Kama chanzo cha uhai kinaweza kubadilika basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti hadi sasa. Je, ni upi msingi wa uhai?

Kama chanzo cha uhai kinaweza kubadilika basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti hadi sasa. Je, ni upi msingi wa uhai?

Hili andiko nimeliandika baada ya kuona hilo neno chanzo limetumika kwenye maandiko almost yote badala ya neno msingi na ndio maana ukilisoma hili andiko utaona limekaa sana kwenye muktadha wa kidini kuliko wa kisayansi ila pia dhima hii hii tukiirudisha upande huo wa kisayansi lazima kuna pahala tutafika na kustack.

Kwahiyo ili tuweze kuchanganya mawazo labda tungeweza kulijibu hili swali kwa mtindo wa kukosoana kwa hoja ili pande zote mbili ziingie labda ndani ya hoja hizo tunaweza kupata pahala pa kuanzia kwenda kuujua ukweli halisi wa jambo hili.
Dhana nzima ya "chanzo" si ya msingi wala ukweli. Ni dhana ya kufikirika na ina maana katika muktadha fulani tu.

Kimsingi chanzo kinategemea chronology, time, cause and effect.

These things are not real. They are not absolute.

Time is relative. One has to only read Einstein's Relativity to know that.

Cause and effect are not always synchronous, one has to only read quantum physics to know that.

If you can travel at the speed of light in a vacuum, the flow of time ceases to exist. In fact, from the perspective of a ray of light in a vacuum, the flow of time does not exist.

Everything, the past, the present, the future, happens at once.

So in reality, time appears to pass because of our position in the universe, because of the fact that we do not move as fast as light in a vacuum.

So time is not absolute, it is an illusion that appears because of the increasing entropy of the universe due to the second law of thermodynamics.

So, if time is not real, chanzo, which depends on causality and time, is also not real.

We can only speak of "chanzo" in relative terms. Not in absolute terms.
 
Mkuu Mimi naamini uwepo wa mamlaka yenye nguvu kuliko sisi, kwahiyo mtu yeyote ambae anaamini uwepo wa hiyo mamlaka bila kujali yuko upande gani Mimi nafungamana nae, iwe wa msikitini, wa kanisani, kilingeni na kadhalika😅😅😅
Kwa hiyo huna dini maalum?
Na mamlaka yenye nguvu kuliko sisi ni yapi hayo?
 
Nijibu swali la Msingi wa Uhai wako.....

Kwa Ufupi kwa mujibu na macho ya nature (Uhai wako ni wewe kutumia nishati unenepe, ili uwe chakula cha Specie nyingine) in short wewe ni part ya recycle ya Nishati, Kufa kwako au kuondoka kwako (hata specie kwa ujumla wake) kutakuwa hakuna massive effect ya viumbe vingine; Ukizingatia wewe Binadamu ni Kama Kirusi tu kwa viumbe wengine (The most destructive Specie) Case in Point kipindi cha lock down kuna viumbe vilishangilia sana na kujinafasi...


View: https://youtu.be/1E_vdNiTlgg?si=vUUUyvQtojs-wWlM

Ili kiumbe kiweze kutumia hiyo nishati inapaswa kiwe hai kwanza,. Si ndiyo? sasa ingekua vizuri kwanza utuambie msingi wa uhai ni nini?
 
Kwahiyo hii point yako inakubaliana na Mimi ya kwamba Mungu ni neno la jumla kama ambavyo neno binadamu lilivyo sio
Ndio ila lazima awe ni mmoja sio kundi sababu ikiwa ni kundi ina maana kuna mwingine aliumba viumbe wengine na sifa moja kubwa ya uungu ni miliki hivyo lazima kungekuwa na vita ya miungu na viumbe wake ili kuwe na mungu mmoja anaye miliki ulimwengu
 
Amini kwamba yuko MUNGU ambaye ni chanzo cha dunia, ulimwengu,viumbe, na vyote vijazavyo ulimwengu.
Ni wazo zuri kufikiria tulitokea wapi na msingi wa chanzo cha yote ni nini. Lakini licha ya brain complexity yetu na intelligence bado hatutapata jibu kamwe, na kama tukijaribu tutaishia kujitengenezea nadharia ambazo hazipo.

