Kama Msuva angevumulia kidogo tu Wydad AC angeandika historia mpya Afrika

Kamgomoli

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2018
Posts
1,896
Reaction score
4,058
Wydad Casablanca wamechukua ndoo ya Klabu bingwa Afrika baada ya kumpiga Alahly 2:0.

Kama Msuva angevuta subira kidogo tu leo ingekuwa storry ingine kabisa.

Angekuwa Mtanzania wa pili baada ya Samata kuchukua CAF CHAMPIONS LEAGUE, mbona tungetamba!.

Lakini ndo hivyo tena kama mlivyosikia. Very sorry for him. Ndio maana kuna msemo mvumilivu hula mbivu.
 
Kachengana na gari la mshahara.
 
Kwani amehamia clabu ipi!?
 
Nadhani wachezaji wetu wanakosa wawakilishi wazuri wa kusimamia maslahi ya mchezaji angekuwa na wakala bora yeye ange focus na mpira wakala kuhakikisha maslahi ya mchezaji yanafikiwa hii ndio shida ya wachezaji wetu. Hatujui story kamili baina yao isije kuwa hata mkataba ali sign bila kujuwa ana sign nini wala usishangae. Maana ile ni team kubwa kule ndio kama team zetu kubwa za hapa sasa kweli wachezaji wote walipwe wewe tu usilipwe? nini hasa kimetokea ngumu kujuwa.
 
Yote ni maisha, msuva hachezi mpira kumfurahisha mwarabu na hakufika pale Kwa bahati mbaya. Msuva anakipaji na anajitambua kama rizki Ipo atapata timu na huwezi jua anaweza kukosa kunyakua Caf champion league akabeba UEFA champions league. Hatujui kesho yake ikoje, Mungu pekee ndiye anajua hatma ya Simon Msuva.
 
Raha ya mashabiki ni kuona mchezaji anakupa/anafika tunapotaka,

Lakini lazima tujue kuwa,mchezaji hayupo kwenye timu kwaajili ya kuwa kuwafurahisha mashabiki tu,

Bali ile ni ofisi yake ambapo anafanya kazi kwa masilahi yake,familia n.k.


Muda mwingi Kuna tabia ya mashabiki kuhoji mchezaji yuko wapi

Ni haki yao,lakini tumekuwa tukipewa majibu tofauti tofauti,tunaambiwa mchezaji Hana nidhamu,mlevi au majeruhi lakini nyuma ya pazia

Ni migongano ya masilahi
 
Tatizo ndumba zakubeba unapaka mafuta yamechanganywa na unga mtishamba
 
Kuna mambo ya kuvumilia kama mwanadamu! Ila siyo njaa. Huwezi kuchezea timu kubwa, halafu hulipwi mshahara mlio kubaliana kwenye mkataba.
 
Wala tusimjutie mtazania mwezetu tulaani kitendo Cha kutumika pasipo kulipwa pesa zake
 
Kwenye football hiyo inatokea, kuna changamoto nyingi wachezaji uwa wanakutana nazo.
Huwezi mlaumu Msuva,ni vizuri tuheshimu maamuzi yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…