Kama kijana nawezaje kuishi kwenye misingi ya dini(mlokole)

Kama kijana nawezaje kuishi kwenye misingi ya dini(mlokole)

Kuna wakati unafika unatamani kuishi katika misingi ya imani lakini ujana ni kama unakwamisha.

Changomoto kubwa ni vishawishi vya uzinzi na ulevi nawazaga sana vijana waliokoka wanawezaje kushindana na dhambi ya uzinzi na ulevi tena katika mji ambao wanawake wanavaa vimini na suruali za kubana mji ambao kuna baa kila kona katika dunia ambayo TV na Social network zimejaa content za ngono.

It's not easy.
huhitaji wakati mwingine wala haya makanisa ya Kilokole ili kuacha tabia mbovu.
wako vijana wameokoka lakini wanakila tabia mbovu hukohuko ulokoleni wanawashughulikia mabinti kupita kiasi na pia ni walevi.
wako pia vijana hawajaokoka lakini ni waaminifu mno kwa MWENYEZI MUNGU wanamweshimu MUNGU kupita hata wanavyomtaja wengi tu.
kwangu ningekushauri cha kwanza jua unataka nini kwa muda gani na kwa kiasi gani na utapataje unachotaka na kama hakipatikani njia gani zitumike ili uwe na maisha halali lakini yenye furaha na sio raha na kwakufanya hivyo fikra zako asubuhi ukiamka utawaza jinsi ya kupambana na malengo yako.
sintashangaa ukakaa siku mbili ukasahau kama Mzigo umesimama au haukusimama kwakuwa si hitaji lako la awali.
 
Haina maana ukiokoka unafanyika kuwa Malaika, hivyo hata hao unaowaona na kudhani wameokoka bado wanaishi kawaida tu.... ukijitesa sana hutoboi.
Waliookoka sio watu wa kawaida, huwezi kujilinganisha na wewe ambaye haujaokoka,na hawana maisha ya kawaida. labda wale waliojiunga tu na dini hao hata kama wapo huku wanabaki vilevile.

Ukiokoka, unafanyika mtoto wa Mungu. Wote waliompokea walifanyika kuwa watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio Jina lake. kwa maana hiyo, God will treat you as his child, jua kuwa hapa duniani unaweza kukabidhi maisha yako kwa shetani, ukawa mtu unategemea hirizi, waganga, uchawi, pesa zako, wanadamu n.k, na kuna wale hawategemei hivyo vyote, wamekabidhi maisha yao kwa Mungu. usifikiri Mungu ataendelea kukutreat wewe mtoto wake wakati umemkana na kwenda kwa shetani, unajifanya unamwomba Mungu na wakati huohuo unaenda kwa waganga, unamchanganya Mungu na hayo mengine, Mungu hadhihakiwi. HATA KAMA ANAWAMULIKIA JUA NA MVUA ANAWAPA WABAYA NA WEMA, ila practically au niseme specifically wapo wale ambao ukiwagusa umegusa mboni ya Jicho la Mungu, hao ndio wale waliokabidhi maisha yao kwa Mungu, wanamtegemea yeye na wanaishi kwa kumtegemea yeye.

hawa ni watoto wa Mungu kwamba hata wakifanya dhambi, they will be treated as watoto wa Mungu. mtoto wako akikosea utamtreat tofauti na mtoto wa wengine (mfano tu), hivyo ukifanya dhambi unakuwa umefanya ukiwa mikononi mwa Mungu hivyo ukitubu Mungu anakusamehe, na akiamua anakuadhibu kama mtoto vilevile. ndio maana wale awapendao huwa anawakemea na kuwarudi, ukiona umeishi kwenye dhambi hadi unaona dhambi ni kawaida tu, uzinzi kawaida tu unaufurahia, wizi, na dhambi zote unafanya na hakuna kukemewa moyoni jua Mungu alishakutapika wewe sio wa kwake.
1YOHANA 2:1 INASEMA: Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, nay endiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.

