Kama huna Vigezo, hii Dunia utakuwa msindikizaji na kulialia!

Kama huna Vigezo, hii Dunia utakuwa msindikizaji na kulialia!

Yakobo ilikuwa ni ahadi kutoka kwa Mungu kabla hata Yakobo na Esau hawajazaliwa, imeandikwa ''mkubwa atamtukikia mdogo, na Mungu anasema nimempenda Yakobo na Esau nimemchukia''. Pia pamoja na yote ule uongo alioutenda Yakobo nae alilipwa kule kwa mjomba wake nae alidanganywa baada ya kutumika miaka saba ili ampate Raeli lakini alipewa Leah, kwahiyo ikamlazimu afanye kazi miaka saba mingine ili ampate Raeli ambaye ndiye chaguo lake.
Sahihi kabisa.
 
Wewe Ukilialia wenzio wanatoboa kupitia kilio chako wanakuacha uendelee kulia tena watoboe tena,Mwisho unazeeka unalia.
 
Yakobo ilikuwa ni ahadi kutoka kwa Mungu kabla hata Yakobo na Esau hawajazaliwa, imeandikwa ''mkubwa atamtukikia mdogo, na Mungu anasema nimempenda Yakobo na Esau nimemchukia''. Pia pamoja na yote ule uongo alioutenda Yakobo nae alilipwa kule kwa mjomba wake nae alidanganywa baada ya kutumika miaka saba ili ampate Raeli lakini alipewa Leah, kwahiyo ikamlazimu afanye kazi miaka saba mingine ili ampate Raeli ambaye ndiye chaguo lake.

Nakubaliana na wewe.
Ila zingatia kuwa sio kila Uovu utaadhibiwa nao, na wala sio kila wema utabarikiwa nao
 
Leo umeandika madini.

Ila tofauti kati ya R na L inasumbua wengi
 
Sahihi kabisa Kuna watu tulilalamika na kulialia kwamba Magufuli mbaya , lakini Kuna watu walitoboa na kuneemeka, kaingia mama wakati wengine wanalia lia Kuna wengine wanasema mama anaupiga mwingi na wananeemeka pia. Wakati wengine wanalia lia kuhusu vita ya Ukraine na Russia kuwa imepandisha gharama za maisha kitu ambacho ni kweli lakini Kuna wengine hizo gharama zilizopanda wamepanda nazo huko huko juu.

Nilichojifunza yatupasa kugangamala/ kukomaa regardless maisha yamebadilika kwa namna gani au Hali imekaaje.

Kuhusu ardhi ni kweli na ndio asili ya mafanikio ambayo Mungu ameachilia kwa mwanadamu tangu kuumbwa kwake, tutafute ardhi kwa ajili ya kuwarithisha watoto wetu, Kuna baadhi ya wazazi kwa uvivu ama kuto kujua wanawaambia watoto wao kuwa mwanangu nimekusomesha, elimu ndio urithi wako kitu ambacho sio kweli elimu haijawahi kuwa urithi popote bali ardhi na mali zingine zisizohamishika ndio urithi. Bibilia unasema Baba mwema huacha urithi kwa watoto wake.
 
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Yakobo alimtendea Uovu Kaka yake Esau Kwa kuiba Baraka, lengo lake lilikuwa kufanikiwa,
Uliona hao waisrael wakiwa wamelaaniwa?

Inategemea na Uovu unaoutenda, na pia Inategemea na wema unaoutenda,

Sio kila wema uufanyao utapata baraka,
Na sio kila Uovu uufanyao utapata Laana.

Hiyo ndio Dunia ilivyo Mkuu.
Na wengi wanaotenda uovu hufanikiwa angalia wazungu walituuwa na kututawala wala hawajapata laana ndyo kila siku wanafanikiwa matajiri wakubwa wanafanikiwa Kwa kuiba na kupora Kwa wengine dunia hii bila roho ngumu huwezi fanikiwa wala kutoboa wengi waliofanya maamuzi magumu ndyo hufanikiwa ukijifanya kunyenyekea watu na kuwanusa matako utabaki ivyoo ivyo sikuzote
 
Kwema Wakuu!

Kwa miaka michache niliyopata kuishi Duniani niliweza kugundua kuwa hii dunia ina vigezo na masharti vinavyozingatiwa, ukiwa huna Vigezo hivyo na Kama hutofuata masharti jua utaendelea kubaki kulialia na kuwa msindikizaji.

Dunia inatisha Ila nilikuambia usiogope.

Tangu nikiwa mdogo nilisikia watu wakilalamika, mpaka napata Akili na kujiita Taikon bado watu walewale wanalalamika kilichobadilika ni ongezeko Lao kwani wasindikizaji huzaa na kuzaliana,

1. Mtu unalialia hakuna Ajira alafu hujasoma hii inafurahisha Sana, hata Ajira zikitoka wataajiriwa waliosoma, Mimi na Wewe madarasa madogo tutaendelea kuwa wasindikizaji.
Hili suluhusho lake ni kusoma, Taikon anawaambia watu kutoka jamii masikini, somesheni watoto wenu kivyovyote, iwe kihalali au kuiba mitihani, kivyovyote mtoto wako asome, maisha huko mbeleni hayataangalia ulikuwa mtenda haki au vipi.

Nina ushahidi wa kutosha juu ya hili, wale walioambiwa wameiba majina miaka Ile ili watoto wao wafaulu leo hii watoto haohao ndio maafisa, linapokuja suala la maisha usiogope, usiwe mzembe mzembe,

Usijejidanganya elimu haina msaada, utakuwa mjinga wa mwisho kabisa, Elimu ni elimu tuu, mpe mtoto wako Elimu ikiwa wewe ulizembea, dunia hii ni ya waliosoma na wenye vipaji.

