Kama kifo ni mapenzi ya Mungu kwa nini mabilionea wanaishi muda mrefu?

Kama kifo ni mapenzi ya Mungu kwa nini mabilionea wanaishi muda mrefu?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kila mtu anapofariki hata kama ni kijana mdogo kabisa kauli utakazozisikia ni "mapenzi ya mungu", "mungu amempenda zaidi" na kauli nyingine za aina hiyo, sasa kwa nini mabilionea mungu hawapendi zaidi mapema na wengi huishi muda mrefu hadi kuzeeka tofauti na masikini?

Ni nadra sana kusikia billionea kafa akiwa na umri chini ya miaka 50.
 
Kila mtu anapofariki hata kama ni kijana mdogo kabisa kauli utakazozisikia ni "mapenzi ya mungu", "mungu amempenda zaidi" na kauli nyingine za aina hiyo, sasa kwa nini mabilionea mungu hawapendi zaidi mapema na wengi huishi muda mrefu hadi kuzeeka tofauti na masikini?

Ni nadra sana kusikia billionea kafa akiwa na umri chini ya miaka 50.
Mfano?
 
Kila mtu anapofariki hata kama ni kijana mdogo kabisa kauli utakazozisikia ni "mapenzi ya mungu", "mungu amempenda zaidi" na kauli nyingine za aina hiyo, sasa kwa nini mabilionea mungu hawapendi zaidi mapema na wengi huishi muda mrefu hadi kuzeeka tofauti na masikini?

Ni nadra sana kusikia billionea kafa akiwa na umri chini ya miaka 50.
Unaujua utajiri wa Lau Mafuru?
 
Kufa hakuna kanuni zaidi ya wakati ukifika(there's always right time for death), huwezi kusema wakati wake ulikuwa bado.

Whitney Houston
Michael Jackson
Nk.
 
Kufa hakuna kanuni zaidi ya wakati ukifika(there's always right time for death), huwezi kusema wakati wake ulikuwa bado.

Whitney Houston
Michael Jackson
Nk.
Michael Jackson, miaka 50
 
Masikini wanaishi katika hatari nyingi, huduma za afya, maji machafu, stress, kurogana. Ndio maana masikini huzaa watoto wengi, wanakuwa kama betting, au insurance scheme.......anajua mmoja anaweza kubebwa na wachawi, mwingine kipindupindu, mwingine magonjwa na mwingine anakuwa wa mapenzi ya Mungu.

Wanabaki wale waliopenya tundu la sindano.

Anyway, ukienda dukani ukaona bidhaa zina expiry date, hata wewe unayo expiry date, ila kimaadili huwezi ambiwa hata kama uko hoi hospitali. Imagine una bango kifuani kwamba umebakiza siku mbili unakatiza nalo kariakoo!
 
Kila mtu anapofariki hata kama ni kijana mdogo kabisa kauli utakazozisikia ni "mapenzi ya mungu", "mungu amempenda zaidi" na kauli nyingine za aina hiyo, sasa kwa nini mabilionea mungu hawapendi zaidi mapema na wengi huishi muda mrefu hadi kuzeeka tofauti na masikini?

Ni nadra sana kusikia billionea kafa akiwa na umri chini ya miaka 50.
kufa maskini au tajiri Tanzania ni uamuzi binafsi tu gentleman,

ni bidii na kutokukata tamaa mambo yanakuendea vizuri, Mungu ni wetu sote 🐒
 
Uzi wako na mada yako umeuliza swali la maana kabisa. Majibu yanaweza kuwa mawili:

1. Mabilionea wengi kupata utajiri huo katika umri mkubwa, hapa tunaongelea 35-50 kwahiyo wengi huwa wanajikuta wapo na muda mrefu wa kuishi mpaka miaka 70-90

2. Matajiri wanapata huduma bora za afya, hali bora za maisha, lishe bora, viwango vidogo vya msongo wa mawazo, muda wa mazoezi na afya, wanafanya kazi zisizochosha mwili, wana bima za afya na rasilimali za kifedha za kutosha.

Sasa ukimlinganisha mtu huyu na kapuku lazima kapuku aage ulingo wa mapambano mapema: elimu juu ya afya hana, masaa 12 yupo kazini, hapati muda wa kupumzika vya kutosha na kufanya mazoezi, afya duni, mawazo kuhusu maisha yake na familia. Kukosa fedha kunaongeza zaidi njia za mtu kufa mapema: kukosa bima za afya, mtindo mbovu wa maisha, kulazimika kutumia miundombinu mibovu inayohatarisha maisha: ndiyo maana waganga njaa wengi wanaondoka kwa ajali za mabasi, mafuriko n.k.
 
Uzi wako na mada yako umeuliza swali la maana kabisa. Majibu yanaweza kuwa mawili:

1. Mabilionea wengi kupata utajiri huo katika umri mkubwa, hapa tunaongelea 35-50 kwahiyo wengi huwa wanajikuta wapo na muda mrefu wa kuishi mpaka miaka 70-90

2. Matajiri wanapata huduma bora za afya, hali bora za maisha, lishe bora, viwango vidogo vya msongo wa mawazo, muda wa mazoezi na afya, wanafanya kazi zisizochosha mwili, wana bima za afya na rasilimali za kifedha za kutosha.

Sasa ukimlinganisha mtu huyu na kapuku lazima kapuku aage ulingo wa mapambano mapema: elimu juu ya afya hana, masaa 12 yupo kazini, hapati muda wa kupumzika vya kutosha na kufanya mazoezi, afya duni, mawazo kuhusu maisha yake na familia. Kukosa fedha kunaongeza zaidi njia za mtu kufa mapema: kukosa bima za afya, mtindo mbovu wa maisha, kulazimika kutumia miundombinu mibovu inayohatarisha maisha: ndiyo maana waganga njaa wengi wanaondoka kwa ajali za mabasi, mafuriko n.k.
Hapa Umefafanua vizuri mkuu
 
Hakunaga cha wakati ukifika, mara nyingi ni changamoto za magonjwa na kushindwa kumudu matibabu.
Ndio wakati wenyewe huo, mda wangu ukifika kwa namna yoyote iwe ajali, ugonjwa au nikiwa nimelala tu nitakufa
 
Ndio wakati wenyewe huo, mda wangu ukifika kwa namna yoyote iwe ajali, ugonjwa au nikiwa nimelala tu nitakufa
Kama utaumwa na kufa kwa kukosa dawa kwa ugonjwa unaotibika utasema hayo ni mapenzi ya mungu?
 
Back
Top Bottom