Kama ni miujiza, Tanzania ya viwanda inawezekana; kama ni mpango mkakati, tumeshindwa kabla ya kuanza

Kama ni miujiza, Tanzania ya viwanda inawezekana; kama ni mpango mkakati, tumeshindwa kabla ya kuanza

They played a plunk to the fools....Sisi wengine tulishajua toka day one kwamba this was another hoax. Tanzania ya viwanda katika nchi ambayo asilimia 70 ya watu wake wanatumia vibatari? give me a very big break.
 
Rais Magufuli anaweza kuwa na ndoto nyingi sana juu ya Taifa hili lkn naamini ameshindwa kabla ya kuanza.

Tuanze na hiki ninachokisikia mara kwa mara kikitamkwa na rais na watendaji wake Tanzania ya viwanda. Je Tanzania ya viwanda yaweza kufikiwa? Jibu ni Hapana.

Sababu ni zifuatazo.
1. Hakuna intelejensia ya uchumi inayohusika na suala hili. Kwa wasiojua, nchi yeyote unayoiona imeendelea kiviwanda ujue wana fanya kitu kinachoitwa "economic intelligence" ambayo kazi yake ni kutafuta taarifa, kuzichambua na kuja na jawabu wapi kijengwe kiwanda gani na kwa nini?.

Pia kikundi cha majasusi wa kiuchumi wanatakiwa kukokotoa malighafi na zao la bidhaa linalozalishwa, pia huangalia masoko ya bidhaa hizo pamoja na ushindani wake.

Katika hili hufanya uchambuzi wa kitaalamu ambao utasaidia kuutazama ushindani wa bidhaa za nje na kutafuta namna ya kufanya fitna juu ya bidhaa za nje zisinunulike ndani kwa lengo la kulinda bidhaa za ndani. Likiliangalia jambo sioni kama serikali inalifanyia kazi lakini naona matamko tu yasiyokuwa na maana.

2. Teknolojia na wataalam. Nilimsikia waziri Jafo akiagiza kila mkoa unatakiwa uwe na viwanda 100. Kiukweli kama mchumi nilipigwa na butwaa. Swali la kujiuliza viwanda gani hivyo vinatakiwa kuwa 100?

Kwa wataalam gani walioandaliwa kufanya kazi kwenye viwanda hivyo? Kwa teknolojia ipi itasaidia viwanda hivyo vizalishe bidhaa bora kwa ushindani katika kizazi hili cha zama za taarifa?. Mathalani, chukulia mkoa wa Shinyanga wenye wilaya nne uwe na viwanda mia, kwa maana kila wilaya iwe na viwanda 25.

Sasa kwa mtu mwenye akili sawia ni malighafi ipi inapatikana Shinyanga vijijini inayoweza kuhimili viwanda 25? Kwa nguvu kazi ipi ipo Shinyanga vijijini kuhimili viwanda 25? Kwa nishati gani itatumika kuendesha hivyo viwanda 25? Ukijiuliza maswali haya utaona ndoto ya Tanzania ya viwanda kwa serikali hii haitatimia.

3. Serikali imeshindwa kufanya kazi kama timu. Nina imani wizara zote zilizoundwa hazina muunganiko wa kufikia dira moja. Katika nchi za Ki- Afrika kila waziri anapuyanga kivyake tu ili mradi aonekane kwenye luninga akisisitiza jambo au akitoa maelekezo. Mathalani waziri wa Kilimo ndani ya nchi anaweza kuwa hana mawasiliano na waziri wa nishati kwa kudhani hakuna wanapokutana kidhamira.

Usishangae DAS akiongea lake na DED akiwa na lake ndani ya wilaya moja. Omba MUNGU akupe muda mrefu wa kuishi uone ukweli huu kuwa kwa serikali hii ya ccm hakuna Tanzania ya viwanda Bali Kuna maneno tu yasikuwa na Mipango mikakati.

