FRANC THE GREAT
JF-Expert Member
- May 27, 2016
- 5,500
- 8,060
Mara tu baada ya mashambulizi kutekelezwa katika kambi mbili za kijeshi zinazotumika na majeshi ya Marekani nchini Iraq, Rais wa Marekani, Donald Trump alikuwa alihutubie taifa la Marekani kwa mujibu wa taarifa rasmi lakini mara baada ya kikao maalumu na maafisa wa ngazi za juu wa masuala ya ulinzi na usalama katika ikulu ya Marekani, White House alisitisha mpango wa kutoa hotuba hiyo.
Lakini hakuishia hapo bali Trump ali-tweet akisema kuwa;
"Kila kitu kipo sawa, kambi zetu mbili za kijeshi zilizopo Iraq zimeshambuliwa na Iran, tunafanya tathmini kujua kama kuna madhara yaliyopatikana au uharibifu wowote wa mali, yote kwa yote tuna vifaa bora vya kivita kuliko nchi yoyote ile Duniani, kwa mbali! Nitatoa tamko kesho asubuhi"
Mpaka sasa taarifa kutoka Marekani zinadai kuwa hakuna taarifa za vifo kwa wanajeshi wao huku Iraq pia ikisema vivyo hivyo, lakini Iran imedai kuwa mashambulizi yao yamefanikiwa kuwaua wanajeshi wa Marekani. Muda upo na tuendelee kuzisubiri taarifa zaidi hususani baada ya hiyo tathmini.
Ila kama hakuna Wamarekani waliouawa katika mashambulizi ya makombora ya Iran, basi sidhani kama Marekani atakuwa na haja ya kuyajibu kijeshi mashambulizi hayo kama Pentagon ilivyokuwa ikiweka wazi hapo awali na kama jambo hili ni kweli, basi wachambuzi mbalimbali wa masuala ya kimataifa wanayaita mashambulizi haya yanayotajwa kama "kisasi" yaliyofanywa na jeshi la Iran kama hatua ya kuokoa nyuso zao (save face) mbele ya wananchi na dunia kwa ujumla.
Tuendelee kusubiri!
Mods sidhani kama kuna haja ya kuunganisha huu uzi, ni vyema ukabaki hivi hivi kama ulivyo.
Pia pitia mabandiko haya hapo chini kwa taarifa zaidi:
www.jamiiforums.com
www.jamiiforums.com
Lakini hakuishia hapo bali Trump ali-tweet akisema kuwa;
"Kila kitu kipo sawa, kambi zetu mbili za kijeshi zilizopo Iraq zimeshambuliwa na Iran, tunafanya tathmini kujua kama kuna madhara yaliyopatikana au uharibifu wowote wa mali, yote kwa yote tuna vifaa bora vya kivita kuliko nchi yoyote ile Duniani, kwa mbali! Nitatoa tamko kesho asubuhi"
Mpaka sasa taarifa kutoka Marekani zinadai kuwa hakuna taarifa za vifo kwa wanajeshi wao huku Iraq pia ikisema vivyo hivyo, lakini Iran imedai kuwa mashambulizi yao yamefanikiwa kuwaua wanajeshi wa Marekani. Muda upo na tuendelee kuzisubiri taarifa zaidi hususani baada ya hiyo tathmini.
Ila kama hakuna Wamarekani waliouawa katika mashambulizi ya makombora ya Iran, basi sidhani kama Marekani atakuwa na haja ya kuyajibu kijeshi mashambulizi hayo kama Pentagon ilivyokuwa ikiweka wazi hapo awali na kama jambo hili ni kweli, basi wachambuzi mbalimbali wa masuala ya kimataifa wanayaita mashambulizi haya yanayotajwa kama "kisasi" yaliyofanywa na jeshi la Iran kama hatua ya kuokoa nyuso zao (save face) mbele ya wananchi na dunia kwa ujumla.
Tuendelee kusubiri!
Mods sidhani kama kuna haja ya kuunganisha huu uzi, ni vyema ukabaki hivi hivi kama ulivyo.
Pia pitia mabandiko haya hapo chini kwa taarifa zaidi:
Iran yatishia kuzishambulia kwa makombora kambi za kijeshi za Marekani zilizopo Mashariki ya Kati
Jeshi la Iran limesema kuwa limejipanga kutumia makombora ya masafa ya kati na ya mbali kuzishambulia kambi za kijeshi za Marekani zilizopo Mashariki ya Kati ikiwa ni mpango wa kulipa kisasi kutokana na mauaji ya jenerali wa kikosi maalum cha Iran, Qassem Suleiman aliyeuawa na Marekani wiki...
Iraq: Iran yashambulia kwa makombora kambi mbili za Jeshi za Marekani, Ain al-Asad na Erbil
Iran imerusha makombora zaidi ya 10 ikilenga Majengo ya Marekani yaliyopo Kaskazini mwa Iraq ikiwemo Kambi ya Jeshi ya Ain al-Asad ambapo kuna Majeshi ya Marekani ikiwa ni siku chache baada ya Marekani kumuua Qassem Soleimani Chaneli ya Taifa ya Iran imesema, Jeshi la Kimapinduzi la Nchi hiyo...