Chief Wingia
JF-Expert Member
- Jul 12, 2013
- 2,653
- 4,744
Wasalaam ndg,
Nianze kwakusema kuna binadam wanateseka na magonjwa ile mbaya analazwa hospital hadi anazoeana na kila mfanyakazi wa hospital kuanzia walinzi, wafanya usafi, manesi na madaktari.
Iko hivi last month jumatatu tarehe 20 nilipata ajali maeneo ya Ngunja Mkuranga nikiwa na pikipiki nikitokea shambani Mkiu.
Nikiri kuwa niliponea chupuchupu kifo kwenye ajali ile maana nilizima na kuja kuzinduka nikiwa Mbagala hospital, huku na huku tiba ikashindikana pale kutokana n mvunjiko wa mfupa hivyo nikapewa rufaa ya kwenda MOI maana nilikuwa nimevunjika mara mbili (olecranon bone) mfupa wa kiwiko cha mkono wa kushoto, basi bana nikarudi home ili siku inayofuata niende MOI.
Basi siku iliyofuata nikaenda MOI nikaonana na wataalam nikafanya vipimo na kuambiwa tiba yangu ni kuwekewa chima hivyo nifanye malipo kwajili ya upasuaji.
Sio siri suala la kuwekewa chuma liliniwazisha sana na kuanza kutafuta tiba mbadala lakini at the end nikakubali nakalipia upasuaji na kupangiwa tarehe.
Tarehe ilipofika nikaenda MOI nikafanya kipimo cha damu kisha nikalazwa kwajili ya upasuaji wa kuwekewa chuma siku ya pili yake na nashkutu Mungu nilipata tiba fresh kabisaa na kulazwa kwa siku tano kisha nikaruhusiwa.
Sasa bana kipindi nipo hapo wodini aisee kuna watu wanaumwa kwa mateso sana unakuta mtu kavunjika nyonga, mguu, uti wa mgongo yaani hajiwezi kwa lolote na hana ndugu wala mtu yoyote yule wa kumuhudumia wala kumletea chakula.
Kuna wengine wamekaa muda mrefu hadi wamepatiwa vyeo vya mwenyekiti au katibu wa wodi.
Na mbaya zaidi wengi ni wazee watu wazima.
Aisee wenye ndugu au wazazi waliopo hospital kuweni serious kuwahudumia jamaa wanateseka na kudhalilika sana.
Nianze kwakusema kuna binadam wanateseka na magonjwa ile mbaya analazwa hospital hadi anazoeana na kila mfanyakazi wa hospital kuanzia walinzi, wafanya usafi, manesi na madaktari.
Iko hivi last month jumatatu tarehe 20 nilipata ajali maeneo ya Ngunja Mkuranga nikiwa na pikipiki nikitokea shambani Mkiu.
Nikiri kuwa niliponea chupuchupu kifo kwenye ajali ile maana nilizima na kuja kuzinduka nikiwa Mbagala hospital, huku na huku tiba ikashindikana pale kutokana n mvunjiko wa mfupa hivyo nikapewa rufaa ya kwenda MOI maana nilikuwa nimevunjika mara mbili (olecranon bone) mfupa wa kiwiko cha mkono wa kushoto, basi bana nikarudi home ili siku inayofuata niende MOI.
Basi siku iliyofuata nikaenda MOI nikaonana na wataalam nikafanya vipimo na kuambiwa tiba yangu ni kuwekewa chima hivyo nifanye malipo kwajili ya upasuaji.
Sio siri suala la kuwekewa chuma liliniwazisha sana na kuanza kutafuta tiba mbadala lakini at the end nikakubali nakalipia upasuaji na kupangiwa tarehe.
Tarehe ilipofika nikaenda MOI nikafanya kipimo cha damu kisha nikalazwa kwajili ya upasuaji wa kuwekewa chuma siku ya pili yake na nashkutu Mungu nilipata tiba fresh kabisaa na kulazwa kwa siku tano kisha nikaruhusiwa.
Sasa bana kipindi nipo hapo wodini aisee kuna watu wanaumwa kwa mateso sana unakuta mtu kavunjika nyonga, mguu, uti wa mgongo yaani hajiwezi kwa lolote na hana ndugu wala mtu yoyote yule wa kumuhudumia wala kumletea chakula.
Kuna wengine wamekaa muda mrefu hadi wamepatiwa vyeo vya mwenyekiti au katibu wa wodi.
Na mbaya zaidi wengi ni wazee watu wazima.
Aisee wenye ndugu au wazazi waliopo hospital kuweni serious kuwahudumia jamaa wanateseka na kudhalilika sana.