Kama kifo ni mapenzi ya Mungu kwa nini mabilionea wanaishi muda mrefu?

Kama kifo ni mapenzi ya Mungu kwa nini mabilionea wanaishi muda mrefu?

Kufa hakuna kanuni zaidi ya wakati ukifika(there's always right time for death), huwezi kusema wakati wake ulikuwa bado
Ndugu ERoni, tambua kuwa wakati mwingine kuna issue ya pre-mature death, yaani wakati unakuwa bado haujafika wa kufa. Mfano: umelewa chakali kisha ukamua kuendesha gari lako pasipo kuzingatia kanuni sheria na taratibu za usalama barabarani, huku na kule ukakutana na semi limechochea speed kisha mkavaana uso kwa uso (head on collision), hatimaye safari yako ya hapa duniani ikaishia hapa.
Kwa mfano huu, je, utasema kuwa wakati wako ulikuwa umefika?
.

Whitney Houston
Michael Jackson
Nk.
 
Je? jiulize matajiri ni wagapi? Ni masikini wapo wagapi! Duniani.
Je umasikini unaupimaje?

Au unaupima katika ago ya ubillionea?.

Kama matajiri ni asilimia 0.09 ya dunia unataka wafe sawa na 99.01% umesomea wapi wewe
 
Kama utaumwa na kufa kwa kukosa dawa kwa ugonjwa unaotibika utasema hayo ni mapenzi ya mungu?
Hakuna mapenzi ya Mungu, itakuwa wakati wangu tu umefika mimi kufa.
 
Mleta mada hana statistical data lakini kuna ukweli ndani yake,mbali na ajali vyanzo vya kifo kama predation disease kwake havina nafasi na hivyo ageing.Sisi masikini maisha yetu yanawindwa na maadui wengi mno.Mfano:maeneo yaliyoathiriwa na ushirikina survival yako nawe uwe mshirikina vinginevyo huna maisha.Kuuana kwa sumu ni kawaida kitu ambacho si rahisi kumfikia bilionea.Kwa nini asifike uzeeni?
 
Kitu ambacho unatakiwa kufahamu ni kwamba billionaires kabla hajaufikia,akipambana yeye kama yeye lazima kuanzia 40's ndo utamsikia billionair, nadra sana kumsikia billionaire mwenye 30's labda pesa iwe ya familia,
Ukipambana na umri ulionao kuufikia lazima tu umri umeenda tayari
 
Je? jiulize matajiri ni wagapi? Ni masikini wapo wagapi! Duniani.
Je umasikini unaupimaje?

Au unaupima katika ago ya ubillionea?.

Kama matajiri ni asilimia 0.09 ya dunia unataka wafe sawa na 99.01% umesomea wapi wewe
Hapa kuna hoja pia, ila hata kama matajiri ni million 1 tu Tanzania tunaweza kuangalia asilimia(%) ya matajiri wanaofariki kwa mwaka tukalinganisha (%) ya masikini wanaokufa kwa mwaka.
 
Ndugu ERoni, tambua kuwa wakati mwingine kuna issue ya pre-mature death, yaani wakati unakuwa bado haujafika wa kufa. Mfano: umelewa chakali kisha ukamua kuendesha gari lako pasipo kuzingatia kanuni sheria na taratibu za usalama barabarani, huku na kule ukakutana na semi limechochea speed kisha mkavaana uso kwa uso (head on collision), hatimaye safari yako ya hapa duniani ikaishia hapa.
Kwa mfano huu, je, utasema kuwa wakati wako ulikuwa umefika?
Law of nature, ni lazima nife ili viumbe wengine wasurvive mkuu, hatuangalii sababu ya mimi kufa, kama ulikuwa wakati sahihi au la. Lazima asili ichukue nafasi yake, nife kwa namna yoyote ili viumbe wengine wapate kuishi.
 
Nimemkumbuka bilionea tanil somaiya

Ova
 
Japo muda mwingine kusema "kuna vifo vinaweza kuepushwa" Ni sawa na kusema kifo sio mpango wa Mungu ambavyo ukiviangalia kwa jicho lingine ni kupinga kuwa Mungu ndiye anaepanga tarehe za watu kufa..