4. Wizi wa teknolojia. Naamini kama nchi hakuna tulikopeleka vijana wetu wakaibe teknolojia baadaye warudi. Naaminisha kuwa tunaweza kupeleka vijana wetu China na wakaajiriwa huko kama wafanyakazi kumbe nyuma ya pazia wajue wameenda kujifunza teknolojia ambayo tunahitajika waifanyie kazi hapa nchi kwa kuiboresha zaidi.

5. Fedha za kuendesha na kuboresha viwanda hazipo. Ukweli usiopingika kwa hali hii ya nchi sioni mwale wa matumaini juu ya viwanda, labda kama ni viwanda vya cherehani kama alivyosema waziri twaweza kujikongoja lakini kama tunataka na sisi tuzalishe pikipiki na magari bado tuko mbali sana.


WanaJF kama kuna mtu anaamini kwa serikali hii ya mwendokasi twaweza kupata viwanda naomba anipe facts lakini kwangu mimi kama mchumi na mtaalamu wa mipango naona safari bado ni ndefu sana haya unayoyaona ni maigizo.
Umetokwa mapovu tu hakuna la maana uliloongea. Argument zako zote hazina nukuu yeyote ya kitaalam, je inchi za kwanza kuanzisha viwanda vilifanya uchunguzi toka nchi zipi? Industrial revolution ilifanyika wapi hiyo intelijensia ya uchumi? Hayo ni mawazo ya Kichadema hayana nafasi kwa Tanzania ya leo.
 
Shinyanga haitazamwi kuwa soko pekee la viwanda hivyo 25, bali Tanzania yote na nne yake, mwekezaji anajua hilo
Hapa kumbuka mpango ni kila mkoa viwanda 100. Maana yake, Shinyanga 100, Tabora 100 vivyo hivyo na mikoa mingine yote 34 Tanzania nzima....

Sasa Shinyanga wakauze wapi Magari, matrekta, vipuri vya magari, vyandarua, nguo zao nk iwapo mikoa mingine nayo inazalisha bidhaa hizohizo? Ndiyo, si kila mkoa una viwanda 100 bwana na mingine pengine kuvuka lengo hata kujenga 1,000?

Nimekupa changamoto hii kwa sababu, labda hujaielewa mantiki ya mleta mjadala huu...

Kwamba, strategically hivi viwanda 100 wanaosisitizwa wakuu wa mikoa wajenge ktk mikoa yao ni vipi hivyo?
Je, vyerehani vya kushonea viraka kama tunavyoambiwa?

Kama ni hili la mwisho, mleta mada kasema wazi kabisa kuwa, basi sera ya ujenzi wa viwanda kwa mujibu wa Pombe Magufuli na CCM inawezekana na tena Tanzania ifikapo 2020 tutakuwa na viwanda vya namna hiyo hata 20,000,000 kwa maana kila mwananchi aweza kuwa anamiliki kiwanda chake kama kumiliki pea ya viatu vile!!
 
Jibu maswali kwanza kwa sababu inawezekana umelikuza sana hili swala la "Tanzania ya viwanda" Kiasi cha kuona haliwezekani. Sasa kwa kuwa wewe umesema ni mtaalam, ungetujulisha hilo kwanza ili tuendelee.
Mimi sijaona kama kalikuza ama kalifanya dogo...

Alichofanya ni kueleza jinsi sera ya ujenzi wa viwanda ilivyo ngumu kutekelezeka kwa mtazamo na vigezo vyake kwa elimu yake ya uchumi aliyonayo...

Kwa maana hiyo, kama kuna mahali unataka kum - challenge, fanya hivyo kwa kukosoa hoja zake na kuweka zako ili wengine tuendelee kujifunza...

Nadhani hii ndiyo maana ya mijadala, au siyo bwana?
 
Mimi sijaona kama kalikuza ama kalifanya dogo...

Alichofanya ni kueleza jinsi sera ya ujenzi wa viwanda ilivyo ngumu kutekelezeka kwa mtazamo na vigezo vyake kwa elimu yake ya uchumi aliyonayo...

Kwa maana hiyo, kama kuna mahali unataka kum - challenge, fanya hivyo kwa kukosoa hoja zake na kuweka zako ili wengine tuendelee kujifunza...

