Kama Mama Malecela hafai, je Mbowe anafaa?

Kama Mama Malecela hafai, je Mbowe anafaa?

Mkuu FMES,
Ushauri mzuri mkuu. Lakini tunalijadili kwa vile limeletwa kwenye thread na ni suala muhimu sana kwa taifa. Kuwa na raisi mwenye elimu ya form six tu kwenye karne hii ya 21 ni hatari na ni uzembe wa hali ya juu. Mbowe alipewa nafasi na Chadema kuiongoza nchi, chamani na uraisi. Kama Chadema wanaridhika na uongozi wake, ni juu yao, lakini anapopendekezwa kuiongoza nchi inakuwa ni suala la taifa na ni vema likajadiliwa wakati wowote anapopendekezwa kuwa raisi.

mbaya zaidi wafuasi wao wanaacha bwana wao aathirike, maana hawajui jinsi ya kumtetea, kila wakimpaka rangi apendeze, jamaa wapi !

eti kuna njimbi inaniambia nimpe cv yangu utadhani niliomba kumtawala !
 
Licha ya kuwa Brazil sio Tanzania, tusiwe wazembe kwa kuwapigia debe watu wasio na minimum qualifications za kuiongoza nchi yetu, kwa vile tu ni wa vyama vyetu, dini zetu au makabila yetu. Form Six na ukarani wa BOT sio minimum qualification tunazohitaji raisi wetu awe nazo.

mwaga mawe mzee hadi wakimbie !!
 
Hii ni kubwa Mbowe ni form six na ukarani wa BOT tu, anawanyima usingizi CCM na MAFISADI! Je angekuwa graduate ingekuwaje? Naona huyu bwana ni tishio sio mchezo.

Kila moto ukiwaka utaona na jina la Mbowe linatokeza kama uyoga, moto ukitulia na jina lake linatoweka kama theluji.

right on ! hata niliposoma kuhusu yale mamilioni ya NSSF, lilitokea jina la mbowe.......kuhakiki kifo cha ballali, MBOWE popped out as well !
 
CV - Curriculum Vitae - A summary of one's education, professional history, and job qualifications, as for a prospective employer.

Ahsante.

Ukarani wa BOT na elimu ya Form VI, ndio summary yote ya professional history na elimu ya Mbowe?


CV nzuri ni ile iliyo na angalau sifa za chini kabisa kwa ajili ya ajira husika. Ukiwa na sifa zaidi ya zile za chini kabisa ni vema zaidi.

Ahsante tena.

Sifa za chini kabisa kwa ajira ya Urais ni zipi, na kwa mujibu wa mwajiri gani wa Rais?
 
Ahsante.

Ukarani wa BOT na elimu ya Form VI, ndio summary yote ya professional history na elimu ya Mbowe?




Ahsante tena.

Sifa za chini kabisa kwa ajira ya Urais ni zipi, na kwa mujibu wa mwajiri gani wa Rais?

kazi nzuri wazee, elimu ya chuo kikuu inahitajika sana kwa mtu anayetaka kuwa raisi. Inabidi watanzania waachane na watu ambao hawajasoma kama hawa.

Elimu ni muhimu kuliko mengine yoyote yale.
 
kazi nzuri wazee, elimu ya chuo kikuu inahitajika sana kwa mtu anayetaka kuwa raisi. Inabidi watanzania waachane na watu ambao hawajasoma kama hawa.

Elimu ni muhimu kuliko mengine yoyote yale.

elimu nzuri bila maadili inasaidia nini? maadili ni muhimu kuliko elimu. hao kina chenge, mramba na ballali wametupatia nini na elimu zao?
 
right on ! hata niliposoma kuhusu yale mamilioni ya NSSF, lilitokea jina la mbowe.......kuhakiki kifo cha ballali, MBOWE popped out as well !

na huyu mbowe inabidi arudi kwenye biashara zake. chadema ni chama cha wafanyabiashara wakati ccm ni chama cha wakulima. mbowe mpaka utoke kwenye siasa. hapa ni kibano tu.
 
elimu nzuri bila maadili inasaidia nini? maadili ni muhimu kuliko elimu. hao kina chenge, mramba na ballali wametupatia nini na elimu zao?

elimu ni muhimu na mbowe na mrema inabidi wasome kwanza la sivyo wataendelea kugalagazwa kwenye chaguzi.
 
elimu ni muhimu na mbowe na mrema inabidi wasome kwanza la sivyo wataendelea kugalagazwa kwenye chaguzi.

kama ni hivyo basi profesa lipumba ndiye anafaa kuwa raisi kwa mtizamo wako na sio hao wezi na mafisadi wa ccm kina kikwete.
 