Japo kwa namna nyingine Mungu alituumba kwa mfano wake, si kimuonekano bali kiutashi lakini kikubwa zaidi kutukabidhi milki na tawala ya dunia nzima. Hivyo tuna uwezo wa kufanya intervention na ikasaidia

Mfano vifo vya wajawazito na vichanga vyao umepungua baada ya maboresho ya sekta za kiafya lakini pia vifo vya ajali vilipungua baada ya kuboresha barabara nchi nzima. Lakini pia kupiga toch na kuzuia safari za usiku ilipunguza pia. Hii nilifanyia research kama data collection assistant wa project flani so nipo 100% sure


Hivyo, naamini kuna vifo vingi vinaweza kuepushwa ambavyo inakuwa reflected na life expectancy ya nchi. Nchi maskini watu wanakufa mapema kuliko nchi zilizoendelea kutokana na poor health care..

Ila mtazamo huu haupigiwi promo kwa sababu serikali yenyewe na wafanyakazi wake kama madaktari, huondolewa ile responsibility yao katika vifo kwa kusema kuwa kama ilipangwa na Mungu wao wasingeweza kuzuia, na hivyo kuepuka mkono wa sheria katika majanga yaliyosababishwa na udhembe wao.

Kwa hiyo naamini kuna vifo vinaepukika
 
Kifo sio mpango wa MUNGU,..... ni maneno ya binadamu tu, kwa kupenda kujifariji ,..✍️✍️
 
Wanamudu gharama zote za matibabu, kula yao ni ya uhakika, wana uwezo wa kuchungulia katika ulimwengu wa roho, mpaka mwili uzeeke ushindwe kufanya kazi, roho inaenda kuanzisha maisha mengine.
 
Kila mtu anapofariki hata kama ni kijana mdogo kabisa kauli utakazozisikia ni "mapenzi ya mungu", "mungu amempenda zaidi" na kauli nyingine za aina hiyo, sasa kwa nini mabilionea mungu hawapendi zaidi mapema na wengi huishi muda mrefu hadi kuzeeka tofauti na masikini?

Ni nadra sana kusikia billionea kafa akiwa na umri chini ya miaka 50.
Akili ni mali!!!!
 
Japo muda mwingine kusema "kuna vifo vinaweza kuepushwa" Ni sawa na kusema kifo sio mpango wa Mungu ambavyo ukiviangalia kwa jicho lingine ni kupinga kuwa Mungu ndiye anaepanga tarehe za watu kufa..

Japo kwa namna nyingine Mungu alituumba kwa mfano wake, si kimuonekano bali kiutashi lakini kikubwa zaidi kutukabidhi milki na tawala ya dunia nzima. Hivyo tuna uwezo wa kufanya intervention na ikasaidia

Mfano vifo vya wajawazito na vichanga vyao umepungua baada ya maboresho ya sekta za kiafya lakini pia vifo vya ajali vilipungua baada ya kuboresha barabara nchi nzima. Lakini pia kupiga toch na kuzuia safari za usiku ilipunguza pia. Hii nilifanyia research kama data collection assistant wa project flani so nipo 100% sure


Hivyo, naamini kuna vifo vingi vinaweza kuepushwa ambavyo inakuwa reflected na life expectancy ya nchi. Nchi maskini watu wanakufa mapema kuliko nchi zilizoendelea kutokana na poor health care..

Ila mtazamo huu haupigiwi promo kwa sababu serikali yenyewe na wafanyakazi wake kama madaktari, huondolewa ile responsibility yao katika vifo kwa kusema kuwa kama ilipangwa na Mungu wao wasingeweza kuzuia, na hivyo kuepuka mkono wa sheria katika majanga yaliyosababishwa na udhembe wao.

Kwa hiyo naamini kuna vifo vinaepukika
Mifano imekaa fresh sana.

Hivi hili jambo viongozi wa kiimani wanasema vipi?
 
Kila mtu anapofariki hata kama ni kijana mdogo kabisa kauli utakazozisikia ni "mapenzi ya mungu", "mungu amempenda zaidi" na kauli nyingine za aina hiyo, sasa kwa nini mabilionea mungu hawapendi zaidi mapema na wengi huishi muda mrefu hadi kuzeeka tofauti na masikini?