2. Kuna watu walikuwa wakilia ukame, hakuna mvua lakini mvua zikinyesha hawana hata mashamba, wanaopata chakula ni walewale hasa wenye mashamba ndio wanakula maisha
Hilo Taikon alishalitambua angali yupo shule ya Msingi, nilisoma Biblia vyakutosha ningali sijabalehe, vita karibu zote za Biblia ilikuwa kugombea Ardhi, nilipokua kidogo nikiwa sekondari nikasoma mambo ya Ukoloni kisha vita karibu vyote vya kihistoria sababu kuu ni kugombea Ardhi, Ardhi ni kitu cha thamani,

Kijana hakikisha unapata Ardhi kadiri uwezavyo, iwe mjini au kijijini, iwe visiwani au barani, kufa kupona upate Ardhi,

Ardhi ndio Urithi wapekee Kwa watoto na wajukuu, mnyime mtoto yote lakini usimnyime Ardhi,

Ukilima huwezi kukosa chakula abadani, Babu yangu, Mzee Clifford Tenga aliyekuwa diwani Kisiwani, Same aliwahi kuniambia; Ukishakuwa na Shamba maisha hayawezi kukusumbua, Hakikisha hata Kama unakazi gani usiache Kulima"
Mungu ailaze Roho yake mahali panapomstahili, nilikuja kumuelewa baadaye nilipomaliza chuo.
Nami bila uchoyo nasema, ukiwa na Shamba maisha hayawezi kukushinda abadani.

3. Wengi wanalialia kusumbuliwa na wenza wao, wanawake wanasema wanaume siku hizi wamebweteka, hawana sifa za kuitwa wanaume.
Huku wanaume nasi tukisema, wanawake WA siku hizi hawana sifa za kuwa mke.
Lakini katika Hilo usipokuwa na vigezo na masharti kwenye ndoa pia utakuwa msindikizaji na hutoacha kulialia.

Mwanamke lazima ujitambue, ujue ukoje na unastahili mwanaume wa Aina gani, halikadhalika na kwetu wanaume.
VIGEZO ni muhimu kuliko Jambo lolote kwenye maisha,
Sio utake mwanamke asiye WA kiwango chako atakusumbua, au sio uchukue mwanaume asiye WA kiwango chako atakusumbua.

Ndio Yale mtu anaona aibu kumtambulisha Mke au mume wake mbele ya watu, kisa vigezo havijadhingatiwa, dunia huwaga inatabia ya kuweka kila kitu sehemu yake, mahali panapostahili, ukijifanya kujiseti usipotakiwa Dunia itakuweka sehemu yako Kwa maumivu makali Sana.

Ngoja nipumzike kwanza,

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Kwa hiyo hapa umekufa maana sijaelewa
 
Sahihi kabisa Kuna watu tulilalamika na kulialia kwamba Magufuli mbaya , lakini Kuna watu walitoboa na kuneemeka, kaingia mama wakati wengine wanalia lia Kuna wengine wanasema mama anaupiga mwingi na wananeemeka pia. Wakati wengine wanalia lia kuhusu vita ya Ukraine na Russia kuwa imepandisha gharama za maisha kitu ambacho ni kweli lakini Kuna wengine hizo gharama zilizopanda wamepanda nazo huko huko juu.

Nilichojifunza yatupasa kugangamala/ kukomaa regardless maisha yamebadilika kwa namna gani au Hali imekaaje.

Kuhusu ardhi ni kweli na ndio asili ya mafanikio ambayo Mungu ameachilia kwa mwanadamu tangu kuumbwa kwake, tutafute ardhi kwa ajili ya kuwarithisha watoto wetu, Kuna baadhi ya wazazi kwa uvivu ama kuto kujua wanawaambia watoto wao kuwa mwanangu nimekusomesha, elimu ndio urithi wako kitu ambacho sio kweli elimu haijawahi kuwa urithi popote bali ardhi na mali zingine zisizohamishika ndio urithi. Bibilia unasema Baba mwema huacha urithi kwa watoto wake.
Cha kusikitisha kizazi cha sasa hivi ingawa siyo wote ukiwaachia urithi ukifa wanauza.

Nimeliona hili sehemu nyingi sana na hakuna ambaye nimeona akiuza nyumba ya urithi zile pesa zikaja kuzaa mali nyingi zaidi, binafsi sijawahi kumuona aliyetobowa kwa kuuza urithi aliorithi.
 
Cha kusikitisha kizazi cha sasa hivi ingawa siyo wote ukiwaachia urithi ukifa wanauza.

Nimeliona hili sehemu nyingi sana na hakuna ambaye nimeona akiuza nyumba ya urithi zile pesa zikaja kuzaa mali nyingi zaidi, binafsi sijawahi kumuona aliyetobowa kwa kuuza urithi aliorithi.
Hilo ndio janga la wavivu wanafikiri katika kuuza Sio kuendeleza, ingefaa sana tungejikita kuendeleza vya urithi mahangaiko na tabu zisingekuwa kubwa, ushaambiwa jasho la Mtu haliliwi ndio Maana wanaouza hizo nyumba huwa hawafanikiwi
 
Tatizo unaweza kujiona unavigezo kumbe hivyo siyo kabisa.Sasa nani ahakikishe kuwa ulivyonavyo ndiyo sahihi,hayupo.
Maisha hayatabiriki!
Leo king msukuma ndo anaoneka kuwa na vigezo!!??
Uliyoyataja yaweza kusaidia kwa kiasi chake lakini si kusema kwamba ukiwa na hayo ndo ushayapatia maisha!
 
Back
Top Bottom