Kama ni miujiza, Tanzania ya viwanda inawezekana; kama ni mpango mkakati, tumeshindwa kabla ya kuanza

Kama ni miujiza, Tanzania ya viwanda inawezekana; kama ni mpango mkakati, tumeshindwa kabla ya kuanza

Elevat Kapela

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2017
Posts
631
Reaction score
1,837
Rais Magufuli anaweza kuwa na ndoto nyingi sana juu ya Taifa hili lkn naamini ameshindwa kabla ya kuanza.

Tuanze na hiki ninachokisikia mara kwa mara kikitamkwa na rais na watendaji wake Tanzania ya viwanda. Je Tanzania ya viwanda yaweza kufikiwa? Jibu ni Hapana.

Sababu ni zifuatazo:

1. Hakuna intelejensia ya uchumi inayohusika na suala hili.
Kwa wasiojua, nchi yeyote unayoiona imeendelea kiviwanda ujue wana fanya kitu kinachoitwa "economic intelligence" ambayo kazi yake ni kutafuta taarifa, kuzichambua na kuja na jawabu wapi kijengwe kiwanda gani na kwa nini?

Pia kikundi cha majasusi wa kiuchumi wanatakiwa kukokotoa malighafi na zao la bidhaa linalozalishwa, pia huangalia masoko ya bidhaa hizo pamoja na ushindani wake.

Katika hili hufanya uchambuzi wa kitaalamu ambao utasaidia kuutazama ushindani wa bidhaa za nje na kutafuta namna ya kufanya fitna juu ya bidhaa za nje zisinunulike ndani kwa lengo la kulinda bidhaa za ndani. Likiliangalia jambo sioni kama serikali inalifanyia kazi lakini naona matamko tu yasiyokuwa na maana.

2. Teknolojia na wataalam. Nilimsikia waziri Jafo akiagiza kila mkoa unatakiwa uwe na viwanda 100. Kiukweli kama mchumi nilipigwa na butwaa. Swali la kujiuliza viwanda gani hivyo vinatakiwa kuwa 100?

Kwa wataalam gani walioandaliwa kufanya kazi kwenye viwanda hivyo? Kwa teknolojia ipi itasaidia viwanda hivyo vizalishe bidhaa bora kwa ushindani katika kizazi hili cha zama za taarifa?. Mathalani, chukulia mkoa wa Shinyanga wenye wilaya nne uwe na viwanda mia, kwa maana kila wilaya iwe na viwanda 25.

Sasa kwa mtu mwenye akili sawia ni malighafi ipi inapatikana Shinyanga vijijini inayoweza kuhimili viwanda 25? Kwa nguvu kazi ipi ipo Shinyanga vijijini kuhimili viwanda 25? Kwa nishati gani itatumika kuendesha hivyo viwanda 25? Ukijiuliza maswali haya utaona ndoto ya Tanzania ya viwanda kwa serikali hii haitatimia.

3. Serikali imeshindwa kufanya kazi kama timu. Nina imani wizara zote zilizoundwa hazina muunganiko wa kufikia dira moja. Katika nchi za Ki- Afrika kila waziri anapuyanga kivyake tu ili mradi aonekane kwenye luninga akisisitiza jambo au akitoa maelekezo. Mathalani waziri wa Kilimo ndani ya nchi anaweza kuwa hana mawasiliano na waziri wa nishati kwa kudhani hakuna wanapokutana kidhamira.

Usishangae DAS akiongea lake na DED akiwa na lake ndani ya wilaya moja. Omba MUNGU akupe muda mrefu wa kuishi uone ukweli huu kuwa kwa serikali hii ya ccm hakuna Tanzania ya viwanda Bali Kuna maneno tu yasikuwa na Mipango mikakati.

4. Wizi wa teknolojia. Naamini kama nchi hakuna tulikopeleka vijana wetu wakaibe teknolojia baadaye warudi. Naaminisha kuwa tunaweza kupeleka vijana wetu China na wakaajiriwa huko kama wafanyakazi kumbe nyuma ya pazia wajue wameenda kujifunza teknolojia ambayo tunahitajika waifanyie kazi hapa nchi kwa kuiboresha zaidi.

