Kama kweli unamchukia Hayati Magufuli fanya haya utuachie tunaompenda

haya huyu ambae si dikiteta amewaletea nn
Kakamilisha bwawa la Nyerere, kakamilisha SGR ya Dar-Dom, kaongeza ukusanyaji wa mapato kutoa 1T za JPM hadi 2T!! Anajenga Kinyerezi 3 ya kuongeza umeme wa gesi, mwendokasi phase 4 and 5, kaongeza ajira zaidi ya mara 4 ya alizotoa JPM, uwekezaji umeongezeka zaidi ya mara 4 ya enzi za JPM na n.k

Lakini licha ya hayo yote bado anaitwa fisadi na dhaifu, unadhani miundombinu ndio itamuokoa?
 
Mkuu nadhani hujanielewa, Mama samia ana mazuri kibao in fact ameongeza makusanyo x2 zaidi ya JPM licha ya kwamba huwa tunamuita dhaifu. Kwanini? Sababu madhaifu yake ya kiuongoze yanazidi mafanikio yake ya kimiundombinu
 
Unataka kutuambia nchi haina dira ya maendeleo na ilikuwa inamsubiria Magufuli awe Rais ili aipe dira?
 
Mapato yameongezeka kwa kuuza rasilimali zetu?!
 
Kwanza kajifunze kusoma na kuandika ndiyo uje JF kubishana na wenye akili. Hakuna neno "ekali" kwenye Kiswahili
Wewe ndo hauna akili naona unajaribu kubishana na majibu ambayo unayo ata wewe..Tujikite kwenye kutetea taifa labda kama wewe unaishi kwa shemeji yako na kila kitu unategemea akupatie kupitia nguvu ya dada yako kitandani.
 
Siwezi bishana na wewe kwa sababu nimeandika kitu kinachoelewaka hapo.
 
Mkuu nadhani hujanielewa, Mama samia ana mazuri kibao in fact ameongeza makusanyo x2 zaidi ya JPM licha ya kwamba huwa tunamuita dhaifu. Kwanini? Sababu madhaifu yake ya kiuongoze yanazidi mafanikio yake ya kimiundombinu
Kwa kuongeza makodi kibao yasiokuwa na kichwa wala miguu yanayowakamua wanainchi bila huruma lazima makusanyo yawe juu.... pamoja na hivyo hayo mapato hata kama yamaongezeka haina maana au umuhimu haonekani ikiwa kama kiasi kikubwa kinaishia mifukoni mwa mafisadi na yeye ameshindwa kuyathibiti.... binafsi huwa naona hata uvivu kuuongelea huu uongozi wa Samia, wanaoufurahia acha waufurahie.
 
Magu alikuwa hovyo sana?
 

Kama kweli unamchukia Hayati Magufuli fanya haya utuachie tunaompenda​



hama Inchnji...in Maasai voice

Unamchukiaje Mwamba aliyejenga Nchi?

Wanaomchukia ni masaliti na vibaraka wa mabeberu.

Wahame!

Hamaki na Nimegonga meza
 
Hata haiitaji akili nyingi sana kulitambua hili.

Ukiskiliza sababu za wengi wa hao wanaomchukia hayati Magufuli kupitiliza wanakwambia alikuwa muuaji,mporaji,mtekaji mara sijui udikteta n.k.

Lakini kiukweli ndani ya mioyo yao hayo si mambo yanayofanya wamchukie Magufuli isipokuwa tu hizo ndio sababu wanazoona zina maana wakizitaja mbele za watu kujustify chuki zao kwa yule mtu...

Si kweli kwamba eti wanaumizwa sana na utekaji wa Mo, si kwamba eti wanaumizwa sana na matukio ya kinyama waliofanyiwa akina Aliphoso Mawazo,saanane na wengineo awamu ile.....nasema hivi si kwa lengo la kubaliki vile vitendo vya kiovu hapana, maana vingeweza kunitokea hata mimi.

Wengi wanaomchukia bwana yule ni kwa sababu zao binafsi tu ambazo ni kuharibiwa mifumo ya kuendesha maisha yao binafsi kwa njia za shortcuts na ujanja ujanja ambazo walikuwa wamezizoea kwa miaka mingi kabla ya awamu yake.

Nakumbuka baada ya jamaa kufariki kuna mzee mmoja pale Mwanza ni mfanya kazi mkongwe wa NIMR alionesha kufurahi mno akisema kabisa kwa watu, kwamba tangu aanze kufanya kazi kwenye hiyo taasisi hakuna kipindi ambacho aliishi kwa shida sana kama kipindi cha Magufuli, sababu pesa zilikuwa hamna yaani ilikuwa kila wakiandika Proposal kwenda wizarani kwa ajili ya kujiingizia pesa zilikuwa zinapigwa chini au kama sio kupigwa chini basi wanawekewa mlolongo mrefu sana wa kuzipata hizo hela za Proposal, mpaka ikafika kipindi wakaacha hata kuandika Proposal wakawa wanasubiri zile za kutumwa na serikali. Kwa hiyo kifo cha Magufuli alitegemea kitampa haueni kubwa sana kwa maana ya kurudi kwenye yale maisha ya miaka ile ya kujichotea tu pesa za serikali...... na hata huyu mzee naye leo hii ukipiga nae stori kwa mtu ambaye hamfahamiani sababu za kumchukia Magu atakazozitaja ndio hizi hizi kama wanazosema hawa jamaa muuaji,dikteta, n.k

Ukitaka kuamini hawa haters wa marehemu Magu hizo wanazotaja sio sababu halisi zinazowafanya wamchukie angalia sasa hivi kuna matukio mengi sana ya kinyama yanaendelea hapa nchini kama ulawiti kwa watoto wadogo,upotevu wa mabinti wadogo kupitia biashara ya kusafirisha watu(humantraficking), mapadre kuuwawa(kumbuka tukio la kule mbeya),utekaji wa nyara na mauaji ya kiholela( kule kawe beach mwaka jana ilikuwa kila ifikapo weekend lazima watu waokote maiti) bado kuna ujambazi uliokithiri raia wanaonewa na kuporwa mali zao.... yote haya yanaendelea lakini huwezi kuwaskia hawa wapenda amani wakiongelea au kukemea sana sana utawakuta kwenye mada kama hizi wakijifanya wanauchungu sijui magufuli alikuwa ni mtekaji,dikteta n.k

Binafsi mimi Nikimskia mtu kama Tundu Lisu au mzazi wa Ben saanane analezea chuki zake kwa magufuli nitamuelewa sababu hawa wachache niliowataja walikuw ni wahanga kweli kweli wa awamu ya tano.... lakini hawa wengine machawa wa mafisadi na watumbuliwaji wa vyeti feki huwa nawadharau sana na ndio wengi.
 
Leo mtasema yote mnatuletea unafiki hapa. Sijawai kupewa pesa na mtu wala rushwa.
Linapokuja swala la kuusema ukweli lazima tuseme.
Kama humpendi kwanini unapita kwenye daraja alilosimamia huoni kama unaumiza moyo wako.
Mnaomchukia Kikwete tafuteni airport ya kupandia ndege, terminal three kajenga Kikwete.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…