Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Ukisoma mitandao ya kijamii hasa twitter utafikiri kweli hii nchi imeibiwa kila kitu na hakuna kitu kimeachwa, kumbe sio kweli.

Watu wanajifanya kushangaa ATCL kupata hasara, hivi mtu mwenye akili timamu unaweza kushangaa atcl kupata hasara? By the way, ni shirika gani la serikali linalopata faida? Lipi? Mashirika yote ni hasara kila mwaka kuanzia Tanesco, TPDC, TTCL, ATCL, NHC na mengine yote, kwa nini shida iwe kwa ATCL?

Halafu watu wanataka kusema Magufuli ange eliminate rushwa ama wizi wa mali za umma 100%, hilo jambo halipo Duniani. Duniani kote, kuanzia China ambapo kosa la rushwa unaweza kuuwawa ama Marekani ambapo mifumo iko strong bado watu wanaiba na kula rushwa, tusimsingizie Magufuli kwa kila kitu.

Kuna kikundi ama kingenge cha wahuni sijui kinalipwa na nani kutaka kumchafua Magufuli na report ya cag
Ni kweli mashirika ya umma jukumu kubwa kwao ni kutoa kwa maana hayakuundwa kwa ajili ya biashara Sasa ikitokea wakavaa sura ya kibiashara mpaka kutangaza faida na kutoa gawio hapo ndipo mkanganyiko unapoanzia ukiambiwa kwa muda wote walipotangaza faida ilikuwa uongo. Mbona hatusikii JWTZ wametoa gawio!!
 
Yaani ni watu kukuza mambo, kwa waliosima uhasibu hakuna wizi wowote kwenye report ya CAG, kilichowasilishhwa ni hoja na mapungufu yanayotakiwa kufanyiwa kazi.
 
Namba gani??? Na kwa ushenzi wenu mliotuonyesha kwa miaka 6 tu sahauni kutoa Raisi Tanzania hadi ipite miaka 1000
We kajamaa utakuwa unafunuliwa Malinda hata hivyo ulisema mme wako Lissu akishindwa Urais utakuwa tayari kufunuliwa Malinda.
 
Wewe umeamua kuwa mjinga na sio kuwa watu nafsi zinawasuta

Kwako serikali iliyopita ni JPM!!! sio watendaji sasa hapa usaidiwe nini?

Na hao unaosema wala rushwa si ndio hawa hawa walikuwa madarakani na bado wapo??[emoji12]

Shida yako ni uwazi? upi?

umeulizwa hivyo vitu vinajengeka? vipo? vinaonekana? sasa kama mtendaji aliamua kuwa apige kazi na siasa zako weka pembeni...that is a true definition ya mwanaume

Labda na wewe unaungana na wale wajinga wanaodhania JPM alikuwa mpigaji? kwa nguo zile na maisha yale kwake nyumbani mpaka hana paved blocks?

JPM angekuwa mroho wa hela angekuwa tajiri kuliko mengi, bakhresa na manji...kakaa wizara ya ujenzi miaka mingapi?...

sasa huwa tunapenda muwaze pande hizo kuwa HE IS MOTIVE was pure, genuine and good...

ila ukiwasikiliza watanzania kama wewe nchi haiendi mahali hii....he decided is own way.....alifaulu JPM...wala report ya CAG isikupe faraja yoyote

Sasa unafikiri Mwendazake kafa akiwa masikini? Jamaa alikuwa tajiri mzuri tu hata kabla hajawa Rais, kwenye ujenzi kapiga vizuri tu!
 