Ni nadra sana kusikia billionea kafa akiwa na umri chini ya miaka 50.
Si unajua dini inafanya kazi kubwa mbili..
Moja, kuwapa binadamu matumaini hewa kwa faida ya wamiliki wa mfumo wa dini.
Pili, kuwajaza binadamu hofu na utii kwa faida ya tawala/serikali.

Hivyo, hizi kauli za bwana ametwaa ni sehemu tu ya kupeana matumaini, ila ukweli ni kwamba mtu hufariki kwa kuwa maarifa ya anyemtibu yamefika kikomo, au mifumo yake ya mwili imeharibiwa sana kwa ajali n.k.
The imaginary God has nothing to do with it.
 
Mifano imekaa fresh sana.

Hivi hili jambo viongozi wa kiimani wanasema vipi?

Sidhani kama hii issue imeshawahi kujadiliwa kiundani haswa kutokana na maandiko.

Mwisho wa siku tunabaki kuamini kuwa kuzaliwa na kifo ni ahadi kuwa lazma mtu utakufa lakini haijaanishwa kama mtu anaweza kuendelea kuishi endapo kama kuna vitu vinaweza kufanyika.

Mfano kuna maskini wengi sana wanafariki kwa kukosa pengine pesa ya dawa na hospital kiasi ambacho wanarudishwa nyumbani kusikiliziwa which is a soft way ya kusema. Tunasubiri afe lakini kwa issue hiyo hiyo kuna mtu anapelekwa india na anapona.

Kwa hiyo ukiangalia kwa ujuujuu unaona tu vifo vingi vinazuilika na kuepukika kama pande zote zikiwa responsible.

Japo mtihani ni kuwa viongozi wa dini wanatuambia tu kifo ni ahadi. Na hawatuambii zaidi ya hapo japo Zaburi ilitaja miaka 70-80 which is below life expectancy ya Tanzania ambayo ipo 60's Ila duniani huko hadi 100 inafika.
 
Kila mtu anapofariki hata kama ni kijana mdogo kabisa kauli utakazozisikia ni "mapenzi ya mungu", "mungu amempenda zaidi" na kauli nyingine za aina hiyo, sasa kwa nini mabilionea mungu hawapendi zaidi mapema na wengi huishi muda mrefu hadi kuzeeka tofauti na masikini?

Ni nadra sana kusikia billionea kafa akiwa na umri chini ya miaka 50.
Mimi kwa kipindi kirefu sana nimekuwa na jiuliza mambo kama haya pale nilipoanza kusikia heti vifo vya watoto vimepungua kutokana na jitihada na huduma ya bure ya mama na mtoto akili yangu ikaanza kufunguka na kuanza uchuguzi
Niligundua kuna aina tatu za kifo

1:Kifo cha kujitakia
2:kifo cha kusababishiwa
3: kifo cha uzee hasa hiki ndio original
Vingine vyote vina epukika kasolo hicho
Kwa mtu asiye tukia akili vizuri akisikia kuna vifo vinavyoepukika ana shangaa

Iko hivi Mungu aliweka kanuni mbalimbali
Kanuni kuu ni kila mwenye mwili ataonja mauti lini na wakati kani hilo sio jukumu lake
Binadamu alipewa nguvu kubwa sana ya kuamua hatima yake
Hosea 4:6 Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako. My people are destroyed for lack of knowledge:

Kumbukumbu la Torati 30:15 Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya; “

Kumbukumbu la Torati 30:19 Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; I
Sasa hapa kuna mambo mengi unatakiwa utulize akili kuelewa

1: kifo kinatokea ikiwa kanunu zimevunjwa au kanuni inachukua mkondo wake

Mwanzo 3:3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.
Hapa tunaona Mungu ameweka kanuni ya kwanza kwamba ikiwa utakula matunda hayo utakufa kwa msingi huu kwamba ikiwa utavunja kanuni hii kifo kitatokea
Sasa twende pamoja

* kanuni zipo nyingi
*kanuni si lazima uvunje wewe anaweza
kuvunja mwingine wewe ukakutano na kifo
Kwa uchache kanuni mbalimbali
Hapa nachahua chache

