Kama kuwa na ofisi ni jambo la maana, CCM isingeyumbisha nchi namna hii

Kama kuwa na ofisi ni jambo la maana, CCM isingeyumbisha nchi namna hii

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Kuwa na Ofisi ni sehemu ya utambulisho wa mahali taasisi fulani inapatikana. Lakini kuwa na Ofisi hakuhusiani na uimara wa taasisi husika. Makampuni yanayofilisika au taasisi zinazoshindwa kujiendesha na hatimaye kufungwa, nazo pia huwa na Ofisi.

Wakati Serikali ilipoamua kuyaunganisha mashirika ya hifadhi ya jamii ili kuleta ufanisi, mashirika hayo yalikuwa na Ofisi lakini yalifikia kwenye hatua ya kufilisika. Kwa ivo mbali ya Ofisi kuwa utambulisho wa Taasisi na sehemu ya kuhifadhia nyaraka mbali mbali za Taasisi husika, Ofisi kama ofisi haina mchango wowote ule kwenye kuifanya Taasisi kuwa Imara.

CHADEMA kwa sasa, inafanya harakati za kujenga ofisi zake nchi nzima. Na ofisi hizo zinajengwa kama hitaji la CHADEMA kuwa na sehemu itakayotumika kwa utambulisho na uhifadhi wa nyaraka zake. CHADEMA haijengi Ofisi ili kujiimarisha, bali inajenga ofisi kama kituo cha kukutania kupanga mipango ya chama.

Nguvu iliyonayo CHADEMA kwa sasa inatokana na Falsafa, Itikadi, Mrengo na Sera zake. Utofauti kati ya CHADEMA na CCM, hauko kwenye kuwa ama kutokuwa na Ofisi, bali utofauti wao unajengwa na mitizamo tofauti linapokuja suala la kusimamia maslahi ya Taifa.

Wakati CCM wanataka madaraka ya nchi ili wajineemeshe, CHADEMA siku zote wanataka madaraka hayo ili kuineemesha Tanzania na kuwafanya watanzania waone ni baraka kuzaliwa na kuwa mtanzania. Utofauti huo ndiyo unaowafanya CCM kutumia nguvu kubwa sana kupambana kiharamu na CHADEMA na siyo utofauti wa kuwa ama kutokuwa na Ofisi.

Kama kuwa ama kutokuwa na Ofisi kingekuwa ni kigezo muhimu kwenye kutambua ubora wa Chama cha siasa, basi leo hii nchi yetu isingekuwa inayumbishwa hovyo hovyo na CCM. CCM inafanya mambo mengi yanayokera na kuharibu nchi yetu, lakini yenyewe ina Ofisi kwenye karibia asilimia tisini na tisa (99%) ya nchi yetu.

Wakati hela za Tegeta - Escrow zinaliwa, CCM walikuwa hawana ofisi? Wakati Kabudi anataja takwimu za uongo za fedha wanazodaiwa Barricks, CCM ilikuwa haina Ofisi? Wakati Professa Assad anafukuzwa kiharamu kwenye nafasi yake ya CAG, CCM ilikuwa haina Ofisi?

Ofisi ni Jambo la muhimu kwa chama cha siasa, lakini si takwa la kikatiba wala si kigezo cha ubora wa chama.
 
Wakati hela za Tegeta - Escrow zinaliwa, CCM walikuwa hawana ofisi? Wakati Kabudi anataja takwimu za uongo za fedha wanazodaiwa Barricks, CCM ilikuwa haina Ofisi? Wakati Professa Assad anafukuzwa kiharamu kwenye nafasi yake ya CAG, CCM ilikuwa haina Ofisi?

Ofisi ni Jambo la muhimu kwa chama cha siasa, lakini si takwa la kikatiba wala si kigezo cha ubora wa chama.
Tafuteni ofisi bhana....acheni kutafuta vichaka mjifiche.
JokaKuu zitto junior
 
Lete hoja yako mzee na sio kutagg raia wa kuja kukupa sapoti!!
Kutag sio kuomba sapoti tu....ni kuwaalika wadau kwenye mjadala...

Na wewe toa hoja maana hamna hoja uliyoweka hapo
 
Kwani ofisi hatuna. Ile mikutano pale ufipa huwa inafanyika kwenye Ofis za tukunyema!!??
Chama kikuu cha upinzani chenye ndoto za kuchukua nchi lazima muwe na makao makuu ya kudumu yenye hadhi ya kuendesha mikutano ya chama ya kitaifa......sio vyumba viwili vya kupangisha.
 
