Kama Lakini Una Moyo.... Nenda Kamchukue Mbuzi Wako

Jeshini kuna adhabu za kukomoana mkuu...!
Huyo mwenye mbuzi, awaachie tu hao wanajeshi wamfanye huyo mbuzi kitoweo.
Ila kama yupo tayari kufuata mbuzi wake, awe pia tayari kupewa hizi adhabu
  • Kubeba dunia
  • Kupiga simu
  • Kunyonya mafuta

waliopitia JKT wanaelewa nazungumzia nini hapo.
 
Kubeba dunia ndio lipoje hilo mkuu [emoji16][emoji16][emoji16]
 
Ila wameandika maneno mazuri kama sio wao vile! sasa jichanganye maana kuna maneno flan inabidi alarm igonge "alikuwa ana zurura na kula penye bustani "
 
Mm yule mbuz angekuwa wangu ningemtuma bibi kikongwe wa miaka 70 akamchukue tuone wangemfanyeje!
Jamaa una akili sana, sasa pale itakapotokea wakampandisha katika zile difenda za jeshi wakimleta nyumbani, wakimkuta kuna kijana yoyote wanaondoka nae
 
Bora niwaongezee mwingine kuliko kumtafuta huyo ..
 
Hii ni sawa na mwizi kufukuzwa kimya kimya hawana nia njema hao huo mwandiko ukiutizama kwa jicho la tatu unaona pana tatizo.Yaani huu uungwana jeshi letu limeutoa wapi?
 
Hahaaa, kuna Police Traffic mmoja alikuwa bingwa wa kula pesa za waendesha pikipiki barabara ya Chalinze - Morogoro, sasa kuna mjeda alimdaka anaendesha pikipiki bila kuvaa kofia, kumbe jamaa alifanya makusudi alimtegea. Alipomdaka bila kujua kuwa ni mjeda akaanza kudai kitu kidogo, jamaa akamuambia kwa wakati ule hana kitu kama vipi apande pikipiki aende nae mpaka kwa uncle wake jirani na pale ili akampe.

Yule Traffic akakubali lakini akataka yeye ndiye aendeshe pikipiki, kumbe jamaa anampeleka kambini. Traffic anashangaa wakati wanafika getini jamaa anapigiwa saluti, kwanza akawa mpole ghafla, yule mjeda wa pale getini amuuliza mwenzie "Umemleta eeeh??" jamaa akadai "Ndiyo" Basi jamaa wakamchukua yule traffic mpaka kiwanjani wakampa adhabu ndogo tu, wakamuuliza "Wewe si unapenda sana kuendesha pikipiki za watu, sasa leo tunataka uendeshee hii pikipiki mpaka mafuta yaishe."
Jamaa wakamjazia full tank wakamwambia azunguke uwanja mpaka mafuta yaishe ndio aende zake.
Sasa huyu mwenye mbuzi ajiandae kama atakwenda kumfuata Mbuzi wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…