Kama ni kweli hawa wasanii wanapelekwa Dubai kwa mission maalum Dubai Port, hakika inafikirisha!

Kama ni kweli hawa wasanii wanapelekwa Dubai kwa mission maalum Dubai Port, hakika inafikirisha!

Li ngunda ngali

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2023
Posts
707
Reaction score
2,572
Watanzania wenzangu hatima ya ustawi wa Taifa letu upo mikononi mwetu. Ni wajibu wetu kama Watanzania tujizuie kwa namna yeyote ima kununuliwa ama kushawishiwa kwa namna yeyote ile ilmradi tuligawe Taifa na rasilimali zetu.

Safari za namna hiyo za watu maarufu na wasanii wetu kwenda huko Dubai kwa nyakati za SINTOFAHAMU kubwa ihusuyo bandari yetu na wao badala ya kueleweka hakika zinaongeza maswali mengi mno kwa wenzetu wenye mashaka na mradi wetu pendwa tarajiwa.

Nakemea kwa nguvu zote, njia za aina yeyote zifananazo na hiyo ya ushawishi kwa jamii yetu kuhusu hilo!

Vilevile, siamini hao wasanii na watu maarufu wanatumia pesa zao kutoka mfukoni kuhimili gharama za hoteli za aina hiyo ya hapo juu kwa zaidi ya siku nne!

JE, KAMA HAWA WASANII WANATUNZWA KIFALME HIVYO (kama ni kweli) ILIKUWAJE KWA WAWAKILISHI WETU WALE 30?!

NAANZA KUHOFIA PENGINE TUPO KWENYE HATARI TARAJIWA!

Chama changu CCM naomba kama kikombe hicho kinaweza kutuepuka kwa kuzingatia MASLAHI MAPANA kwa Taifa letu tulipendalo na tukiepuke!

Kidumu Chama cha Mapinduzi.
 
Ila haya mambo mbona yanafanana na yale yale ya akina Mangungo? Hivi hatuoni kama tunadhalilishwa na watu wetu wenyewe?

Ukijiuliza hivi raia wa nchi zilizoendelea wanaweza kufanywa makatuni hivi na mataifa yao yakakubali?


God help us!
 
Waache wapige pesa za wajinga...Hata ukipewa dili kama hilo na wajinga wewe wapige tu maisha yaende.
HAPANA!

Tunao wajibu wa kuelimishana na kukumbushana ndugu yangu.

Huenda (kama ni kweli) ndugu zetu hao wanalipwa kwa minajili hiyo. Lakini swali ni je vipi kuhusu vizazi vyao vijavyo?! Huoni wanajipalilia laana isiyo na ukomo?!

Naogopa!
 
Deal gani la kishamba hivyo? Yaani uuze urithi wako kwakwenda kulazwa hotel na kulishwa kama mwali huku wewe ni mwanaume rijali si aibu hii mchana kweupe?

HAPANA!

Tunao wajibu wa kuelimishana na kukumbushana ndugu yangu.

Huenda (kama ni kweli) ndugu zetu hao wanalipwa kwa minajili hiyo. Lakini swali ni je vipi kuhusu vizazi vyao vijavyo?! Huoni wanajipalilia laana isiyo na ukomo?!

Naogopa!

Hao hawapo kwenye kusaini madokoment ,hao wapo kikazi zaidi wanaambiwa kuna mchongo huo kazi ya yako ni kupiga ngenga tu tunakupa usd 10,000 na safari yote gharama juu yetu utakataa? wakuwamaindi ni wale wabunge 30 Aunt na mwenzake Dr M-Push wao ndiyo waliouza nchi ,hao wasanii tunawaonea bure ,wao kazi yao ni kupiga ngenga tu.,yeye anamezeshwa script tu.
 
Hao hawapo kwenye kusaini madokoment ,hao wapo kikazi zaidi wanaambiwa kuna mchongo huo kazi ya yako ni kupiga ngenga tu tunakupa usd 10,000 na safari yote gharama juu yetu utakataa? wakuwamaindi ni wale wabunge 30 Aunt na mwenzake Dr M-Push wao ndiyo waliouza nchi ,hao wasanii tunawaonea bure ,wao kazi yao ni kupiga ngenga tu.,yeye anamezeshwa script tu.
Hatusemi juu ya ku sign au kuto sign ni aina ya raia tulionao...Hii ni reflection ya poor citizenry, hata hao wanao sign mikataba wanaonekana ndiyo level yao hiyo, kama siyo binadamu mwenye kujielewa kwa nchi yake anawezaje kukubali kufanywa katuni hivyo kwa mambo serious kama haya?

We are all made fools kama watanzania na ndiyo tafsiri yake hata kama una negotiate hutopewa heshima kama nchi kama raia wako wakipewa pilau tu wanafurahia as if makwao pilao hazipo...What a shame to our country...
 
Kama hili ni kweli basi hizi aibu hakika atazibeba yule anayewatuma, au anayetazama wanavyotumwa na kunyamaza kimya, hili taifa kwa sasa halina kiongozi.

Wajinga wanaodhani yupo wanayemdanganya, kumbe kiuhalisia wanajidanganya wao wenyewe.

Kama maswali ya msingi wameshindwa kuyajibu kuhusu ule mkataba, wanachokifanya hapo kuendelea kuchezea pesa za walipakodi ni sawa na kuendelea kuwatukana tu.

Hawa mawakala wa shetani wamelaanika sawa na shetani anayewatuma, tuna bahati mbaya sana watanganyika kuwa na kiongozi mjinga asiyejali, kiongozi ambaye badala ya kutatua tatizo, yeye ndie analikuza zaidi.
 
Mm naona hawa wajinga waliokubali kutumiwa kiasi hiki na wale watangauzazi watatu ndio tuanze nao.
 
Back
Top Bottom