Kama nidhamu ya uoga inasaidia mambo yaende vizuri, inafaa sana

Kama nidhamu ya uoga inasaidia mambo yaende vizuri, inafaa sana

Wanatekeleza majukumu kinafiki na uogauoga.Haiwezekani ueleze kwamba mtumishi aliyejaa hofu,kutoielewa kesho,kunyanyaswa na Viongozi wa CCM,kipato duni,masimango na kila aina ya kadhia akuletee tija.Kama unaamini anakupa tija,basi ni kwa kiwango duni ambacho nacho kinaitwa kiwango.

Watumishi wengi hasa wa mahospitali, taasisi na ofisi nyingine za umma walikuwa wanatekeleza majukumu ili kulinda vibarua vyao, na hiyo ilihusisha kutoa huduma stahiki kwa wananchi. Au unaongelea wanasiasa?
 
Uko sahihi, lakini kutokuwa na uoga kabisa madhara yake ni makubwa zaidi. Ushajiuliza kwanini watu hawaogopi kukiuka sheria, kanuni na miiko ya maadili ya utumishi wa umma?

Kinachotakiwa ni uoga wenye uzalendo ndani yake,,, yaani unaogopa kufanya kitu fulani kwa dhamira ya kuharibu nchi na sio Mkulu atanifanyaje.... ile inapunguza Creativity sana...

Upo sahihi pia UOGA usipokuwepo kabisa nayo ni hasara x 100....

Nini unashauri kifanyike mkuu?
 
Back
Top Bottom