Kama kweli nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, then "Twende kwenye Serikali Moja!"

hakuna kisichowezekana chini ya jua!, kama mwanzo tuliweza kwa nini sasa tushindwe?.
Pasco

Mwanzo gani uliweza?! Kwanza bwana Pasco, Zanzibar ni nchi au si nchi? Ukijibu tutajadili kwa nini ni serikali 1 na au kidogo 3 na si mbili(2)!
 
Mkuu Tujitegemee, safari ya kuelekea kwenye serikali moja ndio njia pekee ya kuuimarisha muungano kwa dhati, kwa sababu nauhesabu muungano wetu kama ndoa, "mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataandamana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja!". This is a very big sacrifice!.

Ili kuimarisha kuiimarisha hiyo ndoa lazima hizi big sacrifices za kuachana na baba yake na mama yake zifanyike, na kuandamana na mkewe!. Wale wanandoa wanaendelea kukaa kwa wazazi, ndoa zao hukumbwa na matatizo!.

Tanganyika na Zanzibar zilipoungani, ni Tanganyika pekee, ilitoa the biggest sacrifice, ya kuupoteza utaifa wake, ikauua kabisa for the sake of union na kuwa Tanzania!. What sacrifice did Zanzibar did?!. You can't eat your cake and have it!. Kama mmemsikia vizuri Jaji Warioba, wazo la muleta serikali tatu, ili ili kuibembeleza Zanzibar ibakie kwenye muungano kufuatia katiba ya Zanzibar kuuvunja muungano kimya kimya huku bara ikinyamaza, ikimchelea mwana kulia!. Kwenye thima ya Muungano, Tanganyika iliishakufa zamani, hivyo nchi inayoitwa Tanganyika, haiwezi tena kukufufuka!, this is a very big sacrifice!, dhima hiyo ikaitambulisha Zanzibar kuwa "sii nchi" bali "ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" yenye mamlaka yake ya ndani!. Katiba ya Zanzibar ya 1984 (Toleo la 2010), linaitambulisha Zanzibar kama nchi, ndani ya JMT, ina weka mipaka yake!, bendera yake!, wimbo wake wa taifa!, na kumtambulisha rais wa Zanzibar kama Amiri Jeshi Mkuu wa Jeshi la JKU na Vikosi vya SMZ!, uliwahi kuona wapi nchi ndani ya nchi?!.

Inaonekana kana kwamba Zanzibar inabembelezwa ibaki ndani ya muungano kwa kuiacha ifanye kila inanachotanga!, kama ni sacrifices, only Bara!, kila kitu ni Bara!, wajumbe wa tume ya kukusanya maoni 50/50!, kugharimia gharama za tume, ni bara asilimia 100!. Sasa bunge la Katiba, nalo linagharimiwa 100% na bara!.

Sasa kama nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, its about time, Zanzibar nayo, itoe sacrifice, ipoteze utaifa wake!, tende kwenye nchi moja, serikali moja na rais mmoja, tena ili kuwapunguzia machungu, wenzetu, katiba itamke rais wa kwanza, atatoka Zanzibar (awe Dr. Shein).

Nimeitaja CCM kwa sababu tukubali, tukatae, CCM ni chama dola!, kama kiliweza kuamua yale mengine!, na kama nia ya dhati ni kuimarisha muungano, sio serikali tatu!, sio serikali mbili!, ni serikali moja!.
Pasco.
 
Mwanzo gani uliweza?! Kwanza bwana Pasco, Zanzibar ni nchi au si nchi? Ukijibu tutajadili kwa nini ni serikali 1 na au kidogo 3 na si mbili(2)!
Mkuu Chaza, Zanzibar ilikuwa nchi hadi April, 26, 1964, from there, haiku nchi tena bali sehemu ya JMT!, kama ilivyokufa Tanganyika tarehe hiyo hiyo na kuundwa JMT.

Tanganyika ilipoteza utaifa wake na Zanzibar ilipoteza utaifa wake!. Kilichofanywa na Katiba ya Zanzibar ya 1984 toleo la 2010, ilikuwa ni kama kwenye ndoa, mke kaomba talaka ili aachwe, ukagoma, akaamua kufanya vitendo vya kupelekea kuvunjika kwa ndoa, ikiwemo kwenda nje ya ndoa!. Hivyo ilichokifanya Zanzibar ni kutokaq nje ya ndoa ili kupewa talaka!.

