Elections 2015 Kama hii ni kweli, then serikali yetu ni serikali dhalimu na haramu? Hukumu ya karma ijuu yake!

Elections 2015 Kama hii ni kweli, then serikali yetu ni serikali dhalimu na haramu? Hukumu ya karma ijuu yake!

Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali kuhusu figisu figisu za kwenye uchaguzi mkuu ambapo kila anayeshindwa, hakubali kushindwa kihalali kwenye sanduku la kura katika uchaguzi huru na wa haki, na badala yake huja na tuhuma za kuibiwa kura, kupokwa ushindi halali, na kususia matokeo, hivyo bandiko hili ni swali, Kama Tuhuma Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu? iliyoingia madarakani kwa hila, udhalimu na ulaghai?. Kama ni kweli, then Hukumu ya Karma ii Juu Serikali Yetu!. Na kama sii kweli, then tutashuhudia rais Magufuli na serikali yake, wakibarikiwa, nchi yetu ikibarikiwa na kupata neema na ustawi.


Ila pia, endapo tuhuma hizi ni za uongo, ni za kupika na ni uzushi, then rais John Pombe Joseph Magufuli, ndiye rais chaguo la Mungu kwa Tanzania aliyetangazwa mshindi siku yake ya kuzaliwa!, katika uchaguzi huru na wa haki, hivyo atasimama test in time, of which time will tell!.

Kupitia kwa Magufuli, Tanzania itapata neema, mafanikio na maendeleo makubwa ya ajabu kwa sababu ya baraka za Mungu zitakuwa juu yake, nchi yetu inakwenda kageuka kuwa ni ile nchi ya ahadi ya maziwa na asali.


Neno litasimama, mambo mengine yote yatapita, lakini neno litasimama!.

Mungu ibariki Tanzania.

Paskali
Wanabodi, hata janga hili la kirusi cha Corona japo ni janga la kimataifa, na Tanzania ni sehemu ya kimataifa, hali ya Corona kwa Tanzania ukilinganisha na nchi nyingine, ni uthibitisho mwingine kuwa Magufuli ni chaguo la Mungu kwa Tanzania. Kinachoendelea kwenye Corona kwa Tanzania, hatuwezi kujitapa ni preparedness ya taifa kuzuia, ni neema tuu za Mungu na baraka zake kwa taifa letu chini ya mtu wake aliyebarikiwa.

Kwanye Corona, Watanzania tuendelee kumshukuru Mungu sana kwa mpaka hapa tulipo fika kwa kutuepusha na tuendelee kumuomba Mungu aendelee kutukingia mkono wake.
P
 
Wanabodi, hata janga hili la kirusi cha Corona japo ni janga la kimataifa, na Tanzania ni sehemu ya kimataifa, hali ya Corona kwa Tanzania ukilinganisha na nchi nyingine, ni uthibitisho mwingine kuwa Magufuli ni chaguo la Mungu kwa Tanzania. Kinachoendelea kwenye Corona kwa Tanzania, hatuwezi kujitapa ni preparedness ya taifa kuzuia, ni neema tuu za Mungu na baraka zake kwa taifa letu chini ya mtu wake aliyebarikiwa.

Kwanye Corona, Watanzania tuendelee kumshukuru Mungu sana kwa mpaka hapa tulipo fika kwa kutuepusha na tuendelee kumuomba Mungu aendelee kutukingia mkono wake.
P
Ni kweli kabisa Magufuli ile nafasi ya kuwa kiongozi wa malaika huko mbinguni atapewa
JPM amebarikiwa ni chaguo la mungu corona hiwezi kuisumbua TZ ya Magufuli

JPM na Makonda hawa ni chaguo la mungu
Italy USA waje wachukue baraka kwa JPM corona itaisha huko kwao
Jpm baba lao makonda baba lao
 
Duh...!.
P
Kama mtaalamu wa nguvu ya akili, je, hii ndiyo karma uliyoitabiria kama serikali hii ni dhalimu?

Kama sivyo, tukubali ule upande mwingine kuwa nchi yetu imebarikiwa na kuneemeka na uwepo wa serikali hii?

Tuambie P kwani inaonekana sikuhizi unakwepa kujibu maswali ya wachangiaji kwenye threads zako.

Mwaka huu tukiacha ya miaka 4 iliyopita nchi iko kwenye mtanziko WA

Corona

Mafuriko ikiwemo kujaa maji maeneo ya mito, mabwawa na maziwa.

Waziri mkuu ofisi yake imeunda kamati ya jambo moja tu na LA mvua nyingi si tatizo na umma hawajaathirika kwa wingi! Ndivyo?
 