Nadhani hii ndiyo maana ya mijadala, au siyo bwana?
Maswali Ni sehemi mojawapo ya mjadala.

Tanzania ya viwanda inawezekana Sana, bila intelligence au kuiba technology Kama anavyodai mleta mada.

Viwanda kuwepo Tanzania ndiyo kutachochea technology transfer. Unaleta viwanda, na viwanda vinakuletea technology. Wataendesha wageni kwanza, lakini hatimaye sooner or later wazawa watajifunza technology hiyo.

Haya mambo Ni time-consuming na siyo ya kesho au keshokutwa.
Ndiyo maana nikauliza mleta mada unaipimaje nchi kuwa ya viwanda?

Kutokana na data za UNIDO, 2017 Tanzania Ni nchi mojawapo Africa inayo industrialize fast. Hasa enzi za Kikwete manufacturing was growing really fast.

Inawezekana Tanzania kuwa an industrial economy, mbona Bangladesh, Cambodia Ni industrial economies?

Guatemala Ina Manufacturing Value Addition kubwa kuliko East Africa yote na Ina umeme kidogo kuliko Tanzania. Unajua Hilo?
Tusilalamike serikali tu, what about us? Are we manufacturing minded?

Kwa hiyo maswali yangu yapo very valid. Ni kwamba tu hili jukwaa linatumika for bashing the government kwa masuala ya kisiasa. Ukiwa na mawazo tofauti, utatukanwa na kupingwa.
 
Umetokwa mapovu tu hakuna la maana uliloongea. Argument zako zote hazina nukuu yeyote ya kitaalam, je inchi za kwanza kuanzisha viwanda vilifanya uchunguzi toka nchi zipi? Industrial revolution ilifanyika wapi hiyo intelijensia ya uchumi? Hayo ni mawazo ya Kichadema hayana nafasi kwa Tanzania ya leo.
Pu mbavu badala kujibu hoja unaleta ushabiki wa vyama, muwe mnatumia akili za kichwani na sio za makalio.
 
Maswali Ni sehemi mojawapo ya mjadala.

Tanzania ya viwanda inawezekana Sana, bila intelligence au kuiba technology Kama anavyodai mleta mada.

Viwanda kuwepo Tanzania ndiyo kutachochea technology transfer. Unaleta viwanda, na viwanda vinakuletea technology. Wataendesha wageni kwanza, lakini hatimaye sooner or later wazawa watajifunza technology hiyo.

Haya mambo Ni time-consuming na siyo ya kesho au keshokutwa.
Ndiyo maana nikauliza mleta mada unaipimaje nchi kuwa ya viwanda?

Kutokana na data za UNIDO, 2017 Tanzania Ni nchi mojawapo Africa inayo industrialize fast. Hasa enzi za Kikwete manufacturing was growing really fast.

Inawezekana Tanzania kuwa an industrial economy, mbona Bangladesh, Cambodia Ni industrial economies?

Guatemala Ina Manufacturing Value Addition kubwa kuliko East Africa yote na Ina umeme kidogo kuliko Tanzania. Unajua Hilo?
Tusilalamike serikali tu, what about us? Are we manufacturing minded?

Kwa hiyo maswali yangu yapo very valid. Ni kwamba tu hili jukwaa linatumika for bashing the government kwa masuala ya kisiasa. Ukiwa na mawazo tofauti, utatukanwa na kupingwa.

Yeap. Mimi nilitaka uje na counter attack ya mawazo kama haya sasa kuliko kule mlikokuwa mnataka kuelekezana na mleta mada....

Mimi sitasema you are right or wrong. Lakini nategemea mwanzilishi wa mjadala anaweza sasa kusema kitu kuhusu hiki ulichokiandika...
 
Asante mtaalamu Kapela! Kiukweli hata dhamira ya kuwa na viwanda nchi hii haipo. Kilichopo ni kampeni za uraisi 2020. Ulichoandika ni facts kuhusu ndoto hizi za mchana na wachumi wengi humu JF tumelisemea sana hili jambo ambalo halihitaji degree ya uchumi kuelewa kuwa kwa uongozi uliopo litabakia kuwa ndoto.