Kwa imani (naamini usitake nithibitishe maana ni imani huenda unaamini tofauti)
Kumb 29:29
Yaliyofunuliwa kwa mwanadamu ni ya mwanadamu yaliyofichwa ni ya Mungu

Aliposema tumfanye mtu kwa mfano wetu, huenda (naamini tena) alimaanisha viumbe waliopo mbinguni kama wazee 12, wenye uhai wanne, malaika, ama viumbe wengineo walioumbwa kabla yetu.

Mtu chanzo chake cha uhai ni Mungu, aliumba kiumbe kisicho na uhai (udongo) kikabadilishwa kuwa na nyama(flesh),damu,mishipa,mifupa na misuli lakini hakikumilika mpaka pumzi ya uhai(sio oxygen) akawa mtu kamili. Chanzo cha mtu wa pili Hawa hakikuhitaji kuanza upya maana msingi tayari upo Adam.
Mungu hana chanzo(naamini) hana mwanzo wala mwisho
 
Ili kiumbe kiweze kutumia hiyo nishati inapaswa kiwe hai kwanza,. Si ndiyo? sasa ingekua vizuri kwanza utuambie msingi wa uhai ni nini?
Kwa kutumia theories zipi (sababu nadhani theories zipo za kutosha tafuta) ingawa kuna zina za imani na zile ambazo they are known to be factual..., Uhai wa kitu chochote ni favorable conditions ndio maana kuna species zilikuwepo kabla sasa hivi hazipo na kuna nyingine ambazo hatukujua kwamba hazipo sasa hivi zipo....

Mfano huu nautumia kila siku chukua chupa (ondoa kila kitu kwa macho yako ambapo wewe utadhani ni utupu) ingawa sababu kuna space hapo hakuna nothingness, baada ya siku kadhaa with favorable conditions utakuta life forms..., sasa as far as ecosystem is concerned hayo ni kama mashamba unapanda chakula ili kiliwe na ukitaka nikwambie mwisho wa uhai as we know it (current species ambazo zinategemea Nishati ya Jua) ni pale fuel ya jua itakavyokwisha na hata kama ule mlipuko au aftremath haitatuua basi sababu our main Source of Energy will have died na sisi tutafuatia watakaobaki ni some species which can adapt....

Nadhani hapo nimeanzia mbele ili mwenyewe uweze kurudi nyuma na kugundua kwamba uhai / viumbe ni happenstances....
 
Mwanzo 3:22 Bwana Mungu akasema:huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu.
hili fungu huwa nalitafakari sana hata jana usiku
cha ajabu leo nakutana na huu uzi
 
Bila shaka mko salama waungwana...

Kikawaida neno msingi na chanzo ni maneno mawili ambayo ukiangalia kwa jicho la kawaida ni kama yanafanana hivi lakini ni maneno yaliyo na utofauti mkubwa.

Kwa maana chanzo huwa kinatengeneza muendelezo usio na ukomo lakini msingi huwa unatengeneza muendelezo mgumu ambao huwa haueleweki pasipo kurudi tena kwenye msingi kwa maana nyingine ni kwamba msingi ndio unaounda vyanzo mbalimbali.

Ndio maana mkusanyiko wa vyanzo vingi vya habari fulani unaweza kuleta mkanganyiko wa mambo hasa inapotokea vyanzo vyote vinaongelea habari moja ila vinatofautiana katika taarifa zao, hii hufanya mtu ashindwe kuelewa aamini chanzo kipi kati ya hivyo, na ili kuondoa huu mkanganyiko basi mtu hupaswa arudi kwenye msingi wa habari yenyewe na baada ya kufanya hivyo basi ni rahisi kujua kati ya vyanzo hivyo ni kipi na kipi kimeandika habari kwa kuzingatia msingi wake.

Kwahiyo kuna nyakati neno chanzo hutumika zaidi kwenye mambo ambayo msingi wake haujulikani au uhakika wa moja kwa moja juu ya msingi wake haupo lakini msingi ndio ambao unabeba chanzo.

Lakini pia chanzo wakati fulani huwa kinakua na mbadala wake wakati msingi huwa hauna mbadala (ndio maana habari unaweza kuipata jamiiforum, milard ayo na media zingine ila msingi wa habari hiyo hauwezi kubadilika).

