Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

labda yesu
 
Magufuli the best president ever and forever... Wanacheza n akili zetu aiseeee
 
Ashazimwa huyo mtu wenu.
Inabidi MATAGA mkubali kuwa mliyemfanananisha na yesu kesha kufa.
 
Majizi wakubwa sana wa rasilimali za watanzania
 
Mkuu mwanakijiji umewaza peke yako hiki ulichoandika kwa watu wengi wamebebwa na mdundiko hawawezi kukuelewa lakini ni point kali sana!
MATAGA, CHAWA, waramba miguu mmebakia mnalia lia tu
 
wazee wa ku twist maneno washajiwekea mawazo yao kichwani kua kwa hoja walizonazo ni ngumu kumshawishi mtu kua jpm alikua fair na ndio maana watetezi wake wanapindisha maneno
Ni kikundi cha propaganda kinaendeleza propaganda yani wanapindisha maneno nahawakuanza leo. Prof Assad alisea 1.5 tillion hazionekani zilipo, eti mwenda zake akamuuliza eti report yako inasema kuna wizi wa 1.5 tilion? Assad akajibu hapana.
Na alifanya kusudi tu maana Assa hakusema zimeibwa ila alisema matumizi yake hayajulikani.
Sasa wanataka kutumia popaganda kuishusha report ya CAG kwa kugeuza maneno na wajinga wajinga watawaamini.
 
Elimu bure ni sera ya zamani sana ,tangu uchaguzi wa mwaka 2000 ,wapinzani walishalisema hili. Hii haiwezi kuwa hoja kwa sasa. Tafuteni namna ya kumtetea mtu wenu.
Tunao mfano wa Kadata : The guy is the most efficient and very innovative in tax collection, na hata miradi Mikubwa Mwendazake he begun to finance during Kadata tenure, Prucurement of new aircrafts, Nyerere dam financing conception and etc. Lakini ana mkono mrefu.

Sasa mkiwa mnashida mnatumia werevu wake kwa kile wataalamu wengine hawana, mkimalizana anaenda.
 
Subiri kidogo, miradi yote tunayoiona itasimama, ndipo utajua tofauti kati ukweli na uongo. Kati ya Rais na mwimba taarabu.

Awamu zote za marais waislam nchi hii huyumba sana. Subiri tu ujionee.
acha udini
 
Mwanakijiji nawe umejisajili kwenye haya mawazo? Ripoti nzima ya CAG hakuna mahali imesema Magufuli aliiba pesa, bali imeanisha namna mbali mbali ambavyo serikali na taasisi zake zimekiuka ama kutumia pesa ya walipa kodi vibaya. Je hili nalo unaona ni baya? Ama kosa ni sisi kuambiwa haya? Magufuli he may have a lot of good deeds, ila kosa kubwa alilolifanya ambalo nawe unataka kutufanya tuendelee kuamini alikuwa sahihi ni kutaka kuonyesha serikali yake inafanya vizuri kwa kila jambo.
Hili kwa namna moja ama nyingine ilitoa fursa kwa baadhi ya watendaji wapigaji kutumia nafasi zao vibaya wakijua kwa hakika kwa sababu raisi hapendi taarifa mbaya itoke watakuwa salama. Hivi hata haya TBC, clouds media na Kigwangala unataka kusema nayo ni ajenda ya siri!?
Nionavyo mwenda zake alishatufukisha kwenye kiwango fulani cha ujinga na itatuchukua muda sana kusafisha tena akili zetu ili kurudi kwenye ukawaida wake.
Hivi ugomvi wa CAG prof. Assad na Magufuli nani kawasahaulisha? Mtu safi kama Magufuli ya nini kumuandama Assad kwa kiasi kile. Je, mtu safi kama alivyokuwa Magufuli ya nn kuviogopa vyombo vya habari kiasi ya kuvifungia vyote vilivyokuwa na mawazo mbadala? Na je, mtu safi kama Magufuli ya nini kutumia pesa nyingi za umma kwenye mradi ovu wa kununua wanasiasa wa upinzani?
Haya yote ni dhahiri kwamba yalificha mambo mazuri zaidi aliyokuwa nayo huyu ndugu raisi ambayo kwa sasa yanataka kuonekana kama mabaya.
Kwa ushaidi wote huu, ni dhairi kwamba Magufuli alikuwa raisi muoga na hasa wa kukosolewa na hivyo kuruhusu madudu yote haya tunayoyaona kwenye ripoti ya CAG.
 