Watu wanafikiri viwanda vinaanzishwa kwa matamko na kukua kama uyoga. Bila ya kuwa na mikakati iliyokwenda shule tusahau kabisa.

Kwa maoni yangu, tulipaswa kuwa na:
1. Mapinduzi ya kilimo kwanza; mifumo ya umwagiliaji ingejengwa kwa wingi huku ikibidi kuleta wawekezaji wa nje kulima kibiashara.
2. Kuingeza thamani ya mile kinachozalishwa shambani, kiasi cha kuuza nje.
3. Kuboresha diplomasia na intelegensia ya uchumi.
4. Kuboresha elimu katika ngazi zote katika namna ambayo itaongeza human capital inayohitajika sana katika mapinduzi ya viwanda.
5. Nishati ya umeme ya uhakika. Tuna gesi, makaa ya mawe na maji mengi, upepo mwingi na mwanga wa jua wa kutosha.

I DO NOT believe in miracles!
WEKA NAMBA 4 NDIO IWE YA KWANZA.
 
Rais Magufuli anaweza kuwa na ndoto nyingi sana juu ya Taifa hili lkn naamini ameshindwa kabla ya kuanza.

Tuanze na hiki ninachokisikia mara kwa mara kikitamkwa na rais na watendaji wake Tanzania ya viwanda. Je Tanzania ya viwanda yaweza kufikiwa? Jibu ni Hapana.

Sababu ni zifuatazo.
1. Hakuna intelejensia ya uchumi inayohusika na suala hili. Kwa wasiojua, nchi yeyote unayoiona imeendelea kiviwanda ujue wana fanya kitu kinachoitwa "economic intelligence" ambayo kazi yake ni kutafuta taarifa, kuzichambua na kuja na jawabu wapi kijengwe kiwanda gani na kwa nini?.

Pia kikundi cha majasusi wa kiuchumi wanatakiwa kukokotoa malighafi na zao la bidhaa linalozalishwa, pia huangalia masoko ya bidhaa hizo pamoja na ushindani wake.

Katika hili hufanya uchambuzi wa kitaalamu ambao utasaidia kuutazama ushindani wa bidhaa za nje na kutafuta namna ya kufanya fitna juu ya bidhaa za nje zisinunulike ndani kwa lengo la kulinda bidhaa za ndani. Likiliangalia jambo sioni kama serikali inalifanyia kazi lakini naona matamko tu yasiyokuwa na maana.

2. Teknolojia na wataalam. Nilimsikia waziri Jafo akiagiza kila mkoa unatakiwa uwe na viwanda 100. Kiukweli kama mchumi nilipigwa na butwaa. Swali la kujiuliza viwanda gani hivyo vinatakiwa kuwa 100?

Kwa wataalam gani walioandaliwa kufanya kazi kwenye viwanda hivyo? Kwa teknolojia ipi itasaidia viwanda hivyo vizalishe bidhaa bora kwa ushindani katika kizazi hili cha zama za taarifa?. Mathalani, chukulia mkoa wa Shinyanga wenye wilaya nne uwe na viwanda mia, kwa maana kila wilaya iwe na viwanda 25.

Sasa kwa mtu mwenye akili sawia ni malighafi ipi inapatikana Shinyanga vijijini inayoweza kuhimili viwanda 25? Kwa nguvu kazi ipi ipo Shinyanga vijijini kuhimili viwanda 25? Kwa nishati gani itatumika kuendesha hivyo viwanda 25? Ukijiuliza maswali haya utaona ndoto ya Tanzania ya viwanda kwa serikali hii haitatimia.

3. Serikali imeshindwa kufanya kazi kama timu. Nina imani wizara zote zilizoundwa hazina muunganiko wa kufikia dira moja. Katika nchi za Ki- Afrika kila waziri anapuyanga kivyake tu ili mradi aonekane kwenye luninga akisisitiza jambo au akitoa maelekezo. Mathalani waziri wa Kilimo ndani ya nchi anaweza kuwa hana mawasiliano na waziri wa nishati kwa kudhani hakuna wanapokutana kidhamira.