Chama kikuu cha upinzani chenye ndoto za kuchukua nchi lazima muwe na makao makuu ya kudumu yenye hadhi ya kuendesha mikutano ya chama ya kitaifa......sio vyumba viwili vya kupangisha.

..Napingana na hoja yako.

..hata kupangisha ni sawa tu, ilimradi chama kina ofisi.

..Ccm kwa muda mrefu walikuwa wakiendesha mikutano ya kitaifa ktk ukumbi wa Diamond Jubilee.

..Mwalimu Nyerere alitangaza vita vya Kagera ktk ukumbi wa Diamond Jubilee. Na ukumbi ule sio wa serikali au wa chama.

..Na Ccm pamoja na kuwa na majengo ya kifahari kila mahali, bado wamekuwa wakifanya vikao vyao Ikulu jambo ambalo ni matumizi mabaya ya rasilimali za umma.
 
Nchi haiongozwi kw amajengo bali akili.

Mbona hatuna umeme na ccm wana maofisi wameshindwa nini?

..jambo lingine mnalopaswa kuelewa ni mazingira ambayo CCM imejengwa.

..tangu mwaka 1965 mpaka 1992 Tanzania ilikuwa nchi ya chama kimoja, na chama hicho kilikuwa Tanu au Ccm.

..katika kipindi hicho CCM ilikuwa ikitumia fedha, nyenzo, na rasilimali za umma, kujenga chama.

..Ccm ilikuwa na tawi ktk kila taasisi unayoifahamu wewe kuanzia mashirika ya umma, idara za serikali, shule na vyuo vyote, vyombo vya ulinzi na usalama.

..kwa mfano, Ccm ilikuwa na tawi ktk kila kikosi cha jeshi. Mkuu wa kikosi alikuwa ndiye mwenyekiti wa chama kikosini.Pia kila kikosi kilikuwa na kamisaa wa siasa ambaye alikuwa ndiye mkuu wa mafunzo ya siasa kikosini. Kamisaa mkuu wa siasa jeshini ndiye aliyekuwa afisa mkuu namba 3 jeshini, baada ya Mkuu wa majeshi, na Mnadhimu Mkuu.

..kwa hiyo tangu mwaka 1965 mpaka 1992 kipindi cha miaka 27 Cccm ilikuwa peke yake ikifanya siasa bila ushindani, ikijijenga kwa kutumia michango, ruzuku, na rasilimali za umma.

..Baada ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa Ccm ilipewa rasilimali zote ilizochuma wakati wa mfumo wa chama kimoja na kwenda kushindana na vyama vichanga vilivyokuwa vimeanzishwa. Pamoja na advantage hiyo Ccm imeendelea kutumia hujuma za aina mbalimbali dhidi ya vyama mbadala, na mfumo mzima wa demokrasia.

..Tunapolinganisha vyama vya upinzani na Ccm ni vizuri tukazingatia historia.
 
..jambo lingine mnalopaswa kuelewa ni mazingira ambayo CCM imejengwa.

..tangu mwaka 1965 mpaka 1992 Tanzania ilikuwa nchi ya chama kimoja, na chama hicho kilikuwa Tanu au Ccm.

..katika kipindi hicho CCM ilikuwa ikitumia fedha, nyenzo, na rasilimali za umma, kujenga chama.

..Ccm ilikuwa na tawi ktk kila taasisi unayoifahamu wewe kuanzia mashirika ya umma, idara za serikali, shule na vyuo vyote, vyombo vya ulinzi na usalama.

..kwa mfano, Ccm ilikuwa na tawi ktk kila kikosi cha jeshi. Mkuu wa kikosi alikuwa ndiye mwenyekiti wa chama kikosini.Pia kila kikosi kilikuwa na kamisaa wa siasa ambaye alikuwa ndiye mkuu wa mafunzo ya siasa kikosini. Kamisaa mkuu wa siasa jeshini ndiye aliyekuwa afisa mkuu namba 3 jeshini, baada ya Mkuu wa majeshi, na Mnadhimu Mkuu.

..kwa hiyo tangu mwaka 1965 mpaka 1992 kipindi cha miaka 27 Cccm ilikuwa peke yake ikifanya siasa bila ushindani, ikijijenga kwa kutumia michango, ruzuku, na rasilimali za umma.