Kwamfano wewe ni chanzo cha watoto wako kuzaliwa na wao ni chanzo cha wajukuu zako kuzaliwa lakini pia wajukuu zako ni chanzo cha vitukuu kuzaliwa na hii itaendelea namna hii bila ukomo na wewe hujawa msingi kwasababu nyuma yako alikuwepo baba yako ambae alikua chanzo cha wewe kuzaliwa ila pia Kabla ya baba yako alikuwepo babu yako ambae yeye alikua chanzo cha baba yako kuzaliwa na hii itarudi nyuma katika umbali usio julikana na ndio maana tumetumia neno chanzo.

Lakini pia mtu ni roho, na kama hii ndio basi hizo roho ambazo wewe umezileta hapa duniani haimaanishi kwamba wewe ndio mtu pekee ambae unao uwezo wa kuleta roho hizo isipokua wewe uliwin tu kwenye ile probability ila usingezileta wewe basi angekuwepo mtu mwingine ambae angeweza kuzileta, na vivyo hivyo wewe kwa baba yako na baba yako kwa babu yako na kadhalika.

Kwahiyo neno chanzo linapotumika katika eneo lolote ujue tayari kuna hali isiyo na ukomo imetengenezwa kwa kwenda mbele au kwa kurudi nyuma kwa maana ule msingi kamili wa jambo hilo haujulikani au kuna namna mbadala ya jambo hilo kwenye kutokea kwake au kufanyika kwake ukiachana na namna hiyo ambayo imetumika.

Okay, wacha twende mbali kidogo, watu husema Mungu ni chanzo cha uhai, hii tayari ni sentensi ambayo haina ukomo, kwa kurudi nyuma au kwenda mbele, lakini pia kwa kusema hivi unamaanisha asingekua yeye basi chanzo cha uhai kingeweza kupatikana kwa namna nyingine.

Angalia hii, wewe ni chanzo cha mkeo kuolewa au tuseme ni chanzo cha ndoa yenu ila sio msingi wa hiyo ndoa kwa maana hata kama wewe usingemuoa basi angeweza kuolewa na mtu mwingine, na huyo mtu mwingine nae angekua tu chanzo ila wala sio msingi kwa maana huyo mtu mwingine asingemuoa basi angeolewa na mtu mwingine tena, kwahiyo hii unaona inakua ni infinity loop.

Kwahiyo kama Mungu ni chanzo cha uhai basi msingi wa uhai bado haujulikani na ukomo wa uhai huo huo haujulikani pia (naomba usome ukiwa katika utulivu wa akili ili unielewe vizuri hapa).

Hii inamaanisha nini? Hii inamaanisha kwamba ni eidha Mungu ni neno moja linalotumika kuwakilisha jamii ya viumbe fulani kama vile neno binadamu linavyotumika kutuwakilisha Mimi na wewe au ukiachana na Mungu basi kuna viumbe vingine venye uwezo wa kutoa uhai (wacha tusonge taratibu huku tukiongeza tafakuri juu ya tafakuri hapa).

Kama Mungu ni kiwakilishi cha jamii ya viumbe fulani kama lilivyo neno binadamu basi neno la tumfanye mtu kwa mfano wetu halitakua na maana yoyote iliyojificha zaidi ya lilivyo na limekuwepo pale kama uthibitisho wa kwamba Mungu ni neno la jumla linalowakilisha jamii fulani kama ilivyo kwa neno binadamu.

Na kwa uthibitisho zaidi wa jambo hili ni pale Mungu anaposema aabudiwe yeye na wala sio miungu mingine, hii inamaana anajua ya kwamba katika jamii ya kimungu hayupo peke yake.

Ni sawa na wewe utengeneze robot lako ikiwa wewe ndio mkuu wa mradi licha ya kwamba ndani yake kutakua na ma-engineer wengine ambao ni binadamu na ghafla ukaanza kuona yule robot anaanza kuwatii watu wengine kuliko wewe mkuu wa kitengo lazima urudi umwambie unaefaa kunyenyekewa ni wewe na wala sio binadamu wengine.