Wanabodi, hata janga hili la kirusi cha Corona japo ni janga la kimataifa, na Tanzania ni sehemu ya kimataifa, hali ya Corona kwa Tanzania ukilinganisha na nchi nyingine, ni uthibitisho mwingine kuwa Magufuli ni chaguo la Mungu kwa Tanzania. Kinachoendelea kwenye Corona kwa Tanzania, hatuwezi kujitapa ni preparedness ya taifa kuzuia, ni neema tuu za Mungu na baraka zake kwa taifa letu chini ya mtu wake aliyebarikiwa.

Kwanye Corona, Watanzania tuendelee kumshukuru Mungu sana kwa mpaka hapa tulipo fika kwa kutuepusha na tuendelee kumuomba Mungu aendelee kutukingia mkono wake.
P
Ni nchi gani ya afrika imeathirika zaidi ya Tanzania, kuna nchi hazina hata mgonjwa
 
Wanabodi, hata janga hili la kirusi cha Corona japo ni janga la kimataifa, na Tanzania ni sehemu ya kimataifa, hali ya Corona kwa Tanzania ukilinganisha na nchi nyingine, ni uthibitisho mwingine kuwa Magufuli ni chaguo la Mungu kwa Tanzania. Kinachoendelea kwenye Corona kwa Tanzania, hatuwezi kujitapa ni preparedness ya taifa kuzuia, ni neema tuu za Mungu na baraka zake kwa taifa letu chini ya mtu wake aliyebarikiwa.

Kwanye Corona, Watanzania tuendelee kumshukuru Mungu sana kwa mpaka hapa tulipo fika kwa kutuepusha na tuendelee kumuomba Mungu aendelee kutukingia mkono wake.
P


Mkuu bado unasimamia hili bandiko lako au umetengua kauli?
 
Kwenye hii Serikali dhalimu iliyotapakaa damu za Watanzania? Mie siyo mtu wa kununulika ili kuunga mkono udhalimu.
Hili la possibility ya serikali yetu kuwa dhalimu linazungumzwa sana na wapinzani for political scores, lakini tuhuma hii inapoletwa na mwana jf mwandamizi kama wewe Mkuu BAK, ukisema serikali dhalimu iliotapakaa damu za Watanzania, jee una ushahidi?.

Wanabodi,
hili ni swali, Kama Tuhuma Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu? iliyoingia madarakani kwa hila, udhalimu na ulaghai?. Kama ni kweli, then Hukumu ya Karma ii Juu Serikali Yetu!. Na kama sii kweli, then tutashuhudia rais Magufuli na serikali yake, wakibarikiwa, nchi yetu ikibarikiwa na kupata neema na ustawi.
P
 
Kuuawa kwa Ben Saanane, Azory Gwanda na shambulizi la kutaka kumuua Lissu kwako wewe si UDHALIMU na kutekwa na kubambikiwa kesi Watanzania mbali mbali akiwemo Erick Kabendera na viongozi wa juu wa Chadema etc ni utani tu au ni UDHALIMU uliofanywa na MABEBERU.

Hili la possibility ya serikali yetu kuwa dhalimu linazungumzwa sana na wapinzani for political scores, lakini tuhuma hii inapoletwa na mwana jf mwandamizi kama wewe, ukisema serikali dhalimu iliotapakaa damu za Watanzania, jee una ushahidi?.


P
 
Mkuu pasco tupe tathimini yako ya miaka mitano ya serikali je ni laana au imebarikiwa??
Mkuu mliberali, simba Mwendo ni baraka kwa kwenda mbele, mfano kwenye hili janga la Corona, angalia majirani zetu maambukizi yanavyoongezeka na watu wao wanavyokufa kwa wingi, lakini huku kwetu update ya mwisho ilifanywa 17 days ago!, hakuna maambukizi mapya wala kifo chochote!.
No news is good news.
P
 
Kuuawa kwa Ben Saanane, Azory Gwanda na shambulizi la kutaka kumuua Lissu kwako wewe si UDHALIMU na kutekwa na kubambikiwa kesi Watanzania mbali mbali akiwemo Erick Kabendera na viongozi wa juu wa Chadema etc ni utani tu au ni UDHALIMU uliofanywa na MABEBERU.
Kwanza maadam Ben Saanane haijulikani kilichomkuta, huwezi kusema kauwawa!.
Jee una ushahidi hata wa kimazingira tuu kuthibitisha serikali inahusika?.

