Kama ni kweli hawa wasanii wanapelekwa Dubai kwa mission maalum Dubai Port, hakika inafikirisha!

Kama ni kweli hawa wasanii wanapelekwa Dubai kwa mission maalum Dubai Port, hakika inafikirisha!

Ningetegemea katika ziara yake Dubai angetembelea bandarini kujionea uwezo,ufanisi na kuhoji maswali na kudadisi zaidi badala yake akaishia kuendeshwa na vigari.


waAfrika tuna ubinafsi sana, imagine wanashiriki kuwauza wenzao utumwani kwa vitrip vya Dubai.., hii nguvu kubwa hivi inayotumika mjue tunakuja kuumizwa vibaya sana, maana hizi pesa lazima zirudi
 
Nchi ngumu sana hii, siku watanzania tutakapoamua kuungana bila kujali uvyama, udini wetu ndiyo utakuwa mwisho wa ushenzi huo
Wakati wenzetu Kenya wanateswa na Ukabila na sisi tukiwacheka kwa hilo.
Tanganyika yetu inateswa na uVyama + udini na tupo blind hatuoni namna unavyoliangamiza taifa. Kila linapojitikeza jambo la kutetea nchi. Utaona Uccm upo mbele kuliko nchi, na itachomekwa dini ili mradi tu kuvuruga ajenda!
 
Watanzania wenzangu hatima ya ustawi wa Taifa letu upo mikononi mwetu. Ni wajibu wetu kama Watanzania tujizuie kwa namna yeyote ima kununuliwa ama kushawishiwa kwa namna yeyote ile ilmradi tuligawe Taifa na rasilimali zetu.

Safari za namna hiyo za watu maarufu na wasanii wetu kwenda huko Dubai kwa nyakati za SINTOFAHAMU kubwa ihusuyo bandari yetu na wao badala ya kueleweka hakika zinaongeza maswali mengi mno kwa wenzetu wenye mashaka na mradi wetu pendwa tarajiwa.

Nakemea kwa nguvu zote, njia za aina yeyote zifananazo na hiyo ya ushawishi kwa jamii yetu kuhusu hilo!

Vilevile, siamini hao wasanii na watu maarufu wanatumia pesa zao kutoka mfukoni kuhimili gharama za hoteli za aina hiyo ya hapo juu kwa zaidi ya siku nne!

JE, KAMA HAWA WASANII WANATUNZWA KIFALME HIVYO (kama ni kweli) ILIKUWAJE KWA WAWAKILISHI WETU WALE 30?!

NAANZA KUHOFIA PENGINE TUPO KWENYE HATARI TARAJIWA!

Chama changu CCM naomba kama kikombe hicho kinaweza kutuepuka kwa kuzingatia MASLAHI MAPANA kwa Taifa letu tulipendalo na tukiepuke!

Kidumu Chama cha Mapinduzi.
View attachment 2666858
Yaani ukiangalia influencers na role models wa watanzania, unapata picha kwanini nchi inakuwa ya hovyo. Maana hao watu mmewatengeneza nyie, mmewapa umaarufu nyie, mnawapa trnding nyie na mtaji wao mkubwa ni fanbase yao ambayo ni nyie.
Hata akuna DP- World na makampuni mengine yana watumia sababu yanaona ndiyo watanzania wanaofuatiliwa kwa wingi kuliko watanzania wengine
 
Watanzania wenzangu hatima ya ustawi wa Taifa letu upo mikononi mwetu. Ni wajibu wetu kama Watanzania tujizuie kwa namna yeyote ima kununuliwa ama kushawishiwa kwa namna yeyote ile ilmradi tuligawe Taifa na rasilimali zetu.

Safari za namna hiyo za watu maarufu na wasanii wetu kwenda huko Dubai kwa nyakati za SINTOFAHAMU kubwa ihusuyo bandari yetu na wao badala ya kueleweka hakika zinaongeza maswali mengi mno kwa wenzetu wenye mashaka na mradi wetu pendwa tarajiwa.

Nakemea kwa nguvu zote, njia za aina yeyote zifananazo na hiyo ya ushawishi kwa jamii yetu kuhusu hilo!

Vilevile, siamini hao wasanii na watu maarufu wanatumia pesa zao kutoka mfukoni kuhimili gharama za hoteli za aina hiyo ya hapo juu kwa zaidi ya siku nne!

JE, KAMA HAWA WASANII WANATUNZWA KIFALME HIVYO (kama ni kweli) ILIKUWAJE KWA WAWAKILISHI WETU WALE 30?!

NAANZA KUHOFIA PENGINE TUPO KWENYE HATARI TARAJIWA!

Chama changu CCM naomba kama kikombe hicho kinaweza kutuepuka kwa kuzingatia MASLAHI MAPANA kwa Taifa letu tulipendalo na tukiepuke!

Kidumu Chama cha Mapinduzi.
View attachment 2666858
Umaskini na ubinafsi ni jambo baya sana!
 
Nyerere namnukuu na kumuandika sana, hata nyuzi zake nimefunguwa.


Naiona fitna kubwa sana. Lakini sistuki sana kwa hilo, kwa kuwa Uislam umeshaliandika kwenye Qur'an. Fitna kubwa sana ni mali. Na hii ni deal ya karne, ina mali nyingi sana ndani yake, kwa hiyo fitna siyo kubwa tu bali nyingi.

Licha ya hayo, pia Qur'an inatufundisha, kuwa kuna nyakati mnavipenda vitu lakini ndiyo shari yenu na kuna nyakati mnavichukia vitu lakini ndiyo kheri yenu.

Waislam tunaamini kuwa alitakalo Allah hakuna binaadam yeyote anaeweza klizuwia na pia asilolitaka, hakuna binaadam yeyote anaeweza kulifanya.


Kwa aya hizo, hakuna Muislam mwenye kuogopa kufanya chochote cha halali.
Mnduku mkubwaa
Watu wanahoji aina ya mkataba na baadhi ya vipengele vyenye hila kwenye mkataba.
Wewe unatuletea mavitu ya ajabu eti uislam, uislam, uislam
Uislam wa NYOKWE!
 
Mtamlaum bure Baba Levo, katoka Kigoma kaja mjini, fursa zimemfata atafanya nn? Shida ni moja tunatokea kwenye umasikini mkubwa sana na wengine hawakupata hata hizi exposure za kulala kwenye hotel nzuri, kuona ndege n.k ikiwekwa pesa unachanganyikiwa kabisa.

Ila kiuhalisia, inasikitisha na kufurahiaha sana 😂
 
Back
Top Bottom