5. Fedha za kuendesha na kuboresha viwanda hazipo. Ukweli usiopingika kwa hali hii ya nchi sioni mwale wa matumaini juu ya viwanda, labda kama ni viwanda vya cherehani kama alivyosema waziri twaweza kujikongoja lakini kama tunataka na sisi tuzalishe pikipiki na magari bado tuko mbali sana.

WanaJF kama kuna mtu anaamini kwa serikali hii ya mwendokasi twaweza kupata viwanda naomba anipe facts lakini kwangu mimi kama mchumi na mtaalamu wa mipango naona safari bado ni ndefu sana haya unayoyaona ni maigizo.
 
Nishati/umeme wa kuwasha taa za majumbani tu umetushinda, huo wa kuendeshea viwanda tutautoa wapi. Kilimo chenyewe bado cha kusuasua, leo tunasema habari ya nchi ya viwanda. Hizi ni hadaa za wanasiasa kwa wananchi. Budget ya mwaka uliopita ni ishara ya kwamba hatutafika popote kimaendeleo, zaidi ni wananchi kurudi nyuma na kuzidi kuwa mafukara. Viashiria ni hivi;

1. Hakuna nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma.
2. Kupunguzwa kwa wafanyakazi sekta binafsi/vyeti feki kwa walikuwa serikalini.
3. Kushuka kwa mikopo kutoka kwenye mabenki/uwekezaji pia unashuka.
4. Hakuna ajira mpya za kutosheleza walau nusu ya vijana wenye taaluma zao.
5. Kupungua kwa vijana wasomi, hili bodi ya mikopo wanalifahamu.
6. Mauro ya visa kupungua katika soko/ uwekezeji unashuka na ajira unashuka pia.
7. Pesa/ afisa kuwa ngumu unanikana ni dalili ya economic depression.
8. Matumizi yasiofuta budget iliyopitishwa na bunge, rejea bomberdier n.k.
9. Mikopo ya kimyakimya kutoka nje, rejea SGR, Flyover, Ubungo interchange na bado Stiegler gorge then pesa zinarudi hukohuko now mana tenderers wote ni wa nje.

Na mambo mengine mengi yasiyoeleweka yanayofanywa na serikali ya awamu hii.
 
Huwezi ukakitupa kilimo huku ukifikiria unaweza kuleta mapinduzi ya viwanda, tatizo la serikali hii ni kutaka kufanya mambo kisiasa, wanataka wafanye kila kitu within limited time kitu ambacho hakiwezekani, mwisho wa wata fail kwenye kila kitu, hawataka kufanya mambo kitaalamu kwasababu unahitajika muda mrefu wakati siasa ina kipindi maalum na baada ya hapo unatakiwa tena kurejea kwa wananchi kuomba ridhaa.
 
- Kinachozungumzwa hapa ni Tanzania ya Viwanda au Serikali ya viwanda?

- Kumekuwa na malalamiko juu ya ukosefu wa ajira; je, ukosefu / uhaba wa nguvu kazi unaozungumzwa hapa ni upi?

Kwangu mimi cha msingi ni kuwa na njozi (vision), uthubutu /dhamira ya dhati (dare) na kuwa na mpango kazi (road map). Je, ni kweli kwamba nchi haina mambo hayo matatu
?
Natamani kama mjadala huu ungeahirishwa hadi mwishoni mwa 2019, kama itapendeza. Bila hivyo itakuwa ni kama tunapiga ramli japo factors na facts zinaweza zitupe mwanga wa huko tunakotamani kwenda - Tanzania ya Maisha ya Kati / Tanzania ya Viwanda!
 
What were the reasons that allowed Britain to become first industrialized nation in the world? Discuss both geographical and social reasons
  • There are a number of reasons why (according to scholars) the Industrial Revolution began in Britain and not in some other country. Some of these reasons are geographical, while others are social and/or political. Let us examine some of the most important of these factors.

    First, there are at least two major geographic factors that helped Britain industrialize before anyone else did. For one thing, there were huge deposits of coal in Britain that could be used to power the new machines. Just as important was the importance of waterways in Britain. There were many navigable rivers and the coal deposits tended to be near those rivers. Britain also had a long and jagged coastline that made transportation by sea easier. In these ways, Britain had the ability to extract coal and to move it about the country relatively easily. This helped make industrialization possible.