Ukitaka kujua motive zao jaribu kufikiria waliposimamia, mama Samia anatuambia hata madini adimu ambayo mwenda zake aliyaangalia Kwa wivu wa kupindukia tuwaachie waje tu wachimbe, Ndugai anasema Kwa SGR wajichange wabunge walete hayo mabehewa, mchina tunaejua anavyofuonza damu aje tu ajenge Bagamoyo. Hapo mie naamini hawa ni majambazi walio na agenda zao Ila muda utaongea
Lakini muelewe kuwa popote duniani serikali haijawahi kufanikiwa kufanya biashara. Hata China walianza kupata mafanikio makubwa baada ya kuruhusu sekta binafsi. Serikali ibaki kuunda mifumo imara ya kuisimamia sekta binafsi kwa umakini na kukusanya kodi stahili pamoja na kuilea sekta binafsi ili iweze kushamiri na kuleta mapato serikalini. Anachosema Ndugai kuwa treni ya mwendokasi iruhusu mabehewa ya watu binafsi yuko sahihi kwani wafanyibiashara kama Mo na Bakhresa wanaweza kuleta abehewa yao au hata vichwa vya train wakiweza na shirka la reli likaachukua ushuru kwtoka kwa hao wafanya biashara. Suala ni serikali kujipanga na kusimamaia na kuhakikisha mambo yanasimamiwa kwa ukaribu na umakini. Miaka mitano ya mwendazake imeua kabisa sekta binafsi hasa kwenye sekta ya ujenzi, hasa wazawa. Mazingira ya udanganyifu yalitokana na serikali zenyewe kuwa corrupt na hivy na wakandarasi wakawa wanadanganya ili wapate pesa za kuwahonga watu wa serikali.
Ni kweli kwamba sehemu kubwa ya walioko serikalini ni wafanyabiashara na wakati huu watakuwa wanatoa ushauri kwa Rais wakivutia upande wwenye maslahi kwao na mama anapaswa kuwa makini sana. Inashangaza leo hata Muhongo anaponda Hydropower na kushadidia gesi ambayo waliingia mikataba ya kuhuni. Tufike mahali Watanzania tusiangalie maslahi ya mmoja mmoja bali tuangalie maslahi ya nchi yetu kwa ujumla kwani maoni mengi sasa kwenye mitandao ni kila mmoja kumtaka Rais afanye analoona linamfaa yeye binafsi au na kundi lake.
 
Chadema sin mna imani kubwa na mama Samia na mnasema mtamlinda kwa wivu mkubuwa, ??? Kama kweli report ya CAG kweli imebainisha wizi basi wahusika wachukuliwe hatua vinginevyo ni kelele zenu .
 
Huko mbeleni tutakua na serikali zinazoongozwa na robots. Bora kuamini kwenye science kuliko siasa.

Lakini nilichopata kutoka kwako hapa M.M unataka tuanze upya? Je Kuna upya wowote ndani ya CCM? Huko nje ya CCM nani msafi?
 
Upinzani uko kwenye damu yangu; ila sasa hivi naona kama umepotea maana sijui ni nani amebakia upinzani kweli. Labda tuunde upya kabisa... maana upinzani umekubali jukumu lisilo lao...
Kwa nini kama hamridhiki na hali ulivyo msijiengue ccm mkaunda chama chenu?
Halafu unataja bwawa la nyerere hivi linatoa MW ngapi?
Je nani kashapanda treni ya SGR?
Unaongea vitu havipo mzee.
Kubalini tu Magu alikuwa na uungu mtu ambao uliwafanya mumuone Mungu asiye kosea ndio maana hamuamini kama alivurunda.
 
SGR, Rufiji Dam ni picha tu zile🤣

CAG kaamua kishabiki kusema bila aibu akiwa na watendaji wale wale, akitaka kujikomba kwa mama kumbe anachotwa akili!

wa kujiuzulu sio PM tu hata Rais!

Hakuna namna watamzima kirais JPM, he is here to stay with us for long long time
Umesema kweli! Kama ufisadi tunaoambiwa ni kweli, Basi serikali yote ilikuwa corrupt! Watajitengaje kwa mfano!! Hivi wanafikiri tutawasifu wao kuwa Safi wakati Kuna uwajibikaji wa jumla?
Lakini tuende mbele turudi nyuma Magufuli Ni mchapa kazi hakuna mfano! Aliyoyafanya tumeyaona wenyewe hatuhitaji kusimuliwa na mtu! Yeyote akitaka ku-discredit au kubeza na kudharau kazi yake atajidharaulisha tu mwenyewe! Hakuna mzalendo wa kweli atakayemwelewa! Hata dhamiri yake mwenyewe hawezi kuishawishi!
Ilikuwa Ni ngonjera tu habari ya kuhamia Dodoma Kama makao makuu ya nchi. Hakuna aliyekuwa anaamini kuwa inawezekana kuhamia dodoma! Lakini huyu tunayeambiwa sasa kuwa alikuwa "fisadi" yeye kwa "ufisadi" wake amefanikiwa kuhamisha makao makuu kwenda Dodoma! Kwangu Mimi huyo "fisadi" alitufaa Sana kwa kuwa alifanikisha ndoto ya kuhamia makao makuu!
Lakini pia hili la mradi wa Stigler's George wa kujenga bwawa la kufua umeme lilishakuwa Ni ndoto isiyotekelezeka! Hivi tunavyozungumza takribani mradi uko tayari kwa asilimia 50! Lakini ghafla tunaambiwa Hilo pia ni changa la macho! Tunaambiwa upembuzi yakinifu unaotumika Ni wa miaka ya 70!! Umepitwa na wakati!! Wasichokijua Ni kuwa si lazima upembuzi yakinifu wa miaka ya 70 uwe umepitwa na wakati! Wakati wanafanya upembuzi yakinifu wa mradi mkubwa Kama ule ni lazima walifanya projection ya muda mrefu, at least miaka 100 mbele! Kwa akili ya kawaida huwezi kufanya upembuzi yakinifu kwa mradi mkubwa vile halafu ukakadiria uhai wa mradi kuwa miaka 10 au 20! Kwa hiyo uncertainties nyingi zilikuwa taken into conciderations! Ninaamini huu mradi bado unaweza kuongozwa bila matatizo na upembuzi yakinifu wa miaka ya 70. Ila mafisadi walitaka wapige pesa kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu mwingine kwa miaka Kama miwili hivi! Environmental impact assessment (EIA) pia ilifanyika huko nyuma na hakuna matatizo. Wote mnakumbuka mabeberu walivyopiga Vita huu mradi! Hivi unafikiri Kama tungetoa tenda ya kufanya EIA nyingine, mabeberu wangefanya kila wawezalo kupenyeza ushawishi wao huko na huu mradi wangeunyongea baharini.
 