1: kanuni ya afya unakula nini unakunywa nini
Ikiwa utavunja kanuni bora za ulaji kifo kitatokea na sababu umevunja kanuni bora ya ulaji na unywaji
Hii ni pamoja na kanuni za mapumziko,mda wa kulala nk mengi hufundiswa na watahalamu wetu
Wewe ni shahidi mnavyo pingana na docta wa mhimbili kuusu ulaji

2: kanunui ya usalama hii inajumuisha mwienendo yote ya kutenda mazingira ya kazi uangalifu sehemu mbalimbali
Kama kuvunja kanuni za upepo,moto ,maji,
Usalama sehemu za mwitu nk iwe wewe au mwingine kifo kinaweza kuyokea
Mfano yankawaida
Deleva asiyefata kanuni za usalama barabarani anaweza kusababishia wengine na yeye kifo ,
Dakitari asiye na ujuzi au kafanya makosa anaweza kusababisha kifo
Mtu usika asiye zingatia kanuni mbalimbali za kuvuka barabara anaweza kusababisha kifo
Kumbe ni mhimu katika maisha yetu kuzingatia kanuni ili kuwa ma maisha marefu

3:kanuni ya kuishi na watu wengine
Mungu vile vile anazo kanuni za namna ya kuishi na watu wengine, ukivunja kanuni hiyo unaweza kusababisha kifo kutokana na magonvi na kuamisiana ,vita na mambo mabalimbali

4:kifo kutokana na uzee mwili umechoka viungo life time ya viungo vya mwili seli nk zimefika mwisho
Nayo hii kanuni uwezi kuivuka
5: mwisho kwa leo kuvunja kaninu za kiroho kunaweza kusababisha kifo

Kumbukumbu la Torati 28:15-50
 
sasa kwa nini mabilionea mungu hawapendi zaidi mapema na wengi huishi muda mrefu hadi kuzeeka tofauti na masikini?
 
Kila mtu anapofariki hata kama ni kijana mdogo kabisa kauli utakazozisikia ni "mapenzi ya mungu", "mungu amempenda zaidi" na kauli nyingine za aina hiyo, sasa kwa nini mabilionea mungu hawapendi zaidi mapema na wengi huishi muda mrefu hadi kuzeeka tofauti na masikini?

Ni nadra sana kusikia billionea kafa akiwa na umri chini ya miaka 50.
Uwepo wa bilionea ni faida kwa watu wengi sana
 
Ayubu 21:7, aliuliza swali kama lako au linaendana na lako


"Mbona wabaya wanaishi, wanakuwa wazee, naam, wanakuwa na nguvu nyingi?"

Swali hili linaonyesha mshangao wa Ayubu juu ya dhana ya haki ya Mungu katika ulimwengu unaoonekana kutozingatia matendo ya mtu. Wabaya mara nyingi huonekana kufanikiwa, huku watu wema wakipitia mateso.

Katika mjadala wa Ayubu:

1. Mtazamo wa binadamu kuhusu haki: Wanadamu mara nyingi wanadhani kwamba watu wema wanapaswa kufanikiwa, na wabaya wanapaswa kuadhibiwa mara moja.


2. Majibu ya Ayubu kwa marafiki zake: Ayubu anapinga wazo kwamba mateso huwapata tu waovu. Anatambua kuwa, kwa macho ya kibinadamu, mara nyingi maisha yanaonekana kinyume na matarajio haya.


3. Hekima ya Mungu: Mwisho wa kitabu cha Ayubu, Mungu anamjibu, akionyesha kuwa njia na mipango ya Mungu ni ya kina sana kuliko uwezo wa binadamu wa kuelewa. Mungu anafafanua kwamba haki ya kweli inatimia kwa wakati wake, hata kama haionekani mara moja.



Maandiko mengine yanayohusiana na swali hili ni pamoja na:

Zaburi 73: Mtunga Zaburi anauliza swali kama hilo lakini anahitimisha kwamba mwisho wa waovu ni uharibifu.

Mhubiri 8:14: Sulemani anasema kuna mambo yasiyoeleweka, kama jinsi waovu wanavyoishi kama wema, na wema wanavyoteseka kama waovu.


Swali hili linakualika kufikiria juu ya uaminifu kwa Mungu hata wakati mambo hayaeleweki, ukijua kuwa Mungu ndiye mwenye maarifa na haki ya mwisho.
 
Back
Top Bottom