Kama kweli Mo Dewji kamuuza Chama katukwaza wana Simba

Mtu aweke mpunga wake alafu aje kukuuliza wewe jinsi ya kufanya biashara?

Kama umetoa chozi utakuwa sio mzima wewe. Hayo ni matumizi mabaya ya machozi.

TRA washapata chao tayari naamini.
 
Lakini si mlisema kila kitu mmemwachia Mo ispokuwa tu nyie mashabiki mnataka furaha ya kushinda mechi, sasa mnalalamika nini?
Mimi ni shabiki wa Simba Sc ila sinaga huo ujinga, shabiki wa kweli wa mpira lazima auseme ukweli kila inapotakiwa(criticism). Hata ukiangalia hoja mbalimbali humu sijawahi kuside na Mo eti simply kwasababu ana hela, anapofanya la msingi nitapongeza na anapopunyanga nitasema.

Ukisema Team umemuachia Mo ati unachotaka ni furaha, vipi siku hiyo furaha isipokuwepo umuhimu wake utaonekana? Kama kuna mtu anadhani mafanikio katika mpira ni kitu cha kudumu awaangalie kwanza AS VITA, MAZEMBE na ZAMALEK ,PYRAMIDS na wengine wengi.Hao wote wanampunga mrefu kuliko SIMBA SC,lakini kwasasa hawazungumziwi kabisa.
 
Tuombe Mungu replacement itayofanyika ikidhi mahitaji, vinginevyo team ikishuka performance haya maneno mtakuja kuyakataa wenyewe.
 
Team haifi...tumetumia B21 ndani ya miaka4.. Sasa tunataka irudi hiyo hela haraka iwezekanavyo ndani ya muda mfupi😂😂 tunajaribu kuona hata kama tunawez kuuza na baadhi ya mashabiki ili tufidie hiyo hela kwa haraka😂😂
 
Mkuu hata Kama mpira Ni biashara,Sasa tunauza key players kwa wakati mmoja?nimesikitishwa.
Kwa hiyo kuna muda maalum wa kumuuza mchezaji?!! Sio kama ukihitajika leo, bado na kesho utahitaji, hata wakihitajika watano uza tu, tena pesa zenyewe hizo!! Siachi
 
Chama kaondoka aisee, pia dharau za Mo kwenye Instagram Ile siku ukute imechangia pia Chama kuondoka.
Aende tu....wakati wake wa kuondoka ndio ulikuwa huu.
 
Chama ameshazeeka, anatuambia anayo miaka 30, ukijumlisha na 10 atakuwa na 40.

Heri ameuzika
 
Hujui mpira wewe!!
 
Dr. H. Manara tusamehe baba, Yaliyopita si Ndwele, Tugange Yajayo.

Boss alitaka kwenye nembo iwekwe kichwa chake!

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…