Kama Cloutus Chama tunayemwimba kwenye mpira wetu wa Bongo kwenye Timu yake ya Taifa hayupo hata reserve basi Ligi yetu ya Bongo ina walakini

Kama Cloutus Chama tunayemwimba kwenye mpira wetu wa Bongo kwenye Timu yake ya Taifa hayupo hata reserve basi Ligi yetu ya Bongo ina walakini

Mawembasa1979

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2015
Posts
2,540
Reaction score
3,333
Juzi kati nilikuwa nasoma majina ya Wachezaji walioitwa kwenye Timu ya Taifa ya Zambia na Kocha Mkuu wa timu hiyo Bw. Micho. Nilistaajabu nilipoona jina la mchezaji na kiungo pendwa wa ligi yetu kutokuwemo kwenye orodha ya wachezaji wa timu hiyo. Pia, kiungo mwingine fundi Larry Bwalya naye hakuwemo kwenye orodha hiyo. Nikajiuliza mpira wetu una tatizo gani?

Iweje leo kiungo tunayemwona kuwa asipokuwepo kwenye mechi ya Simba na timu nyingine tuanona kama hakuna timu, leo anakosekana kwenye timu yake ya taifa. Kwa kweli sikuyaamini macho yangu kuhusu hilo. Chama huyu huyu aliyeimpandishia dau la kumsajili timu yake ya Simba baada ya kutakiwa na mahasimu wao Yanga anakosa hata kuwa kwenye wachezaji wa akiba (Reserve)?

Nilipoendelea kushangaa nikakutana na mchambuzi mmoja mahiri alikuwa akieleza kuhusu ubora na udhaifu wa timu ya Simba inapocheza uwanjani. Kwa kumnukuu mchambuzi huyo alieleza kuwa "Timu ya Simba ni bora kwa kuchezea mpira hasa wa pasi fupi za kufurahisha mashabiki (wenyewe wanaita pira biriani) lakini ni dhaifu ikikutana na timu zinazocheza mpira wa nguvu".

Akaendelea kusema ubora wa Simba unamtegemea zaidi Cloutus Chama, ingawa naye hana uwezo wa kucheza mpira wa nguvu. Sehemu kubwa ya mpira anaocheza Chama anatumia unyumbufu wa mwili wake kuwadanganya wapinzani wake kwa vyenga vya hapa na pale.

Hivyo, kama taifa yatupasa tujitathmini kuhusu Ubora wa Ligi yetu ambayo ina wachezaji wanaoimbwa midomoni kama Chama na wengine.
 
Mimi kinachonishangaza ni ubishani WA mpira mitaani na maofisin
Ma Gruop ya watsap hadi kero..

Sasa mpira wenyewe ukija tazama
Ukisikia ubishani,ukisoma headlines za magazeti, ukisikiliza vipindi vya michezo wale wanaojiita wachambuzi,ukiwasikiliza hao wachumia domo (wasemaji) na ukienda field (Kiwanjani) unaona bora ungelala tu home ni upuuzi mtupu.
 
Timu ya taifa ya nchi ni mkusanyiko wa wachezaji mbali mbali bora wa nchi hiyo na mara nyingi wanachaguliwakutokana na viwango vyao kisoka katika muda fulani. Zambia ni moja ya nchi ambazo zimekuwa na wachezaji wanaocheza kwenye ligi kubwa duniani na ni wengi, hivyo inatosha kusema kuwa wana wachezaji wengi sana ambao kocha anaweza kuchagua kuunda kikosi kwa wakati husika.

Mchezaji kuwa bora au si bora kwenye timu yake anayochezea sio sababu ya yeye kuitwa timu ya taifa. Mfano unaweza kuta katika nafasi ya Chama timu ya Zambia kuna wachezaji wengi ambao pengine wanamzidi kiwango kutokana na namna mfumo ambao kocha angetaka kumtumia, lakini Chama huyo huyo kwenye mfumo wa uchezaji wa Simba akawa muhimu sana kwenye nafasi na mfumo anaotumika.

Mimi kama mtazamaji wa mpira, kweli nakubali kwa uchezaji wa Simba mpira wao ni laini laini sana, wakikutana na timu zenye kutumia nguvu na kukaba sana lazima watapoteana.

Kwa ligi yetu bado hatujakuwa bora sana, lakini mpaka sasa tuko kwenye muelekeo mzuri. Kwa mfano kwa sasa utaona kuwa wachezaji wa nchi nyingi wanatambua na kukimbilia kusajiliwa kwenye timu zetu, huu ni mwanzo mzuri.

Nawakilisha.
 
Mtoa mada siyo mtu wa mpira na hajui kinachoendelea. Kwa taarifa yako chama ndiye captain wa timu ya taifa ya zambia.

Kutoitwa kwake Ni kutokana na tatizo lilitokea mwezi wa kumi. Chama aliitwa timu ya taifa na akachelewa kwenda zambia kitu ambacho kilimkasirisha Sana kocha wa timu ya taifa na kuamua kumuacha kabisa. kilichomchelewesha chama ilikuwa mechi tuliyoenda kucheza dodoma na kushinda nne.