Unaandika mithili ya layman. Kwani kuwa mpinzani lazima ujinasibishe na wapinzani unaowaita wamepotea?

Wewe binafsi ume compromise nafsi yako kwakua wengine wamepotea? Really?

Hivi misimamo na ideology za mtu huwa kwa wengine au wewe binafsi?

Kwahiyo huko nyuma ulifanya upinzani kwakua wengine walifanya?

Au kauli na matendo yako yanadhihirisha ulifanya mambo kwa chuki binafsi, chuki za kimaslahi, kikanda, kidini na kirangi? Seriously mtu mwenye upinzani wa Moyoni unaweza sema nilishindwa fanya upinzani maana sikumjua mpinzani wa kweli?

Seriously mtu wa kariba yako ulikuja kuwa simply brainwashed na siasa za watu aina ya akina Magufuli really?
Maswali magumu😂😂😂 .Mzee yupo yupo tu hajui ashike wapi, umemuuliza maswali ya msingi sana kwenye post yabkwanza, hakuna alilojibu
 
But kumbuka Lake Zone tuna numbers

..unajidanganya.

..unadhani mnaweza kufua dafu ikiwa CCM wataamua kutangaza matokeo wanayoyataka wao?

..lake zone ilishakuwa na chama kinaitwa UDP kilianzishwa na John Cheyo lakini hakikufua dafu mbele ya CCM / chama dola.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli.

Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea.

Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufisadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!
MMM, sikuwahi kukupa LIKE tangu JPM alipoingia madarakani, lkn leo nimekupa LIKE baada ya miaka mingi.

Vv
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli.

Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea.

Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufisadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!
Nimezipenda hoja zako si kwasababu ni nzito sana , bali ni kwasababu zina maswali magumu unayoyapatia majibu rahisi sana. Mwl Nyerere aliwahi kusema kwamba watanzania ni watu wa ajabu sana kwasababu wana majibu rahisi kwa maswali magumu sana. Nami nasema usemi huo ni wako muandika thread hii.

Kwa mfano unashangaa watu waliokuwa wakimuunga mkono sana Magu leo wamemgeuka na hata miradi yote iliyokuwa inatajwa ni kama haipo/haikufanywa. Umeenda mbali zaidi na kumtaja Ndugai kwa kushangaa kwanin bandari ya Baga-yo haikujengwa. Na na na............

Swali langu kwako ni moja tu, sijui mwenzetu ulikuwa wapi kati ya 2015-2020? Kwa sababu katika kipindi hicho sauti ilikuwa moja tu na kila aliyejaribu kufungua kinywa cha alikipata cha mtemakuni. Hivyo ulitaka Ndugai wakati ule aseme nini? Na hapo ndio utafahamu umuhimu wa kuwapa watu wako uhuru wa kuzungumza na kutoa mawazo yao amaye pengine ni tafauti nawe.

Hayati Magu, nilimpenda lakini doa kubwa lililoniudhi ni kuwabana wanataaluma kuzungumza wanayoyaju. Kilichompata Prof Assad si kikla mmoja anaujasiri namna hiyo, na wataalam wengine wengi tu waliosahau taaluma zao, kisa eti kuna simba mmoja tu anayojua kila kitu.

