Kama kweli nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, then "Twende kwenye Serikali Moja!"

Kama kweli nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, then "Twende kwenye Serikali Moja!"

Mkuu Tujitegemee, safari ya kuelekea kwenye serikali moja ndio njia pekee ya kuuimarisha muungano kwa dhati, kwa sababu nauhesabu muungano wetu kama ndoa, "mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataandamana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja!". This is a very big sacrifice!.

Ili kuimarisha kuiimarisha hiyo ndoa lazima hizi big sacrifices za kuachana na baba yake na mama yake zifanyike, na kuandamana na mkewe!. Wale wanandoa wanaendelea kukaa kwa wazazi, ndoa zao hukumbwa na matatizo!

Tanganyika na Zanzibar zilipoungani, ni Tanganyika pekee, ilitoa the biggest sacrifice, ya kuupoteza utaifa wake, ikauua kabisa for the sake of union na kuwa Tanzania!. What sacrifice did Zanzibar did?!. You can't eat your cake and have it! Kama mmemsikia vizuri Jaji Warioba, wazo la muleta serikali tatu, ili ili kuibembeleza Zanzibar ibakie kwenye muungano kufuatia katiba ya Zanzibar kuuvunja muungano kimya kimya huku bara ikinyamaza, ikimchelea mwana kulia!

Kwenye thima ya Muungano, Tanganyika iliishakufa zamani, hivyo nchi inayoitwa Tanganyika, haiwezi tena kukufufuka!, this is a very big sacrifice!, dhima hiyo ikaitambulisha Zanzibar kuwa "sii nchi" bali "ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" yenye mamlaka yake ya ndani!. Katiba ya Zanzibar ya 1984 (Toleo la 2010), linaitambulisha Zanzibar kama nchi, ndani ya JMT, ina weka mipaka yake!, bendera yake!, wimbo wake wa taifa!, na kumtambulisha rais wa Zanzibar kama Amiri Jeshi Mkuu wa Jeshi la JKU na Vikosi vya SMZ!, uliwahi kuona wapi nchi ndani ya nchi?!.

Inaonekana kana kwamba Zanzibar inabembelezwa ibaki ndani ya muungano kwa kuiacha ifanye kila inanachotanga!, kama ni sacrifices, only Bara!, kila kitu ni Bara!, wajumbe wa tume ya kukusanya maoni 50/50!, kugharimia gharama za tume, ni bara asilimia 100!. Sasa bunge la Katiba, nalo linagharimiwa 100% na bara!.

Sasa kama nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, its about time, Zanzibar nayo, itoe sacrifice, ipoteze utaifa wake!, tende kwenye nchi moja, serikali moja na rais mmoja, tena ili kuwapunguzia machungu, wenzetu, katiba itamke rais wa kwanza, atatoka Zanzibar (awe Dr. Shein).

Nimeitaja CCM kwa sababu tukubali, tukatae, CCM ni chama dola!, kama kiliweza kuamua yale mengine!, na kama nia ya dhati ni kuimarisha muungano, sio serikali tatu!, sio serikali mbili!, ni serikali moja!

Pasco.
Very interesting
 
Naunga mkono hili bandiko.

Inashangaza ana kuona eti kuna muungano lakini Zanzibar kuna ZSSF,ZRA,Bodi yake ya mikopo nknk ambavyo ni kwa ajili ya wazanzibar tu Mtanganyika huruhusiwi kusogeza pua halafu kuna NSSF,HELSB nknk ambavyo ni kwa ajili ya Mtanganyika na Mzanzibari

Hiyo Tanzania iko wapi?
 
Serikali moja ndio wazo la wasio na uchu na tamaa za madaraka Serikali 3 ni mzigo wananchi masikini kuzilisha zote
 
Leo tunapo adhimisha miaka 60 ya huu muungano wetu adhimu, nafanya tafakuri, niliwahi kuandika nini humu kuhusu muungano wetu.
Nawatakia maadhimisho mema ya miaka 60 ya muungano wetu adhimu.
Ujumbe wangu ni muungano wetu adhimu udumu milele, na sasa ni muda muafaka tuachane na huu muungano wa kimaghumashi, wa union na federation, sasa twende kwenye muungano wa kweli wa union wa nchi moja, serikali moja, na rais mmoja!.
Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Tusaidie
P
 
Back
Top Bottom