CV ya Mbowe







http://www.parliament.go.tz/bunge/Mp_Cv3.asp?PTerm=2000-2005&fpkey=261&vusername=GUEST")


  1. Jamani hivi kweli hii CV ya Mbowe inafaa kuwa kiongozi nchi au wa chama au hivi vyeo tunapeana tu?
  2. Licha ya elimu ndogo, form six, experience aliyonayo ni ya ukarani tu, BOT. Je hivi vinatosha kuongoza nchi au hata chama cha siasa?
  3. Hivi akina Dr. Slaa, Zitto n.k. wamekubali vipi au wanajisikiaje kuongozwa na mtu wa elimu ya form six?
  4. Je elimu ndogo na uwezo mdogo wa Mbowe ni kikwazo kwa Chadema katika kuwabana vihiyo ndani ya CCM?

wewe dogo mgaya hebu soma nondo hizi toka kwa great thinkers wa ccm, je una jibu hapa?
 
kama ni hivyo basi profesa lipumba ndiye anafaa kuwa raisi kwa mtizamo wako na sio hao wezi na mafisadi wa ccm kina kikwete.

lipumba na chama chake cha kidini hawezi kutawala tanzania.
 
wewe dogo mgaya hebu soma nondo hizi toka kwa great thinkers wa ccm, je una jibu hapa?

haya maswali yatasaidia kuondoa ufisadi tanzania? yaani mafisadi kwa vile mmekosa namna ya kutetea sera zenu sasa mnakuja kwenye elimu ya Mbowe.
 
kama cuf ni chama cha kidini basi na ccm ni chama cha kidini. wewe unasemaje?

huwezi kulinganisha viongozi wa kidini wa cuf na wale wa ccm. ccm kuna wakristo lakini cuf hakuna.
 
huwezi kulinganisha viongozi wa kidini wa cuf na wale wa ccm. ccm kuna wakristo lakini cuf hakuna.

hata cuf kuna wakristo. viongozi wa ccm nao ni waislam, tena halmashauri kuu na kamati kuu ya ccm ni waislam kwa asilimia 75. ccm ndio chama cha kiislam na cuf ina wanachama wa dini zote.
 
Mama Anne Kilango Malecela, Mbunge,

kwanza Mwalimu wa Sekondari ya Kisutu, huku akiwa mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kionondoni, akawa Accountant ATC, akawa Senior Accountant Gulf Air, huku akiwa mmoja wa Directors wa Casino pale Sea View, akawa mbunge wa kuteuliwa na rais, baadaye akaw mbunge wa kuchaguliw na wananchi hadi sasa, pia ni mfanya biashara maarufu wa bidahaa mbali mbali toka USA na Europe, akimiliki maduka makubwa ya bidhaa hizo kati ya Dar, Dodoma, na Same, sasa hivi pia ni makamu mwenyekiti kamati ya bunge ya Miundo Mbinu, na pia mwenyekiti wa kamati ya maadili ya viongozi ya bunge,

Toka awe mbunge wa kuchaguliwa amekuwa kiongozi hodari wa kukataa ufisadi, ndiye aliyeongoza mapambano ya kumuondoa madarakani aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani Lowassa, baada ya hapo ndiye aliyepigana sana mpaka kuufuta mkatba wa kifisadi ulikouwepo bandarini kwa miaka kumi na ulikuwa uwepo kwa miaka 15 zaidi, akiwa kama mwenyekiti wa muda wa kamati ya Miundo Mbinu ya bunge kutokana na mwenyekiti wa kamati Ndugu Misanga, kutoweza kushiriki kikamilifu kwenye kamati hiyo kutokana na kuumwa sana ugonjwa wa kisukari, Mama mbunge pia kwa sasa yupo Chuo Kikuu Huria akimalizia Degree ya Uchumi.