Kama hiyo haitoshi lakini pia kuna maeneo kadhaa Mungu alijitokeza kwa kujitambulisha ya kwamba yeye ni Mungu wa vita mara Mungu wa maarifa na kadhalika, hii sio bahati mbaya na wala huna haja ya kuilazimisha ikae kwa namna tofauti na hiyo kwa maana hivyo ndivyo ilivyo na hii inaweza kuthibitisha kwamba Mungu ni sawa na kusema binadamu (yote ni maneno yanayowakilisha jamii ya viumbe fulani).

Na kwa hoja hiyo sasa, ndio maana ukisema Mungu ni chanzo cha uhai inamaana si Mungu wote ambao walishiriki kwenye mradi wa kumpa uhai binadamu ila ni jopo tu la Mungu kadhaa ndio ambao walifanya hii project na ndio maana neno chanzo limetumika kwa maana ya kwamba kama hao waliokaa wasingekaa basi Mungu wengine wangeweza kukaa na kumpa uhai binadamu kama wangeamua kufanya hivyo.

Lakini kama tukiendelea kubaki na msimamo wetu wa kwamba Mungu ni mmoja na wala sio jamii ya viumbe fulani basi hapa tunaweza kuibua hoja mpya ya kwamba kumbe ukiachana na Mungu katika puzzle hii pia kunao uwezekano wa kuwepo jamii fulani ya viumbe wenye uwezo wa kutengeneza watu au kumpa mtu uhai, na kama kweli chanzo cha uhai kinaweza kubadilika kinamna hii basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti.

Na hii ndio sababu ya neno chanzo kutumika badala ya neno msingi.

Najua kuna mtu hapa anaweza asielewe ila kama unataka uelewe zaidi unaweza Kutafakari kwa kina juu ya neno chanzo na msingi kisha ukishapata point urudi usome tena hili andiko.

Kwa mfano huwa tunasema chanzo cha mapato wala sio msingi wa mapato kwa maana kuna njia nyingi ambazo mtu anaweza akazitumia ili zimuingizie mapato.

Chanzo cha furaha yangu ni wewe, kwa maana usipokua wewe basi anaweza akawa mtu mwingine ambae anaweza akanipa hii furaha unayo nipa kwakua duniani binadamu haupo peke yako.

Chanzo cha Mimi kupata kazi ni wewe, hii inamaanisha hata usingekua wewe ningepata kazi kwa maana nisingekutana na wewe basi ningekutana na mtu mwingine ambae angekuwa chanzo kama ambavyo wewe umekua(kwa maana wewe si mtu wa kwanza na wa mwisho kuwa na connection au roho ya upendo wa namna hii).

Tengeneza msingi wa maisha yako, kwasababu wewe pekee ndio mwenye uwezo wa kutengeneza maisha yako na wala hakuna mbadala wa wewe.

Kwahiyo ukisoma kwa umakini na Kutafakari hapa, utagundua ya kwamba ndani ya chanzo kuna msingi, na msingi mmoja unaweza ukatengeneza vyanzo mbalimbali (usichanganyikiwe sasa na wewe, ili uelewe hapo rudi mwanzo mwa andiko nilikwambia msingi ndio hutengeza complex things na ili uweze kuondoa ucomplex ni lazima uanze kuyagawa mambo hayo kwenye namna fulani rahisi ili uufikie msingi wake).

Ndio maana mtu akifariki huwa wale watu wanaomfahamu wanapopata taarifa huwa wanauliza chanzo cha kifo chake ni nini, kwa maana wanajua kifo kinaweza kusababishwa na mambo mengi ya msingi ambayo ndio huweza kuunda chanzo.

Kwahiyo kama haujui msingi wa jambo fulani huwezi kusolve puzzle yake, na hapa duniani mambo mengi yapo kwenye puzzle na puzzle ni muunganiko wa mambo mbalimbali ya msingi na ili uweze kusolve puzzle nyingi za kilimwengu lazima uuelewe vizuri msingi wake ni nini.

So, kama Mungu ndio chanzo cha uhai basi hii tayari inakua ni complex puzzle kwa maana iko na vyanzo vingi hadi kufikia ule msingi wake na ili tuweze kuisolve lazima tuujue msingi wake ni upi.