The same applies to Azory Gwanda, hakuna uthibitisho wowote kuwa ameuwawa na hakuna ushahidi wowote hata wa kimazingira, wa uhusika wa serikali.

Kwenye shambulio la Lissu, kila mtu anajua limepangwa na limetekelezwa na watu wasiojulikana. Jee una ushahidi wowote wa serikali kuhusika?. Yaani ushahidi wa wasiojulikana ni serikali yetu tukufu?.

Nijuavyo mimi, wasiojulikana wa Lissu ni hawa

Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums

P
 
Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali kuhusu figisu figisu za kwenye uchaguzi mkuu ambapo kila anayeshindwa, hakubali kushindwa kihalali kwenye sanduku la kura katika uchaguzi huru na wa haki, na badala yake huja na tuhuma za kuibiwa kura, kupokwa ushindi halali, na kususia matokeo, hivyo bandiko hili ni swali, Kama Tuhuma Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu? iliyoingia madarakani kwa hila, udhalimu na ulaghai?. Kama ni kweli, then Hukumu ya Karma ii Juu Serikali Yetu!. Na kama sii kweli, then tutashuhudia rais Magufuli na serikali yake, wakibarikiwa, nchi yetu ikibarikiwa na kupata neema na ustawi.


Naomba kuanza na angalizo. Hli ni bandiko swali la dhana tuu ya kufikirika, hypothetical situation kuwa if A is true, then B is true, if it is not true, then its not!. Hivyo kwa euelewa wa mashaka wa wengi wetu humu, msije kushangaa wakashindwa kuiona hicho kitangulizi cha "kama ni kweli", na kupelekea kudhania nimesema serikali yetu ni serikali dhalimu!, ninachosema hapa ni kama hii tuhuma iliyotolewa leo na Edward Lowassa ni kweli, then..

Tuhuma yenyewe imetolewa hapa
Tamko la Edward Lowassa Baada ya NEC Kumtangaza Dr Magufuli Kuwa Mshindi wa Kiti cha Urais - JamiiForums


Kama tuhuma hii ni kweli, then serikali ya rais Magufuli itakuwa ni serikali haramu na serikali iliyopatikana kwa njia za udhalimu na udanganyifu wa kwenye sanduku la kura, kitu ambacho sio kizuri kwa mustakabali mwema wa taifa letu kwa mujibu wa sheria ya karma.

Kwa mujibu wa katiba yetu, Tume ya Uchaguzi, ikiisha kumtangaza fulani ndie mshindi, kwa tangazo hilo ndio limehitimisha rasmi mchakato wote wa uchaguzi wa urais.

Mgombea urais akiishatangazwa kuwa ni mshindi, regardless amepatikanaje, kihalali au kiharamu, by means of hooks or crooks, kwa bao la kisigino, faulo au bao la mkono, as long as yeye ndie ametangazwa mshindi, this is the end that justifies the means!, there is nothing more anyone can do, ukubali usikubali matokeo, uwe ulimchagua, au hukumchagua, umtambue, au usimtambue, its never gonna change a thing!, huyu sasa ndie rais wetu and this is a fact!.

Kitu kizuri kuhusu haki, haki kamwe huwa haipotei, hata kama sio kwa dunia hii, bali kwa dunia ijayo, na ubaya siku zote huwa haulipi na malipo yote ni hapa hapa duniani, hata kama sio kwako, then kwa kizazi chako!.

Then namshauri Edward Lowassa, kuwa umetimiza wajibu wako, kutaka kuwatumikia Watanzania!. Umefanya kazi yako, imekamilika!. Sasa nakuomba statement yako hii iwe ndio ya mwisho, usiendelee kulalamika popote, bali sasa nenda zako kajipumzikie kwa amani kwa kuchunga ng'ombe wako kama ulivyoahidi, tena usipeleke malalamiko yako mahali pengine popote zaidi ya kwa aliye JUU, hivyo haya meingine yote muachie Mungu!, YEYE ndiye atakulipia!. kuna mahakama ya haki kuliko mahakama zote za dunia hii, au za ulimwengu huu!, hii ni mahakama ya karma, ndio mahakama pekee ya haki bin haki!.

Kwa wale wote waliomchagua Lowassa lakini haki zenu zikadhulumiwa, poleni sana!, Mungu atawalipia.

Na wale wengine wote wanaoshangilia ushindi haramu, ushindi dhalimu, hawa wanashangilia ujinga!, hawa nao pia watakuwa na sehemu ya malipo yao kwenye karma.