Umeandika kama umechanganyikiwa! Hakueleweki unamaanisha nini..Ni kama uliandika huku unalia! Kwasababu hata hoja unazosema hazipo, unavyosema miradi mliyoambiwa imefanyika kumbe haijafanyika! Hakuna mtu yoyote aliyesema miradi haijafanyika, bali imefanyika lakin kuna ufisadi mkubwa sana humo. Na hilo ni wazi. Kila mtu anajua mwendazake alikuwa hataki kusikia kitu kingine zaidi ya sifa, hivyo hata kumtoa Assad kumuingiza Kichere alikuwa anataka amuweke mtu anaemmudu. Usijisahaulishe chini ya Magu ofisi ya CAG ilipunguziwa bajeti yake ili isifanye kazi ya kuchimba kwa kina madudu ya Magu. Usijisahaulishe
 
Kuna mambo mazuri yaliyofanyika chini ya utawala wa awamu ya 5 lakini ukweli ni kuwa mafanikio madogo yalipigiwa propaganda kubwa ili yaonekane makubwa ya ajabu.

Kiuhalisia, hakuna kitu kikubwa cha ajabu kilichofanyika wakati wa awamu ya 5 ambacho kilikuwa hakijafanywa na watangulizi wake. Na kuna mambo makubwa zaidi yaliyofanywa na watangukizi wake lakini yalibezwa ili ionekane hawakufanya kitu.
 
wanajinafasi kwa unafki ila nafsi zinawasuta

Nafurahi kuona baadhi ya wadau wanaendelea kumlamba miguu
 
Hakuna aliyefisadi kwenye utawala wa Magufuli,watu hawajaelewa tu, ilikuwa ni hela ilikuwa ikihitajika site ilitoka on time na ilifika site on time bila ya kufuata taratibu. Magufuli aliamini sheria zilizopo ni mbovu zinachelewesha maendeleo.
Ndio maana alifika sehemu Kuna mradi au uhitaji wa mradi hapo hapo aliagiza billions of money kuolewa kwa dharura ndani ya siku chache na mambo yalienda. Hospital kila wilaya, vituo vya afya, kila halmashaur Kuna lami, shule kongwe kufanyiwa ukarabati,nyuma za askar magereza kujengwa, ikulu na maofisi, mahakama n. k. Wamuache mtu huyu wa kipekee. T unakoelekea ni kugumu, Rip Magufuli.
 
JPM alikuwa waziri kwenye serikali za JK na Mkapa. Ni wazi alikuwa hakubaliani na mengi ya marais hao. Lakini mbona hakuwahi kujiuzuru kuonesha kutokubaliana nao? Kwa maelezo ya JPM mwenyewe, aliwahi 'kuomba' kujiuzuru pale alipopewa sumu! So naye alikuwa mnafiki tu kama hawa wenzake tu
 
Tukusanye kodi kwa akili sio nguvu, hahahaaa hapo unategemea nini mkuuu tayari mwendo wa kinyonga umeanza.

Ukiona mtu anataka kuwachekea walipakodi ujue hatutaweza kwenda kwa spidi ya Magu tena.

Watanzania tunajijua wenyewe tulivyo wajanjawajanja kwenye kodi, mtu akipata mwanya wa kukwepa anaita na wenzake anawafundisha, ama kuwaunganisha na huyo anaewezesha ukwepaji kodi.

Tukitaka maendelea nilazima tubanane kisawasawa kwenye kodi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…