Swali langu ninalojiuliza mwenyewe ni moja tu; Hivi Hayati ukali wote ule juu ya wanataaluma (Kuzuia takwimu n.k), alikuwa anaogopa nini? Au alikuwa anaficha nini? Kama kulikuwa alichokificha, pengine ndicho kinachoanikwa hapa hadharani leo. Endelea na uchambuzi wako bila kusahau maswali hayo makuu na utupe jibu. Alamsik!
 
Mijitu mijizi, mizushi inayofikiria karibu including Mosoga
imeshangalia sana kifo cha Jemedari Shupavu JPM... Ni kushangalia ujinga na uzushi.... Utadhani macho yao yapo makalioni....mpaka kushindwa kuona aliyoyasimamia JPM while is tangible na yatakuwepo kwa miaka mia+.

Msoga huwa anajilaumu sana kwa madudu aliyofanya hili linajidhihirisha utetezi anaofanya kila platform.. ni kum-outshine mwendazake na kujifanya aliyosimamia yote zilikuwa plan zake.. Serikali ilikuwa masikini wa kutupwa ilitegemea kufadhiliwa almost kwa kila kitu... Ninahakika JPM angepewa maisha marefu tungeishuhudia nchi yetu ikimeremeta kwa infrastructure za maana zenye viwango maridhawa kama tulivyo shuhudia..

Mama yetu Samia hakuwa amejiandaa kuongoza nchi.. viatu ni vikubwa mno anaongea vijineno vya wambea na watu wasio thabiti kwenye wanacho simamia... Its to early to conclude the analysis but sioni mtu imira kama tuliye muhitaji... JPM popote alipo JPM is will remain the best president JMT ever had.
 
Nimezipenda hoja zako si kwasababu ni nzito sana , bali ni kwasababu zina maswali magumu unayoyapatia majibu rahisi sana. Mwl Nyerere aliwahi kusema kwamba watanzania ni watu wa ajabu sana kwasababu wana majibu rahisi kwa maswali magumu sana. Nami nasema usemi huo ni wako muandika thread hii.

Kwa mfano unashangaa watu waliokuwa wakimuunga mkono sana Magu leo wamemgeuka na hata miradi yote iliyokuwa inatajwa ni kama haipo/haikufanywa. Umeenda mbali zaidi na kumtaja Ndugai kwa kushangaa kwanin bandari ya Baga-yo haikujengwa. Na na na............

Swali langu kwako ni moja tu, sijui mwenzetu ulikuwa wapi kati ya 2015-2020? Kwa sababu katika kipindi hicho sauti ilikuwa moja tu na kila aliyejaribu kufungua kinywa cha alikipata cha mtemakuni. Hivyo ulitaka Ndugai wakati ule aseme nini? Na hapo ndio utafahamu umuhimu wa kuwapa watu wako uhuru wa kuzungumza na kutoa mawazo yao amaye pengine ni tafauti nawe.

Hayati Magu, nilimpenda lakini doa kubwa lililoniudhi ni kuwabana wanataaluma kuzungumza wanayoyaju. Kilichompata Prof Assad si kikla mmoja anaujasiri namna hiyo, na wataalam wengine wengi tu waliosahau taaluma zao, kisa eti kuna simba mmoja tu anayojua kila kitu.

Swali langu ninalojiuliza mwenyewe ni moja tu; Hivi Hayati ukali wote ule juu ya wanataaluma (Kuzuia takwimu n.k), alikuwa anaogopa nini? Au alikuwa anaficha nini? Kama kulikuwa alichokificha, pengine ndicho kinachoanikwa hapa hadharani leo. Endelea na uchambuzi wako bila kusahau maswali hayo makuu na utupe jibu. Alamsik!
Hata kama walizuiliwa kuongea wanapopata nafasi sasa sio kuongea ujinga... Nampongeza sana JPM kuwaziba midomo kama ndio ujinga huu wanaoungea sasa.
 
Nimewasikia mahali watu kutoka kanda ya ziwa wakisema kwa kile baadhi ya watanzania na viongozi wanavyomdhalilisha hayati JPM ama hadharani, kwa uficho au kupitia mitandao ya kijamii wanawasubiria hao watu na viongozi wawafuate kutaka kupewa mtihani wa kufanya kwamba wenyewe ndio watausahihisha na kutoa maksi (itakuwa ni sawa na ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kwa mwanasiasa kupewa maksi zaidi ya saba (7%)

Yetu macho
Msiwagawe watanzania kwa sera zenu za ukabila.

Mimi niko kanda ya ziwa,mbona sijasikia hayo unayojaribu kudanganya mchana kweupe.
 
Back
Top Bottom