Kama ni mzima wa afya mshukuru Mungu, kuna watu wanateseka na maradhi

Kama ni mzima wa afya mshukuru Mungu, kuna watu wanateseka na maradhi

Chief Wingia

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2013
Posts
2,653
Reaction score
4,744
Wasalaam ndg,

Nianze kwakusema kuna binadam wanateseka na magonjwa ile mbaya analazwa hospital hadi anazoeana na kila mfanyakazi wa hospital kuanzia walinzi, wafanya usafi, manesi na madaktari.

Iko hivi last month jumatatu tarehe 20 nilipata ajali maeneo ya Ngunja Mkuranga nikiwa na pikipiki nikitokea shambani Mkiu.

Nikiri kuwa niliponea chupuchupu kifo kwenye ajali ile maana nilizima na kuja kuzinduka nikiwa Mbagala hospital, huku na huku tiba ikashindikana pale kutokana n mvunjiko wa mfupa hivyo nikapewa rufaa ya kwenda MOI maana nilikuwa nimevunjika mara mbili (olecranon bone) mfupa wa kiwiko cha mkono wa kushoto, basi bana nikarudi home ili siku inayofuata niende MOI.

Basi siku iliyofuata nikaenda MOI nikaonana na wataalam nikafanya vipimo na kuambiwa tiba yangu ni kuwekewa chima hivyo nifanye malipo kwajili ya upasuaji.

Sio siri suala la kuwekewa chuma liliniwazisha sana na kuanza kutafuta tiba mbadala lakini at the end nikakubali nakalipia upasuaji na kupangiwa tarehe.

Tarehe ilipofika nikaenda MOI nikafanya kipimo cha damu kisha nikalazwa kwajili ya upasuaji wa kuwekewa chuma siku ya pili yake na nashkutu Mungu nilipata tiba fresh kabisaa na kulazwa kwa siku tano kisha nikaruhusiwa.

Sasa bana kipindi nipo hapo wodini aisee kuna watu wanaumwa kwa mateso sana unakuta mtu kavunjika nyonga, mguu, uti wa mgongo yaani hajiwezi kwa lolote na hana ndugu wala mtu yoyote yule wa kumuhudumia wala kumletea chakula.

Kuna wengine wamekaa muda mrefu hadi wamepatiwa vyeo vya mwenyekiti au katibu wa wodi.
Na mbaya zaidi wengi ni wazee watu wazima.

Aisee wenye ndugu au wazazi waliopo hospital kuweni serious kuwahudumia jamaa wanateseka na kudhalilika sana.

IMG_20230413_153000.jpg
 
Pole sana mkuu, ila ukweli ni kwamba hata hao walio na afya nzuri leo, kesho yao ya taabu inakuja na lazima ije tu.

Yaani hakuna binadamu ataishi kwa raha tu hadi kufa. Leo kuna wapo ocean road wanateseka balaa, kesho kuna sie tutaenda huko kupatilizwa, inakuja kwa zamu.
 
Mara nyingi huwa hatuthamini uzima wetu mpaka maradhi yatukumbe.

Wanadamu tungejua hasa ni jinsi gani uzima ni tunu nadhani tungekuwa tunaishi kwa kujitunza mno.

Mbaya zaidi uzima huo huo tunaochukulia for granted unaweza potea kwa jambo la sekunde tu. Mfano muanzisha uzi ulikuwa mzima ulipokwenda safari yako lakini ajali ya sekunde ikakulaza hospitali.

Pole sana mkuu, Mungu azidi kukupa ahueni na ampe uzima kila alie na maradhi.
 
Ukitaka ona thamani ya maisha
Tembelea Ocean Road
Tembelea Mwaisera
Tembelea JKCI kwa Watoto
Tembelea MOI wodi ya boda boda
Tembelea Psych ward MNH
Tembelea Clinic ya Figo


Ukifika huko ndo utaona thamani ya Uhai na hakika hizo BIA, Sigara utaziacha bila kupenda
 
Hakuna atakae pona kwenye hii dunia mkuu...tulizaliwa hospital na tutafia hospitali
Waliozaliwa home nao watafia home mkuu au sio? Au na wale waliozaliwa Ikulu nao watafia Ikulu , ndo unachomaanisha Mkuu?

OYA, ACHA BANGI DOGO!!!

Najua upo kijiweni saa hii umelala juu ya pikipiki unaperuzi tu Jamii forum!!! Uongo Mkuu? Njoo unichukue huku bunju unipeleke AFRIKANA,..nina buku!!!!
 
Duniani hapa ukipita kila Kona unaonyeshwa jinsi watu wanavoenjoy na starehe lakini upande wa pili wa mateso ya hospital hauonyweshi ndio maana unakuta mtu anakunywa vinywaji vikali na ulaji mbovu, bodaboda anaona Raha tu kukimbia kimbia speed etc..lolote linaweza mtokea mtu wakati wowote...Jambo la kusema ndani ya nafsi Yako kuwa huwezi pata ugonjwa Fulani au ajali limejaa ndani ya hurka ya watu...

Mungu awabariki Sana wale wanaowasaidia wagonjwa wasio na ndugu au msaada , maana ukienda muhimbili utakuta watu wa taasisi Fulani ya dini huwa wanajitolea Sana kuwasambazia angalau hata chochote asubuhi..
 
Pole sana mkuu, ila ukweli ni kwamba hata hao walio na afya nzuri leo, kesho yao ya taabu inakuja na lazima ije tu.

Yaani hakuna binadamu ataishi kwa raha tu hadi kufa. Leo kuna wapo ocean road wanateseka balaa, kesho kuna sie tutaenda huko kupatilizwa, inakuja kwa zamu.

Ni maneno magumu sana ila ndo hakuna namna wote lazima tupitie
 
Back
Top Bottom