    A second factor was the empire that Britain controlled overseas. The British Empire provided raw materials for British mills and captive markets for its finished goods. For example, a great deal of the cotton that Britain used in its textile mills came from the American colonies. Since Britain had a larger empire than any other country, it had an advantage in the process of industrializing.

    Finally, we can look at political and social factors. Britain had an economy that was much less regulated than the economies of other countries. This relatively laissez-faire system helped to promote innovation of the sort that led to the technology used in the Industrial Revolution. Britain had also been relatively free from domestic conflict for some time. This made it easier for businesses to grow and prosper. A final factor was the enclosure movement. British landlords had been able to push their peasants off the land. Those peasants then became a large supply of labor that could be used to work in the new factories that were springing up.

    All of these factors helped make Britain the first country to industrialize.
 
Economic intelligence ipo kwa sana tu, na ndio maana unaona wakijenga na kuimarisha miundo mbinu rafiki kwa mwekezajj maana serikali haifanyi shughuli hizo.

Miti inatereza kwa kujitekenya kwao
 
Shinyanga haitazamwi kuwa soko pekee la viwanda hivyo 25, bali Tanzania yote na nne yake, mwekezaji anajua hilo
 
Serikali ni timu moja ambapo ktk kila wiki, makatibu wakuu hukutana pamoja na rais Mara moja.
 
Asante mtaalamu Kapela! Kiukweli hata dhamira ya kuwa na viwanda nchi hii haipo. Kilichopo ni kampeni za uraisi 2020. Ulichoandika ni facts kuhusu ndoto hizi za mchana na wachumi wengi humu JF tumelisemea sana hili jambo ambalo halihitaji degree ya uchumi kuelewa kuwa kwa uongozi uliopo litabakia kuwa ndoto.

Watu wanafikiri viwanda vinaanzishwa kwa matamko na kukua kama uyoga. Bila ya kuwa na mikakati iliyokwenda shule tusahau kabisa.

Kwa maoni yangu, tulipaswa kuwa na:
1. Mapinduzi ya kilimo kwanza; mifumo ya umwagiliaji ingejengwa kwa wingi huku ikibidi kuleta wawekezaji wa nje kulima kibiashara.
2. Kuingeza thamani ya mile kinachozalishwa shambani, kiasi cha kuuza nje.
3. Kuboresha diplomasia na intelegensia ya uchumi.
4. Kuboresha elimu katika ngazi zote katika namna ambayo itaongeza human capital inayohitajika sana katika mapinduzi ya viwanda.
5. Nishati ya umeme ya uhakika. Tuna gesi, makaa ya mawe na maji mengi, upepo mwingi na mwanga wa jua wa kutosha.

I DO NOT believe in miracles!
 
Umeambiwa ukiwa na vyerehani vinne ni kiwanda, hivyo jafo hajakosea kusema kila mkoa uwe na viwanda 100
 
Serikali ya awamu hii ina matamanio ya kuiona nchi inakuwa na viwanda lakini haina mipango ya kusababisha viwanda viweze kujengwa.

Hakuna nchi au mtu anayependa kuwa maskini lakini utofauti wa mipango ndiyo unaoamua nani awe tajiri na nani aendelee kuwa maskini. Mipango yetu inadhihirisha kuwa tumeamua kuendelea kuwa maskini.
 
Kwanza ungetueleza nini maana ya nchi ya viwanda?

Tunamaanisha nini tunaposema "Tanzania ya viwanda?

Tupo wapi sasa na tutapimaje (evaluate) progress na tutajuaje kuwa tumefikia lengo?

What makes a "semi-industrialized country?"

Anza kujibu hilo, halafu upambanue ubovu wa mipango na matendo yetu kama nchi. Siyo kuanzia juujuu.
 
Kwanza ungetueleza nini maana ya nchi ya viwanda?

Tunamaanisha nini tunaposema "Tanzania ya viwanda?

Tupo wapi sasa na tutapimaje (evaluate) progress na tutajuaje kuwa tumefikia lengo?

What makes a "semi-industrialized country?"

Anza kujibu hilo, halafu upambanue ubovu wa mipango na matendo yetu kama nchi. Siyo kuanzia juujuu.
Unajibu hoja zangu au unaniuliza maswali? Jibu hoja?
 
Back
Top Bottom