Je, msingi wa uhai ni nini?

NITARUDI.
Nimesoma na kurudia tena. Ngoja nikujibu kwa mtindo huu nafikiri itakusaidia na wewe.

Niliwahi kumuuliza Mwalimu wangu swali, "Sir hivi unaamini uwepo wa freemasons na ni kweli wana nguvu?".

Majibu ya teacher " rafiki yangu, muda wa kutafuta ukweli juu ya swali lako ni vyema ukautumia kuendelea kusoma Aya/sura za kitabu chako kitakatifu unachokiamini, (akimaanisha Bible au Quran) hio itakujenga zaidi."

Jibu la teacher wangu, naomba nikupatie na wewe japo wewe hauhoji kuhusu freemasons though somehow unachokihoji ndio point zao kudhohofisha uhalali wa nguvu za huyu tunaemuita na kuamini ni Mungu.

Mwandishi Una IQ kubwa kwa namna umestructure content ya Uzi wako. Naamini ukielekeza IQ hio katika Imani utapata majibu sahihi kabisa.

Huko utafanya tafakari more spiritually na huenda sikumoja ukaanda andiko kutujibu swali lako la chanzo na Msingi kwa mlengo wa kiimani zaidi.
 
Time is relative. One has to only read Einstein's Relativity to know that.
Sagittarius would tell you that Time is absolute. And I always stand with Sagittarius.

Time is absolute not relative. It's just Albert Einstein didn't understand how to master the art of timing.
 
Sagittarius would tell you that Time is absolute. And I always stand with Sagittarius.

Time is absolute not relative. It's just Albert Einstein didn't understand how to master the art of timing.
What is Sagittarius?

Do you understand what is Einstein's Relativity?
 
Kwa kutumia theories zipi (sababu nadhani theories zipo za kutosha tafuta) ingawa kuna zina za imani na zile ambazo they are known to be factual..., Uhai wa kitu chochote ni favorable conditions ndio maana kuna species zilikuwepo kabla sasa hivi hazipo na kuna nyingine ambazo hatukujua kwamba hazipo sasa hivi zipo....

Mfano huu nautumia kila siku chukua chupa (ondoa kila kitu kwa macho yako ambapo wewe utadhani ni utupu) ingawa sababu kuna space hapo hakuna nothingness, baada ya siku kadhaa with favorable conditions utakuta life forms..., sasa as far as ecosystem is concerned hayo ni kama mashamba unapanda chakula ili kiliwe na ukitaka nikwambie mwisho wa uhai as we know it (current species ambazo zinategemea Nishati ya Jua) ni pale fuel ya jua itakavyokwisha na hata kama ule mlipuko au aftremath haitatuua basi sababu our main Source of Energy will have died na sisi tutafuatia watakaobaki ni some species who can adapt....

Nadhani hapo nimeanzia mbele ili mwenyewe uweze kurudi nyuma na kugundua kwamba uhai / viumbe ni happenstances....
Sawa twende taratibu,.. ulisema "uhai wako ni wewe kutumia nishati,...." nikakuuliza kwamba ili kiumbe kiweze kutumia nishati si inabidi kwanza kiwe na uhai? Je, huo uhai msingi wake ni nini before an organism consumes the energy? mbona kama nishati inapelekea uhai uendelee na sio kwamba ndiyo msingi wa uhai wenyewe?


NB: UKishasema theory maana yake hiyo si fact kama unavyosema,.. ni assumptions tu.
 
ulimwengu wa roho ni mpana sana na una mambo mengi sana
na haya yote yanayoendelea hapa duniani yote yanatoka huko
Sasa Inategemea na wewe unaleta nini huku
Na hiv vitabu vya kiimani vinatusaidia na vinatupa msingi wa kujua yaliyoko huko
Tuendelee kutafakari
 