Mbona yakubu huwa anaitwa timu ya taifa ya ghana, miquison mozambique, n.k

Sent from my TECNO B1p using JamiiForums mobile app
 
Oyaaa simple ni hivi,

Hata wazambia wenyewe wamepanic tena baada ya kufungwa Jana, wameanza kuwakumbuka patson daka, chama na wengineo tena walikua wanalalamika kwanini hakuna mchezaji wa Nkana red devils alieitwa timu ya taifa.

Ni hivi chama aliitwa timu ya taifa ile kipindi kabla ya derby haijaairishwa so alichelewa kwenda kambini hapo ndio Micho akaona dogo anazingua so akamtoa kwenye mipango yake. Kwanza hata huyo Micho Siku zake zinahesabika tu hapo Zambia.simba
 
Yanga Chama anawaumaaaaaaaaa! Na vile mbinu yao ya kuwadanganya mashabiki imebuma wamebadilisha gia angan sahiz ni watu wa kuibua mara hili mara lile ila kiukweli,,, utopolo united mtapata tabu sana.

Kama Yanga wanaweza kumlipa Senzo wanashindwaje kumlipa Chama.

Halafu hizo tetesi za Chama kutakiwa na Yanga ni za kipropaganda tu, lengo ni kuitaka Simba ikusanye pesa haraka kumlindikia Chama kama signing fee ili wasiipeleke hiyo pesa kwenye sajili nyingine zijazo.
 
Chama ni mchezaji mzuri hapa EAC tu.Sijawahi kusikia waarabu wakimtaka

Zesco walivyomtema, Al Ittihad wakamtaka. Cha ajabu zaidi hakufanikiwa kucheza hata mechi moja ya ligi kwa kipindi chote cha nusu msimu.

Akarudi zake lusaka Dynamos.
 
Mtoa mada siyo mtu wa mpira na hajui kinachoendelea. Kwa taarifa yako chama ndiye captain wa timu ya taifa ya zambia.

Kutoitwa kwake Ni kutokana na tatizo lilitokea mwezi wa kumi. Chama aliitwa timu ya taifa na akachelewa kwenda zambia kitu ambacho kilimkasirisha Sana kocha wa timu ya taifa na kuamua kumuacha kabisa. kilichomchelewesha chama ilikuwa mechi tuliyoenda kucheza dodoma na kushinda nne.

Mbona yakubu huwa anaitwa timu ya taifa ya ghana, miquison mozambique, n.k

Sent from my TECNO B1p using JamiiForums mobile app
Yawezekana kweli mimi sio mtu wa mpira. Hata hivyo, kutokana na hoja zako hapo juu umeonesha kuwa alichelewa kujiunga na wenzake kipindi kilichopita ndio maana hajaitwa timu ya taifa, ambayo inaonesha kuwa ni utovu wa nidhamu wa kutozingatia muda. Kwa hili naungana na kocha. Kwa hiyo, itoshe kusema kuwa hakuitwa kwa sababu ya utovu wa nidhamu.
 
Timu ya taifa ya nchi ni mkusanyiko wa wachezaji mbali mbali bora wa nchi hiyo na mara nyingi wanachaguliwakutokana na viwango vyao kisoka katika muda fulani. Zambia ni moja ya nchi ambazo zimekuwa na wachezaji wanaocheza kwenye ligi kubwa duniani na ni wengi, hivyo inatosha kusema kuwa wana wachezaji wengi sana ambao kocha anaweza kuchagua kuunda kikosi kwa wakati husika.

Mchezaji kuwa bora au si bora kwenye timu yake anayochezea sio sababu ya yeye kuitwa timu ya taifa. Mfano unaweza kuta katika nafasi ya Chama timu ya Zambia kuna wachezaji wengi ambao pengine wanamzidi kiwango kutokana na namna mfumo ambao kocha angetaka kumtumia, lakini Chama huyo huyo kwenye mfumo wa uchezaji wa Simba akawa muhimu sana kwenye nafasi na mfumo anaotumika.

Mimi kama mtazamaji wa mpira, kweli nakubali kwa uchezaji wa Simba mpira wao ni laini laini sana, wakikutana na timu zenye kutumia nguvu na kukaba sana lazima watapoteana.

Kwa ligi yetu bado hatujakuwa bora sana, lakini mpaka sasa tuko kwenye muelekeo mzuri. Kwa mfano kwa sasa utaona kuwa wachezaji wa nchi nyingi wanatambua na kukimbilia kusajiliwa kwenye timu zetu, huu ni mwanzo mzuri.

Nawakilisha.
Well said! Ni kweli Zambia ilishawekeza katika soka toka muda mrefu na hivyo wana hazina kubwa ya wachezaji kuliko TZ.
Fikiria miaka ya 90 ilikufa timu nzima kwa ajali lakini miaka michache tu wakarudi na moto uleule na hata kuja kutwaa kombe!
Hebu niambie hii Tanzania yetu wafe stars wote akiwemo Samata, tutachukua muda gani kama si zaid ya 10yrs kupata wakali wengine!
Pia tujipe moyo ligi yetu ina muelekeo mzuri hasa kwa sasa ambapo tunajaribu kuiendesha sambamba na mifumo ya kimataifa, serikali iongeze support ya kuwekeza hasa katika shule za soka kama ilivyo katika nchi zilizopiga hatua kisoka.
 
Back
Top Bottom