Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Mwanakijiji,
Zamani kuna watu walikuwa wanaitwa Nyumbu, mie nilikuwa sijui, sasa ndiyo nimeamini humu Nyumbu ni hawa wafuasi wa wapinzani, sometimes na wapinzani wenyewe. Kwanza wana attack individual, wanasahau kuwa system ndiyo mbovu. Angalia wamesahau kabisa kuwa Kikwete ndiyo alikuwa mtesaji wao kile kipindi cha awamu ya nne, sasa kawa JPM. Hawajui hao wote ni system ambayo ipo na CCM, na itakuwepo wakati wote.

Pili baada ya kifo cha JPM wanaongea mengi sana, ok I am independent, sikupenda JPM his part of human rights, lakini kwa kazi zake ni nani kama yeye? Sasa angalia Nyumbu wamebadirishiwa "narrative" na hiyo hiyo system kuwa JPM alikuwa fisadi sasa wanaamini na kushangilia ati mnaona? Ukweli upo pale pale CCM na system iliyopo ndivyo ilivyo. Angalia huyu mama Samia, mimi naona ni mama wa Mipasho tu, alikuwa na magufuli pamoja yeye ni VP atajitengaje na yale aliyoyafanya magufuli?? Or let say, JPM was sleeping with the Devil? Unam-support mtu kwa maneno kumbe moyoni sivyo? What I am seeing ni kuwa huyu Mama wa Mipasho na JK were very patient, the Vultures, are Patient Birds. Na kweli sasa wanabadirisha "Narrative" sasa Nyumbu wanashangilia. Hawajui kuwa muda si mrefu watalia.

Halafu kuna Group la tatu, hawa watendaji waliokuwa na JPM, wachumia tumbo. Hawa lazima waonyeshe mwelekeo wao maana lazima wajue watakula wapi. Kama tunavyoona Ngugai, kabadirika ghafla, CAG kabadirika ghafla, HK kabadirika ghafla, Nape katoa makucha, they must show where they are.

"The way the coockie crumbles" JPM itakuwa ndvyo alifikiria alipoona kifo kinakuja, we only live once!!

..kwa hapa Tz kila awamu mpya ya uongozi huzodoa watangulizi wake.

..Nyerere alikuwa haishi kuzodoa waingereza kwa hili na lile.

..awamu ya pili ya Mzee Mwinyi walikuwa wakizodoa utawala wa Mwalimu Nyerere.

..watu wa Mkapa walikuwa alikuwa wakizodoa utawala wa Mzee Mwinyi.

..hata awamu ya marehemu Magufuli nao walikuwa wakizodoa utawala wa Kikwete.

..hivyo basi msione ajabu kwa hiki kinachotokea ktk awamu ya Rais Samia. Jambo la msingi ni kutofautisha ukweli na uzushi/propaganda.
 
Nchi imepata hasara kubwa sana ndani ya miaka mitano ya dhalimu kuliko kipindi kingine chochote kile tangu tupate uhuru. Kaiacha kila sekta hoi bin taabani. Mwenyezi Mungu kainusuru nchi na maovu mengi sana ya kutisha.

Ndio maana walipitisha sheria za kujikinga ili wasishitakiwe yeye na pm,ndugai kwa kufanya mambo ya hovyo hvyo kama hayo.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Hata miradi ikiisha itakuwa sio ya Magufuli.. itakuwa ya mama, maana yeye ndo ameimalizia. Tatizo umejaa chuki ya udini. Hapo ndo upumbafu wako unapodhihirika
Hakuna mradi wa mama samia, ndio maana anaiita miradi ya urithi.
 
uyo anamtetea Magufuli, na pia anasema turudi kwenye uchaguzi mkuu,SAMIA asigombee, asimamishwe msukuma yoyote kama Chenge, ili wasukuma washike tena hatamu, Tatizo ni uraisi wa Samia hapo,,, mwendazake alikuwa fisadi mkuu
upo kwenye mwezi?
 
Nime note kitu kimoja kutoka kwako nayo ni 'wapinzani' kumbe ulishajiweka tawi la watawala?

Ok ni haki yako lakini kwa binadamu kamili angehoji je, kwanini aliyeninasibu kuwa msafi mithili ya sufi apende kufanya mambo gizani kiasi kile?

Kweli mtu msafi ajiondoe kwenye mikataba ya uwazi?

Kwanini mtu msafi hakuitaji transparency ili umma umsaidie kuwa msafi?

Mnachofanya sasa ni nafsi zinawasuta, mmeachwa kwenye tope msijue nani atawachomoa, mli compromise nafsi zenu kwa vitu vya kipuuzi na kishenzi.

Kinachowauma zaidi mlizoea kuuza maneno sasa hakuna atakaewaamini tena.