Sawa twende taratibu,.. ulisema "uhai wako ni wewe kutumia nishati,...."
Nope nimesema wewe faida yako (kwa nature) ni kutumika kama nishati ya viumbe wengine
nikakuuliza kwamba ili kiumbe kiweze kutumia nishati si inabidi kwanza kiwe na uhai?
Nishati hio ndio huenda ni chanzo ya kiumbe hicho lets start na mbegu ukipanda kwenye favorable conditions inatumia chakula ilichotunza inakuwa kubwa na kuanza kunyonya nishati ya jua (na mwisho wa siku ni chakula cha wengine)

hata wewe ni muunganiko wa single cells (wanyama kwa ujumla) now ukiniambia hata hizo single cell zilitokea wapi ndio hapo nakuuliza does nothingness really exists ? To me that's a fundamental question....
Je, huo uhai msingi wake ni nini before an organism consumes the energy? mbona kama nishati inapelekea uhai uendelee na sio kwamba ndiyo msingi wa uhai wenyewe?
How did you come to that conclusion, leo hii ikitokea mlipuko fulani mkali tunajua kwamba we are all elements (humans are made up of chemical elements. The human body is made up of about 99% of six elements: oxygen, carbon, hydrogen, nitrogen, calcium, and phosphorus. The remaining 0.85% is made up of sulfur, potassium, sodium, chlorine, and magnesium. ) kwahio kama nishati hio ikipelekea formation ya kitu fulani ambacho sasa hivi hakipo huenda kukawa na different life form...
NB: UKishasema theory maana yake hiyo si fact kama unavyosema,.. ni assumptions tu.
Nimesema kuna theory ambazo ni known to be factual.....; sio assumptions kutokana na mtiririko wa what we know, sasa kama unapinga njoo na plausible arguments with some vivid proofs na logically sound uone kama hatutaamia kwako na kuchukulia unachosema kuwa factual... (that's the beauty about science tunatafuta majibu na sio kuanza na jibu na kutumia maisha yetu yote tunajaribu kutetea na kubadilisha kila hoja iendane na majibu yetu)
 
Nope nimesema wewe faida yako ni kutumika kama nishati ya viumbe wengine

Nishati hio ndio huenda ni chanzo ya kiumbe hicho lets start na mbegu ukipanda kwenye favorable conditions inatumia chakula ilichotunza inakuwa kubwa na kuanza kunyonya nishati ya jua (na mwisho wa siku ni chakula cha wengine)
Kitu kizuri ni kwamba umetumia neno "Huenda" that means unadhania huna uhakika kuhusu hilo,.. umetoa mfano mzuri wa mbegu,. ambapo hapo tunapaswa maswali au swali lingine la kujiuliza, Kama nishati ndiyo msingi wa mbegu na uhai kwa ujumla,. Je nishati imetumia mechanism gani mpaka kufanya mbegu fulani (let's say mbegu ya Parachichi) kubeba taarifa za Parachichi tu na sio taarifa za mmea mwingine? Je nishati ni Intelligent being? inajua kuweka code ambazo ni ngumu au impossible kuwa completely manipulated/modified?

Nimesema kuna theory ambazo ni known to be factual.....; sio assumptions kutokana na mtiririko wa what we know, sasa kama unapinga njoo na plausible arguments with some vivid proofs na logically sound uone kama hatutaamia kwako na kuchukulia unachosema kuwa factual... (that's the beauty about science tunatafuta majibu na sio kuanza na jibu na kutumia maisha yetu yote tunajaribu kutetea na kubalisha kila hoja iendane na majibu yetu)
Narudia kwamba,. Something cannot be a theory and a fact at the same time; it doesn’t make sense logically...... Mimi naona kinachotokea ni kwamba kuna muda tunaamua kuita idea fulani ni fact then baada ya miaka 100, 1000, 2000........ tunagundua kwamba tuliuishi uongo baada ya kupata njia mpya ya kuelewa jambo husika.
 
Kitu kizuri ni kwamba umetumia neno "Huenda" that means unadhania huna uhakika kuhusu hilo,.. umetoa mfano mzuri wa mbegu,. ambapo hapo tunapaswa maswali au swali lingine la kujiuliza, Kama nishati ndiyo msingi wa mbegu na uhai kwa ujumla,. Je nishati imetumia mechanism gani mpaka kufanya mbegu fulani (let's say mbegu ya Parachichi) kubeba taarifa za Parachichi tu na sio taarifa za mmea mwingine? Je nishati ni Intelligent being? inajua kuweka code ambazo ni ngumu au impossible kuwa completely manipulated/modified?
Mkuu unajua maana ya Nishati ? Kwamba nikitumia nishati ya moto kupika nyama ni moto ndio unaiambia nyama zile protein ziwe denatured ...