..Baada ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa Ccm ilipewa rasilimali zote ilizochuma wakati wa mfumo wa chama kimoja na kwenda kushindana na vyama vichanga vilivyokuwa vimeanzishwa. Pamoja na advantage hiyo Ccm imeendelea kutumia hujuma za aina mbalimbali dhidi ya vyama mbadala, na mfumo mzima wa demokrasia.

..Tunapolinganisha vyama vya upinzani na Ccm ni vizuri tukazingatia historia.
Ukweli mtupu. Kimsingi ofisi zote za ccm ni mali ya serikali iliyoporwa.
 
Chama kikuu cha upinzani chenye ndoto za kuchukua nchi lazima muwe na makao makuu ya kudumu yenye hadhi ya kuendesha mikutano ya chama ya kitaifa......sio vyumba viwili vya kupangisha.
CHADEMA pale Ufipa haijapanga na kama unadhani wamepanga. mtaje basi aliyewapangisha. Hata TANU haikuwa na Ofisi kama walizo nazo leo CCM. Si kazi rahisi kwenye siasa za mgandamizo kama za Tanzania chama kama CHADEMA kujenga Ofisi zake kirahisi.

Hata hivyo CHADEMA inajenga ofisi Kadhaa mikoani. Au hizo nazo siyo ofisi?
 
Kuwa na Ofisi ni sehemu ya utambulisho wa mahali taasisi fulani inapatikana. Lakini kuwa na Ofisi hakuhusiani na uimara wa taasisi husika. Makampuni yanayofilisika au taasisi zinazoshindwa kujiendesha na hatimaye kufungwa, nazo pia huwa na Ofisi.

Wakati Serikali ilipoamua kuyaunganisha mashirika ya hifadhi ya jamii ili kuleta ufanisi, mashirika hayo yalikuwa na Ofisi lakini yalifikia kwenye hatua ya kufilisika. Kwa ivo mbali ya Ofisi kuwa utambulisho wa Taasisi na sehemu ya kuhifadhia nyaraka mbali mbali za Taasisi husika, Ofisi kama ofisi haina mchango wowote ule kwenye kuifanya Taasisi kuwa Imara.

CHADEMA kwa sasa, inafanya harakati za kujenga ofisi zake nchi nzima. Na ofisi hizo zinajengwa kama hitaji la CHADEMA kuwa na sehemu itakayotumika kwa utambulisho na uhifadhi wa nyaraka zake. CHADEMA haijengi Ofisi ili kujiimarisha, bali inajenga ofisi kama kituo cha kukutania kupanga mipango ya chama.

Nguvu iliyonayo CHADEMA kwa sasa inatokana na Falsafa, Itikadi, Mrengo na Sera zake. Utofauti kati ya CHADEMA na CCM, hauko kwenye kuwa ama kutokuwa na Ofisi, bali utofauti wao unajengwa na mitizamo tofauti linapokuja suala la kusimamia maslahi ya Taifa.

Wakati CCM wanataka madaraka ya nchi ili wajineemeshe, CHADEMA siku zote wanataka madaraka hayo ili kuineemesha Tanzania na kuwafanya watanzania waone ni baraka kuzaliwa na kuwa mtanzania. Utofauti huo ndiyo unaowafanya CCM kutumia nguvu kubwa sana kupambana kiharamu na CHADEMA na siyo utofauti wa kuwa ama kutokuwa na Ofisi.

Kama kuwa ama kutokuwa na Ofisi kingekuwa ni kigezo muhimu kwenye kutambua ubora wa Chama cha siasa, basi leo hii nchi yetu isingekuwa inayumbishwa hovyo hovyo na CCM. CCM inafanya mambo mengi yanayokera na kuharibu nchi yetu, lakini yenyewe ina Ofisi kwenye karibia asilimia tisini na tisa (99%) ya nchi yetu.

Wakati hela za Tegeta - Escrow zinaliwa, CCM walikuwa hawana ofisi? Wakati Kabudi anataja takwimu za uongo za fedha wanazodaiwa Barricks, CCM ilikuwa haina Ofisi? Wakati Professa Assad anafukuzwa kiharamu kwenye nafasi yake ya CAG, CCM ilikuwa haina Ofisi?

Ofisi ni Jambo la muhimu kwa chama cha siasa, lakini si takwa la kikatiba wala si kigezo cha ubora wa chama.
CCM kumejaa majangili tupu
 
Back
Top Bottom