Bahati nzuri au mbaya, sijui tuiite Tanganyika ni mume zoba, au ndio anampenda sana mkewe!, hata baada ya kuushuhudia uzinifu huo wa mkewe, bado anampenda sana!, na kosa moja haliachi mke!, hivyo amesamehe na ndoa inaendelea, huku huyu mke akiendelea na visa hivi na vile kudai talaka yake!.

Pasco.
 

Mmmmh. Mkuu basi hata kukemea jambo la kuandikwa katiba kinyemela sijamsikia kiongozi yeyote mkuu wa Kitaifa akikemea jambo hilo, kwa nini? Huko si ni kulea maradhi, hayawezi kuleta madhara makubwa baadae? Wewe kaka Pasco unasimamia wapi? Unajemea au unaona ni sawa tu walichofanya Zanzibar?
 
Kwa Wazanzibar, hizi ni ndoto za mchana na labda masihara au matusi
 

Sorry, unajemea nilimaanisha unakemea! Android keyboard zinazingua kidogo
 
Waheshimiwa mkia hapo Dodoma tuleteeni Serikali moja ili kudumisha umoja wa Watanzania. Sababu nyingine nawaachia wenzangu wachangie.
 
That is a point muungano utaimarika zaidi na utapunguza gharama kwa sana tu
 
.....wewe hausomi,serikali moja haiwezekani,Zanzibar itapoteza na siku watadai tena zanzibar yao serikali 3 iko poa maana mguu moja ndani moja nje.
 
Bwana Bobwe, nahisi umechangia kichuki zaidi kwa Nyerere kuliko mada ilivyokua ikipendekeza ya bwn Pasco, mapendekezo ya Pasco yanataka tuwe na serikali moja, kinyume na matakwa ya Nyerere na ccm yake, hapa wewe unawapinga wote, Nyerere na Pasco, lete mapendekezo yako, unataka serikali ngapi? kama 2 basi kubali kwamba unamuunga mkono Nyerere na kama 1 basi weka like kwenye huu uzi wa Pasco au kama 3 basi kubaliana na Warioba, huwezi kupinga wote tu bila kuja na mmbadala wa hili jambo.

Hivi vitisho vya eti Wazanzibari wa 64 sio wa sasa, hayo nayo ni majigambo tu, mtu mzima hatishiwi Nyau mkuu!
 
Maoni yalishakusanywa na tume ya Warioba Pasco. Kilichobakia ni kwa bunge la katiba kuyathibitisha maoni ya raia wa Tanzania.

Kwa upande wa ZNZ na Bara wengi wanataka serikali tu, ikifuatiwa na mbili. Moja haina support usiturudishe nyuma bhana!

Time is precious!

Zanzibar kwanza halafu Tanganyika ifuatie.
 
Hii nimeikuta mahali nikaipenda, nikaiona itafiti sana hapa!.
Mkuu Buchanan, asante kwa hili, na mimi nililizungumzia hapa [h=3]Kama Kweli Nia ya Dhati ni Kuimarisha Muungano, Then, Twende Kwenye Serikali Moja!"!.[/h]Pasco
 

Ili kuimarisha muungano nchi hii iitwe Zanzibar na kwa vile Zanzibar siko kunakozalishwa mazao ya kilimo mji mkuu wa nchi hii uwe Zanzibar!
 
Serikali moja ndio italeta maana hasa ya muungano, vinginevyo ni usanii uleule wa1964; mmoja anakufa mmoja anabaki. Kwa sababu ya uroho wa madaraka, serikali tatu angalau itaonyesha nchi zimeungana. Huu wa sasa ni kiini macho tu.

Unaonaje tukaacha kugombana na wenzetu tukakimbilia kwenye muungano wa Afrika Mashariki? Kitu kizuri kila kikiwa kikubwa ni bora zaidi!
 
Katika Africa Tanzania ni taifa pekee ambalo limejiunda lenyewe, mipaka yake inatokana na utashi na uamuzi wa watu wake sio wakoloni. Kuulinda Muungano nikukuza tamaduni tuliyoianzisha wenyewe! Watanzania hatukuishia kuuondoa ukoloni tu bali hata mambo yao ya kijinga tuliyakataaa.
 
Kwel mdau kama kwel ccm wanaupenda sana muungano bas wajikite kwenye serikali moja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…