Unaongelea kwamba kwanini parachichi isitoe muembe au ? Mbona hio ni rahisi sana ukienda leo kutoa photocopy ya NIDA kitatokea kitambulisha cha kupigia Kura.

Na kuhusu mbegu mbona rahisi sana kuna chakula kipo stored kwenye mbegu ukikipa favorable conditions; maji n.k. kunatokea germination ambayo baada ya majani kutoka inaanza kupata chakula kwa usaidizi wa jua... (photosynthesis

Narudia kwamba,. Something cannot be a theory and a fact at the same time; it doesn’t make sense logically.
What don't you understand na ninaposema what is known to be factual ?!!! Which means kutokana na kufuatilia tumefikia conclusion fulani hata kama we can not prove it directly hence we know it to be a fact (the truth)
 
Dhana nzima ya "chanzo" si ya msingi wala ukweli. Ni dhana ya kufikirika na ina maana katika muktadha fulani tu.

Kimsingi chanzo kinategemea chronology, time, cause and effect.

These things are not real. They are not absolute.

Time is relative. One has to only read Einstein's Relativity to know that.

Cause and effect are not always synchronous, one has to only read quantum physics to know that.

If you can travel at the speed of light in a vacuum, the flow of time ceases to exist. In fact, from the perspective of a ray of light in a vacuum, the flow of time does not exist.

Everything, the past, the present, the future, happens at once.

So in reality, time appears to pass because of our position in the universe, because of the fact that we do not move as fast as light in a vacuum.

So time is not absolute, it is an illusion that appears because of the increasing entropy of the universe due to the second law of thermodynamics.

So, if time is not real, chanzo, which depends on causality and time, is also not real.

We can only speak of "chanzo" in relative terms. Not in absolute terms.
Hoja kwamba muda si kitu halisi kwa sababu ya nadharia ya Uhusiano wa Einstein na hiyo Relativity theory yake pamoja na fizikia ya Quantum kwa maana ya Quantum Mechanics, ni sahihi kwa muktadha wa kisayansi, kwamba ni kweli mwanga unasafiri bila kufuata mtiririko wa muda kwa mtazamo wake, na ni kweli pia kuwa sababu na matokeo yaani cause and effect hayafuati utaratibu wa kawaida katika kiwango cha quantum.

Lakini nikuulize mkuu, je, hii hoja yako inamaanisha kwamba muda haupo kabisa kwa hali zote?

Kwasababu tukiangalia katika uhalisia wa kila siku, muda ni jambo lenye athari kwa wanadamu, na ndio maana ulivyokua miaka 20 iliyopita sivyo ulivyo leo, na hii inamaanisha kutokea kuzaliwa, hadi kuzeeka na hadi kufa ni kwamba muda umetumika, kwasababu wewe na Mimi wote ni mashahidi ya kwamba mabadiliko haya yote yana mwelekeo fulani kwa maana ya kwamba haubaki kama ulivyo (ndio maana mtoto huanza kuzalia, anajifunza kukaa chini, anatambaa, kisha kusimama na kutembea, hivi vyote hutokea baada ya muda fulani).

Kwahiyo ingawa nadharia za kisayansi zinaonyesha kuwa muda ni wa mlinganisho kwa maana ya relative, lakini hii haiwezi kuwa sababu ya kutufanya tuukane kabisa katika maisha yetu ya kawaida, hivyo basi, kwakua chanzo ni kitu kinachotegemea sana muda na uhusiano huo wa kisababishi basi si sahihi kusema eti chanzo ni kitu ambacho hakipo kabisa.

Na hapa wacha niseme hivi, ya kwamba chanzo kinaweza kuwa hakipo katika uhalisia wa juu kabisa kwa maana ya ultimate reality, lakini ni kitu ambacho kipo katika uhalisia wetu wa kawaida kwa maana ya practical reality na sidhani kama unapingana na hii hoja.