kwahiyo, kwasababu Yesu alikufa kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako, ukitenda dhambi ukiwa mikononi mwake, yeye (kama nafsi mojawapo ya Mungu) Damu yake inanena kwamba huyu nilikufa kwa ajili yake hivo asamehewe, wale ambao hawajakabidhi maisha kwa Yesu hawana mwombezi.
 
huhitaji wakati mwingine wala haya makanisa ya Kilokole ili kuacha tabia mbovu.
wako vijana wameokoka lakini wanakila tabia mbovu hukohuko ulokoleni wanawashughulikia mabinti kupita kiasi na pia ni walevi.
wako pia vijana hawajaokoka lakini ni waaminifu mno kwa MWENYEZI MUNGU wanamweshimu MUNGU kupita hata wanavyomtaja wengi tu.
kwangu ningekushauri cha kwanza jua unataka nini kwa muda gani na kwa kiasi gani na utapataje unachotaka na kama hakipatikani njia gani zitumike ili uwe na maisha halali lakini yenye furaha na sio raha na kwakufanya hivyo fikra zako asubuhi ukiamka utawaza jinsi ya kupambana na malengo yako.
sintashangaa ukakaa siku mbili ukasahau kama Mzigo umesimama au haukusimama kwakuwa si hitaji lako la awali.
wewe ndio umepotea mazima, na haujui kama umepotea. hauwezi kushinda dhambi bila kuokoka ili Yesu ayaongoze maisha yako, kwa nguvu zako huna uwezo kushinda dhambi hata ujitahidi vipi. pia, uwepo wa vijana waovu kwenye makanisa ya kilokole hakumaanishi makanisa hayo ni mabaya. na tukiongelea makanisa ya kilokole ondoa kichwani mwako makusanyiko yanayouza maji, mafuta na kutoa uchawi. ya kilokole yanajulikana. though haya ni madhehebutu lakini kinachofanya moja liwe zuri litakalokusaidia na lingine siliwe zuri lisiloweza kukusaidia ni MISINGI YAKE, nini wamesimamia.

1. Je, wanaamini kuokoka?
2. Je wanaamini ujazo wa Roho Mtakatifu aliyeahidiwa na Yesu mwenyewe?
3.Je wanahubiri utakatifu na kuacha dhambi? au mafuta, maria, maji na takataka zingine?
4. Je? Mungu anaonekana katikati yao? watu wakienda wanabadilika?
5. wakisema tuombe, wanaomba au wanasoma kitabu/katekisimo n.k wameandikiwa maombi na hakuna kupindisha miaka yote as if maisha au mahitaji ni yaleyale kila siku.
6. wananena kwa Lugha, manake bila hivyo, hakuna anayewasaidia kwenye maombi.

kwa ufupi tu, hiyo misingi ikiwepo, kanisa hilo linaweza kumsaidia mtu akamwona Mungu. sasa jichuje mwenyewe na jiulize kama upo kwenye makanisa ya aina hiyo, kama sio, unapoteza muda wako.
 
wewe ndio umepotea mazima, na haujui kama umepotea. hauwezi kushinda dhambi bila kuokoka ili Yesu ayaongoze maisha yako, kwa nguvu zako huna uwezo kushinda dhambi hata ujitahidi vipi. pia, uwepo wa vijana waovu kwenye makanisa ya kilokole hakumaanishi makanisa hayo ni mabaya. na tukiongelea makanisa ya kilokole ondoa kichwani mwako makusanyiko yanayouza maji, mafuta na kutoa uchawi. ya kilokole yanajulikana. though haya ni madhehebutu lakini kinachofanya moja liwe zuri litakalokusaidia na lingine siliwe zuri lisiloweza kukusaidia ni MISINGI YAKE, nini wamesimamia.

