kundalini ndiyo chanzo cha uhai, basi tunahoji: Je, nishati hii inaweza kubadilika? Ikiwa inawezekana kubadilika, basi inamaanisha kuwa hakuna msingi wa uhai ulio thabiti, kwani msingi wake unategemea hali zinazoweza kubadilika.





3. Je, Uhai Una Msingi Thabiti?


• Ikiwa uhai ni nishati inayobadilika, basi hauna msingi wa kudumu, lakini unategemea hali zinazobadilika.


• Ikiwa uhai una chanzo thabiti, basi tunahitaji kuelewa chanzo hicho—je, ni akili, nishati, au kitu kingine?





Katika falsafa na sayansi:


• Sayansi inasema uhai umetokana na michakato ya kibaolojia na kemikali.


• Falsafa ya Kiroho inasema uhai ni fahamu, nguvu ya kiungu, au nishati isiyokufa.
Umejikita zaidi kwenye dhana ila haujaja kwenye mada halisi bado, isipokua umezidi kutengeneza puzzle juu ya puzzle na kuendelea kutupatia maswali yanayoendelea kuengeza uwanda mpana wa kuendelea kujadili.
 
Umejikita zaidi kwenye dhana ila haujaja kwenye mada halisi bado, isipokua umezidi kutengeneza puzzle juu ya puzzle na kuendelea kutupatia maswali yanayoendelea kuengeza uwanda mpana wa kuendelea kujadili.
Sio mzuri wa kuhandika ila elimu hii labda kama unataka kuelezewa kwa sauti.
Hata sayansi uwezi kuelewa unavyo tumia mfano hii teknolojia
 
Kuna vitu vingi vipo, vinatokea vina chanzo lakini havina msingi.

Mfano ajali.

Ajali haina msingi wa kutokea, Bali ajali ina chanzo cha kutokea kwake. kama vile uzembe wa dereva, mwendokasi, ulevi, barabara mbovu n.k

Sasa unaona kwamba ajali ina chanzo, Lakini hakuna msingi wowote unaosababisha vyanzo mbalimbali vya ajali.

Hakuna msingi wa kila kitu, ila kuna vyanzo mbalimbali vya kitu.

Hakuna msingi wa uhai, Kuna vyanzo vya uhai.

Chanzo sio lazima kiwe na msingi.

Ndio maana hata Ajali husababishwa na vyanzo mbalimbali bila msingi wowote ule.
Swala la ajali limenifanya nifikirie upya ila linaonekana linaweza kuingia kwenye mafungu yote kutokana na namna utakavyolichukulia, na hii ndio hufanya hii loop iendelee kurudi nyuma kuanzia hapo ilipo au kwenda mbele kutokea hapo ilipo.

Na kutokana na sababu hii basi pengine inapaswa turudi kwenye hoja ya Kiranga na tujiulize swali kwamba chanzo ni cyclic or linear?

Lakini kwa muktadha wa uhai tunapata jibu ya kwamba chanzo ni linear na kama ndivyo basi kwa kurudi nyuma tunaweza kukutana na msingi wake, sasa ni umbali kiasi gani tunapaswa kurudi hili ndio swali ambalo hufanya watu wengi wajipe majibu mepesi ya kurahisisha mambo ili kuepuka kuumiza kichwa kuendelea kuwaza zaidi.
 
Umejikita zaidi kwenye dhana ila haujaja kwenye mada halisi bado, isipokua umezidi kutengeneza puzzle juu ya puzzle na kuendelea kutupatia maswali yanayoendelea kuengeza uwanda mpana wa kuendelea kujadili.
Hatuwezi kujua tusivyo vijua ila tunaendelea kupunguza tusivyo vijua kwa utafiti, uchunguzi, udadisi na majaribio zaidi.

We cannot solve the ultimate mysteries of nature because we ourselves are the part of the mysteries we are trying to solve.
 
Lakini si ulisema chanzo kinaingia kwenye muktadha wowote wa ulimwengu?
Kwenye muktadha wowote ila katika Kila muktadha kuna namna ya kukielezea kulingana na hali ya jambo lenyewe.
 
Hatuwezi kujua tusivyo vijua ila tunaendelea kupunguza tusivyo vijua kwa utafiti, uchunguzi, udadisi na majaribio zaidi.

We cannot solve the ultimate mysteries of nature because we ourselves are the part of the mysteries we are trying to solve.
Hapa unajibana mkuu na kujipa excuse ya kurudi nyuma katika kuyafikira mambo.
 
Back
Top Bottom