Usishangae DAS akiongea lake na DED akiwa na lake ndani ya wilaya moja. Omba MUNGU akupe muda mrefu wa kuishi uone ukweli huu kuwa kwa serikali hii ya ccm hakuna Tanzania ya viwanda Bali Kuna maneno tu yasikuwa na Mipango mikakati.

4. Wizi wa teknolojia. Naamini kama nchi hakuna tulikopeleka vijana wetu wakaibe teknolojia baadaye warudi. Naaminisha kuwa tunaweza kupeleka vijana wetu China na wakaajiriwa huko kama wafanyakazi kumbe nyuma ya pazia wajue wameenda kujifunza teknolojia ambayo tunahitajika waifanyie kazi hapa nchi kwa kuiboresha zaidi.

5. Fedha za kuendesha na kuboresha viwanda hazipo. Ukweli usiopingika kwa hali hii ya nchi sioni mwale wa matumaini juu ya viwanda, labda kama ni viwanda vya cherehani kama alivyosema waziri twaweza kujikongoja lakini kama tunataka na sisi tuzalishe pikipiki na magari bado tuko mbali sana.


WanaJF kama kuna mtu anaamini kwa serikali hii ya mwendokasi twaweza kupata viwanda naomba anipe facts lakini kwangu mimi kama mchumi na mtaalamu wa mipango naona safari bado ni ndefu sana haya unayoyaona ni maigizo.

Elevat Kapela, kama mchumi ulivyojitambulisha, heshima kwa uchambuzi wako.

Lakini maelezo yako ni ya Mchumi mwenye mawazo tegemezi ya uchumi wa nadharia kwa dhana kuwa unaamini unaweza kujenga kiwanda cha gari wakati hata mkokoteni hujaanza.

Soko la Tanzania limejaa bidhaa za nje hata tooth pick. Hii ina maana bado tunauza nje malighafi za mazao, uvuvi madini, misitu nk zaidi leo kuliko hata kabla ya uhuru.

Msingi wa kuwa na viwanda ni kuwepo malighafi, miundo mbinu imara ya kupeleka malighafi viwandani na kusafirisha bidhaa zilizozalishwa viwandani, "processing drivers" km nishati, ardhi na rasmaliwatu.

Naamini unajua Serikali inaimarisha miundo mbinu na nishati. Kuna rasmaliwatu isiyo na ajira, mbali ya ardhi kubwa.

Kwamba hakuna mawasiliano kati ya Wizara, unahitaji kutupa ushahidi wa hilo. Rejea hotuba za bajeti za Wizara mbali mbali kuhusu kuelekea ujenzi wa viwanda. Ni bajeti zilizotengezwa kwa "holistic intergration and coordination".

Msomi aliyeelimika hutambua na kukubali wasomi wenzako kama wewe ulivyofanya kwenye mada yako kwa wachumi wa nje. Hivyo ni vyema wakati tunaheshimu mawazo yako ya kiuchumi, na wewe waheshimu wachumi wenzio wanaotayarisha bajeti ya Serikali na Wabunge wanaoichambua na kutoa mapendekezo.

Kama mchumi tafuta mtaji japo ujenge kiwanda cha kuhifadhi mazao ya shamba yanayoharibika haraka kama nyanya. Kwa teknolojia ilivyowazi mitandaoni, hakika hutokosa inayofaa toka "labour intensive" hadi "high tech". Ushahidi kama umetembelea maonesho ya biashara km Nanenane, Sabasaba au ya Vyuo utaelewa nazungumzia nini.

Kinachokosekana ni dhamira na uthubutu wa Viongozi walioko madarakani, kuhimiza ujenzi wa viwanda na kulinda viwanda vya ndani. Labda swali la msingi ni kwa nini viwanda vilivyoanzishwa na Baba wa Taifa vimekufa?

Kwa hitimisho: The wheel has long been inverted what is required is the use of the wheel for our current needs.
 
Back
Top Bottom