1. Je, wanaamini kuokoka?
2. Je wanaamini ujazo wa Roho Mtakatifu aliyeahidiwa na Yesu mwenyewe?
3.Je wanahubiri utakatifu na kuacha dhambi? au mafuta, maria, maji na takataka zingine?
4. Je? Mungu anaonekana katikati yao? watu wakienda wanabadilika?
5. wakisema tuombe, wanaomba au wanasoma kitabu/katekisimo n.k wameandikiwa maombi na hakuna kupindisha miaka yote as if maisha au mahitaji ni yaleyale kila siku.
6. wananena kwa Lugha, manake bila hivyo, hakuna anayewasaidia kwenye maombi.

kwa ufupi tu, hiyo misingi ikiwepo, kanisa hilo linaweza kumsaidia mtu akamwona Mungu. sasa jichuje mwenyewe na jiulize kama upo kwenye makanisa ya aina hiyo, kama sio, unapoteza muda wako.
umeandika mengi sana na mengine umeihukumu bila sababu lakini lililokubwa ni kwamba umejihesabia haki na wengine ukawaona ni takataka; lakini kaa ukijua kanisa haliendi mbinguni safari ya mbinguni ni ya mtu binafsi.
injili ya kuwatenga wadhambi imepitwa na wakati tunahitaji wadhambi waje jinsi walivyo wafanye mabadiliko ya mioyo yao.
aliyetumbukia ndani ya shimo anahitaji kamba au ngazi ili aweze kutoka na si vinginevyo.
Inawezekana wewe ukawa bado hujaokoka ila unasali kwa walokole
 
Kuna wakati unafika unatamani kuishi katika misingi ya imani lakini ujana ni kama unakwamisha.

Changomoto kubwa ni vishawishi vya uzinzi na ulevi nawazaga sana vijana waliokoka wanawezaje kushindana na dhambi ya uzinzi na ulevi tena katika mji ambao wanawake wanavaa vimini na suruali za kubana mji ambao kuna baa kila kona katika dunia ambayo TV na Social network zimejaa content za ngono.

It's not easy.
Tafiti zinaonyesha kuwa watu wengi wanaojifanya kuokoka ama kuishi kwa kufuata misingi ya dini za karne ya 1 na ya 6 hawana akili timamu. Huwezi ishi kufuata misingi ya dizi za watu zisizo na manufaa kwako kabla hujachanganikiwa na maisha. Jaribu uone.
 
Kuna wakati unafika unatamani kuishi katika misingi ya imani lakini ujana ni kama unakwamisha.

Changomoto kubwa ni vishawishi vya uzinzi na ulevi nawazaga sana vijana waliokoka wanawezaje kushindana na dhambi ya uzinzi na ulevi tena katika mji ambao wanawake wanavaa vimini na suruali za kubana mji ambao kuna baa kila kona katika dunia ambayo TV na Social network zimejaa content za ngono.

It's not easy.
Kujazwa kwa roho mtakatifu.
Kwa kutumia akili hutaweza.
 
umeandika mengi sana na mengine umeihukumu bila sababu lakini lililokubwa ni kwamba umejihesabia haki na wengine ukawaona ni takataka; lakini kaa ukijua kanisa haliendi mbinguni safari ya mbinguni ni ya mtu binafsi.
injili ya kuwatenga wadhambi imepitwa na wakati tunahitaji wadhambi waje jinsi walivyo wafanye mabadiliko ya mioyo yao.
aliyetumbukia ndani ya shimo anahitaji kamba au ngazi ili aweze kutoka na si vinginevyo.
Inawezekana wewe ukawa bado hujaokoka ila unasali kwa walokole
Ndugu yangu, tukija kwenye suala la kumwabudu Mungu, unapaswa kuambatana na wale wenye mlengo mmoja na wewe. ila kwenye maisha ya kawaida hautakiwi kuwatenga. Hakuna ushirikiano katika kuabudu kati ya mtu anayeshinda kwa waganga wa kienyeji au aliyevaa hirizi na anayemwabudu Mungu katika kweli. Utajifariji sana lakini ukweli ndio huo.

2 WAKORINTHO 6:14 - 18 INASEMA:

14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? 15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini? 16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 17 Kwa hiyo,
Tokeni kati yao,
Mkatengwe nao, asema Bwana,
Msiguse kitu kilicho kichafu,
Nami nitawakaribisha.
18 Nitakuwa Baba kwenu,
Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,
asema Bwana Mwenyezi

.
 
Back
Top Bottom