Ila kama hiyo haitoshi, basi chukulia mfano huu, tunaposema "mimi ni chanzo cha furaha yako," hatumaanishi kwamba hakuna hali nyingine inayoweza kuleta furaha ila tunamaanisha kuwa katika mazingira fulani, uhusiano wa kisababishi upo, na ndio maana chanzo kina maana katika muktadha huo lakini chanzo hiki kinaweza kubadilika baadae (naongelea juu ya muda kaka).

Na kama wewe bado utaendelea kupinga chanzo kwa misingi ya nadharia ya uhusiano au Quantum Mechanics, basi pia unapaswa kukana dhana ya maisha ya kila siku, pamoja na effect zake (na sidhani kama unaweza kufanya hivyo).

Kwa hiyo, badala ya kukana kabisa uwepo wa chanzo, ni bora tukubali kwamba ni dhana inayotegemea muktadha, iwe ni katika maisha ya kila siku, falsafa, au imani za kidini, kwahiyo rudi katika mada na tuendelee kujadili chanzo cha uhai ni nini katika muktadha ambao andiko limelenga.

Tusijibane kwenye kaeneo fulani kadogo na kujinyima uwanda mpana wa Kutafakari juu ya mambo fulani fulani, embu tujipe uhuru wa Kutafakari kwanza halafu tuone tunaweza kufikia wapi.
 
Nimesoma na kurudia tena. Ngoja nikujibu kwa mtindo huu nafikiri itakusaidia na wewe.

Niliwahi kumuuliza Mwalimu wangu swali, "Sir hivi unaamini uwepo wa freemasons na ni kweli wana nguvu?".

Majibu ya teacher " rafiki yangu, muda wa kutafuta ukweli juu ya swali lako ni vyema ukautumia kuendelea kusoma Aya/sura za kitabu chako kitakatifu unachokiamini, (akimaanisha Bible au Quran) hio itakujenga zaidi."

Jibu la teacher wangu, naomba nikupatie na wewe japo wewe hauhoji kuhusu freemasons though somehow unachokihoji ndio point zao kudhohofisha uhalali wa nguvu za huyu tunaemuita na kuamini ni Mungu.

Mwandishi Una IQ kubwa kwa namna umestructure content ya Uzi wako. Naamini ukielekeza IQ hio katika Imani utapata majibu sahihi kabisa.

Huko utafanya tafakari more spiritually na huenda sikumoja ukaanda andiko kutujibu swali lako la chanzo na Msingi kwa mlengo wa kiimani zaidi.
Huwa nasoma maandiko ila maandiko karibia yote yanazungumzia chanzo na wala sio msingi.
 
Mkuu unajua maana ya Nishati ? Kwamba nikitumia nishati ya moto kupika nyama ni moto ndio unaiambia nyama zile protein ziwe denatured ...

Unaongelea kwamba kwanini parachichi isitoe muembe au ? Mbona hio ni rahisi sana ukienda leo kutoa photocopy ya NIDA kitatokea kitambulisha cha kupigia Kura.

Na kuhusu mbegu mbona rahisi sana kuna chakula kipo stored kwenye mbegu ukikipa favorable conditions; maji n.k. kunatokea germination ambayo baada ya majani kutoka inaanza kupata chakula kwa usaidizi wa jua... (photosynthesis
Hujajibu direct, Nimeuliza nishati ni intelligent being maana ina uwezo wa ku transfer taarifa na kuzihifadhi kwa code kiasi ambacho haziwezi kuwa modified easily,.yaani What naturalistic process explains the origin of this information, given that information is not a property of matter or energy but requires an intelligent source?......unaongea simple lakini uhalisia ni complex zaidi,.. ngoja nisiende deep maana hutokua na majibu ya maswali husika.


What don't you understand na ninaposema what is known to be factual ?!!! Which means kutokana na kufuatilia tumefikia conclusion fulani hata kama we can not prove it directly hence we know it to be a fact (the truth)
Ila si unajua kwamba Dunia nzima tunaweza kukubaliana kwamba jambo fulani ni fact lakini kumbe kiuhalisia wote tupo wrong? Yaani kimsingi ni kwamba baada ya kudadisi tunafikia hitimisho at a certain point in time na kuona kwamba tumefikia ukweli even though hicho tunachoita ukweli sio ukweli halisia!
 
Back
Top Bottom