Kama kweli tunataka kujenga uchumi tupunguze bei ya vifaa vya ujenzi

Kama kweli tunataka kujenga uchumi tupunguze bei ya vifaa vya ujenzi

Shoctopus

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
3,434
Reaction score
1,985
Asalam-aleikoum Wana-JF,

Nimeona nitoe hoja yangu kuhusu maamuzi ya wanasiasa ya kuanzisha tozo kubwa za miamala ya mitandao kwa kisingizio cha kujenga uchumi. Lakini matokeo yake tunayaona, watu wanalia kila kona ni maumivu.

Hoja yangu ni kwamba badala ya tozo hizi mpya ambazo ni kuongeza makodi juu ya makodi, na ni jambo ambalo linadhoofisha shughuli za uchumi kupitia mitandao ya simu, serikali ingeshusha bei za vifaa vya ujenzi kama cement, mbao, mabati, misumari, nondo nk ili kuchochea shughuli za ujenzi nchi nzima.

Siku serikali ikifanya uamuzi huo nchi nzima itarindima kwa ujenzi kila kona! Na hivyo wananchi wengi watapata ajira, watalipa kodi zaidi ili serikali nayo iendelee na ujenzi wa hayo ma-SGR, madaraja nk. Lakini uamuzi huo utawawezesha wananchi wengi kujenga nyumba bora za kuishi, kuliko hivi mlivyopandisha bei za vifaa vya ujenzi marudufu hadi watu wamekata tamaa, hakuna ujenzi hakuna ajira.
 
Utaratibu huo utawachelewesha sana. Wao wanahitaji kuchukua chao mapema!

Chukua Chako Mapema (CCM)!

Waongeze tu makodi. Kwanza hata hizi tozo za miamala tuliridhia wenyewe.

Tozo na kodi zote zingeongezwa maradufu ingependeza zaidi.
 
Kuna baadhi ya binadamu hawatamani kuona unajenga nyumba yakuishi, furaha yao wakuone unaishi nyumba ya kupanga ndiyoroho zao zitarizika mkuu.

Cement, bati, nondo, mbao, misumali yote inatengenezwa apa nchini lakini bado tunapigwa.

Mama samia asipokua makinu watanzania wote watamchukia, na ataacha watu wakinung'unika nyuma yake kwa shida na tabu.
 
Nafikiri kodi ingepunguzwa zaid kwa vitu kama magari kutoka nje ili serikali ipige pesa kwenye mafuta nk
 
Nafikiri kodi ingepunguzwa zaid kwa vitu kama magari kutoka nje ili serikali ipige pesa kwenye mafuta nk
Uko sahihi sababu wengi wangemiliki magari.Na effect ya Kodi ingekuwa juu magari yakiwa mengi kuna Kodi kwa lita,Kodi vipuri,halafu ajira zingezeka za mafundi makenika na madereva ,pia gereji zingeongezeka .Chain ya kukusanya Kodi ingekuwa kubwa
 
Ushauri mzuri hivi mnawapa hawa mumiani maccm?? Mnapoteza muda wenu
 
Utaratibu huo utawachelewesha sana. Wao wanahitaji kuchukua chao mapema!

Chukua Chako Mapema (CCM)!

Waongeze tu makodi. Kwanza hata hizi tozo za miamala tuliridhia wenyewe.

Tozo na kodi zote zingeongezwa maradufu ingependeza zaidi.
Mpaka watu watakapo pata akili
 
Back
Top Bottom