Kama machafuko yatakuja kutokea Venezuela na damu kumwagika wakulaumiwa ni jeshi la polisi ! Polisi haijulikani ni jeshi au kikundi cha kisiasa

Kama machafuko yatakuja kutokea Venezuela na damu kumwagika wakulaumiwa ni jeshi la polisi ! Polisi haijulikani ni jeshi au kikundi cha kisiasa

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Ninamashaka makubwa na sera za polisi hapa Venezuela hasa kutoka makao makuu ya jeshi Hilo hapa mjini Colombo kama linalinda raia na mali zao ama lipo kupambana na wanasiasa ! Polisi hapa mjini Colombo kwa sasa linapambana na kauli za mapambano ya wanasiasa hasa kipindi hiki ambacho mabondia wakisiasa wanatambiana ! Polisi wanaingilia kauli zinazotolewa na wapinzani lakini hawafuatilii kauli zinazotolewa na viongozi wa chama tawala ! Leo hata mtu akiamua kutoa malalamiko au kero zake kwa serikali ni jinai ! Waalimu wasio na ajira wamejaribu kutoa kero zao wameishia kunigwa roba na sasa tunasikia wako mahabusu ! Kuna mtu analipeleka jeshi hili mahali pabaya Sana! Kuna mtu anatufanya wanavenezuela tuliona jeshi kama kikwazo na sio usalama Tena ! Mbinu za ukamataji nazo pia zimebadilika ,polisi wanamkamata mtu kwa magari binafsi na kupambana nae kama jambazi katikati ya makutano ya watu ! Polisi wa sasa wamefuga Rasta na wananyoosha bastola hadharani ! Kama Kuna siku nchi ya vene itaingia kwenye vurugu na haitatawalika Tena basi chanzo litakuwa ni jeshi la polisi ! Venezuela sio sehemu salama
 
Back
Top Bottom