Sasa mnyonge mnyongeni lakini haki apewe, ningeomba mtoa mada hii atuwekee qualifications za hao anaosema kuwa wameangalia CV ya huyu mbunge wetu wa taifa na kuona hafai, maana nina wasi wasi kuwa sio rahisi mwananchi mwenye CV ya wasi wasi kuweza kuielewa CV inayofaa au isiyofaa, au kuelewa kuwa ni kiongozi yupi anafaa na yupi hafai, halafu ikiwezekana atupe historia ya hao wanachi jinsi ambavyo wamewahi kulisaidia taifa letu na hizi hukumu, ambazo pia watuambie wamezi-base on CV za viongozi wapi hao wa taifa letu wanaofaaa!

Ninasema kuwa Mama Anne Kilango Malecela, anazo qualifications zote anazozihitaji kuwa na nafasi aliyonayo sasa, yaani mbunge wa kuchaguliwa na kuwawakilisha wananchi bungeni.
 
kubwa jinga kwa faida ya mjadala rejea post ya mwisho ya nyama hatari, na fanya kama anavyofanya fmes, no wonder unapata majibu ya chooni, unahoji cv ya mbowe naamini na wewe cv yako imetulia ndo maana una ballz za kuhoji za wenzako, tumia basi kidogo hiyo elimu yako kuuliza maswali vizuri yaliyoenda shule, kama sivyo basi majibu mwafrika wa kike yanakutosha.
 
Mama Anne Kilango Malecela, Mbunge,

kwanza Mwalimu wa Sekondari ya Kisutu, huku akiwa mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kionondoni, akawa Accountant ATC, akawa Senior Accountant Gulf Air, huku akiwa mmoja wa Directors wa Casino pale Sea View, akawa mbunge wa kuteuliwa na rais, baadaye akaw mbunge wa kuchaguliw na wananchi hadi sasa, pia ni mfanya biashara maarufu wa bidahaa mbali mbali toka USA na Europe, akimiliki maduka makubwa ya bidhaa hizo kati ya Dar, Dodoma, na Same, sasa hivi pia ni makamu mwenyekiti kamati ya bunge ya Miundo Mbinu, na pia mwenyekiti wa kamati ya maadili ya viongozi ya bunge,

Toka awe mbunge wa kuchaguliwa amekuwa kiongozi hodari wa kukataa ufisadi, ndiye aliyeongoza mapambano ya kumuondoa madarakani aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani Lowassa, baada ya hapo ndiye aliyepigana sana mpaka kuufuta mkatba wa kifisadi ulikouwepo bandarini kwa miaka kumi na ulikuwa uwepo kwa miaka 15 zaidi, akiwa kama mwenyekiti wa muda wa kamati ya Miundo Mbinu ya bunge kutokana na mwenyekiti wa kamati Ndugu Misanga, kutoweza kushiriki kikamilifu kwenye kamati hiyo kutokana na kuumwa sana ugonjwa wa kisukari, Mama mbunge pia kwa sasa yupo Chuo Kikuu Huria akimalizia Degree ya Uchumi.

Sasa mnyonge mnyongeni lakini haki apewe, ningeomba mtoa mada hii atuwekee qualifications za hao anaosema kuwa wameangalia CV ya huyu mbunge wetu wa taifa na kuona hafai, maana nina wasi wasi kuwa sio rahisi mwananchi mwenye CV ya wasi wasi kuweza kuielewa CV inayofaa au isiyofaa, au kuelewa kuwa ni kiongozi yupi anafaa na yupi hafai, halafu ikiwezekana atupe historia ya hao wanachi jinsi ambavyo wamewahi kulisaidia taifa letu na hizi hukumu, ambazo pia watuambie wamezi-base on CV za viongozi wapi hao wa taifa letu wanaofaaa!

Ninasema kuwa Mama Anne Kilango Malecela, anazo qualifications zote anazozihitaji kuwa na nafasi aliyonayo sasa, yaani mbunge wa kuchaguliwa na kuwawakilisha wananchi bungeni.


Mama Malecela ana sifa zote za kuwa kiongozi wa ngazi yoyote nchini. Lakini nafikiri nchi yetu inao wazalendo wengine wengi wenye sifa bora zaidi kwa nafasi ya uraisi.
 
haya Leo ni Leo!!
Naona ule ubishani kati ya Chadema na CCM umerudi tena!(Which for the fact huwa siupendi)

ES asantea kwa kudadavua vizuri.Na tuache wabishanao waendelee!!
Sisi watu wa chama cha DEMOKRASIA MAKINI walaa yetu macho tu
 
Back
Top Bottom