Na kama ni kweli Magufuli ameupata urais wa Tanzania kwa hila, na udhalimu, then tutashuhudia utawala wa mkono wa chuma, the reign of terror and iron hand. Mtashuhudia udikiteta na udhalimu wa ajabu, kuna watu kwa sasa wanashangilia, lakini mwisho wa siku, watakuja kulia na kusaga meno!.

Kama uchaguzi mkubwa hivi wa rais na wabunge kumeweza kufanyika hila, hii inamaanisha kule ambako wapinzani wameshinda ni maeneo ambako hila zimeshindikana, hivyo kwa uchaguzi wa 2020, wapinzani jiandaeni kuyarejesha majimbo karibu yote na nchi kurejea kwenye mfumo wa chama kimoja.

Kipimo cha hili kitapimwa kwa chaguzi ndogo zozote zitakazotokea hapa katikati, kwanza upinzani hautaweza tena kushinda uchaguzi wowote, na kama kiti cha ubunge au udiwani kilichokuwa kinashikiliwa na upinzani kitakuwa wazi, uchaguzi wa marudio utakirudisha CCM kwa mbinu zile zile dhalimu by hooks and crooks!.

Kama tuhuma hizi za Edward Lowassa ni kweli kuwa ushindi wa Magufuli umetokana na hila na dhulma katika uchaguzi mkuu, then hasira ya Mungu itatuwakia juu ya Tanzania yetu, tutapata mabalaa na majanga ya ajabu ajabu kwa sababu ya hasira ya Mungu, na sisi wote kama taifa, we will all suffer!, tutasuffer sana na kuna watu hadi wataangamia!.

Ila pia, endapo tuhuma hizi ni za uongo, ni za kupika na ni uzushi, then rais John Pombe Joseph Magufuli, ndiye rais chaguo la Mungu kwa Tanzania aliyetangazwa mshindi siku yake ya kuzaliwa!, katika uchaguzi huru na wa haki, hivyo atasimama test in time, of which time will tell!.

Kupitia kwa Magufuli, Tanzania itapata neema, mafanikio na maendeleo makubwa ya ajabu kwa sababu ya baraka za Mungu zitakuwa juu yake, nchi yetu inakwenda kageuka kuwa ni ile nchi ya ahadi ya maziwa na asali.


Neno litasimama, mambo mengine yote yatapita, lakini neno litasimama!.

Mungu ibariki Tanzania.

Paskali

Kwa rejea mambo ya karma, karibu mitaa hii
"The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili
"Bora Katiba", Tuikubali!, Tusiichukie CCM!, Kwa Sababu
When Karma comes calling, she stings like a bitch
Psychic Powers: Ni Nguvu za Kufanya Miujiza. Wengi wanaz
"Will Powers!", "Faith Healing!"-Nguvu ya Miujiza Ya Uponyaji kwa
Paschal, heshima kwako! Hebu in future jaribu kusummarize posts zako, watu hawana muda mwingi wa kusoma. Nawakilisha maoni ya wengi, jaribu kulifanyia kazi mkuu!
 
Paschal, heshima kwako! Hebu in future jaribu kusummarize posts zako, watu hawana muda mwingi wa kusoma. Nawakilisha maoni ya wengi, jaribu kulifanyia kazi mkuu!
Asante, hili nimeisha anza kulifanyia kazi kwenye bandiko hili nimelichinja. Mimi ni story teller, ila nakubaliana na wewe, Watanzania wengi ni wavivu kusoma, na sijui wangapi humu wana soma novels, au kuangalia telenovelas!.

Nitajitahidi sana kila bandiko langu in future kuwa na summary kwa ajili ya wavivu wa kusoma, halafu kuwe na long version ya wapenda mastori.

P
 
Pasco nimeanza kujiogopa aisee
nilisema lazima Pasco atazungumzia karma....nikawa naingia JF nitazame thread gani utaanzisha
halafu nakuta kweli umeanzisha thread kuhusu Karma....nimejiogopa mkuu..

Kwa kuongeza mkuu Pasco.....nimejiuliza ni bahati mbaya makamu mteule anaitwa Suluhu?
tazama hilo jina.....vowels zinajirudia kama Nyerere Kawawa Makamba Jakaya...nafikiri umeelewa kitu hapo..
Mkuu The Boss, japo hoja yako hii ni ya zamani, lakini umetisha sana!. I think something was going to happen, ili kuzuia that something isi happen, ndio mkambidi mtu aitwe, achukuliwe na kuleta Suluhu ili kuleta suluhu ya hali iliyokuwepo!.
P
 
Back
Top Bottom