Kama haujawahi kunywa energy drinks Hongera na Jiepushe nazo. Kama umezoea kuzitumia Tafadhali weka mpango wa kupunguza na kuacha

Kama haujawahi kunywa energy drinks Hongera na Jiepushe nazo. Kama umezoea kuzitumia Tafadhali weka mpango wa kupunguza na kuacha

Mimi sio energy, nina tabu na Pepsi bariiiidi. Umekuwa ni ugonjwa sasa pia angalieni na hivyo vipombe kali vya kwenye makopo
 
Acha ubishi usiokuwa na kichwa wala miguu mzee mo energy wakati zinatoka ziliandikwa kwa maandishi kabisa mekundu kuwa

Haruhusiwi kunywa mja mzito
Mtu mwenye matatizo na caffein
Mtu anayenyonyesha
usimwe zaid ya mbili
Na usinywe wakati wa kulala
Then baadae mo wakatoa hayo maelezo kwenye chupa zao.

Na moja ya madhara ya moja kwa moja ni kukosa kabisa usingizi kama unasafiri na gari usiku kunywa hutalala ngo na kama utakunywa then ulale basi hutopata usingizi na hata ukipata usingizi unaweza kufa kwa shinikizo la damu
Wewe ndo huelewi
Hiyo mo extra Ina caffeine tu ndo inayokosesha usingizi... caffeine hata kwenye vinywaji vya cola ipo Ila huwezi ukaiita ni energy drink
Halafu kuandika tahadhari siyo matakwa ya mo ni matakwa ya mamlaka zinazokagua vinywaji hivyo
 
Ukitumia kupita kiasi lazima upate madhara .

Then hivyo vinywaji ni kwa ajili ya WATU masikini ili viwasaidie kufanya kazi ngumu.

Na kuhusu kuumwa moyo na figo hiyo ni kweli watu wanaumwa Sana na kufa Sana Ila kwakuwa kundi kubwa ni WATU masikini huwezi kusikia hili jambo mahala popote.

Binafsi nimetumia Energy drink wakati nafanya maandalizi ya mitihani yangu ya mwisho Form four na form na six .
 
Kinywaji pekee nipendacho ni maji na juisi ya asili (ya kutengeneza na matunda og)

Nina miaka kadhaa sinywi soda wala kinywaji chochote cha kiwandani
Juicy pekee niipendayo ni ya miwa sijawahi kunywa energy Wala soda situmii miaka sasa
 
Kwa uzoefu wangu energy sio salama,nikinywa hata moja saa mbili usiku basi usingizi ntaupata kuanzia saa Tisa usiku,halafu ni kama inasisimua sana mwili ,lakini pia Ina addiction,najitahd sana kuachana nazo
 
Kwaiyo ata redbull ni mbaya au ni mo na azam energy tu ebu fafanua vizuri maana naona km umewalenga Mo na Azam engery

Najua ni mafundi na boda boda wachache sana wanaweza kununua redbull so mreta mada ugomvi wako ni energy drink zote au ni mo na Azam
 
Hakuna kisicho na madhara hasa ukikizidisha

Kuleni mboga za majani mbichi mbichi, nyama nyingi na mazoezi ya kukimbia kila siku
 
Kuna cocaine kwa mbaaili enewi ungewanunulia nyingi ungewawekea ktk friji wanyweee mpka waseme .poo alafu ungewaelezea mazara yake ila vijana wengi watapata magonjwa kama kiharusi stroke na mshtuko wa moyo uko mbeleni
 
 
Peace,

Awali ya yote niweke wazi andiko langu halina kusudi la kuhafifisha au kuathiri biashara ya mtu yeyote ila ni ushuhada wa kweli na dhairi wa watu wanaonizunguka.

Nimekuwa nikisikia na kuona vijana wengi wakipendelea vinywaji vya kusisimua mwili alimaarufu "energy drinks" ziko za aina mbali mbali na bei tofauti. Vijana kama boda boda, wanafunzi na vibarua wa kazi za mikono wamekuwa watumiaji sana wa vinywaji hivi.

Nilipata kusikia na kwa sasa nimeshuhudia kuwa vinywaji hivi vina uraibu mkali sana na pia athari za moja kwa moja kwa watumiaji wa mara kwa mara. Nina mifano mingi ila nitataja michache kwa lengo la kujenga hoja na kujifunza kwa pamoja.

Kuna vijana kwenye maegesho ya boda boda nimekua nawasikia kua ili siku iende sawa lazima wanywe energy wengine wamekua hata na utaratibu wa kununua za ziada na kuifadhi ili anapoamka tu cha kwanza ni kunywa energy ndio hujiisi utayari wa kuanza kazi.