Kwa tuliomfahamu Magufuli tangu enzi hatukua tayari kuuza nafsi zetu kwa sifa za kipuuzi na kijumla jumla namna ile.
Pole sana mtafute kazi ya kufanya sasa.
Mkuu tena walikuwa hawamjui JPM kabisaaa!
Lile jengo pale la Kebby's litamsuta legacy yake, hakuwa msafi.
Alilijenga alipokuwa Waziri wa Ujenzi, pesa alipata wapi?
Na kwa biashara ipi, huyu mtetezi wa wanyonge!!
 
Majambazi waliokubuhu hawajulikani kirahisi kwa kuwa hata Mali zao haziwi na majina yao kutuambia hana pavement nyumbani kwake ndio unamuona hakuwa mpigaji ni ujinga wako maana yote ni kiini macho nani asiyejua alihusika kuuza nyumba za serikali akiwa waziri barabara ya mwendokasi hasara kiasi gani tunaipata jagwani tuu pekee yake ndio urisi aliotuachia kwa ajili tuu ya poor design na upigaji uliofanywa chini ya wizara aliokuwa akiiongoza??? Unaongozwa na propaganda za kijinga unasahau maslahi ya nchi hiyo SGR Ilitakiwa kuisha tangu mwaka2019 na operation ianze mpaka Leo hola na bado haitaisha hata mwaka huu na sio kitu kigeni maana mkandarasi aliyepewa hiyo kazi hana historia mahali popote alipojenga reli ya aina hii yenye urefu huu na kumaliza kazi ethiopia yenyewe ameshindwa kumaliza na haya sio mageni alipigwa bungeni na akinazito kabwe na tukawaona wapinga maendeleo na tukawatukana na kuwaita pandikizi na wananchi tulikawalipa mshahara 2015 wa kuwafukuza bungeni kwa kutishiwa tukiwachagua tena hatutapata maendeleo kwenye majimbo yetu. injinia msimamizi anaendelea kulipwa na pesa za walipaka kodi kinyume na mkataba ili hali mkandarasi alitakiwa ailipe serikali kwanzia 2019 mpaka atakapomaliza kazi lkn hilo hatushughiuliki nalo unajua kwanini??? ngoja nikuibie siri wasimamizi wote ni ndugu na magufuli sukuma boy kwaanzia mkurugenzi wa shirika ndugu masanja kadogosa ambaye kitaaluma sio hata mhandisi na meneja mradi masanja machibya ambaye sijui ndio mtoto wa baba mkubwa sijui baba mdogo hapo sasa utaongea nini akati pesa inapigwa na mtoto wa mjomba kesi inamalizwa kifamilia na yeye mwenyewe alikuja kuikagua na kuendelea kumsifu mkandarasi ilihali akijua IPO nyuma ya wakati. Kunamengi sana ya kuandika ndugu zangu lkn kwa sababu ya uchungu na hasira siwezi kuendelea naomba niishie hapa na mwendazake alazwe mahali anapostahili.
Sawa Baba Somoe binti Chiputa kutoka Chienjele tumekuelewa ila siku nyingine unda vifungu vidogo vidogo kwenye maandishi yako (aya)
 
Hata akivunja Katiba hakuna neno kwani nia yake ni nzuri!
Hata akiiba hakuna neno kwani nia yake ni nzuri!
Hata Watanzania wakitekwa, wakateswa na wakapotezwa hamna neno kwani nia yake ni nzuri!
Kwa unafiki na ujinga wa baadhi ya Watanzania, Magufuli, kwa vitendo hivyo ataenziwa kama malaika...!

mtakatifu.jpg

Hii hakika ni kufuru...! Dunia nzima inatucheka!​

Kwa kiwango cha uovu wake mwendazake hata Adolph Hitler angeweza kumuonea wivu.
 
Kwenye SGR nilitegemea CAG angesema Km 250 zilizotandikwa reli ni hewa, yaani hakuna kilichofanyika. Na kwamba pesa yote aliyolipwa Mturuki kalipwa pasipo kazi yoyote kufanyika.
Mema aliyofanya JPM kwa taifa hili hayafutiki kirahisi kama watesi wake wanavyotaka iwe. JPM kamwe hakuwa malaika kama ambavyo wewe na mimi tusivyo.
JPM mwizi tu! Hayo mema kayafanya kwa pesa ya kutoka mfukoni mwake? Hivi nyie watu mbona wajinga namna hii? Kaifanyia mema nchi wakati huo huo kaiingiza nchi kwenye mizgo ya kipumbavu kama ile ya kununua ndege zinazoendelea kulitia hasara taifa? Isitoshe asilimia kubwa ya miradi Jiwe kaikuta, halafu mnataka kudanganya watu kwamba eti inatokana na "wema wa Jiwe"
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli.

Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea.

Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufisadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!
Kwenye sayansi ya Giza mwendabure yupo sahihi kwani alishawahi kusema hii inchi imechezewa sana na imeliwa sana napia wamecheleweshwa sana na wapinzani, lkn hajawahi kusema amekomesha kazia hiyo bali alikuwa anatupa tu habari tujue hivyo nayeye anafuata muendelezo huo ila kwa style nyingine, kimtindo mwingine na kwa namana nyingine na lawama ziwe mwiko.Ndivyo nilivyomwelewa.Natani anyway.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli.

Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea.

Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufisadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!
Mzee mwanakijiji utahangaika sana!

Kumtetea Magufuli kwa watu waelewa ni vigumu sana! Labda kwa watu wasiojitambua ambao walikuwa brainwashed.

Wewe mwenyewe unajua Magufuli alizuia kabisa ushuru wa vyombo vya habari. Kila aliyesema mapungudu yake alikiona cha mtema kuni! Kama alikuwa msafi na miradi yake haikuwa na kasoro,alikuwa anaficha nini?

Wacha watu waseme sasa upande mwingine wa utawala wake ambao yeye,alipokuwa hai, hakutaka ujulikane
 
SGR, Rufiji Dam ni picha tu zile🤣

CAG kaamua kishabiki kusema bila aibu akiwa na watendaji wale wale, akitaka kujikomba kwa mama kumbe anachotwa akili!

wa kujiuzulu sio PM tu hata Rais!

Hakuna namna watamzima kirais JPM, he is here to stay with us for long long time
Kweli mkuu, wawajibike watendaji wote.
 
SGR, Rufiji Dam ni picha tu zile🤣

CAG kaamua kishabiki kusema bila aibu akiwa na watendaji wale wale, akitaka kujikomba kwa mama kumbe anachotwa akili!

wa kujiuzulu sio PM tu hata Rais!

Hakuna namna watamzima kirais JPM, he is here to stay with us for long long time
Nimewasikia mahali watu kutoka kanda ya ziwa wakisema kwa kile baadhi ya watanzania na viongozi wanavyomdhalilisha hayati JPM ama hadharani, kwa uficho au kupitia mitandao ya kijamii wanawasubiria hao watu na viongozi wawafuate kutaka kupewa mtihani wa kufanya kwamba wenyewe ndio watausahihisha na kutoa maksi (itakuwa ni sawa na ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kwa mwanasiasa kupewa maksi zaidi ya saba (7%)

Yetu macho
 
Sawa Baba Somoe binti Chiputa kutoka Chienjele tumekuelewa ila siku nyingine unda vifungu vidogo vidogo kwenye maandishi yako (aya)

Kaandika utadhani anafoka [emoji3][emoji3][emoji3]
 
Unaandika mithili ya layman. Kwani kuwa mpinzani lazima ujinasibishe na wapinzani unaowaita wamepotea?

Wewe binafsi ume compromise nafsi yako kwakua wengine wamepotea? Really?

Hivi misimamo na ideology za mtu huwa kwa wengine au wewe binafsi?

Kwahiyo huko nyuma ulifanya upinzani kwakua wengine walifanya?

Au kauli na matendo yako yanadhihirisha ulifanya mambo kwa chuki binafsi, chuki za kimaslahi, kikanda, kidini na kirangi? Seriously mtu mwenye upinzani wa Moyoni unaweza sema nilishindwa fanya upinzani maana sikumjua mpinzani wa kweli?

Seriously mtu wa kariba yako ulikuja kuwa simply brainwashed na siasa za watu aina ya akina Magufuli really?
Huyu sikutaka kumjibu, nimeona aandiko lake ni ujinga mtupu huyu alikuwa mpambape wa Dr slaa au huenda akawa mwenyewe, aliamuaga akili aweke tumboni na tumbo aliweke kichwani
 
Hata Magu amerithi miradi mingi tu na sasa inajulikana Ni yake wakati Ni ya JK. Mfano Ni daraja la Kigamboni na fly over
Fly over kuanzia tofali la kwanza mpaka gari zinapita ni kazi ya JPM usiwe maamuma. JPM ana rekodi ya kipekee Africa ndio maana Facebook na Instagram wanamlilia mnavyomwandama.
 
Akili huna usiniulize kwanini
Ukisoma mitandao ya kijamii hasa twitter utafikiri kweli hii nchi imeibiwa kila kitu na hakuna kitu kimeachwa, kumbe sio kweli.

Watu wanajifanya kushangaa ATCL kupata hasara, hivi mtu mwenye akili timamu unaweza kushangaa atcl kupata hasara? By the way, ni shirika gani la serikali linalopata faida? Lipi? Mashirika yote ni hasara kila mwaka kuanzia Tanesco, TPDC, TTCL, ATCL, NHC na mengine yote, kwa nini shida iwe kwa ATCL?

Halafu watu wanataka kusema Magufuli ange eliminate rushwa ama wizi wa mali za umma 100%, hilo jambo halipo Duniani. Duniani kote, kuanzia China ambapo kosa la rushwa unaweza kuuwawa ama Marekani ambapo mifumo iko strong bado watu wanaiba na kula rushwa, tusimsingizie Magufuli kwa kila kitu.

Kuna kikundi ama kingenge cha wahuni sijui kinalipwa na nani kutaka kumchafua Magufuli na report ya cag
 
Back
Top Bottom