Mwezi uliopita nilikua na project ya ujenzi nikawa napita kutazama mradi unakwendaje kulinganisha na report ya msimamizi wa mradi ajabu pale site palikua na makopo ya mo-energy na azam energy mengi sana wala sikujali ila cha kushangaza kuna siku nilikuta wamepiga kazi kwa makisio ya kua mbele ya estimated target kwa zaidi ya kama 25% nilifurahi sana nikaamua kuwalipia bili zao za chakula kwa siku tatu.

Mshangao ulikua wangu waliponisihi sana sana niwaongezee bajeti kucover pia "energy" nilipohoji kulikoni msisitizo ule wakajibu "yani hata chakula hakina maana kama hakuna energy" looo !! Nikasema sawa nitaongeza bajeti ya kinywaji hicho kwa kila mmoja aise shangwe walilopiga ni kubwa mara dufu ya nilipowapatia ahadi ya kulipia chakula. Vijana wako adicted mbaya.

Kuna classmate wangu kwa sasa ni muajiriwa shirika fulani la uma kama afisa manunuzi anakiri bila kunywa energy drink anajihisi kupoteza umakini na uwezo wa kuconcetrate mpaka apate vinywaji hivi.

Sasa hivi karibuni amekua analalamika kuhisi kutetemeka hasa kipindi cha usiku na kifua kuuma na kuhisi moyo kwenda mbio sana hasa anapopata wasiwasi wa jambo hata dogo tu na kuhisi kizunguzungu mda wa jua kali akanishirikisha basi nikajaribu kubrowse mtandaoni ya kwamba nini hasa kinaweza kupelekea matatizo haya ajabu ajabu kote majibu yanahusishwa na matumizi ya kupindukia ya energy drinks.

Nikamshirikisha jamaa akasema pia yeye alikua anahisi watatizo hayo yanahusiana na vinywaji ya kusisimua mwili kwa kua matatizo yote hayo yanapomkuta na basi akapata fursa na akipiga energy mbili chap chap anakua fresh kabisa aise jamani tujihadhari.

Nikaona nifanye ufuatiliaji wa jambo hili nikawafuata boda boda nikawauliza kama kuna nyakati wanajihisi kutetemeka mikono, au kuhisi moyo kwenda mbio au kuhisi kupoteza umakini au kifua kuuma na kizunguzungu.

Kwa mshangao wakasema yote hayo yanawakuta kwa nyakati tofauti ila wakanishangaza kwa mara nyingine kwa kuniambia yote hayo yanapowakuta hununua energy ya baridiiii na kunywa na shida zote na mashwahibu hayo hupotea kwa sekunde chache tu.

Ikumbukwe vinywaji hivi havina hata muda wa miaka 10 sokoni lakini madhari yake yameanza kushuhudiwa punde tu mtumiaji anapotumia je matumizi ya muda mrefu yatakua na madhara kiasi gani ?!

Mimi sio daktari wala sina ujuzi wowote wa kitabibu lakini naona viashiria dhahiri vya madhara ya vinywaji hivi. Niliwahi kuona clip fupi ya Mo Dewji akisema hajawahi kuonja ladha ya vinywaji vyake, (jambo fikirishi sana)

Karibuni tujadili nini uzoefu wako katika matumizi ya vinywaji hivi?


View attachment 2906241
Acha wajimalize
 
Duuh hatari Mimi nakamtindo ka kumix smart gin na energy kumbe najiandalia ka njia ka kwenda kukula bikra mbinguni
Kunywa sana. Sio mtu unakufa halafu viungo vyako vingine vizima kabisa! Inatakiwa unakufa maini, figo, mapafu hayatazamiki yapo nyang'anyang'a.
 
Huku kutishana kote ni mbinu za kukwepa kifo? Au maradhi?

Anyway ushauri wangu mimi ni kila mtu aishi atakavyo tusitishane maana kifo hakikwepeki kuna miaka kadhaa mbele sisi wote tunaokunywa energy na wasio kunywa wote hatutakuwepo, cha msingi kama unaifurahia we kunywa tu mkuu, tusiogopeshane...kila kitu ni hatari kwa afya yako hata hiyo sim unayotumia kuchati kutoa ujumbe nayo inaaminika ina mionzi ambayo ni hatari kwa Afya, hiyo bodaboda unayotumia nayo ni hatari kwa afya yako, hiyo gari unayotumia nayo ni hatari kwa afya yako, hilo gorofa unaloishi pia ni hatari kwa hatari kwa Afya yako.... TUSITISHANE WALA USIHARIBU BIASHARA YA MTU KWA KUPANDIKIZA CHUKI ZA KIJINGA.
 
Back
Top Bottom